Dowans: Another Richmond in making?

Dowans: Another Richmond in making?

Mwanakijiji, nitadiscuss zaidi kwenye ile topic nyingine ya Dowans, lakini points zako ni nzuri lakini umeshindwa kuonyesha hasa Nguvu za kununua Dowans zinatoka wapi. Kumbuka serikali hata iseme vipi kuna sehemu iko accountable (Bungeni), sasa huko ndiko Zitto ametumiwa ili kutumaliza wananchi, kwa hiyo kwenye ili sakata mkombozi ni bunge, sasa tuangalie bunge tutalitumia vipi wakati baadhi ya nguvu tulizokuwa tunazitegemea awali kununuliwa/kuwablackmailed/au hata sijui niseme vipi.

Moelex, sikufanya hivyo kwa sababu hilo linahusiana na siasa za makundi, maslahi ya watu mbalimbali. Kupinga kwetu ununuzi wa mitambo hiyo haijalishi nani anasukumiza mradi huu. Ni wajibu wetu kuupinga kwa sababu it simply corrupt from the get go. Hata mradi huu ukisukumwa na Malaika Gabrieli bado tunatakiwa kuukataa!!
 
Mafisadi fooled us once before, shame on them. But if they fool us once again, the shame will be on us. If it backs like a dog......
Hii haina tofauti kabisa na ndege ya serikali ilivyopigiwa debe, kuuza nyumba za serikali tulivyoambiwa ni muhimu, na rada jinsi itakavyoongeza idadi ya ndege za watalii !!
 
Sasa jamani hapa lazima tuwe proactive. Suala la kununua mitambo Dowans litafanywa na serikali, lakini BUNGE ndio msimamizi wa serikali kwa hiyo issue iliyobaki ni kumake sure kuwa BUNGE liko behind wananchi kwenye hili. Sasa bunge tunajua kuna wabunge ovyo, lakini muhimu ni wale wabunge wetu wakombozi kina Mama Kilango, Mwakyembe, Seleli na wengine wawezeshwe kwenye ili kiutaalamu ili waweze kudefend nchi kitaalamu. Kamati ya PAC na Nishati na Madini ni lazima ziwe na wazalendo wanaotuwakilisha sisi wananchi 100% all the time.

Sasa kamati ya Nishati kwenye ili wako kwenye right track.
Bunge asilimia kubwa ya wabunge makini hasa kwenye ile ofisi kuu wako nasi.
Hii kamati ya PAC ndio issue iko, especially kwa huyu mwenyekiti.

Sasa naona mbinu zitumike ili either yafuatayo yafanyike::
1) Zitto ajiuzulu uenyekiti mwenyewe kwa manufaa ya wananchi
2)Mbinu za activism zitumike ili huyu mtu awe forced kujiuzulu

Uko tunakoenda tunahitaji PAC kusimamia mambo ya TPA (ili TICTS wabanwe), ATC(ili upumbavu wa zile Airbus ukomeshwe), TRL (Ili gharama zinazotukumba kusupport Rites Mama huko India kwa kukodi mitambo kwa bei kubwa iishe), sasa huyu Mwenyekiti ameanza kuonyesha kuwa yeye anajali misimamo yake, ambayo ni hatari sana kwetu sisi.

Zitto tulimtegemea sana lakini naona ameamua kwa matakwa yake kutuonyesha true colors zake na hiyo confidence yake against almost 90% ya wanaJF kwenye ili imeonyesha huyu mtu ni hatari sana uko mbeleni. Dr. Slaa naye kwenye ili alikuja na mapigo ya kumsupport mwenzake lakini akagundua mapema, lakini na yeye nimemtoa vile vile kwenye wabunge niliokuwa nawapa 100% support regardless.

Tusubiri spin watakazokuja nazo leo uko nyumbani, tuone labda nitaweza kufuta misimamo yangu hapo juu.
 
toleola29.jpg


tunaweza kukaa pembeni kunung'unika au kuamka na kuhamasika; tunaweza kuwa wachambuzi wa mambo wasiotaka kuchukua msimamo au tukachukua msimamo kuonesha uchambuzi wetu wa mambo. Tuna uchaguzi wa kukubali kluwa serikali ifanye ipendalo na sisi tubakie kulialia pembeni au kusimama na kunyosha mikono yetu kama maaskari wa usalama barabarani na kuiambia serikali "stop"!

