Dowans: Another Richmond in making?

Dowans: Another Richmond in making?

Kwako SteveD, Zitto akiwa criticized unasema aachwe; haya sasa ndio matokeo yake.

Cool aid na massage ya watu aina yako (wanaosema mitambo ya Dowans inunuliwe kwa sababu April kutakuwa na shida ya umeme!) imempelekea Zitto kuyumba. Mwisho wa siku maslahi ya Taifa nyuma au kando!

Mama
Sijayumba na wala sitayumba. Mimi ni mtu mwenye msimamo katika ninaloamini na nipo tayari kusulubiwa kwa lile ninaloamini. Sifanyi mambo kufurahisha watu na hivyo kuogopa kufanya yale yatakayochukiza.

Ninaamini kabisa suala hili linakuwa spinned mno kwa interest fulani fulani. Mimi sikatai criticisms. Lakini criticisms ziwe on facts. Sasa anapokuja mtu na kusema nimepewa mlungula, mie nacheka kwani najijua mwenyewe kuwa mlungula sio vocab yangu. Lakini kwa kuwa watu wengi wameoza kwa rushwa basi wanaamini kuwa mtu yeyote hawezi kuamua bila rushwa.

Ninasimamia uamuzi wa Kamati yangu kuwa suala hili liangaliwe objectively na kama itaonekana kuwa ununuzi wa mitambo hii ni manufaa kwa nchi inunuliwe.
 
Hakuna anayekataa option ya kununua mitambo mipya kabisa. Hakuna na hakna sehemu nimesema lazima Dowans. Unatukana wabunge kuwa ni ****** na flip flop? Natumai umeropoka tu katika hili.
Tupo wabunge makini, tumesoma vizuri na kuendele kujisomea na tunaelewa. TANESCO wamesema waziwazi kuwa mbadala wa kununua mitambo ya dowans ni kununua mitambo mipya kabisa.

Kamati ya Bunge imesema kamati mbili zikae na kujadili kupata mwafaka. Sijui la ziasa ni nini hapa.

Zitto watu tulikuamini sana lakini kwa hili la Dowans umetuvunja moyo na tukuone kuwa na wewe kumbe unaweza kuhongeka tu kirahisi na huyu fisadi Rostam Azizi. Hiyo Dharura mnayoisema kumbe ni ya miaka miwili ijayo na pia bei mnaambiwa ya kununua mitambo mipya ni rahisi kuliko hii mitumba ya Dowans. Kwanini mnang'ang'ani kununu hii mitumba? Maana kuna gazeti moja juzi kama sikosei limekuquote ukisema kuwa sheria ya manunuzi ibadilishwe ili mitumba ya Dowans inunuliwe. Hapa si bure mwenzetu umeshachukua chako tayari. Na kuna uvumi usio rasmi kuwa wewe siku hizi unatembelea gari la nguvu "Hammer" na inaonekana ni mojawapo ya zawadi ulizopewa ufumbe mdomo juu ya hawa mafisadi na ufanikishe biashara zaoa haramu. Kwakweli umetuangusha sana vijana wenzako. Tulikutegemea kuwa wewe ungeweza kuwa Obama wetu kumbe wapi.
 
Siungi mkono ujambazi wowote.Pia nipo tayari kusimama mwenyewe na kuelezea ninachoamini. Nipo tayari kubaki peke yangu iwapo ninachofanya ninaona ni sahihi na nipo genuine. Katika hili mimi na kamati yangu tupo genuine na hatuna maslahi yeyote zaidi ya kuona shirika linaendeshwa kwa faida na hivyo nasi kuwa na national champion.

I stand with the decision of my committee kwamba Kamati mbili zikutane na kujadili suala hili. Kiongozi lazima awe tayari kuchukua maamuzi magumu. nipo tayari kuwajibika kwa hili.

Hii nimei-copy toka Nipashe:

Mbunge wa Kyela (CCM), Dk. Harrison Mwakyembe, amesema ni vigumu kununua mitambo ya kufua umeme ya Dowans, kwa sababu licha ya kukiuka Sheria ya Manunuzi ya Umma na maazimio ya Bunge, kampuni hiyo imefungua kesi dhidi ya serikali na Tanesco katika mahakama ya usuluhishi huko Paris.

Mwakyembe amesema anashangazwa na hatua ya Tanesco kung`ania mitambo ya Dowans, wakati tayari wamiliki wake wamewashtaki serikali na Tanesco huko Ufaransa.

``Dowans wametupeleka Paris katika Mahakama ya Usuluhishi, sasa iweje tung`ang`anie kununua mitambo yao katika hali kama hii,`` alisema Dk. Mwakyembe katika mahojiano maalum na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

Alisema uamuzi wa kununua au kutonunua mitambo hiyo upo mikononi mwa Tanesco, iwapo shirika hilo linang`ang`ania kufanya hivyo kinyume na ushauri wa maamuzi ya Bunge.

Alisema kumekuwa na ujanja ujanja mwingi unaotumiwa na menejimenti ya Tanesco kuhakikisha kwamba inafanikiwa kununua mitambo hiyo kinyume na Sheria ya Manunuzi ya Umma na maazimio ya Bunge.

Alisema uongozi wa Tanesco ``unafanya usanii`` katika kutaka kuhalalisha uamuzi wake wa kununua mitambo ya kufua umeme ya kampuni ya Dowans.

Dk. Mwakyembe ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, alisema Tanesco imekuwa ikitafuta mbinu za kuhalalisha uamuzi wao wa kununua mitambo ya Dowans ambayo kisheria hairuhusiwi kufanya hivyo.

Dowans ambayo ilirithi mkataba batili wa kampuni tata ya Richmond Development LLC ya Marekani, haifahamiki mmiliki wake kisheria.

``Sisi tunasema kama kununua wanunue, wameomba vibali mara ngapi, wananunua sijui nguzo!!! wamekuja lini kwetu. Naamini kwenye hili wamegundua kuna kitu hakiko vizuri ndio wanataka kuhalalisha,`` alisema.

