Dowans: Another Richmond in making?

Dowans: Another Richmond in making?

Nilijua toka mwanzo kuwa hii issue itatumika Kisiasa...
Ni mtego ulowekwa maji ya ufukweni.. kwetu tunaita Migonzo...samaki akiingia ndani hawezi toka!
 
Kama huna viatu na akatokea jamaa akatembea na mkeo na ukang'amua. Kesho yake akaja kukuuzia viatu utanunua? Na viatu hivyo vimetumika na ni bei ya kurusha!!!
 
Ukiwa mwanasiasa na hasa mwanasiasa unayewabana wengine, chunga sana. Kamba inakufuata, ukikanyaga tu, wanavuta tayari uko chini. It is SAD Zitto kunasa kirahisi hivi, ... tena kwenye DOWANS!!! uuups.

Ataacha kugombea Ubunge, yes Keshapata alichokuwa anatafuta. Ila siasa forget about it kwani hilo Joho la DOWANS hawezi kulivua tena.
 
Kwamba unaweza kununua kitu bila kujali unanunua kwa nani? .... provided it works. Hizi ni statement za mitaani kabisa si mtaalam mwenye mashule kibao. Kwani unanunua Colgate? Hiyo mitambo ukiinunua ikafanya kazi siku mbili siku ya tatu ikafa, ukaambiwa kuirudishia uhai inatakiwa ununue kifaa chenye gharama nusu ya mtambo utaenda kwa nani?
 
"An honest politician is one who, when he is bought, will stay bought" - Anonimous
 
Kwa muda nimekuwa msomaji wa mjadala huu,

Naona kuna haja nami kujaribu kuweka mawazo ya kwanagu kwani kama mwana JF nina kila sababu ya kuchangia.

Itakumbukwa kuwa mwaka 2006 taifa liliingia mikataba mikubwa ya kukodisha mitambo kwa ajili ya kuzalisha umeme wa dharura kutokana na matatizo ya ukame ambayo inasemekana ulikumba taifa.

Mikataba ya kukodisha mitambo hiyo na gaharama zake ilikuwa kama ifuatavyo,

1.Mkataba na Richmond ambao walikuwa na mitambo ya kuzalisha 100MW ambayo inatumia gasi na Taifa tuliwalipa Dola milioni 88,700,000.

2.Mkataba na Aggreko ambao walikuwa na mitambo ya kuzalisha 40MW ,ambao tuliwalipa Dola milioni 61,000,000.

3.Mkataba na Alston Power Rentals ambao walikuwa na mitambo ya kuzalisha 40MW iliyokuwa inatumia diseli ,tuliwalipa Dola milioni 21,000,000.

4.Mkataba na Wartisila ambao walikuwa na uwezo wa kuzalisha 100MW ,tuliwalipa Euro milioni 57,550,000 .

Mikataba yote hii ilikuwa ni kwa ajili ya kuweza kupata mitambo ya kukodisha na sio kununua mitambo.

Ilipofika mwaka 2008 tulifuta mikataba hiyo na wakati tayari tulishaingia kwenye gharama kubwa kiasi hicho , na kiasi cha fedha ambacho nimekitaja hapo ni kile ambacho kulikuwa kwenye mikataba , sasa walilipwa kiasi gani sijui.

Suala la kununua mitambo , kwa sasa pamoja na ukweli kuwa limechukua sura tofauti na kuwa la kisiasa na kushambuliana zaidi , ila kuna ukweli ambao haupingiki nao ni kuwa ni lazima sasa tuwekeze kununua mitambo ya kuzalisha umeme na sio kusubiri kisha tuje kuanza kukodisha mitambo ambayo inatupotezea mabilioni ya pesa kiasi hicho kama nilivyoonyesha hapo juu kuwa 2006 tulipoteza kiasi gani cha pesa.

Nafikiri mjadala uwe tununue mitambo ama tusubiri mpaka janga likitufika basi tuanze kutafuta mitambo ya kukodisha kama tulivyozoea.

Kamati ya Nishati na Madini inapaswa kutuambia kuwa tunapaswa kununua mitambo ama tunapaswa kusubiri yatufike ndipo tuanze kukodisha?

