zitto bado yuko sahihi kwani ushauri wake hauna hisia kama wafanyavyo sitta, mwakyembe na wenzao.
ccm wana mambo yao na zitto amewashika patamu kwani tabia yao mbaya ya kuendekeza ushabiki kwenye masilahi ya nchi imepitwa na wakati.
zitto asonge mbele na maoni yake kwani hata ile ya buzwagi sitta alimkebehi na kumwadhibu kupitia genge laooooo.
kwa nn akina sitta na wenzao hawakemei mambo chungu mbovu yaliyomo zaidi ya dowans ila kwa kuwa hili wana masilahi bianafsi wanajifanya vinara???
mangapi ushabiki wa ccm unaendelea kukumbatia na sitta kama kada amayanyamaziaaaa...
Zitto waeleimishe kuwa hizo kamati sio siasa ni utendaji na utaalamu tena unaotakiwa kuwa muwazi kila mambo kwa mustakabali wa taifa letuuu..
kwa hili zitto anazidi kuijenga chadema kwa watu MAKINI.....
Ndugu yangu Nyauba, naweza kukubaliana nawe kwenye moja tu kati ya ninayoamini unamaanisha. Nalo ni kuwa, Zitto anayo haki ya kusema anachokiamini. Basi.
Mkuu, nimesikiliza mahojiano ya waheshimiwa wote watatu (Dr. W. Slaa, Zitto na Mwakyembe) kupitia ITV jana jioni. Nilichokiona kutoka kwao ni uelewa usiolingana wa issue iliyoko mbele yetu.
Mh. Dr. W. Slaa, alielezea jinsi anavyoona inafaa kushughulikia suala la manunuzi ya mitambo ya DOWANS. Alikuwa mwangalifu sana katika kauli zake. Ila ni dhahiri kuwa busara zake hazimtumi kukubaliana na mawazo ya Zitto katika kushughulikia suala hilo. Dr. Slaa alikwepa kukosoa moja kwa moja mtazamo wa mwenzake (Zitto) kuhusiana na suala hilo. Vile vile Dr. Slaa alielezea kama ambavyo imekuwa ikielezewa hapa JF na kuomba kupata maelezo zaidi ya reports za Kamati za Bunge (Madini na Nishati na Matumizi ya Umma) kuhusiana na sakata hili.
Mh. Zitto alinisikitisha sana. Maelezo yake yalikuwa yakipingana pingana kadiri alivyokuwa akiendelea kuzungumza. Alionyesha either kutokujua alichokuwa anakiongea, au kutokiamini alichokuwa akikisema. Kwa mfano, Mh. Zitto alisema "suala ni je, mitambo hiyo inafanya kazi au lah". Kwa mtazamo wangu, kufanya kazi au kutofanya kazi kwa mitambo ya DOWANS hakuifanyi ikubalike hasa kama inatakiwa kununuliwa kinyume cha sheria. Mitambo hata iliyo chakavu na inayouzwa duniani, pia inafanya kazi. Suala ni je tuko tayari kutupilia mbali sheria za nchi yetu kwa manufaa ya DOWANS? Kama jibu ni ndio. Swali la nyingeza tunalotakiwa kujiuliza ni
"Kwa manufaa ya nani"?
Nakubaliana sana na maelezo ya Mwakyembe kuhusiana na issue ya TANESCO kukusudia kununua mitambo ya DOWANS. Mwakyembe alisema kuwa:
1. TANESCO wakitaka kununua mitambo hiyo wanaweza kufanya hivyo, kama wanavyofanya kwenye manunuzi mengine yote (Bunge halihusiki kuamua juu ya hilo)
2. Kamati ya Bunge (Nishati na Madini) haioni manunuzi hayo kuwa ni sahihi kwa kuzingatia mchakato mzima wa manunuzi hayo toka mwanzo (Richmond na sasa DOWANS). Mkataba uliorithishwa kwa DOWANS, ni batili na umevunjwa. Leo hauwezi kuwa halali bila kuusafisha.
3. Sheria za manunuzi ya umma zifuatwe ili kukidhi matakwa ya sheria.
4. Na mengine mengi aliyosema
Kwa maoni yangu, suala la manunuzi ya mitambo ya DOWANS litafufua tena scandal kubwa sana ambayo ilishaanza kufifia. Scandal hiyo haina manufaa yote zaidi ya kupoteza muda tu, na labda hatua za kisheria kuchukuliwa baadae kwa watakaohusika (hata kama itakuwa ni baada ya miaka 10).
Nadhani Zitto amejiingiza kwenye mtego mbaya wa kisiasa. Mtego ambao waliomwingiza ndio wanaofahamu madhara yake. Naamini hivyo kwa kuwa yeye ndie aliewaumiza kwenye scandals nyingi ikiwemo hii ya Richmond, Buzwagi n.k. Hivyo inawezekana wanataka aonje maumivu kidogo kabla uchaguzi haujafika, na hatimae apotee kisiasa. Kama mawazo yangu si sahihi, basi serikali ndio itakayokuwa inaingizwa mkenge na Zitto. Vyovyote iwavyo, kuna mmoja ataumia sana tu.
Naamini mtego anaoingia Mheshimiwa Zitto, si tu utamgharimu yeye binafsi kama mwanasiasa, bali pia chama chake ambacho hakionekani kuweka msimamo wake kuhusiana na suala hili.