Dowans: Another Richmond in making?

Dowans: Another Richmond in making?

Jamani,

Nataka kutathmini niwe upande gani kuhusu ununuzi wa mitambo... bila influence ya mitambo ni ya nani?

Naomba kuambiwa faida na hasara za kununua au kutonunua mitambo hiyo... ninachomba kwenye uchambuzi huo... muondoe issue ya umiliki wa mitambo.

Mkuu Kasheshe, nadhani unachotakiwa kufanya ni kuwa upande wa maslahi ya Taifa.

Kwa sasa kuna pande mbili. Moja ni wenye hoja ya kununua mitambo iliyofungwa na wengine kununua mipya. Kampuni inayotajwa si hoja kwakuwa hutaki kusikia majina ya wamiliki. Mimi kwa upande wangu nadhani hakuna haja ya kununua mitambo iliyofungwa (iliyotumika) kwa sababu zifuatazo;

1. Mitambo hiyo sio mipya
2. Mitambo hiyo ni ya bei ya juu kuliko mingine inayoweza kupatikana (hasa kama upya si hoja). Ipo ya hadi $20mil
3. Kauli ya Mhe. Waziri kuhusu running hours hairidhishi kulinganisha na iliyopo kwenye market (alizungumzia uwezekano wa ku-run kwa 10 years (approx 88,000 hours) kabla ya major maintenance, na baadae ku-run kwa 10 more years). Total 176,000 hours. Reference: Mahojiano na Mwanakijiji.
4. Mitambo inayozungumziwa haina uharaka wa kuinunua. Hivyo harakati za kupata mitambo mipya zinaweza kufanyika sasa.
5. Mitambo inayozungumziwa ilinunuliwa kwa third party (sio manufacturer) kwa hiyo haitakuwa na proper after sale support, best offer na guarantee ya maana
6. Mitambo inayozungumziwa ina migogoro mahakamani ambayo bado inaendelea.
7. Na mengine niliyoyasahau hapa

Ili kuweza kutoa picha walau kidogo, naomba nionyeshe aina nyingine ya mitambo (sina uhakika iliyopo TANESCO sasa ni ya aina gani, nani kaitengeneza) ambayo ina capacity kubwa, running hours nyingi zaidi na inayoweza kuwa na msaada zaidi. Angalia quote hiyo hapo chini.

Advanced SGT6-5000F Development
presented at Power-Gen International 2008 - Orlando, Florida


The SGT6-5000F engine has demonstrated an exceptional operational record over a 15-year, 4.7+ million fleet hour history. Since its introduction in 1993, this F-Class gas turbine has undergone continuous development to improve performance, reliability and operational flexibility and to reduce emissions and life cycle costs. The result is a gas turbine with an excellent operational record and customer value. In 2008, Siemens Energy started production of the latest upgraded version of the SGT6-5000F. The capabilities of this newest offering include a dual-fuel gas turbine which can deliver 150MW of power to the grid within 10 minutes, Ultra Low NOx combustion system (9ppm) and hot gas path components designed for extended maintenance intervals. This paper describes the technological advances now available in the SGT6-5000F gas turbine which will further improve performance, reliability, operational flexibility and customer value.

For more info, you can also download a document regarding this engine from

http://www.powergeneration.siemens....B5B-9D1D1B07BD7B/0/PowerGen2008_SGT65000F.pdf
 
Nina wasiwasi na mheshimiwa amiri jeshi mkuu wa nchi yetu, nahisi kama kuna kijiusanii tunachezewa. Haiwezekani mambo makubwa kama hayo yanatokea bila kusikia sauti yake angalau ikikemea upuuzi huo.

Bila shaka utapeli huu ndo ulimweka madarakani.

Mpori.
 