Alisema kamati yake ilitoa maoni, ila kuna ujanja wa aina fulani, ``Sijui wanataka nini, kana kwamba kamati nyingine ina mamlaka ya kupokea rufani dhidi ya kamati nyingine kuna aina fulani ya usanii kwenye uongozi wa Tanesco.``

Alifafanua kwamba 14, Desemba, 2008, kamati yake ilipokutana na uongozi wa Tanesco, Wizara ya Nishati na Madini pamoja waziri mhusika, waligundua kwamba Bodi ya Tanesco ilikaa siku 10 kabla na kukataa kata kata wazo la kununua mitambo ya Taneco.

``Hata hivyo, menejimenti ya Tanesco iliizunguka Bodi na kuja kwetu na sasa wamezunguka na kwenda kwa Kamati ya Hesabu na Mashirika ya Umma , ikiomba kibali cha kununua mitambo hiyo,`` alisema.

Alisema kazi ya Bunge ni kusimamia na sio kujiingiza katika shughuli za utendaji wa kila siku wa Tanesco, lakini akaonya kwamba iwapo itabainika kuwa taratibu zimekiukwa katika ununuzi huo na kuliingiza taifa katika balaa, wahusika watawajibishwa.

Alisema uongozi wa Tanesco, ``unafanya usanii`` katika kutaka kuhalalisha uamuzi wake wa kununua mitambo ya Dowans.

Dk. Mwakyembe alifafanua kwamba Tanesco imekuwa ikitafuta mbinu za kuhalalisha uamuzi wao wa kununua mitambo ya Dowans ambayo kisheria hairuhusiwi kufanya hivyo.

Alisema menejimenti imekuwa na ujanja ujanja mwingi kiasi cha kuizunguka kamati yake, na kuwasilisha maombi ya kununua mitambo hiyo kwa kamati nyingine ya Hesabu na Mashirika ya Umma (POC).

``Sisi tulitoa maoni, Tanesco ina ujanja wa aina fulani, sijui wanataka nini, kana kwamba kamati nyingine ina mamlaka ya kupokea rufani dhidi ya kamati nyingine,kuna aina fulani ya usanii kwenye uongozi wa Tanesco,`` alisema na kuongeza

``Kama wanataka kununua, wanunue…na sisi kazi yetu ni kusimamia tu na sio kuwaagiza kwamba wanunue au wakatae. Watakapoamua kununua wajue kwamba wanafanya hivyo kwa misingi ya kanuni na sheria, la sivyo watawajibika,`` alisema.

Akizungumzia mjadala wa ununuzi wa mitambo ya Dowans, Dk. Mwakyembe alisema anaona umepata sura ya kisiasa, na anaona kama ni mwendelezo wa Operesheni Sangara.

``Nimesikia na kusoma kuhusu Mwenyekiti wa POC, Zitto Kabwe kwamba kamati haijawasilikiliza Tanesco. Kamati ilikutana na Tanesco na Wizara 14 Desemba mwaka jana na kuwasikiliza, kwamba hatujawasikiliza hilo si kweli,`` alisema.

Naye mbunge wa Nzega CCM, Lucas Selelii, amesema hatua ya baadhi ya wabunge na viongozi wa serikali kupigia debe ununuzi wa mitambo ya kufua umeme ya kampuni ya Dowans kinyume na maamuzi ya Bunge, inaleta wasiwasi.

Alisema ana wasiwasi kwamba huenda kuna mkono wa mtu, anayeshinikiza kununuliwa kwa mitambo hiyo, kinyume na maazimio ya Bunge.

Hivi karibuni, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma, Zitto Kabwe, amenukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari akitaka Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) liinunue mitambo hiyo.

``Kuna mkono wa mtu, tena mkono wenyewe ni wa chuma, kwanini maamuzi yetu wenyewe tunayakanyaga, kama wanapinga, turudi bungeni,`` alisema Selelii jana wakati akizungumza na Nipashe kwa njia ya simu kutoka jimboni kwake.

Alisema suala la ununuzi wa mitambo hiyo lilitolewa kama pendekezo na Kamati Teule ya Bunge na kuridhiwa na Bunge kwamba mitambo hiyo isinunuuliwe.

Alisema kwanza, katika uchunguzi wa kamati hiyo iligundulika kwamba mitambo hiyo ni mibovu na pili gharama za ununuzi wake ni kubwa.

Kwa mujibu wa Sheria ya Manunuzi ya Umma, ni makosa kwa serikali kununua vifaa ambazo vimetumika (mitumba).

Alisema kiasi cha fedha ambacho kinatakiwa ili kununua mitambo hiyo, kinaweza kununua mitambo mingine mitatu yenye ukubwa na uwezo huo huo wa kuzalisha umeme.

Selelii alisema serikali inaweza kufanikisha ununuzi huo kwa kutuma barua pepe Marekani ambako mitambo hiyo hutengenezwa au inaweza kumpeleka ambaye atashughulikia ununuzi wake na hivyo kurudi nchini akiwa na mitambo mitatu.

Alifafanua kwamba Kamati Teule ya Bunge ilikwisha kamilisha kazi na mapendekezo yake yaliridhiwa na Bunge na suala hilo sasa lipo chini ya Kamati ya Nishati na Madini ya Bunge.

Alisema atashangaa iwapo Kamati hiyo ambayo ipo chini ya Mwenyekiti, William Shellukindo, itakapokiuka maazimio ya Bunge.

Kwa upande wake, Mbunge wa Karatu, Chadema, Dk. Wilbrood Slaa, alisema kinachohitajika katika suala hili ni taarifa kwa taifa.

``Tunaingizwa katika mjadala, wakati hatujui yaliyomo kwenye Kamati ya Shellukindo na wala katika Kamati ya Zitto,`` alisema na kuhoji: ``Kwa nini kamati hizi mbili kila moja inashikilia msimamo wake.``

Alisema haijulikani serikali na Tanesco walikubaliana nini katika Kamati ya Zitto, na kuongeza kuwa ni vema kujadili suala ambalo mmoja amepewa taarifa zake.