Soma kijarida cha Cheche ili upate sababu za nyongeza kwanini ni suala la uzalendo, utaifa, utawala bora, na utawala wa sheria kuizuia Dowans kupata hata senti moja ya Watanzania.

Hadi hivi sasa hakuna mnunuzi mwingine yeyote ambaye yuko tayari kununua mitambo hiyo tangu tenda hiyo waitangaze karibu miezi minne iliyopita. Mnunuzi pekee ni Serikali. Serikali isiponunua Dowans watapata hasara kubwa kwani "kitawadodea".

Asante kwa wale wote ambao wamefanya kazi yao leo na matunda tumeanza kuyaona. Wale wengine ambao hawajatambua bado ni kwanini we have to stop this menace to our energy sector please read and distribute.

It is time to move from Criticism to Activism!!


Dowans must be stopped.

Hizi ni chuki binafsi au? Dowans imewakosa nini?
 
Moelex, sikufanya hivyo kwa sababu hilo linahusiana na siasa za makundi, maslahi ya watu mbalimbali. Kupinga kwetu ununuzi wa mitambo hiyo haijalishi nani anasukumiza mradi huu. Ni wajibu wetu kuupinga kwa sababu it simply corrupt from the get go. Hata mradi huu ukisukumwa na Malaika Gabrieli bado tunatakiwa kuukataa!!

Haya ni chuki binafsi, ndio maana wa Tanzania hatuendelei, ikiwa watu wenyewe fikra ni kama zako na kuna wanae kukubalia hizi hoja zako zingine, hatari kubwa.
 
Salva amekanusha taarifa ya gazeti la MWananchi, amesema Rais hakuzungumzia hata chembe kuhusu Dowans.

Dharura!!!!!! mwaka 2001, 2002, 2003, 2004 (realocation na bajeti), mwaka 2005 (Uchaguzi) mwaka 2006 (Richmond), mwaka 2007 (???) Mwaka 2008 (????), mwaka 2009 (Dharura, Dowans haraka, jamani giza!!!!!).

Huhitaji akili nyingi. Soma taarifa za HALI YA HEWA katika website ya TMA za kuanzia mwaka 2001... Soma taarifa za hali ya hewa za ICPAC zamani ikiitwa Drought Monitoring Center Nairobi (DMCN) utabaini kwamba ilifahamika miaka mingi kuwapo kwa ukame. Hiyo dharura inatoka wapi?

Mwaka 2004, bwawa la Mtera lilifungwa kwa ukame lakini hakukuwa na mgawo, kutokana na realocation ya burget ya serikali iliyotoa fedha kwa Tanesco (Kuzalisha umeme) na SGR (Kununua chakula) jamani, hebu tusitumwe tukapigiwa wimbo tukaimba kama kasuku bila kujua wimbo huo ni wa matusi matupu kwa watanzania wa sasa ambao Mwakyembe alisema SI MABWEGE TENA.
 
But Sir,wat about that 'tununue mitambo ya Dowans yaishe&free Gire' or I didnt get the tone right!?

Huyo si mpayukaji tu, mara akutie huku akutowe huku, anacheza na maneno, ndio kazi yake, na ogopa mtu anepindisha pindisha maneno.
 
Zitto kajidhalilisha na kwa kweli CHADEMA wasipoangalia huyu jamaa anawamaliza kwani ankoelekea si kuzuri.Sijui kama Slaa naye yupo kwenye uchuro huu kama yupo tumekwisha.Tusubiri CCM watupatie wapinzani wa kweli au wawaondoe CCM mtandao,maslahi na mpasuko na kutuachia CCM yetu ya tangu enzi za Nyerere.
 
Jamani,

Nataka kutathmini niwe upande gani kuhusu ununuzi wa mitambo... bila influence ya mitambo ni ya nani?

