Dowans: Another Richmond in making?

Dowans: Another Richmond in making?

TUZINGATIE: Rostam anamiliki 35% ya Vodacom, Dk. Rashid alikuwa Mkurugenzi wa Vodacom, Ngeleja alikuwa mtumishi wa Vodacom.

Note: Wakati mitambo ya Richmond inawasili pale uwanja wa ndege wa Dar, Salva kupitia kampuni yake ya G&S alikuwa ndiye PRO wa Richmond


.....A CIA/KGB Spy story couldnt get more Intriguing than this. Poor Tanzania.....!
 
Soma Cheche la Mzee Mwanakijiji

Huyo nae keshapoteza makali, hana kitu, kuanzia alivyoanza na kuleta uongo, kafuatia kushabikia kununua mtambo wa Dowans, halafu leo leo ahamasishe tukatae kununua mtambo huo!

Opportunists, anaangalia maslahi au fulani kasema nini. Kwa vile kamati ya Zitto ilisema mtambo ununuliwe, basi akaja na kistory eti mtambo ununuliwe kwa vile mwezi wa nne kutakuwa na uhaba wa umeme!

Zitto, Mwanakijiji denounced!
 
TUZINGATIE: Rostam anamiliki 35% ya Vodacom, Dk. Rashid alikuwa Mkurugenzi wa Vodacom, Ngeleja alikuwa mtumishi wa Vodacom.

Note: Wakati mitambo ya Richmond inawasili pale uwanja wa ndege wa Dar, Salva kupitia kampuni yake ya G&S alikuwa ndiye PRO wa Richmond


.....A CIA/KGB Spy story couldnt get more Intriguing than this. Poor Tanzania.....!
=========

Kuna habari za karibuni kuwa Rostam ameuza hisa zake zote za Vodacom na anahamishia biashara zake nyingi Kenya. Kuna watu makini walio karibu na Jengo Kuu la Magogoni, waliomwendea na kumweleza "with all due respects, aondoke vinginevyo he is bringing this presidency down, na inaweza kum-cost akifanya hivyo". Habari zinaeleza alizingatia ushauri huo and he is working on it.

Kama hii ni kweli, maybe, ndiyo kasi hii ya kuuza mtambo.
Kama hii ni kweli, maybe, ndicho kigugumizi cha JK kumgusa
Kama hii ni kweli, ndiyo sababu ya Kagoda kutoguswa.

Wana jamvi nisiwaondoe kwenye hoja ya msingi.
 
Huyu jamaa sasa, ameanza kuharibu. Katika wabunge niliokuwa nikiwaheshimu na yeye yumo na ana max nyingi saana. Kwanza kitendo cha kutwambia wanchuku wataalam kutoka nje kuhakiki,kinatudharaulisha watanzania.Nasema hili kwa sababu c kweli kwamba hakuna watanzania waliosoma wenye ujuzi hata wa kumzidi huyo waliyemtumia kukagua hiyo mitambo. Jamani wizi serikalini muache,wananchi wakawaida tunaumia pasipo kosa,kwani hata garama za umeme zikipanda mwananchi wa kawaida ndo anayeumia na nyie viongozi mkiwa hamana wasiwasi wa umeme kwani hata mgao hauwagusi kabisa. Hivi haiwezekani tukapata mitambo mingine mpaka ya dowans? Mbona serikali ilileta mitambo ya aggreko? Acheni kutudanganya,hapa kuna watu wanataka cha juu kupitia mpango huu.Na Mheshimiwa zitto kama yupo hapo kakosea saaana tena saana. Kwa kweli umeondoa imani ya watanzania ambao ni wanachama wa chadema na wale ambao walikuwa wana mpango wa kujiunga pia. Hapa hamna vyama vingi tanzania.
A.k.a Kuwa mwangalifu.
 
Uwe unaunga au huungi mkono msimamo huu mpya wa Rais kuhusu ufuataji sheria ya manunuzi, walichoripoti Guardian hapo juu kwamba Rais amekisema sio kilichomo kwenye taarifa ya Ikulu.

Mara nyingi tunaumiza vichwa kutatua vitendawili vya nini kinaendelea ndani ya serikali kwa sababu magazeti hayaripoti mambo kwa usahihi. Hatuna waandishi. Waziri Ngereja, kwa mfano, alilisharipotiwa mpaka kupigwa picha akisema kwamba serikali imeghaili kununua mitambo ya Dowans baada ya wao, Wizara, kuona busara ya mapendekezo ya Tume ya Kudumu ya madini ya Bunge ikipinga jambo hilo. Ghafla bin vuu sakata limeibuka upya, sasa hakuna anaejua je, ni kweli serikali ilitangaza imeghaili au tulipotoshwa. Mwandishi mmoja jana kamuhoji Ngereja kwenye redio za mtandao wa inteneti kwa dakika 30 na ushee bila ya jambo hilo kujibiwa wala kuulizwa. Moja ya laana inayokwamisha mambo nchini ni kukosa waandishi, hivyo hatujui kinachoendelea. Huwezi kuendelea kama hujui kinachoendelea.
leave the guy alone......mwanakijiji kajitahidi sana kw hii ishu....weka tofauti pembeni mkuu.....suala la waandishi hata mie wananiudhi sometimes......lakini mkuu una maoni gani kwa hili?
 