Chama Cha Kweli ni Chama Cha wananchi,au CUF kama wengi wanavyopenda kukiita ,ni Chama ambacho hakijatetereka na kimeshavuka vigingi vingi,kimeitwa Cha Udini kimeogelea na shutuma hizo ,mpaka kikavuka kimeitwa Cha Wapemba kimeogelea na shutuma hizo na kimevuka na mambo mengi tu ambayo wafuasi wa Sultani CCM wakikurupuka huwa wanarudia yale yale mpaka wakumbushane kuwa hayo tayali tumeshawabambikizia na hatukufua dafu ndio utawaona wanatafuta jingine na hili lamwisho la kupandikiza pandikizi limepigwa dafrau.

Sasa wanaume wanakuja na mabadiliko ya Katiba hizi geresha za mafisadi zinawekwa mwiku au kiporo mpaka hapo Katiba na mahakama zake zitakapokaa sawa ,si ajabu wafuasi wa Sultani CCM wakasema turudi kwa wananchi kuwauliza au kutuambia nani anaedai katiba ,kama tunavyozidi kuwazoea na mambo ya ajabu ajabu ,yaani Sultani CCM anakuja na mambo mambo ya ajabu kabisa hakuna na mauza uza ya mtu anaekufa.
 
Nina wasiwasi na mheshimiwa amiri jeshi mkuu wa nchi yetu, nahisi kama kuna kijiusanii tunachezewa. Haiwezekani mambo makubwa kama hayo yanatokea bila kusikia sauti yake angalau ikikemea upuuzi huo.

Bila shaka utapeli huu ndo ulimweka madarakani.

Mpori.

Weka wazi, kama huna kaa kimya. Mtu kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Tanzania huwezi kumshutumu kwa ''usanii'' kwa hisia zako tu. Mambo makubwa yepi unayoyasema hapo? hebu weka wazi. nini akemee?
 
Zitto, hapa kuna watu hawakuelewi kabisa.
 
Huyo si mpayukaji tu, mara akutie huku akutowe huku, anacheza na maneno, ndio kazi yake, na ogopa mtu anepindisha pindisha maneno.
Lakini baada ya kunijibu nimemuelewa datz y nkaulza kuwa au sijaipata tone ya ule ujumbe.Ona wanavyomuacha Zitto ajikaange mwenyewe kwenye hili...Salva anakanusha,Ngeleja anasema co kitu cha haraka,Sitta anasema kuwa Dowans ni uwizi mtupu,Mwakyembe anasema kuwa ni ukiukaji wa sheria at its best...Ni Dr.Rashid tu ndo anasema kuwa ni whether kununua mitambo au kwenda gizani....
 
There's NO leadership in this country. Kila mtu anajisemea kivyake vyake tu🙁

CHIEF hilo tuliliona siku nyingi sana, na kulisemea siku nyingi sana lakini bado linaendelea. Sasa hivi ajabu hata Spika ameanza kujiona yeye ni serikali, na serikali soon itaanza kujiona kuwa yenyewe ni Bunge, ni vurugu tupu mafisadi wao wanaendelea kupeta tu.
 
Zitto, hapa kuna watu hawakuelewi kabisa.

Zito na Chadema yake kwisha khabari kabisa. Anatuletea mambo ya DOWNS??????????????? Eti kisa, Masrahi ya TAIFA. Wameshindwa kusoma alama za nyakati, basi wamejimaliza Wenyewe, Hapa mtaani kwetu kila mtu kichwa chini, haamini aliyoyasikia toka kwa hawa viongozi wa CHADEMA.

Dar ES Salaam: mumewapa nini hawa wasaliti wa upinzani.??????. CCM kawarushia chambo wakakimbilia, kwisha khabari.
Hakuna cha cha ZITO, SLAA wala Chadema tena, na Operation SANGARA ndio imeangamia kabisa. Nani saa hivi yuko tayari kupigwa na jua kuwasikiliza hawa jamaa.????? Wizi Mtupuu
 
Zito na Chadema yake kwisha khabari kabisa. Anatuletea mambo ya DOWNS??????????????? Eti kisa, Masrahi ya TAIFA. Wameshindwa kusoma alama za nyakati, basi wamejimaliza Wenyewe, Hapa mtaani kwetu kila mtu kichwa chini, haamini aliyoyasikia toka kwa hawa viongozi wa CHADEMA.

