Dark City
JF-Expert Member
- Oct 18, 2008
- 16,253
- 11,598
Issue ya kukamata % kadhaa kwenye mambo kama ya EPA, RICHMOND e.t.c naona yanaweza yakaangaliwa kwa jicho la makini zaidi. Kuhusu jamaa kubanchua hao akina dada hapa naona tusijikite sana kwani siku hizi imefikia mahali hawa dada zetu wanakuambia ni bora kufa kwa UKIMWI kuliko kufa kwa UPEMI (Ukosefu wa PEsa MIfukoni), hivyo inawezekana wanajipeleka wenyewe kwa kujua jamaa anazo vinginevyo malalamiko yangesikika mapema.
Hapa kazi ipo. Yaani tunafikia mahali pa kushawishiana kuwa uzinzi mahali pa kazi si jambo nyeti?? Au mimi ndiye sielewi vizuri?? Kwa ufahamu wangu na jinsi dunia inavyokwenda, huwezi kuwa mkuu wa taasisi nyeti kama CRDB kama wewe ni mpenda totoz kwa sababu huwezi kutenda haki! Kama kumbukumbu zangu ni nzuri basi wenzangu watakumbuka kuwa boss wa IMF (if not WB) alibwaga manyanga kwa sababu ya kashfa ya ngono na mfanyakazi mwenzake.
CRDB inazo shea za WaTz binafsi na serikali na hizi tuhuma ni nzito. Tusipoteze muda kumjadili aliyetupa taarifa hizi. Kwanza tungetakiwa kumshukuru (hata kama si kweli). Baada ya hapo tuombe (nadhani hili ndilo la muhimu) PCCB na polisi wazifanyie kazi. Kwa mtu makini (hasa wale wanaofanya kazi za intelijensia), tetesi zozote ni mali ghafi (raw materials) za maana sana. Kwa hiyo kazi ianzie hapo ili ukweli ujulikane na kama Kimei anapakwa matope asafishwe (ila si ile safisha safisha ya kisanii kama ya Richmond).