DP WORLD: Mkataba wa Bandari kwa Kiswahili (tafsiri isiyo rasmi)

Tunahangaika na kitu fake,

Mkataba una mianya kibao kuuvunja.

Tukiwadhibiti tu waliyohongwa, kitu inavunjwa.

Asante, Adam kigoma Malima nawe kusaini petition.

Asante sana tai mwenye jicho Kali.
Petition inapatikana wapi aisee sijaisaini
 
Makosa mengi kwenye mkataba huu yako wazi ila ajabu kuna watu hapa wanachangia as if bado kuna teuzi za ma dc, njaa ikihamia kichwani ni tatizo kubwa.
 
Kwa mantiki hiyo huo mkataba tayari ni batili kwani sahihi zimekosewa, na kama ulivyosema mkataba wa serikali lazima utiwe sahihi na mtumishi/mtendaji wa serikali ambaye kwa muktadha huu ni katibu mkuu wa wizara na siyo waziri ambaye ni mwanasiasa, jambo ambalo linatakiwa kushuhudiwa na mwanasheria mkuu wa serikali kwani ndo mwenye wajibu wa kuhakikisha maswala ya kisheria ya nchi ikiwemo mikataba ambayo nchi inaingia.
Wanasema walipewa ruhusa na Mkuu kutoa Saini kwa barua yenye Saini ya Mkuu.
 
Embu niambie! Hapa hapatoshi kuwa na wasisi na mkataba huu kuwa kuna namna tunamendewa tuliwe?

Kwa Upande wa Tanzania
1. Mkataba ulitakiwa usainiwe na Katibu Mkuu na Kushuhudiwa na Mwanasheria mkuu wa Serikali.

#Mkataba umesainiwa na Waziri na umeshuhudiwa na Katibu mkuu.

Sehemu ya mshuhudia usainishaji ina rangi 2 za wino!

Sijui wakiwah nn!

Upande wa Dubai.

1. Mkataba umesainiwa na muhuni gani sijui ata cheo hana, umeshuhudiwa na Muhuni mwenzie ambae hajulikani cheo wala jina!

Tujisahihishe!
Tumejukwaa kwakweli.
PASCAL -SHIJAH
Pascal abely
FaizaFoxy
VUTA-NKUVUTE
ki2c
View attachment 2684113
 
Embu niambie! Hapa hapatoshi kuwa na wasisi na mkataba huu kuwa kuna namna tunamendewa tuliwe?

Kwa Upande wa Tanzania
1. Mkataba ulitakiwa usainiwe na Katibu Mkuu na Kushuhudiwa na Mwanasheria mkuu wa Serikali.

#Mkataba umesainiwa na Waziri na umeshuhudiwa na Katibu mkuu.

Sehemu ya mshuhudia usainishaji ina rangi 2 za wino!

Sijui wakiwah nn!

Upande wa Dubai.

1. Mkataba umesainiwa na muhuni gani sijui ata cheo hana, umeshuhudiwa na Muhuni mwenzie ambae hajulikani cheo wala jina!

Tujisahihishe!
Tumejukwaa kwakweli.
PASCAL -SHIJAH
Pascal abely
FaizaFoxy
VUTA-NKUVUTE
ki2c
View attachment 2684113
Rangi mbili kwenye sahihi, inaonekana kama mwarabu alitaka adondoke sahihi kwa niaba ya waziri.. afu akastuka.
 
Nguvu kubwa inatumika kutetea hili jambo la DP World.. Na watu wengi wanapinga .. Ni ishara ya kwamba kuna vitu havipo sawa.. ni swala la mda tu
Nimetembelea mitandao yote na nikagundua kuwa ni JF na Clubhouse tu ndio wanatumia nguvu sana na pesa kupinga Mkataba wa DP World. Nikajiuliza, hivi hawa watu wanalipwa na nani?
 
Mimi ngoja niwasaidie ili msiparurane, huyo mama tunanuonea bure.

Nchi inauzwa na Watanganyika wenzetu, wabunge wangekuwa wazalendo wala leo tusingekuwa na mjadala huu.

Tujifunze kuwajuwa maadui wetu halisi badala ya kuangalia na mtu ambaye hana uwezo wa kujuwa ubaya au uzuri wa huu uhuni.

Maadui zetu ni Watanganyika na si Wazanzibar wala waislamu.

Mnaokumbuka kundi la G55 lililoongozwa na Njelu Kasaka mtakuwa najuwa nguvu ya bunge.

Na haya ni madhara aliyotuachia Magufuli hili ndio bunge alilotaka yeye kuwa rubber stamp ya serikali.

Kwa bunge hili hata Lowasa angekaa kwenye uwaziri mkuu mpaka mwisho wa muda wake.
Kuwafananisha wabunge wa enzi za mwl na hawa wa sasa hivi ni uzalilishaji hili la sasa hivi ni genge la walanguzi linatumia jengo la bunge kuhalalisha ulanguzi
 
Samia amefanya kazi kubwa sana kuikuza nchi kisiasa na kijamii na kujenga uchumi kwa kumaliza miradi iliyoanzishwa na mtangulizi wake.

Tuendelee kumkosoa kwenye suala la Bandari na DP WORLD kwa staha lakini tusimkosee heshima kwa matusi na dharau.

Tanzania bado iko mikono salama chini ya Samia kwa hii miaka 3 kuliko ilivyokuwa kati ya 2015 -2021
Nahisi ukiielewa kazi aliyoifanya kuibuwa madudu ya bandarini na hii vita anayopigwa utaelewa kwanini Mama Samia ni chaguo la Mwenyezi Mungu na kwanini hatetereki.
 
Hakuna mkataba hapo ni kanjanja tu. Kila siku ukichunguza sana unakutana na tukio la kijuha kwenye huo mkataba. Daah mtu asie na chogo hana maumivu kabsaaa na Mali ya Tanganyika, almradi ni Mali ya Tanganyika bas we puyanga tu, watajijua wenyewe almradi sisi ni WaZanzibar basi tupo salama kina chogo hawanaga shida.
Tuwekee mkataba usio feki tuusasambuwe.
 
 
Nguvu kubwa inatumika kutetea hili jambo la DP World.. Na watu wengi wanapinga .. Ni ishara ya kwamba kuna vitu havipo sawa.. ni swala la mda tu

Upo sahihi sana mkuu kele ni nyingi sana,tupaze sauti
 
Ukitaka kujua vzr kuwa uelewa wa watanzania bado sana njoo kweny uzi kama huu afu anza kupitia coments..
 
Ubovu wake uko wapi?
Lugha ni ya kisheria mpaka mtaaluma wa sheria akufafanulie otherwise huwezi kuelewa kitu hapo.
Hata hivyo, huwezi jua aliyetafsiri, kwamba, anao weledi wa kutafsiri lugha, au, yupo upande upi; wanaopinga, au, wasiopinga.
 
Kwanza hujausoma, na umetoka mtupu hujaelewa chochote, pili huyu mhuni inaonekana ametumia google kutafsiri mkataba halisi ndio maana kimekuja kioja. Kuna maneneo ya kiingereza ndani ya Kiswahili, aliyeleta hiki kitu ni mhuni flani tu mwenye nia ya kipuuzi. Lete mkataba halisi km ulivyoandikwa kwa Kiingereza. Tafsiri iwe rasmi siyo huu upuuzi
Kumbe umetafsiri kupitia machinery. Ana lake jambo huyu. Halafu, kwa nini jamaa zetu waislamu wamejipambanua kuutetea kwa nguvu zote Makubaliano haya??
 
Back
Top Bottom