Dar ES Salaam: mumewapa nini hawa wasaliti wa upinzani.??????. CCM kawarushia chambo wakakimbilia, kwisha khabari.
Hakuna cha cha ZITO, SLAA wala Chadema tena, na Operation SANGARA ndio imeangamia kabisa. Nani saa hivi yuko tayari kupigwa na jua kuwasikiliza hawa jamaa.????? Wizi Mtupuu

System always works kwa Maslahi ya Taifa. Na nyinyi hamuelewi tu? Nilishasema humu mara nyingi, Slaa, Mbowe wote hao ni system.

Na nampongeza sana Zitto kwani kweli hafanyi kazi kichama na anapoona kuna maslahi ya Taifa ndipo anapong'ang'ania bila kujali itikadi za kichama. Hiyo ndio system nzuri na ya haki kabisa.
 
Zitto kajidhalilisha na kwa kweli CHADEMA wasipoangalia huyu jamaa anawamaliza kwani ankoelekea si kuzuri.Sijui kama Slaa naye yupo kwenye uchuro huu kama yupo tumekwisha.Tusubiri CCM watupatie wapinzani wa kweli au wawaondoe CCM mtandao,maslahi na mpasuko na kutuachia CCM yetu ya tangu enzi za Nyerere.
Mkuu,
Dr.Slaa alikuja hapa na kujaribu kuzimazima moto lakini alipoona kuwa moto unazidi alitoweka akidai kuwa kuna missing information!
a
 
Niliwahi kugusia katika thread nyingine kuhusu Dowans kwamba Zitto tayari amenasa kwenye asali ya mafisadi ambao sasa wanamtumia kuwapigia debe. Ripoti za uhakika zinasema kuwa Ijumaa ya tarehe 27/2/09 majira ya jioni alionekana katika maeneo ya ofisi za wachapishaji wa magazeti ya Habari Corporation ambayo sasa ynamilikwa na Rostam na kufanya mazungumzo ya faragha na Mhariri Mkuu aitwaye Muhungo, ambaye ni swahiba mkubwa wa Rostam tangu wakati wa kampeni ya JK mwaka 2005.

Mazungumzo hayo yalifanyika ndani ya ofisi ya Muhingo kwa takriban masaa 2 na baadaye nje karibu na shangingi la Zitto wakati Mbunge huyo anaondoka.

Kama itakumbukwa huyu Muhingo alifukuzwa kutoka magazeti ya Mwananchi baada ya wamiliki wake kubaini kuwa alihusika katika hujuma dhidi ya mgombea mmoja wa urais kwa kufanya ughushi katika picha ya mgombea huyo iliyochapishwa katika gazeti.

Jee Zitto alikwenda kuongea nini, maana baada ya hapo tu ndiyo tukasikia anaunga mkono ununuaji wa mitambo ya Dowans. Ni rahisi kujumlisha 2 na 2 kupata jawabu lililo sahihi, au siyo? Ushujaa wa Zitto unaanza kupotea kwa tamaa -- inashangaza kweli kweli!
 
Wacha au waaachieni wenyewe mambo hayo ,hayo ni yao na wameshavuruga sasa wanatafuta mtu wa kulinywa ,Sultani CCM hilo utalinywa mwenyewe ,WaTanzania ni lazima wajieke kando wala msitake kujichanganya ila anaetaka kujichanganya mwacheni atumbukie mwenyewe kama alivyotumbukia Zitto sasa mpira unamuelekea.