Mwaka 2006 wakati tunaenda kukodisha mitambo hiyo uchumi wa taifa uliporomoka kwa asilimia 2 sasa je?ni kipi cha muhimu kwa sasa?

Nafikiri kuwa ni muhimu sheria za nchi zikafuatwa na kuzingatiwa katika maamuzi yeyote yale ambayo tunataka kufanya ama kununua au kukodisha .

Mjadala mwema .
 
Siku za Zitto kisiasa zinahesabika.
Yaani amesahau nini ni chimbuko la DOWANS!Leo hii anaipigia chapuo.
Zitto! Zitto! Angalia usije ukaingia kaburini alafu ukarudi CCM kimya kimya... Ukirudi CCM hata ubalozi wa nyumba kumi huwepi elewa hilo. Hii ishu ya DOWANS ni wizi mtupu kuna watu mnawasafisha bila nyie kujijua.
 
Kama walishachukua teni pasenti zao kwa ajili ya uchaguzi wa 2005 sasa chama twawala na watu wake watafute means zingine za kulipa wezi wa Richmond na Dowans. Hakitoki kitu hapa bwana.

Slaa, Mwakyembe, Sitta na wengine wenye uchungu na nchi hebu tumeni watu nje au pigeni simu kuulizia tutapata mitambo mingapi ya umeme toka China au Korea na au Brazili na nchi nyingine kama hizo kwa mtambo mmoja mbovu na uliochakaa wa Dowans.

Hii mijitu tunayoiita viongozi wetu inanishangaza sana. Midume na mijike mizima hamna aibu kuunda chombo cha kitaalamu cha kuagiza na kununua vitu kisha mnakisaidilaini na kuanza biashara zenu rejareja.

Hivi nyie wote kweli mnataka mkumbukwe hapa chini kwa lipi jema kwa Watanzania. WIIIZI MTUUUPU. Kwendeni zenu.

Nawaonea wivu Bangladeshi, Guinea Bissau na Guinea Conakry, mama yangu viiiile kama msipotaka kubadilika!
 
Wana JF kwanza niwapongeze kwa kazi nzuri ya utaifa mnayoifanya! masikitiko yangu ni kwamba viongozi wetu hususani kada hii ya vijana wanakosa uzalendo na kugeuka kuwa vibaraka wa mafisadi! udhaifu mkubwa wa viongozi wetu ni kutojiamini katika kufanya maamuzi ya maana kwa manufaa ya umma.

Wana JF suala la Richmond na dada yake DOWANS kuwa wamiliki wake ni RA na EL halina ubishi. Swali je, kwanini waziri wa madini na nishati anang'ang'aniza ununuzi wa mitambo hiyo wakati bodi aliyoiteua imeshauri tofauti? Ngereja anataka kulipa fadhila kwa mfadhili wake aliyemuingiza kwenye uwanja wa siasa RA. Kabla ya kuingia kwenye ulingo huu wa siasa mh ngereja alikuwa mwajiliwa wa kampuni ya fisadi RA kama mwanasheria.

Wakati uchaguzi unakaribia aliandaa vijana kadhaa kugombea ubunge akiwemo Ngereja, Bashe wa UVCCM, Nchimbi na wengine wengi. Bashe aliangushwa na mjumbe wa kamati ya mwakyembe Mhe. Selerii wa Nzega ambaye pia mara kadhaa amekuwa akitishiwa maisha yake na kundi hili la mafisadi.

Kwa kifupi kundi hili la mafisadi linao mtandao ndani ya wabunge ambao wanaonekana kuzidiwa nguvu na wabunge waadilifu. Kwa mfano Mhe Peter Selukamba alidandia hii meli ya mafisadi bila kujua! Anataka mambo yanayotokea kwao burundi yaje Tz. Huyu ni mhutu ambaye wazazi wake (warundi) waliamia Tanzaia akiwa mtoto mdogo.

Mwisho ni masikitiko yangu kwa jinsi mh Zitto alivyoshabikia jambo hili hadi kuishiwa pumzi! Kumbe njaa kitu kibaya sana. Jambo hili ni baya na endapo mitambo ya mafisadi haya itanunuliwa itakuwa ni ushindi kwa mafisadi na aibu kubwa kwa serikali ya JK!
 