Zitto toka juzi tulikuwa tunakupa heads hapo mambo yalivyo sababu wengi humu ndani wana access na habari nyingi za huko juu, ungepreempt hili suala toka sunday/monday ili uonekane uko upande wa wananchi baada ya makosa uliyofanya.

Lakini wewe ni mbishi na umetushangaza sana, tulikueleza kabisa price utakayopay kwenye hili lakini wapi.

Ok tusubiri tusikie hayo mahojiano uko ITV tuone utaruka vipi hiki kitanzi.

All the best Mh. Zitto.
 
leave the guy alone......mwanakijiji kajitahidi sana kw hii ishu....weka tofauti pembeni mkuu.....suala la waandishi hata mie wananiudhi sometimes......lakini mkuu una maoni gani kwa hili?

Umeongea pointi tupu! Watu wako fixated sana na Mwanakijiji...I wonder why? He must be doing something right....kwa sababu zaidi ya kusema yuko hivi au yuko vile, hakuna anayefanya zaidi ya ayafanyayo Mwanakijiji. Hakuna mwenye kijarida kinachotoa competition kwa Mwanakijiji, hakuna athubutuye kuwatufa wahusika wa mambo mbalimbali na kuwahoji, hakuna mwenye redio yake anayehoji watu maswali ambayo supposedly Mwanakijiji haulizi....waliopo ni wale wasubirio Mwanakijii afanye kitu ndio na wao wanajitokeza na kuanza kumkosoa na kumlaani. Hawana nyodo za kufanya anayoyafanya au hata kumzidi kwani wangekuwa nazo wala wasingefikiria mara mbili wangefanya two times better.....
 
Hebu niwakumbushe kidogo.

Jakaya Mrisho Kikwete aliteuliwa kuwa Waziri wa Maji, Nishati na Madini mwaka 1990 na Raisi wa wakati huo, Ali Hassan Mwinyi. Mheshimiwa Kikwete alishiriki moja kwa moja katika kusaini mikataba mibovu ya madini na makampuni ya madini ya kimataifa ambayo kwayo taifa lilipoteza utajiri mkubwa na hivyo Serikali kunyimwa uwezo wa kifedha wa kuhudumia wananchi.

Mwishoni mwa mwaka 1993 aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu, Gilman Rutihinda, alifariki kwa ugonjwa katika mazingira ya kutatanisha. Mwaka 1994 Jakaya Mrisho Kikwete alihamishiwa Wizara ya Fedha na Dr. Idris Rashidi kuteuliwa Gavana wa Benki Kuu. Mwaka huo, 1994 ndiyo IPTL ilizaliwa kama "joint venture" kati ya Mechmar Corporation of Malaysia (70%) and VIP Engineering and Marketing Limited (30%).

Kama siyo kwa shinikizo la Hayati Mwalimu Nyerere, Jakaya Mrisho Kikwete angeutwaa Uraisi mwaka 1995. Kwamba hivi sasa Jakaya Mrisho KIkwete ni Raisi na Dr. Idris Rashidi ni Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, hakuwezi kushangaza hata kidogo. Tukishanunua mitambo chakavu ya Dowans, kitu gani kitatuzuia kununua mitambo chakavu ya IPTL ? "Sabotage" kidogo tu kwenye mabwawa itazaa dili nyingine ?
 
Hebu niwakumbushe kidogo.

Jakaya Mrisho Kikwete aliteuliwa kuwa Waziri wa Maji, Nishati na Madini mwaka 1990 na Raisi wa wakati huo, Ali Hassan Mwinyi. Mheshimiwa Kikwete alishiriki moja kwa moja katika kusaini mikataba mibovu ya madini na makampuni ya madini ya kimataifa ambayo kwayo taifa lilipoteza utajiri mkubwa na hivyo Serikali kunyimwa uwezo wa kifedha wa kuhudumia wananchi.

Mwishoni mwa mwaka 1993 aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu, Gilman Rutihinda, alifariki kwa ugonjwa katika mazingira ya kutatanisha. Mwaka 1994 Jakaya Mrisho Kikwete alihamishiwa Wizara ya Fedha na Dr. Idris Rashidi kuteuliwa Gavana wa Benki Kuu. Mwaka huo, 1994 ndiyo IPTL ilizaliwa kama "joint venture" kati ya Mechmar Corporation of Malaysia (70%) and VIP Engineering and Marketing Limited (30%).