Geresha hizi za Sultani CCM na mauzauza ya kufa ,ndio maana yake ,inakuwaje baada ya Miaka 47 tunaambiwa wananchi wapige kura kuwatambua au kuwataja watuhumiwa wa ujambazi,wauaji wa vikongwe na maalbino hatujakaa vizuri kubadilisha fedha lazima uende kwa balozi wa nyumba kumi ajue unataka kubadilisha kiasi gani ili nae umtengee 10% ,Sultani CCM ameshindwa kuiongoza Nchi na kuiweka katika mfumo mzuri ,iliyobaki mara anatupeleka huku mara anaturudisha huku utafikiri gegereka au Kaa( Crab) na wananchi na upinzani wao wanaelekea huko huko ,nasema sivyo kabisa lazima Sultani asimamishwe hapo hapo alipo mambo ya kututingisha kama anatengeneza samli ya maziwa ya ng'ombe yaishe ,tunataka Katiba Mpya ,Tume ya Uchaguzi Mpya ,muundo wa mahakama mpya ,nguvu za Raisi zipunguzwe na baadhi yake kumegewa bunge.

Katiba mpya ndio ngao ya maendeleo ya Tanzania hakuna jingine tusichezeshwe gwaride na Sultani CCM ,ni kutufanya watu tusioelewa tunalolitaka haiwezekani iwe tunaimwandama Sultani CCM na mafisadi wake huku Katiba inawalinda,mahakimu ni wao mawakili ni wao ,hivi tutafanikiwa vipi katika kuliendesha na kulipandisha gurudumu la maendeleo ? Wanachofanya ni kiini macho ,maana walipokuwa wakikarabati gereza la Keko na kulifanya liwe na Vyumba vya VIP ,tulipiga makelele sana lakini wakaruka kiunzi na sasa wanaenda kuwahifadhi na kuwalinda wenzao huko huku wakiwapatia huduma za kiVIP ,huu ni mchezo Sultani CCM anaucheza ili kubaki palepale katika kulindana huyu ni mwenzetu.

Hakuna kitu kama KATIBA na hawa viongozi wa Upinzani ambao ni taa ya mwananchi ya kumurikia dhuluma zinazofanywa na Sultani CCM japo Sulatani CCM anajaribu kumteka mmoja mmoja kwa kumpa sinia ya halua naamini kabisa wapo viongozi walioamau kuikataa sinia hiyo ya halua na wako tayari kufa na Sultani mpaka kieleweke ,hivyo wasipoteze muda watangaze mgogoro wa Katiba katika kuendesha siasa za vyama vingi.

Mgogoro wa Katiba katika kuendesha siasa za vyama vingi ndio ufunguo wa maendeleo ya Mtanzania ,tusidanganyane hapa kwa kupigishana makelele na wanausalama wachache ambao wamejiunga JF kupinga kwa kila hali yale ambayo ni mwiba kwa Sultani CCM ,wanajaribu kupindisha hoja na kuwafanya wapinzani wazubae katika kupigia makelele matatizo yanayowakumba wafuasi wa Sultani CCM ,matatizo ambayo kwa sasa hayatatuliki kisheria bali kimapenzi kwa kuwa huyu ni mwenzetu ni mfuasi mwenzetu katika kumdumisha Sultani CCM ,waajiriwa wa Usalama wa Sultani CCM wapo hapa kuwalaghai na kuwababaisha na kuwachezesha gwaride na kuwayumbisha na kubamiza na kuwaweka ndani ya mada za ufisadi tu wakizizungulusha huku na huku ,lengo lao ni kuificha hoja ya Katiba mpya isijitokeze hapa JF na kushika kasi,na ikianza kuja juu mkubwa wao hujitokeza na kusema kwa sasa haihitajiki kufanya mabadiliko na karibu watasema muda hautoshi,

Wandugu muda huohuo utakaokuwepo, huohuo itabidi utumike ili kuiweka sawa Tanzania na vilevile kuwekana sawa maana wafuasi wa Sultani CCM bado wanajiona ni wao tu ndio wenye hati miliki ya Nchi hii.