Tunamuona Mugabe chizi lakini viongozi ndio chizi zaidi. Hivi una habari kwamba jamaa huyu baada ya kuona kawaibia Wazim. mpaka kawamaliza akafanza geresha toto. Ipi? Eti kuisaidia Congo Kinshasa kuweka amani kusini kwenye madini kibao. Hivi juzi mke wa swahiba wake mkubwa Mugabe mama Mujuru kabainika akiuza laivu goldi tani sio kilo zaidi ya sita Uswizi.

Sasa Sisiemu jamani si mnajua sisi tulivyochooka kabisa. Tupeni nafasi tupumue. Waambieni maburushi na wahindi wenu mnawatumia kama mawakala wa kuwatafutia vyanzo haramu vya feza waende Kongo, Chad, Central Africa wakawatafutie mtaji wa uchaguzi mkuu 2010!
 
Kila binadamu ananunulika (kwa bei yake). RA is desparate on this. Pengine anataka akomboe walau dola milioni 4 tu, kiasi kilichobaki ameahidi wadau wanaopigia debe (mitambo inunuliwe) wagawane. Ndio maana watu wasiotegemewa wanatetea ununuzi huu.
 
Kwa muda nimekuwa msomaji wa mjadala huu,

Naona kuna haja nami kujaribu kuweka mawazo ya kwanagu kwani kama mwana JF nina kila sababu ya kuchangia.

Itakumbukwa kuwa mwaka 2006 taifa liliingia mikataba mikubwa ya kukodisha mitambo kwa ajili ya kuzalisha umeme wa dharura kutokana na matatizo ya ukame ambayo inasemekana ulikumba taifa.

Mikataba ya kukodisha mitambo hiyo na gaharama zake ilikuwa kama ifuatavyo,

1.Mkataba na Richmond ambao walikuwa na mitambo ya kuzalisha 100MW ambayo inatumia gasi na Taifa tuliwalipa Dola milioni 88,700,000.

2.Mkataba na Aggreko ambao walikuwa na mitambo ya kuzalisha 40MW ,ambao tuliwalipa Dola milioni 61,000,000.

3.Mkataba na Alston Power Rentals ambao walikuwa na mitambo ya kuzalisha 40MW iliyokuwa inatumia diseli ,tuliwalipa Dola milioni 21,000,000.

4.Mkataba na Wartisila ambao walikuwa na uwezo wa kuzalisha 100MW ,tuliwalipa Euro milioni 57,550,000 .

Mikataba yote hii ilikuwa ni kwa ajili ya kuweza kupata mitambo ya kukodisha na sio kununua mitambo.

Ilipofika mwaka 2008 tulifuta mikataba hiyo na wakati tayari tulishaingia kwenye gharama kubwa kiasi hicho , na kiasi cha fedha ambacho nimekitaja hapo ni kile ambacho kulikuwa kwenye mikataba , sasa walilipwa kiasi gani sijui.

Suala la kununua mitambo , kwa sasa pamoja na ukweli kuwa limechukua sura tofauti na kuwa la kisiasa na kushambuliana zaidi , ila kuna ukweli ambao haupingiki nao ni kuwa ni lazima sasa tuwekeze kununua mitambo ya kuzalisha umeme na sio kusubiri kisha tuje kuanza kukodisha mitambo ambayo inatupotezea mabilioni ya pesa kiasi hicho kama nilivyoonyesha hapo juu kuwa 2006 tulipoteza kiasi gani cha pesa.

Nafikiri mjadala uwe tununue mitambo ama tusubiri mpaka janga likitufika basi tuanze kutafuta mitambo ya kukodisha kama tulivyozoea.

Kamati ya Nishati na Madini inapaswa kutuambia kuwa tunapaswa kununua mitambo ama tunapaswa kusubiri yatufike ndipo tuanze kukodisha?

Mwaka 2006 wakati tunaenda kukodisha mitambo hiyo uchumi wa taifa uliporomoka kwa asilimia 2 sasa je?ni kipi cha muhimu kwa sasa?