Naomba kuambiwa faida na hasara za kununua au kutonunua mitambo hiyo... ninachomba kwenye uchambuzi huo... muondoe issue ya umiliki wa mitambo.

Soma Cheche la Mzee Mwanakijiji tleo la wiki hii
 
duh.. nilisema "mwachieni Gire, nunueni mitambo ya Dowans". NIlisema hivyo kwa sababu haya mazungumzo tunayoendelea nayo hayana maana uamuzi ulishachukuliwa kununua mitambo ya Dowans..

Ndiyo maana nikasema kwanini tuendelee kuzungushana, si wanunue tu wamuachie Gire ili hili la Richmond na Dowans lifikie mwisho wake kuliko huu mchezo wa kidali po tunaoucheza?

Hizi ni cheche za chuki binafsi, hebu niulize hawa Dowans wamekukosa nini? na hiyo mitambo imekukosa nini? au ulinyimwa mgao?
 
Moelex, sikufanya hivyo kwa sababu hilo linahusiana na siasa za makundi, maslahi ya watu mbalimbali. Kupinga kwetu ununuzi wa mitambo hiyo haijalishi nani anasukumiza mradi huu. Ni wajibu wetu kuupinga kwa sababu it simply corrupt from the get go. Hata mradi huu ukisukumwa na Malaika Gabrieli bado tunatakiwa kuukataa!!

Sasa mkuu sehemu ya kupinga kisheria si Bungeni?? Sasa utapinga vipi kisheria wakati wenyeviti wa baadhi ya kamati muhimu wako bought?? Anyways don't worry tunashughulikia ili suala kwa mbinu nyingi na as long as wote tunataka end result moja its all good.
 
Sasa mkuu sehemu ya kupinga kisheria si Bungeni?? Sasa utapinga vipi kisheria wakati wenyeviti wa baadhi ya kamati muhimu wako bought?? Anyways don't worry tunashughulikia ili suala kwa mbinu nyingi na as long as wote tunataka end result moja its all good.

Kupinga kisheria si bungeni tu, hata mahakamani unaweza kwenda kama utayaweza.
 
Wasibabaishe watu wote hao lao moja,wanajaribu kuzuga zuga ili wasidaiwe ,madai ambayo ni hatari kwao.

Utawala wa Sultani CCM upo kwenye kona ,kila siku nasema na nitaendelea kusema kuwa kunahitajika mabadiliko ya KATIBA ,Tume ya Uchaguzi ,mfumo wa Mahakama na kupunguzwa kwa nguvu za Raisi na viongozi wawepo chini ya sheria.

Haya malumbano ni yao wao kwa ukweli kabisa hayawahusu wengine ,wao ndio wenye serikali ,wao ndio wenye usukani, wengine ambao wanaingia kwenye kundi ni wale ambao wanampigia na kumshangilia mwendawazimu ,hivyo kila ukizidi kushangilia ndipo vituko vinapozidi.

Wale wote ambao hawaupendi mwenendo wa Sultani CCM ni lazima waungane ili kuiletea Jamhuri ya Shirikisho ya Tanzania mabadiliko makubwa ,kwa muda huu tulionao CCM waachwe kama walivyo wakiuza ,wakinunua ,wakiwatafuta majambazi kwa kupiga kura ,waachwe wafanye watakavyo kwani ,zote hizo ni dalili za kukata roho na kumalizika Utawala wa CCM Empire hapa Tanzania .

Mbio hizi za kufukuzana na kudhaniana wao kwa wao zisituvurugie lengo ni lazima muwasome kwani wananunua wakati na kupoteza nguvu za upinzani.

Fikiria tokea wakati tulipoanza kuwanadi kuwa ni wezi hadi leo ,ingelikuwa vifijo na mayoe na makelele ni kudai Katiba huru na tume huru leo hii tungelikuwa tumeshafikishana nao mbali.

Haya ambayo tunakwenda nayo kwa kweli hayatusaidii chochote na yanapelekwa kwa mwendo wa kinyonga au yanakwenda mwendo wa gegereka au kaa ,ndio maana yake mara yanapelekwa huku mara yanapelekwa huku.