Nchi imeingia katika mfumo wa vyama vingi hakuna sababu ya kuibakiza Katiba ya Chama kimoja iwaamulie WaTanzania mambo ambayo yanachanganyisha wafuasi wa vyama mbalimbali ni lazima mabadiliko yafanywe na yajadiliwe kitaifa na kushirikisha wadau wote ,tusikae na kuambiwa muda bado,au hakuna haja, haja ipo tena in urgent manners ,ubabe wa wafuasu wa Sultani CCM unavuka mipaka kwa kasi ya hatari tu ,DC kuwapiga walimu,Mkapa anakinga ,PM kutaka mauaji ya papo kwa papo ,majambazi na waua vikongwe na maalbino kupigiwa kura ya siri, haya ni baadhi tu ya mambo ambayo yanaamuliwa kibabe na ni juzi tu polisi wameua watu ambao walikuwa chini ya himaya yao mbali ya wale wa Zombe kuna hawa wa Arusha kama si ubabe wa wafuasi wa Sultani CCM ni nini ?

Vyombo vilioko chini ya Sultani CCM ambavyo vinamlinda vinafanya vurugu mechi majeshi wanaingia uraiani na kupiga watakavyo polisi anaua saa yeyote ile ,hakuna wa kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria maana ni wao kwa wao na hata wakifikishwa inakuwa ni mwendo wa kinyonga au yule gegereka ,mara wayapeleke huku mara wayapeleke kule au sivyo ? si tunasikia mara jalada lipo mahakamani mara limerudisha mwisho unaambiwa halijulikani lilipo ? Kwa maana mambo yanaendeshwa kienyeji ,inakuwaje mtu anasema jalada silijui lilipo wakati yeye ndio mhusika mkuu,siku hizi wamekuja na kamtindo cha msemaji anaehusika hayupo na ndio hutamuona tena wala simu hapokei ,kumwaga misimu ya uongo ,eti wapigiwe ikiwa kuna ushauri ,ni uongo tu na hawana msimamo wa kweli ,isipokuwa anategemea Sultani CCM atamkingia kifua kwani wote ni wao kwa wao wafuasi wanaomuunga mkono ,hivyo ni kulindana tu ,hakuna la maana litakalofanywa likaonekana. Mabadiliko ya Katiba ya Nchi ni muhimu ili Sultani atenganishwe na mashimo aliyoyachimba ya kujificha yeye na wafuasi wake.
 
Last edited:
Hivi Dowans walipotangaza tenda hii ya kuuza mitambo yao kwa bilioni zaidi ya 60 walikuwa wanatarajia kampuni au mtanzania gani atakayenunua? Au walitangaza wakijua fika kuwa kuna chombo/mtu mmoja tu mwenye uwezo wa kununua mitambo hiyo kwa vile ana/atahiitaji?
 
Halisi:

Move yeyote ya kuunga mkono ununuzi wa Dowans is politically incorrect and illogical, kwa kuzingatia madudu ya Richmond. Mwanasiasa yeyote atakayekubaliana au kuunga mkono wazo la kununua Dowans, ama moja kwa moja au kinyemela, atakuwa anajikaanga kisiasa hata kama anaamini anachokifanya ndio sahihi! Kwa hili, kwa kuwa Zitto ni mwanasiasa, it's politically incorrect, and indeed stupid, for him to support any move to buy Dowans, directly or indirectly. Unfortunately, the repurcations of this political insanity go beyond Zitto; it is costing the whole opposition, and especially CHADEMA. Ngoja niwasikilize leo jioni may be anaweza kutushawishi.

Having said all that we should note that worldwide, almost all astute politicians are naturally controversial. It is thus not very surprising, given his political acuity, to see Zitto behaving as controversially as we have seen!
 
But Sir,wat about that 'tununue mitambo ya Dowans yaishe&free Gire' or I didnt get the tone right!?

Kuna thread inayouliza kama Rostam ametushinda kwenye Dowans, hii inasema Stop Dowans na this is despite the fact kwamba mwenye kutakiwa kuwa stoped ni kamati ya kina Zitto....Kama alivyobainisha mchangiaji mmoja kwenye thread yenye kuhusiana na hii hapa kuwa kuna stages wakati wa kuwa shocked, na nafikiri uko kwenye mojawapo ya stages alizobainisha mchangiaji yule....Je ni Stop Rostam na Zitto ama? Kama sivyo naomba maelezo kuwa wakati wa kuistop Dowans, Rostam na kamati ya Zitto watakuwa upande gani? Upande wa Dowans ama upande unaotaka iwe stoped? Na itakuwa vipi stoped bila ku stop hao wasiotaka iwe stoped?
Hayo ni maswali kwa mwenye mada.
 