Nafikiri kuwa ni muhimu sheria za nchi zikafuatwa na kuzingatiwa katika maamuzi yeyote yale ambayo tunataka kufanya ama kununua au kukodisha .

Mjadala mwema .

Well said MpakaKieleweke,

1. kwenye manunuzi kuna option ya kukodisha au kununua....one would ask why Tanzanians we opted all that money kukodisha.......there are so many things to be discussed kwenye hilo

2. ukiangalia gharama za kukodi ulizotuwekea ni karibu sawa na kununua brand new generators kutoka kwa manufacturers (sio middleman RDC or whoever)...kwanini hatukununua?.....only God knows

3. Zitto et all wanasema inabidi kununua ili pamoja na mengine ni kukwepa wimbi la capacity charges ambazo zimekuwa zikituumiza wananchi...why didn't we buy them in the first place.?........again only God knows

4. It is the fact kuwa hayo makampuni uliyoyaorodhesha hapo juu yalipata LC (wakati mwingine udhamini remember IPTL) kutoka serikalini ili ku-procure hiyo mitambo ili watukodishe.......i.e. tuna uwezo wa kujenga nyumba yetu sisi wenyewe......lakini tunampa/kopesha/dhamini mtu hela ya kujengea halafu anatupangisha.........VERY FUNNY.....ndio ukweli wenyewe

5.Mahitaji ya umeme wa nchi...its not something you wake up in the morning and realise you need something......nikimaanisha mahitaji ya nishati ya nchi yanajulikana in short, medium and longer terms....kwa nini leo hii tushtukizane kukodisha/kununua mitambo?....only God knows

6. hivi unaweza kutueleza uchumi wa nchi unaporomoka vipi kwa ufisadi unaoendela hapa nchini, kuanzia Utalii, Miundombinu, uvuvi, madini, kilimo.....etc ambayo sehemu kubwa hawategemei huo umeme wa kifisadi.

mpaka sasa mnafikiria kubadilisha sheria za manunuzi kwa kisingizio cha dharura.......ONLY IN TANZANIA

tuendelee kujadili
 
Umesikia mashitaka ya kesi ya Liyumba? Mojawapo ni kufanya maamuzi bila kuishirikisha Bodi ya BoT.

Kusema kwamba MD/CEO ndiyo mhusika mkuu hapo ni kutudanganya mchana kweupe. Yeye yuko responsible kwa Bodi na wao Bodi kazi yao ni kupokea mapendekezo/taarifa za maendeleo ya shirika/kampuni na then wanaweza kutoa ushauri, kugoma ama kukubali utekelezaji wa mependekezo yaliyotolewa na MD/CEO.

Keil & SMU tuko pamoja wakuu.........
 
Hivi mradi wa kuunganisha umeme wa Zambia kwenye gridi ya Taifa umefikia wapi?

...kule miradi mingi inakoishiaga.....

btw, kwa nini waunganishe umeme wa Zambia kwenye grid yetu? ina maana Wazambia wana umeme wa uhakika zaidi kuliko sisi?
 
Siku za Zitto kisiasa zinahesabika.
Yaani amesahau nini ni chimbuko la DOWANS!Leo hii anaipigia chapuo.
Zitto! Zitto! Angalia usije ukaingia kaburini alafu ukarudi CCM kimya kimya... Ukirudi CCM hata ubalozi wa nyumba kumi huwepi elewa hilo. Hii ishu ya DOWANS ni wizi mtupu kuna watu mnawasafisha bila nyie kujijua.

========

Wahenga wana msemo unaoenda hivi: "Kifo cha Mbwa huanza pale anapopoteza uwezo wa kunusa" au "Kifo cha Mbwa huanzia puani".
 
Ukiangalia mkataba wa Aggreko na Wartisila ambao wote walikuwa na uwezo wa kuzalisha MW40 ,tofauti ya malipo ni kubwa sana sana , kwani mmoja kalipwa 61 milioni USD na mwingine kalipwa 21milioni USD.

Kama mitambo ni ya kukodisha , iweje wanaouwezo sawa ila malipo yawe na tofauti ya dola milioni 40?

Kwa staili hii ya kukodisha kwanini TANESCO isife?
 
Back
Top Bottom