Alisema hadi sasa hakuna mtu anayejua kwa uhakikia nini yaliyomo katika Kamati hizo, suala ambalo ni gumu kulijadili.

Alisema Kamati ya Mwakyembe ilitoa taarifa kuhusu mitambo ya kufua umeme ya Dowans, kwamba serikali inaweza kupata na kununua mitambo hiyo huko inakotengenezwa tena kwa bei nafuu.

Lakini alisema: ``Tunataka kujua maazimio ya Bunge kuhusu sakala la Richmond yamefikia wapi kwa sababu kwa mujibu wa Sheria ya Manunuzi ya Umma, iwapo mtu amebainika kughushi na kuingia mikataba, mali zake zinatakiwa kutaifishwa.``

Alihoji iwapo mkataba wa kufua umeme wa dharura kati ya Tanesco na kampuni ya Richmond, (sasa Dowans), ulibainika kuwa umeghushiwa, sheria imefuatwa ya kutaifisha mitambo hiyo.

Alisema badala yake kuzingatia taratibu hizo za kisheria, tunazungumzia hitaji la kununua mitambo hiyo.

Hata hivyo, alisema dharura hii ya umeme si ya leo, na ina tofauti gani na ile ya miaka iliyopita.

Juzi (Jumamosi), Mkurugenzi mtendaji wa Tanesco, Dk. Idris Rashid, alitoa taarifa kwenye vyombo vya habari kuelezea hali ya umeme katika Grid ya Taifa pamoja na mambo mengine, akapendekeza kuwa mtambo wote wa Dowans ununuliwe na serikali pamoja na vifaa vyote vya kuunganishia kwenye grid suala la ununuzi wa mitambo iliyotumia katika sheria ya Manunuzi iangaliwe kwa makini kwa manufaa ya sekta ya umeme na mbadala wa kununua mtambo wa Dowans ni kuagiza mara moja mitambo ya kukodisha ya umeme ya kiasi cha megawati 150 kwa njia ya dharura, ambayo inapaswa kuwepo kwa kipindi kisichopungua miaka miwili.

Mhe Zito:
Kila unapojaribu kujitetea ndio unavyozidi kujichafua..... nakushauri warudishie hela waliyokuhonga!!!!
 
Rostam Azizi ni fundi wa kuwaingiza kwenye anga zake wale wote wanaoonekana kumnufaisha kwa gharama yoyote. Mtakumbuka kwa jinsi alivyomnunua marehemu Wangwe kuwasambaratisha CHADEMA hasa akimlenga kummaliza nguvu Slaa aliyeonekana kuwa mwiba kwake. Sasa hivi mitambo yake anaona inamdodoea kwani hana pa kuipeleka. Alichoona ni kuhakikisha kuwa Rashid anayejulikana kuwa ni fisadi wa siku nyingi anapewa kitita na Zitto ambaye ni mwenyekiti wa kamati yenye kuigusa TANESCO naye analambishwa asali ili wote wasimame kidete kutetea ununuzi wa mitambo hiyo kwa nguvu zao zote. Dharura inayosemwa hapa ni ya miaka miwili ijayo na si leo sasa utaona hii nguvu inayotumika kupigia debe hii mitambo si bure bali kuna katapila nyuma yake linasukuma kwa nguvu zote. Mpaka hapa sote twaweza kusema Zitto hafai hata kidogo maana anaweza kubadilika haraka sana na kuwa fisadi la kupindukia na kuizamisha nchi hii kiuchumi. Wengi tulimwona mpiganaji lakini kwa hili amejimaliza kabisa na mimi binafsi hatakaa anishawishi tena, nimebadili msimamo wangu juu yake.
 
Ninasimamia uamuzi wa Kamati yangu kuwa suala hili liangaliwe objectively na kama itaonekana kuwa ununuzi wa mitambo hii ni manufaa kwa nchi inunuliwe.

Wewe Zitto umepata access ya taarifa zote muhimu. Umepata fursa ya kuhojiana na wataalam wa TANESCO. Umepata wasaa wa kujadili sheria ya manunuzi. Sasa leo ukianza kuzungumza kama hivi unakuwa sio kiongozi. Kama kiongozi mpaka sasa unatakiwa uwe una msimamo wako-uliotokana na taarifa ulizo nazo. Wewe inabidi uwe straight forward kama unaunga mkono ununuzi au lah. Na kama unaunga mkono basi ueleza wananchi why so? Hata wasipokuunga mkono, hakuna shida lakini sema unachoamini - kwa sababu una taarifa ambazo wengine hawana. But please at this time usije na kauli kama hizi as if hujui kama inafaa au haifai. Na kama mpaka sasa hujui kama mitambo hiyo inafaa au lah, basi jitoe tu kwenye hiyo kamati, kwa sabbau hiyo kazi huiwezi. Huhitaji kukaa na kamati yoyote ili uwe na msimamo. Kukaa na kamati kukuwezeshe kutetea hoja yako tu. Sasa basi elezea waziwazi msimamo wako hapa JF-of course kama unao- na achana na kauli za kutaka vikao vya kisiasa.
 
Kwa hiyo unasimamia uamuzi wa kununua mitambo ya Dowans iwe at the expense ya watu kula majani, au hata kama hiyo mitambo ni mikuu kuu, au mipya ya hiyo inayoweza kupatikana kwa bei ya chini zaidi?

Unamaanisha ni wewe (unasimama) pekee unayeweza kufanya kitu sahihi na genuine. U-dictator au unaona Watanzania wote ni vilaza isipokuwa wewe tu ndio unayejua/kuona/kupembua sahihi na genuine!

Umeniwekea maneno. Ninasimamia uamuzi wa kamati yangu kuliangalia suala hili objectively na kama nchi itafaidika mitambo inunuliwe. Kama kuna mitambo ya bei nafuu zaidi na mizuri zaidi MIPYA inunuliwe.

I am never a dictator, but a bold leader. I am able to tell people what they dont want to hear. I always subordinate my personal interest to those of the nation. Always and i can prove that. I stand to be counted

I am never materialist. I am never corrupt. I am genuine. I am honest. I speak my mind. Never been slippery.