Hii ni taarifa ya salva:
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

GAZETI la Mwananchi la leo, Jumatano, Machi 4, 2009 limeandika habari zenye kichwa cha habari: “Kikwete ajitosa sakata la umeme” kikifuatiwa na habari iliyoonyesha kuwa Mhe. Rais amejiingiza katika suala la ununuzi wa mitambo ya umeme ya Dowans.

Mwananchi limeandika habari hiyo, kama ilivyofanywa na vyombo vingine vyote vya habari, kutokana na taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais kufuatia kikao cha jana cha tathmini ya utendaji wa Serikali kati ya Rais Kikwete na uongozi wa Wizara ya Nishati na Madini na taasisi zake.

Vyombo vingine vyote vimeripoti habari hii kwa usahihi kama ilivyotolewa.

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais inapenda kuwaarifu wananchi kuwa gazeti la Mwananchi limesema uongo kwa kupindisha ukweli na kupotosha habari iliyotolewa. Huu ni upotoshaji wa makusudi ambao shabaha yake inajulikana kwa gazeti la Mwananchi peke yake. Ni uchochezi tu wa kumwingiza Mhe. Rais katika suala ambalo hahusiki nalo kabisa. Suala la Dowans halikujadiliwa kabisa katika kikao cha jana.

Kwa hakika, ni ukosefu mkubwa wa heshima kwa chombo chochote cha habari kumlisha maneno Rais wa nchi likijua kuwa maneno hayo siyo ya kweli kama Mwananchi lenyewe linavyokiri katika habari yake.

Katika aya yake ya pili ya habari hiyo, Mwananchi linasema na ninanukuu: “Lakini taarifa kuhusu makubaliano yaliyofikiwa katika kikao cha ufuatiliaji baina ya Rais Kikwete na uongozi wa Wizara ya Nishati na Madini na taasisi zake, haikutaja mitambo ya Dowans kuwa ni sehemu ya mambo yaliyojadiliwa.”

Sasa kama Mwananchi linajua ukweli kuwa suala la Dowans halikujadiliwa katika kikao hicho, limepata wapi habari za kumhusisha Rais na suala zima la mitambo ya umeme ya Dowans?

Jibu ni rahisi. Hili ni gazeti ambalo limeanza kubobea katika kutunga na kupindisha habari zinazohusu Serikali na shughuli za Mhe Rais. Limeanza kubobea katika kuwapotosha kwa makusudi wananchi kwa malengo ambayo yanajulikana kwa gazeti lenyewe. Limebobea katika kuichokonoa Serikali kwa kupindisha ukweli ulio wazi.

Mifano michache ifuatayo inatosha kuthibitisha ukweli huo:

(a) Jumatano, Januari 21, mwaka huu, 2009, Toleo Namba 03145 la gazeti hilo liliandika kichwa cha habari kikisema kuwa “Ikulu ilichukua faili la Kagoda” wakati likijua kuwa siyo kweli.

(b) Ijumaa, Januari 23, mwaka huu, 2009, Toleo Namba 03147 la gazeti hilo liliandika habari yenye kichwa cha habari: “Kikwete achafua hali ya siasa Zanzibar” likijua kuwa hiyo siyo kweli.

(c) Jumamosi, Januari 24, mwaka huu, 2009, Toleo Namba 03148 la gazeti hilo liliandika, miongoni mwa mambo mengine, na nanukuu “Kikwete anamaanisha Serikali itaendelea kuwekwa na wao…Wazanzibar hawana haki ya kujichagulia Rais wanayemtaka, bali CCM na Serikali ndiyo itawachagulia Rais wa kuwaongoza.. basi sasa tusubiri tuone.” Kauli hii inalenga dhahiri kujenga chuki miongoni mwa wananchi wa Zanzibar dhidi ya Rais Kikwete na Serikali ya Muungano.