Tunaona viongozi wanapoteza nguvu na kupoteza umaarufu wao kwa kupigizana na kubishana na wezi au mafisadi wa Sultani CCM. Jambo ambalo lilitakiwa sio kubishana nao bali ni kuelekea kwa wananchi na kuwaeleimisha mpaka wakafahamu maana kuzidi kuwafahamisha kila siku mwisho wake wangeelewa tu anachofanya Sultani CCM ,jamani kamba inakata jiwe halikadhalika maji yanapasua milima na majabali.

Kama tutakaa na kubishana na Sultani CCM juu ya unyama anaoutenda na anao ubariki ,siku zote tutakuwa kwenye malumbano ambayo tija yake ni dhaifu sana ,lazima nguvu hizi zielekezwe kwa wananchi na kuwaelewesha umuhimu wa Kuifanyia marekebisho Katiba ili iendane na mfumo wa vyama vingi jambo ambalo litakuwa na manufaa sana sana.
 
Salva amekanusha taarifa ya gazeti la MWananchi, amesema Rais hakuzungumzia hata chembe kuhusu Dowans.

Kama hakuongelea swala la Dowans, je, kile kipengele (e) cha Press Release aliyoitoa kwa waandishi wa habari kilikuwa kinahusu nini? Hivi hawa watu kwanini bado wanatuona sisi ni mabwege na kwamba hatuwezi kujumlisha 1 na 1 na kupata jibu sahihi?
 
Jamani,

Nataka kutathmini niwe upande gani kuhusu ununuzi wa mitambo... bila influence ya mitambo ni ya nani?

Naomba kuambiwa faida na hasara za kununua au kutonunua mitambo hiyo... ninachomba kwenye uchambuzi huo... muondoe issue ya umiliki wa mitambo.

Ni hivi: Kabla hujaamua ununue mtambo upi na kwa nani

1. Tambua hitaji la kuongeza uzalishaji
2. Angalia njia mbalimbali za kushughulikia hitaji husika
3. Anza mchakato wa kupunguza na kubaki na njia moja muafaka zaidi
4. Tafuta watoa huduma katika njia uliyochagua ya kukidhi hitaji lako
5. Chagua mmoja wapo kwa kufuata taratibu zinazokubalika.

Jiulize katika swala hili bila kujani mitambo ni ya nami je utaratibu husika umefuatwa?
 
Jamani,

Nataka kutathmini niwe upande gani kuhusu ununuzi wa mitambo... bila influence ya mitambo ni ya nani?

Naomba kuambiwa faida na hasara za kununua au kutonunua mitambo hiyo... ninachomba kwenye uchambuzi huo... muondoe issue ya umiliki wa mitambo.

Soma Cheche la Mzee Mwanakijiji
 
Zitto, Unakuwa kama Masha? Kumuandikia Barua Rais na Waziri Mkuu barua ya maoni?

Zitto hawa wanaokupinga wewe hujawajuwa kwa nini tu mpaka sasa? wanajifanya hawaelewi chochote unachowaeleza, bado hujajuwa sababu tu?

Wana macho lakini hawaoni...

Labda you will get the hint, hata useme mpaka povu likutoke, hawatokuelewa kwani hawataki kukuelewa, wewe cha msingi ni kuachana nao na kufanya kile ambacho unajuwa hakitokunyima usingizi. Fanya unachoona hicho ndicho kina manufaa kwa uma unaoutuimikia, kwa haki na usawa na Mwenyeezi Mungu atakuwa na wewe.
 
TANESCO inataka kununua turbines zile kwa sababu ina upungufu wa umeme... capacity iko already chini.... anytime mtambo wowote ukiwa unahitilafu taifa linaingia kwenye mgao... is that what you want...

Kuweni wazalendo na nchi yenu... think big.

Kuagiza na kufunga mitambo mipya inachukua sio chini ya mwaka kama sikosei... sasa angalieni athari za kukosa umeme na athari za kununua mitambo.... ili akili zenu zifanye kazi kwanza ondoeni mawazo ya mtambo ni wa nani.

You can't think big when this daylight robbery is being carried on right before our eyes with people we have entrusted to lead us and the likes of you see there is no problem there.
 
Back
Top Bottom