Facts peke yake ndio zinanifanya nibadili msimamo. Sio hisia za kupoteza umaarufu nk. Umaarufu nilionao (kama ninao) ni earned popularity, na sio sought! Siwezi kuogopa kuchukua maamuzi eti kwa sababu ya kupoteza umaarufu. Kama ni maamuzi magumu na ninaamini ni sahihi nitachukua na one day the truth will be known. Truth prevails.
 
Kama kuna mitambo ya bei nafuu zaidi na mizuri zaidi MIPYA inunuliwe.

Mimi nadhani Zitto hapa umeshaprove failure. Na kama kweli wewe ni mjali maendeleo ni bora ujitoe kwenye hiyo kamati ili uwapo fursa wanaoweza kuiongoza. Wewe ulipaswa mpaka sasa uwe na taarifa za uwezekano wa kupata mitambo kwa bei nafuu. Na ulipaswa uje hapa JF na data kuwa mitambo nafuu ipo au haipo. Sio mpaka sasa unazungumza lugha kama hizi. Hupaswi kuuliza kama kuna mitambo ya bei nafuu, wewe unalipwa kwa pesa za walipa kodi wa Tanzania ili ufanye utafiti utakaoliwezesha Taifa kufanya matumizi yenye manufaa kwa mashirika yake. Sasa unapouliza hapa unadhihirisha kuwa you didnt do your work. Wewe ni kijana huu ni muda wa kuchapa kazi, acha maneno yasiyo match na vitendo. Chapa kazi wakati wa kazi, sio kila wakati siasa.
 
Zitto,
kuna hoja kuhusu maendeleo ya mkoa wa kigoma. wewe na wabunge wenzako mmefanya jitihada gani kuinua maendeleo katika wilaya zenu? kuna mchangiaji anawashutumu kwamba hamjafanya lolote tangu mchaguliwe. tunaomba umjibu huyu jamaa ambaye anaonekana na mpigakura wako.
 
Wewe Zitto umepata access ya taarifa zote muhimu. Umepata fursa ya kuhojiana na wataalam wa TANESCO. Umepata wasaa wa kujadili sheria ya manunuzi. Sasa leo ukianza kuzungumza kama hivi unakuwa sio kiongozi. Kama kiongozi mpaka sasa unatakiwa uwe una msimamo wako-uliotokana na taarifa ulizo nazo. Wewe inabidi uwe straight forward kama unaunga mkono ununuzi au lah. Na kama unaunga mkono basi ueleza wananchi why so? Hata wasipokuunga mkono, hakuna shida lakini sema unachoamini - kwa sababu una taarifa ambazo wengine hawana. But please at this time usije na kauli kama hizi as if hujui kama inafaa au haifai. Na kama mpaka sasa hujui kama mitambo hiyo inafaa au lah, basi jitoe tu kwenye hiyo kamati, kwa sabbau hiyo kazi huiwezi. Huhitaji kukaa na kamati yoyote ili uwe na msimamo. Kukaa na kamati kukuwezeshe kutetea hoja yako tu. Sasa basi elezea waziwazi msimamo wako hapa JF-of course kama unao- na achana na kauli za kutaka vikao vya kisiasa.

Nimepata taarifa zote ni kweli. Kamati yangu ilikubaliana na TANESCO kimsingi lakini tukasema sio vizuri kamati mbili za Bunge kupingana na hivyo kuomba kamati mbili zikutane labda wenzetu wana sababu zaidi.

Sheria ya manunuzi inasemwa kweli ndugu yangu lakini hakuna hata mtu mmoja hapa ambae kaja na kutoa kipengele gani cha sheria ya manunuzi kinakataza. Sijakiona mie. Hebu tazama na wewe, just google the Act na utueleze. Unajua sheria ya manunuzi inazungumzia kuanzia chaki shuleni mpaka vifaa complicated vya jeshi. Sheria haiwezi kuwa general (nunua kitu kipya...............). Huo mjadala pia hapa sijauona. Tunasema tu, sheria ya manunuzi, hatusemi kipengele gani na kwa mazingira gani.

Pia katika ununuzi huu, TANESCO ndio walibid kununua na sio TANESCO waliotangaza tenda. Katika mazingira kama haya sheria ya manunuzi inasemaje?

Ndio maana katika kikao hicho Kamati yangu ilishauri kuwa PPRA wawepo ili kuwa clear na masuala ya sheria ikiwemo kama kuna waiver inatolewa katika mazingira gani.

Tatizo mjadala huu umechukua emotions zinazotokana na richmond etc (which i understand) na hivyo kupoteza objectivity kwa kiasi kikubwa
 
Zitto watu tulikuamini sana lakini kwa hili la Dowans umetuvunja moyo na tukuone kuwa na wewe kumbe unaweza kuhongeka tu kirahisi na huyu fisadi Rostam Azizi. Hiyo Dharura mnayoisema kumbe ni ya miaka miwili ijayo na pia bei mnaambiwa ya kununua mitambo mipya ni rahisi kuliko hii mitumba ya Dowans. Kwanini mnang'ang'ani kununu hii mitumba? Maana kuna gazeti moja juzi kama sikosei limekuquote ukisema kuwa sheria ya manunuzi ibadilishwe ili mitumba ya Dowans inunuliwe. Hapa si bure mwenzetu umeshachukua chako tayari. Na kuna uvumi usio rasmi kuwa wewe siku hizi unatembelea gari la nguvu "Hammer" na inaonekana ni mojawapo ya zawadi ulizopewa ufumbe mdomo juu ya hawa mafisadi na ufanikishe biashara zaoa haramu. Kwakweli umetuangusha sana vijana wenzako. Tulikutegemea kuwa wewe ungeweza kuwa Obama wetu kumbe wapi.

Oh siku hizi natembelea HUMMER? Unaamini uvumi huo sio? Nilinunua HUMMER mwaka 2007 na nilianza kuitumia mwezi June na sikuipenda maana ilikaa kitajiri mno na kuiuzilia mbali.
Sasa unasema sasa hivi nina HUMMER....... Haya unaweza kutunga uongo na ukauamini.
 