(d) Katika hotuba ya Salamu za Mwaka Mpya kwa Wananchi iliyotolewa Desemba 31, mwaka jana, 2008, Rais alisisitiza umuhimu wa kulinda amani na utulivu wa Tanzania. Hata hivyo, ukweli huo haukulizuia gazeti hilo la Ijumaa, Januari 2, mwaka huu, 2009 Toleo Namba 03126 kukariri wapinzani wakisema kuwa tadhahari hiyo ilikuwa ni vitisho, wakati likijua dhahiri kuwa hilo siyo kweli.

Kurugenzi ya Mawasilianao ya Rais inapenda, kwa mara nyingine, kusisitiza kuwa uandishi wa upotoshaji na kupindisha ukweli ni hadaa kwa wananchi.

Serikali ya Mhe. Kikwete itaendelea kuheshimu na kuimarisha uhuru wa habari nchini. Lakini pia ni matarajio ya Serikali kwamba vyombo vyetu vya habari vitakijita na kuongozwa na maadili ya taaaluma yanayosisitiza kuandika habari za kweli na kuepuka uandishi na utangazaji wa habari unaokiuka maadili ya taaluma yenyewe ya uandishi wa habari.

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

04 Machi, 2009
 
Kuna thread inayouliza kama Rostam ametushinda kwenye Dowans, hii inasema Stop Dowans na this is despite the fact kwamba mwenye kutakiwa kuwa stoped ni kamati ya kina Zitto....Kama alivyobainisha mchangiaji mmoja kwenye thread yenye kuhusiana na hii hapa kuwa kuna stages wakati wa kuwa shocked, na nafikiri uko kwenye mojawapo ya stages alizobainisha mchangiaji yule....Je ni Stop Rostam na Zitto ama? Kama sivyo naomba maelezo kuwa wakati wa kuistop Dowans, Rostam na kamati ya Zitto watakuwa upande gani? Upande wa Dowans ama upande unaotaka iwe stoped? Na itakuwa vipi stoped bila ku stop hao wasiotaka iwe stoped?
Hayo ni maswali kwa mwenye mada.
Mkuu nakusoma vizuri sana!Ila katika hili la kununua hiyo mitumba itabidi tuchore mstari...Its whether ur with 'us' or ur against 'us'...Ni/tunasema hatutaki kununua mitambo ya Dowans kwani hiyo option/threat ya kuingia gizani ni changa la macho(at least in the near future where we can order and secure some new plants) so...Hao Dowans waliosema kuwa wanauza hiyo mitumba,hao wanakamati wanaowasupport hao TANESCO,hao wanaTANESCO wanaong'ang'aniza ununuzi huo wote wapo ng'ambo ya pili ya mto.Hakika si wenzangu/wenzetu.
 
mwkjjj.

zumari limelia nasi tupo kulichezaaaaa.. mambo ya dowans natumai yatatupa picha nyingine ya uwezo wa serikali hiii katika kutendaaa maamuzi yake.

Hakuna lolote hayo ni kutupotezea muda waTanzania katika kudai KAtiba mpya ,Katiba ambayo haitakuwa na swahiba au haitakuwa na huyu ni mwenzetu ,haya mambo yanayoletwa na wafuasi wa Sltani CCM ni kutaka kutuchanganya WaTanzania ili baadae ionekane sote tulishiriki ,walilolikoroga waachwe walinywe wenyewe kama wewe ni MTanzania unaetaka mageuzi ya kweli ambayo yatakultea maendeleo huna budi kuachana na ubabaishaji huo ambao unaonekana kusukwa ili waingie waliokuwemo na wasio kuwemo.