Kama siyo kwa shinikizo la Hayati Mwalimu Nyerere, Jakaya Mrisho Kikwete angeutwaa Uraisi mwaka 1995. Kwamba hivi sasa Jakaya Mrisho KIkwete ni Raisi na Dr. Idris Rashidi ni Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, hakuwezi kushangaza hata kidogo. Tukishanunua mitambo chakavu ya Dowans, kitu gani kitatuzuia kununua mitambo chakavu ya IPTL ? "Sabotage" kidogo tu kwenye mabwawa itazaa dili nyingine ?
=====

Dohhh, history is indispensable! Hii si ajali ni mpango wa "mungu".
 
In the final analysis we should have seen this coming. When the Richmond saga hit the fan the President told us that not a single Tanzanian cent has gone to the fake company. Eventually we were told that the turbines had arrived in the country. Then when Richmond was rejected we were told they had sold their deal to Dowans. So Richmond did not leave Tanzania empty handed. And how was Dowans going to recoup its money? We should have seen it coming!
 
Hebu niwakumbushe kidogo.

Jakaya Mrisho Kikwete aliteuliwa kuwa Waziri wa Maji, Nishati na Madini mwaka 1990 na Raisi wa wakati huo, Ali Hassan Mwinyi. Mheshimiwa Kikwete alishiriki moja kwa moja katika kusaini mikataba mibovu ya madini na makampuni ya madini ya kimataifa ambayo kwayo taifa lilipoteza utajiri mkubwa na hivyo Serikali kunyimwa uwezo wa kifedha wa kuhudumia wananchi.

Mwishoni mwa mwaka 1993 aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu, Gilman Rutihinda, alifariki kwa ugonjwa katika mazingira ya kutatanisha. Mwaka 1994 Jakaya Mrisho Kikwete alihamishiwa Wizara ya Fedha na Dr. Idris Rashidi kuteuliwa Gavana wa Benki Kuu. Mwaka huo, 1994 ndiyo IPTL ilizaliwa kama "joint venture" kati ya Mechmar Corporation of Malaysia (70%) and VIP Engineering and Marketing Limited (30%).

Kama siyo kwa shinikizo la Hayati Mwalimu Nyerere, Jakaya Mrisho Kikwete angeutwaa Uraisi mwaka 1995. Kwamba hivi sasa Jakaya Mrisho KIkwete ni Raisi na Dr. Idris Rashidi ni Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, hakuwezi kushangaza hata kidogo. Tukishanunua mitambo chakavu ya Dowans, kitu gani kitatuzuia kununua mitambo chakavu ya IPTL ? "Sabotage" kidogo tu kwenye mabwawa itazaa dili nyingine ?

Mkuu umesahau na Caspian imeanzishwa lini? i mean Construction or mining division na sasa nasikia kuna RHINO
 
Namsikia Slaa hapa anajichanganya tu. anaingia zitto sasa. Anasema kuwa alifanya kama mwkti wa mashirika ya uma. Walipiitia taarifa za khs pesa. Yale yale ya 84%
 
kuwa na uwekezaji for 10 yrs alishaandika huku nyuma i don have to repeat. aahaaa waliwatuma tanesco walete jinsi ya kujinasua na matatizo no wakaleta solution ya dowans
 
wao kama kamati wanailinda tanesco na walikuwa wamewaagiza wakutane kamati zote
 
bla bla za socket na transformer. aliongea kama mbunge, mwykt wa kamati ila nataka mitambo tu hana haja na mmiliki
 
anasema tunawadai mana serikali ilitoa advance, serikali inadai dowans bil 8, na waliwaaguiza kuwa pesa hio ikatwe
 
kamati yake iliagiza sheria zote zifuatwe but tanesco walipendekeza kuwa sheria ziangaliwe.
 
anaulizwa dharura hii ni ya leo tu? anajibu kuwa kulikuwa na umeme wa ziada akina richmond na sasa kuna upungufu wa mw 150 na matumizi yameongezeka. anasikitika watu wengine hawataki mjadala. kazi ya kamati ni kuoversight, anasingizia kuwa kamati ya mwakiembe hawakusikiliza tanesco na tanesco watasingizia wanasiasa pale nchi ikiwa giza.
 
anasema kuwa waliagiza kuwa tenda itangazwe na sheria zifuatwe, anaelezea kuwa mwanza leo kuna mgawo pamoja na arusha. ni kweli? anazungumzia umeme wa upepo wa singida, kiwira na mega 60 za mwanza.
 
anasema kuwa serikali kuwa wamepoteza bil 58 kwa kusamehe kodi ya mafuta kwa kutouza umeme kwa migodi. je migodi yenye umeme inalipa sh ngapi kwenye hili? Mhe Zito tusaidie. ngoja nikale mana ameingia Mwakiembe na kwa kuanza tu anasita sana kuongea kwa kuwa hajakaa na wenzaki. ila anachangia kwa kuwa anahisi hii ni operation sangara. kwanza anasema kuwa wamekutana na tanesco tarehe 14/12/2008 siku ya jumapili. HILI ZITO NILAKWAKO....
 
Back
Top Bottom