Nimepata taarifa zote ni kweli. Kamati yangu ilikubaliana na TANESCO kimsingi lakini tukasema sio vizuri kamati mbili za Bunge kupingana na hivyo kuomba kamati mbili zikutane labda wenzetu wana sababu zaidi.

Sheria ya manunuzi inasemwa kweli ndugu yangu lakini hakuna hata mtu mmoja hapa ambae kaja na kutoa kipengele gani cha sheria ya manunuzi kinakataza. Sijakiona mie. Hebu tazama na wewe, just google the Act na utueleze. Unajua sheria ya manunuzi inazungumzia kuanzia chaki shuleni mpaka vifaa complicated vya jeshi. Sheria haiwezi kuwa general (nunua kitu kipya...............). Huo mjadala pia hapa sijauona. Tunasema tu, sheria ya manunuzi, hatusemi kipengele gani na kwa mazingira gani.

Pia katika ununuzi huu, TANESCO ndio walibid kununua na sio TANESCO waliotangaza tenda. Katika mazingira kama haya sheria ya manunuzi inasemaje?

Ndio maana katika kikao hicho Kamati yangu ilishauri kuwa PPRA wawepo ili kuwa clear na masuala ya sheria ikiwemo kama kuna waiver inatolewa katika mazingira gani.

Tatizo mjadala huu umechukua emotions zinazotokana na richmond etc (which i understand) na hivyo kupoteza objectivity kwa kiasi kikubwa


Nimekupata haswa, ila tatizo linalojitokeza ni kwamba wewe hutoi msimamo wako bonafsi. Watu wanataka kujua ukiingia kwenye kikao utapigania msimamo upi? na mimi pamoja na wengi humu tunaamini kuwa umepata muda na taarifa za kutosha kukuwezesha kuwa na msimamo wako. Tuweke mambo ya kamati pembeni, je wewe kama the informed representative unaunga mkono ununuzi au hauungi mkono. Matokeo ya vikao hayategemei na msimamo wako peke yako, ila ni muhimu sana wana JF wajue wewe ulisimamia upande gani?
Mtu anayeheshimu nguvu ya taarifa hawezi kukulaumu kwa msimamo utakaouchukua kwa sababu as i have already said unajua mengi ambayo wengi hawayajui juu ya hili. Lakini ni jukumu lako kutujulisha msimamo wako baada ya kuwa na taarifa ulizo nazo.
 
Umeniwekea maneno. Ninasimamia uamuzi wa kamati yangu kuliangalia suala hili objectively na kama nchi itafaidika mitambo inunuliwe. Kama kuna mitambo ya bei nafuu zaidi na mizuri zaidi MIPYA inunuliwe.

I am never a dictator, but a bold leader. I am able to tell people what they dont want to hear. I always subordinate my personal interest to those of the nation. Always and i can prove that. I stand to be counted

I am never materialist. I am never corrupt. I am genuine. I am honest. I speak my mind. Never been slippery.

Facts peke yake ndio zinanifanya nibadili msimamo. Sio hisia za kupoteza umaarufu nk. Umaarufu nilionao (kama ninao) ni earned popularity, na sio sought! Siwezi kuogopa kuchukua maamuzi eti kwa sababu ya kupoteza umaarufu. Kama ni maamuzi magumu na ninaamini ni sahihi nitachukua na one day the truth will be known. Truth prevails.

Hayo maneno niliyoapigia msitari; that is what you think you are, and that is what we thought you were. What we think of you now is "A TRAITOR." Haya mambo ya kudai eti maslahi ya taifa ni kututukana wananchi kwani hata Lowasa wakati anahalalisha Richmond alisema hayo unayojaribu kutueleza, dharura, mitambo inauwezo, watu wanapinga kwa sababu fulanifulani, sijachukua chochote. Bila kijisahihisha na hili umekwisha hata kama wamekupa pesa ambayo unaona huhitaji ubunge tena kumbuka maisha siyo ubunge wala pesa tu
 
Umeniwekea maneno. Ninasimamia uamuzi wa kamati yangu kuliangalia suala hili objectively na kama nchi itafaidika mitambo inunuliwe. Kama kuna mitambo ya bei nafuu zaidi na mizuri zaidi MIPYA inunuliwe.


Kwa hiyo, hiyo kamati yenu inakubaliana mnunue mzigo toka kwa wezi? Maana hao Dowans ni cohort ya Richmond ambao walinunua mitambo hii kwa fedha walioiibia serikali ya Tanzania.

Nakumbuka kampuni ya Richmond haikuwa na mtaji, ikabidi ipewe na serikali (kwa kumbukumbu zangu za kizee, I stand to be corrected ).
 
Oh siku hizi natembelea HUMMER? Unaamini uvumi huo sio? Nilinunua HUMMER mwaka 2007 na nilianza kuitumia mwezi June na sikuipenda maana ilikaa kitajiri mno na kuiuzilia mbali.
Sasa unasema sasa hivi nina HUMMER....... Haya unaweza kutunga uongo na ukauamini.

duh yaani mh.zitto unatutambia kabisa kuwa ulinunua hummer na kuliuzilia mbali.yaani hii acha zile vx zenu sijui prado
kweli ubunge dili bongo!!nitafanya juu chini 2015 nigombee...
 
Kwako Zitto

Katika mahojiano na gazeti la serikali la Daily News yaliyofanyika Juni 31, 2008, Dk. Rashid alisema kuwa "taratibu zote za kuingia mkataba baina ya Richmond na Tanesco zilikiuka Sheria ya Manunuzi ya Umma na hivyo kuwa batili na kwamba hata kama usingekuwa batili, taratibu za utoaji wa majukumu ya tenda hiyo kutoka Kampuni ya RDEVCO badala ya Dowans Holding SA na baadaye Dowans Tanzania Limited haukuwa na msingi wa makubaliano na hivyo kuwa batili".