Madai ya Mtanzania yeyote yule ambae ameamua kuondokana na umasikini hana budi kuyahamisha na kuyapeleka katika kudai KATIBA mpya,Katiba ambayo haitakuwa na nafasi kucheza na wababaishaji wanaowaburuza wananchi katika masuala nyeti wakati hakuna la maana hata moja litakalopatikana zaidi ya kupasiana majukumu na kuishia hewani.

WaTanzani ni lazima tuamke katika kudai mabadiliko makubwa ambayo yataendana na kufuata mfumo wa vyama vingi,kufuata matakwa ya wengi na sio kufuata yale ya ukichagua ndio ,ndio yeye na ukichagua hapana ,hapana mwengine isipo kuwa yeye ,huko ni kuburuzwa.

Sultani CCM na wafuasi wake wanajaribu kuyatwist mambo ili kuwazubaisha wananchi na kuzidi kuwapotezea muda wa kufikia maendeleo ya uhakika ,haya maendeleo ya kupigiwa kura wanaoua vikongwe na maalbino pamoja kuwatambua majambazi ni kuishiwa kwa sera za maendeleo kwa Sultani CCM na ni kuwadharau wananchi ,wananchi ambao kwa kauli za aina hii kutoka kwa wafuasi wa Sultani CCM ni za kuwakatisha tamaa juu ya maisha yao na vizazi vyao vya baadae.

Hakuna faida juu ya mambo haya ambayo ni madudu ya Sultani CCM yaliyofanywa na wafuasi wake ,na hayawezi kutatuliwa kwa kununua au kutonunuliwa ,zaidi ya kufanikisha ubabaishaji wao.

Mmoja wa wafuasi wa Sultani CCM ambae ndie kinara kila siku anasikika akisema nina majina,nina orodha nina hiki na kile akikusudia wanaohujumu uchumi,sio vibaya ni vizuri kabisa kuwa anafahamu wanaolihujumu Taifa ni ushahidi tosha hata wa yeye kufikishwa mahakamani (Wanasema anakinga),maana ukiwajua wahalifu na kuwahifadhi ni kosa na haswa pale unapojulikana kuwa unawajua ,seuze umesema unawajua ,inamaana kutowataja au kutowachukulia hatua ni kuwaachia waendelee kuhujumu,jamani umekwisha kuwajua unapoteza muda wa nini ? Kwa nini unawapa muda wezi mafisadi ? Unapata faida gani ? Eti wajirekebisheh !! Wezi wajirekebishe ,Taifa linaingia au limeingia hasara unasema wajirekebishe na ile hasara waliyoisababisha hata ukapatiwa orodha ndio basi ! tunaibeba wananchi ? Tunaibeba hasara iliyosababishwa na watu wanaojulikana ! Toka alipopatiwa orodha ,sijui kama kati yetu yupo anaejua mpaka leo ni muda gazi zaidi ya aliepeleka orodha hiyo ? Je ni rate gani Taifa limepata hasara kwa muda huo ?

Hii ni kesi ikiwa kinara wa Sultani CCM haelewi ,moja kwa moja inaweza kumpeleka mahakamani.Kwa kuwahifadhi wahujumu uchumi ,aliempelekea orodha alikuwa na imani Taifa litasimamishiwa hasara hiyo ,lakini wenzetu wameambiwa wajirekebishe.

Sasa hayo nasema ni ya Wafuasi wa Sultan CCM ,ni madudu ,ni mauzauza ni dharau ambazo zinafanywa na kutekelezwa na wafuasi wa Sultani CCM ni mambo yao ambayo yanalindwa na Katiba ya uongozi chini ya mfumo wa Chama kimoja.

Katiba ambayo haifai kwa muda huu tulionao haina budi kubadilishwa mara moja.
 
Katika hili Zitto kachemsha,ushauri wangu kwake ni bora awaombe radhi watanzania na akiri kukosea,atasamehewa,akiendelea na msimamo wake huu hakika utakuwa usaliti mkubwa,atakuwa amesaliti imani za watanzania kwake,na historia itamuhukumu,,,time will tell,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,
 
Back
Top Bottom