"Ukweli ni kwamba mkataba ulikuwa kati ya Richmond Development Company LLC na Tanesco na na sio Redvco na Tanesco," Dk. Rashid alikaririwa na Daily News wakati huo huku akifafanua kuwa jina la RDC LLC lilikuwa la kufikirika kwenye mkataba na kwamba kampuni hiyo haikusajiliwa Texas, Marekani.


Alidokeza kuwa Dowans Holding SA ilisajiliwa nchini Costa Rica ikiwa na mtaji wa dola 100 za Marekani (takriban Sh 131,000 za Tanzania).


Baada ya kuvunja mkataba huo, Dowans iliishtaki Tanesco kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Biashara iliyo Paris, Ufaransa, uamuzi uliolifanya shirika hilo kushikilia mitambo ya Dowans likidai kuwa itatumika kama fidia iwapo Dowans itashindwa kesi"

Swali kwako Zitto: Je hii kesi kati ya Dowans na Tanesco imeshakwisha na mamuzi yakoje? Mbona mitambo iliyoshikiliwa kwa kufidia kesi kamaTanesco watashinda sasa inauzwa kwa Tanesco wenyewe? Hapa kuna mkanganyiko na kila dalili za rushwa. Bwana Zitto hebu tupe maelezo kuhusu hili.
 
Hii nimei-copy toka Nipashe:

Mbunge wa Kyela (CCM), Dk. Harrison Mwakyembe, amesema ni vigumu kununua mitambo ya kufua umeme ya Dowans, kwa sababu licha ya kukiuka Sheria ya Manunuzi ya Umma na maazimio ya Bunge, kampuni hiyo imefungua kesi dhidi ya serikali na Tanesco katika mahakama ya usuluhishi huko Paris.

Ni kweli kuna kesi. Ni kesi ya kuvunjwa kwa mkataba. Hakuna kesi ya equipments. Kuna tofauti kati mambo haya. Suala hili la kesi linakuja sasa na sio kabla. Kamati ya Nishati na Madini inajua zaidi kwa nini suala hili halikusemwa kabla. Kipengele gani cha sheria ya manunuzi kinachosemwa hapa?

Mwakyembe amesema anashangazwa na hatua ya Tanesco kung`ania mitambo ya Dowans, wakati tayari wamiliki wake wamewashtaki serikali na Tanesco huko Ufaransa.

``Dowans wametupeleka Paris katika Mahakama ya Usuluhishi, sasa iweje tung`ang`anie kununua mitambo yao katika hali kama hii,`` alisema Dk. Mwakyembe katika mahojiano maalum na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

Alisema uamuzi wa kununua au kutonunua mitambo hiyo upo mikononi mwa Tanesco, iwapo shirika hilo linang`ang`ania kufanya hivyo kinyume na ushauri wa maamuzi ya Bunge.

Bunge halijawahi kukaa mahala popote na kuiambia TANESCO msinunue mitambo. Wala Bunge halijawahi kupokea taarifa ya Kamati ya Nishati na Madini kuhusu suala hili. Kanuni za Bunge zinasema maamuzi ya Kamati ni yale yaliwasilishwa Bungeni na kuamuliwa. Hilo halijawahi kutokea. Uamuzi gani wa bunge unaosemwa hapa?


Alisema kumekuwa na ujanja ujanja mwingi unaotumiwa na menejimenti ya Tanesco kuhakikisha kwamba inafanikiwa kununua mitambo hiyo kinyume na Sheria ya Manunuzi ya Umma na maazimio ya Bunge.

Alisema uongozi wa Tanesco ``unafanya usanii`` katika kutaka kuhalalisha uamuzi wake wa kununua mitambo ya kufua umeme ya kampuni ya Dowans.

Dk. Mwakyembe ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, alisema Tanesco imekuwa ikitafuta mbinu za kuhalalisha uamuzi wao wa kununua mitambo ya Dowans ambayo kisheria hairuhusiwi kufanya hivyo.

Dowans ambayo ilirithi mkataba batili wa kampuni tata ya Richmond Development LLC ya Marekani, haifahamiki mmiliki wake kisheria.

``Sisi tunasema kama kununua wanunue, wameomba vibali mara ngapi, wananunua sijui nguzo!!! wamekuja lini kwetu. Naamini kwenye hili wamegundua kuna kitu hakiko vizuri ndio wanataka kuhalalisha,`` alisema.

Alisema kamati yake ilitoa maoni, ila kuna ujanja wa aina fulani, ``Sijui wanataka nini, kana kwamba kamati nyingine ina mamlaka ya kupokea rufani dhidi ya kamati nyingine kuna aina fulani ya usanii kwenye uongozi wa Tanesco.``

Alifafanua kwamba 14, Desemba, 2008, kamati yake ilipokutana na uongozi wa Tanesco, Wizara ya Nishati na Madini pamoja waziri mhusika, waligundua kwamba Bodi ya Tanesco ilikaa siku 10 kabla na kukataa kata kata wazo la kununua mitambo ya Taneco.

``Hata hivyo, menejimenti ya Tanesco iliizunguka Bodi na kuja kwetu na sasa wamezunguka na kwenda kwa Kamati ya Hesabu na Mashirika ya Umma , ikiomba kibali cha kununua mitambo hiyo,`` alisema.

Alisema kazi ya Bunge ni kusimamia na sio kujiingiza katika shughuli za utendaji wa kila siku wa Tanesco, lakini akaonya kwamba iwapo itabainika kuwa taratibu zimekiukwa katika ununuzi huo na kuliingiza taifa katika balaa, wahusika watawajibishwa.

Alisema uongozi wa Tanesco, ``unafanya usanii`` katika kutaka kuhalalisha uamuzi wake wa kununua mitambo ya Dowans.

Dk. Mwakyembe alifafanua kwamba Tanesco imekuwa ikitafuta mbinu za kuhalalisha uamuzi wao wa kununua mitambo ya Dowans ambayo kisheria hairuhusiwi kufanya hivyo.

Alisema menejimenti imekuwa na ujanja ujanja mwingi kiasi cha kuizunguka kamati yake, na kuwasilisha maombi ya kununua mitambo hiyo kwa kamati nyingine ya Hesabu na Mashirika ya Umma (POC).

``Sisi tulitoa maoni, Tanesco ina ujanja wa aina fulani, sijui wanataka nini, kana kwamba kamati nyingine ina mamlaka ya kupokea rufani dhidi ya kamati nyingine,kuna aina fulani ya usanii kwenye uongozi wa Tanesco,`` alisema na kuongeza

``Kama wanataka kununua, wanunue…na sisi kazi yetu ni kusimamia tu na sio kuwaagiza kwamba wanunue au wakatae. Watakapoamua kununua wajue kwamba wanafanya hivyo kwa misingi ya kanuni na sheria, la sivyo watawajibika,`` alisema.

Akizungumzia mjadala wa ununuzi wa mitambo ya Dowans, Dk. Mwakyembe alisema anaona umepata sura ya kisiasa, na anaona kama ni mwendelezo wa Operesheni Sangara.

``Nimesikia na kusoma kuhusu Mwenyekiti wa POC, Zitto Kabwe kwamba kamati haijawasilikiliza Tanesco. Kamati ilikutana na Tanesco na Wizara 14 Desemba mwaka jana na kuwasikiliza, kwamba hatujawasikiliza hilo si kweli,`` alisema.



Kamati ya Nishati na Madini hawakuisikiliza TANESCO tarehe 14 kwani walisikiliza serikali. Taarifa za Bunge zinaonesha dhahiri kabisa kuwa TANESCO hawakusema katika kikao hicho kwani kamati ilipomsikiliza Waziri ikatoa uamuzi.

Naye mbunge wa Nzega CCM, Lucas Selelii, amesema hatua ya baadhi ya wabunge na viongozi wa serikali kupigia debe ununuzi wa mitambo ya kufua umeme ya kampuni ya Dowans kinyume na maamuzi ya Bunge, inaleta wasiwasi.


Alisema ana wasiwasi kwamba huenda kuna mkono wa mtu, anayeshinikiza kununuliwa kwa mitambo hiyo, kinyume na maazimio ya Bunge.

Hivi karibuni, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma, Zitto Kabwe, amenukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari akitaka Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) liinunue mitambo hiyo.

``Kuna mkono wa mtu, tena mkono wenyewe ni wa chuma, kwanini maamuzi yetu wenyewe tunayakanyaga, kama wanapinga, turudi bungeni,`` alisema Selelii jana wakati akizungumza na Nipashe kwa njia ya simu kutoka jimboni kwake.

suala hili halijawahi kupelekwa Bungeni. Ninaelewa kwa nini baadhi ya wajumbe wa Kamati hawataki mjadala huu kwani wanajua kuwa sehemu ya maamuzi yao yalikuwa sio sahihi na hayakufuata kanuni za Bunge.

Alisema suala la ununuzi wa mitambo hiyo lilitolewa kama pendekezo na Kamati Teule ya Bunge na kuridhiwa na Bunge kwamba mitambo hiyo isinunuuliwe.

Alisema kwanza, katika uchunguzi wa kamati hiyo iligundulika kwamba mitambo hiyo ni mibovu na pili gharama za ununuzi wake ni kubwa.

Kamati ya Nishati na Madini haijawahi kufanya uchunguzi kuhusu mitambo hii maana wao hawana utaalamu huo na wala fedha za kufanya uchunguzi wa kitaalamu. Iwapo Kamati mbili zingekutana na kuamua kufanya uchunguzi ingetakiwa Bunge litanagaze tender ya kupata consultant wa kufanya kazi hiyo. Hakuna taarifa Bungeni za uchunguzi huo ambao Selelii anasema walifanya na kugundua kuwa mitambo ni mibovu. TANESCO wao mefanya uchunguzi wa kitaalamu. Sasa tuwasikie wanasiasa au wataalamu?

Kwa mujibu wa Sheria ya Manunuzi ya Umma, ni makosa kwa serikali kununua vifaa ambazo vimetumika (mitumba).

Kipengele gani cha sheria ya manunuzi na katika mazingira yepi?

Alisema kiasi cha fedha ambacho kinatakiwa ili kununua mitambo hiyo, kinaweza kununua mitambo mingine mitatu yenye ukubwa na uwezo huo huo wa kuzalisha umeme.

Selelii alisema serikali inaweza kufanikisha ununuzi huo kwa kutuma barua pepe Marekani ambako mitambo hiyo hutengenezwa au inaweza kumpeleka ambaye atashughulikia ununuzi wake na hivyo kurudi nchini akiwa na mitambo mitatu.

Rhetorics ambazo hazitaipeleka nchi popote. Unawezaje kununua turbines kwa barua pepe? let us be serious

Alifafanua kwamba Kamati Teule ya Bunge ilikwisha kamilisha kazi na mapendekezo yake yaliridhiwa na Bunge na suala hilo sasa lipo chini ya Kamati ya Nishati na Madini ya Bunge.

Alisema atashangaa iwapo Kamati hiyo ambayo ipo chini ya Mwenyekiti, William Shellukindo, itakapokiuka maazimio ya Bunge.

Kwa upande wake, Mbunge wa Karatu, Chadema, Dk. Wilbrood Slaa, alisema kinachohitajika katika suala hili ni taarifa kwa taifa.

``Tunaingizwa katika mjadala, wakati hatujui yaliyomo kwenye Kamati ya Shellukindo na wala katika Kamati ya Zitto,`` alisema na kuhoji: ``Kwa nini kamati hizi mbili kila moja inashikilia msimamo wake.``

Alisema haijulikani serikali na Tanesco walikubaliana nini katika Kamati ya Zitto, na kuongeza kuwa ni vema kujadili suala ambalo mmoja amepewa taarifa zake.

Alisema hadi sasa hakuna mtu anayejua kwa uhakikia nini yaliyomo katika Kamati hizo, suala ambalo ni gumu kulijadili.

Slaa shows leadership here. Kwa nini kamati ya Nishati na Madini inakwepa kikao cha pamoja?

Alisema Kamati ya Mwakyembe ilitoa taarifa kuhusu mitambo ya kufua umeme ya Dowans, kwamba serikali inaweza kupata na kununua mitambo hiyo huko inakotengenezwa tena kwa bei nafuu.

Lakini alisema: ``Tunataka kujua maazimio ya Bunge kuhusu sakala la Richmond yamefikia wapi kwa sababu kwa mujibu wa Sheria ya Manunuzi ya Umma, iwapo mtu amebainika kughushi na kuingia mikataba, mali zake zinatakiwa kutaifishwa.``

Alihoji iwapo mkataba wa kufua umeme wa dharura kati ya Tanesco na kampuni ya Richmond, (sasa Dowans), ulibainika kuwa umeghushiwa, sheria imefuatwa ya kutaifisha mitambo hiyo.

Alisema badala yake kuzingatia taratibu hizo za kisheria, tunazungumzia hitaji la kununua mitambo hiyo.

Hata hivyo, alisema dharura hii ya umeme si ya leo, na ina tofauti gani na ile ya miaka iliyopita.

Juzi (Jumamosi), Mkurugenzi mtendaji wa Tanesco, Dk. Idris Rashid, alitoa taarifa kwenye vyombo vya habari kuelezea hali ya umeme katika Grid ya Taifa pamoja na mambo mengine, akapendekeza kuwa mtambo wote wa Dowans ununuliwe na serikali pamoja na vifaa vyote vya kuunganishia kwenye grid suala la ununuzi wa mitambo iliyotumia katika sheria ya Manunuzi iangaliwe kwa makini kwa manufaa ya sekta ya umeme na mbadala wa kununua mtambo wa Dowans ni kuagiza mara moja mitambo ya kukodisha ya umeme ya kiasi cha megawati 150 kwa njia ya dharura, ambayo inapaswa kuwepo kwa kipindi kisichopungua miaka miwili.

Mhe Zito:
Kila unapojaribu kujitetea ndio unavyozidi kujichafua..... nakushauri warudishie hela waliyokuhonga!!!!

Sijitetei ndugu yangu. Ninaweka facts clear. suala la kuhongwa sina haja ya kukujibu maana umeshajihaikishia hivyo na sina cha kukufanya.
 
Kwako Zitto

Swali kwako Zitto: Je hii kesi kati ya Dowans na Tanesco imeshakwisha na mamuzi yakoje? Mbona mitambo iliyoshikiliwa kwa kufidia kesi kamaTanesco watashinda sasa inauzwa kwa Tanesco wenyewe? Hapa kuna mkanganyiko na kila dalili za rushwa. Bwana Zitto hebu tupe maelezo kuhusu hili.

Hii ni hoja ya msingi sana. TANESCO ndio waliofungua kesi na ni TANESCO hao hao waliokuja kwenye kamati kutaka ridhaa ili wanunue mitambo hii. Swali hili to be frank halikuulizwa katika kamati na hivyo litatusaidia kwenye kikao cha kamati mbili. Tutawauliza TANESCO swali hili. Ni zuri sana. Maana kesi iliyopo mahakamani ni kesi ya mkataba na sio kesi ya mitambo. TANESCO walishikilia kwa ajili ya fidia. Sasa wakishanunua na kesi ikahitaji fidia na mitambo wameshanunua inakuwaje? Asante sana kwa hoja hii
 
Umeniwekea maneno. Ninasimamia uamuzi wa kamati yangu kuliangalia suala hili objectively na kama nchi itafaidika mitambo inunuliwe. Kama kuna mitambo ya bei nafuu zaidi na mizuri zaidi MIPYA inunuliwe.

I am never a dictator, but a bold leader. I am able to tell people what they dont want to hear. I always subordinate my personal interest to those of the nation. Always and i can prove that. I stand to be counted

I am never materialist. I am never corrupt. I am genuine. I am honest. I speak my mind. Never been slippery.

Facts peke yake ndio zinanifanya nibadili msimamo. Sio hisia za kupoteza umaarufu nk. Umaarufu nilionao (kama ninao) ni earned popularity, na sio sought! Siwezi kuogopa kuchukua maamuzi eti kwa sababu ya kupoteza umaarufu. Kama ni maamuzi magumu na ninaamini ni sahihi nitachukua na one day the truth will be known. Truth prevails.


Kijana unajiona una akili sana kuliko sisi wote jamvini hapa kwa sababu tu wewe mbunge, unataka sisi wote tuwe wabunge? Itawezekana?.
Kama uliwaambia wenzio mafisadi basi wewe ndio FISADI na JAMBAZI mkubwa wa mali ya watanzania.

Tena rushwa yako kama ya polisi dogo sana, "HUMMER", Unakubali kupoteza utu wako kwa sababu ya gari.??????? kama siyo Ulimbukeni ni nini?
 
Hivi Ndugu/Mbunge Zito ni Strategy ya Energy ya Tanzania? Na nakumbuka Serikali ilitoa fedha kwa ajili ya umeme wa dharura au kama nimekosea bado serikali inaweza ki-gurantee tanesco kupata mikopo ya ki-maendeleo, sasa kama yawezekana nini hatua za serikali ku-chukua hatua zifaazo.
Pili Uganda ni nchi ya kibepari zaidi kuliko sisi na hii issue ya serikali kujitoa katika mambo fulani fulani, je inakuwaje sisi kitu sensitive kama hichi tumeshindwa kufanya Project kama za wenzetu Uganda? na in time. Maana kama ubinafsi shaji Uganda nao walikuwa na PSRC yao but the name was different. Na nmajua wewe kama Mbunge/Kiongozi /msomi huwa unajisomea na kujaribu kulinganisha mambo ya Tanzania na nchi zingine ili uone ni jinsi gani tunaweza kuboresha mambo yetu.
 
Zitto,
inakuwaje mbunge wa jimbo masikini na lilolo nyuma kimaendelea ukaendekeza ufahari na anasa kuendesha HUMMER? umelifanyia nini jimbo langu tangu uchaguliwe? tafadhali kajibu hoja inayohusu maendeleo ya Kigoma.
 
Back
Top Bottom