Don't bet against Magufuli, utaliwa...

Don't bet against Magufuli, utaliwa...

Tunataka na waliohusika na ufisadi wa kivuko kibovu,uuzaji wa nyumba za serikali,meremeta,kagoda,n.k nao wafikishwe mahakamani pamoja na wale waliochota mabilionoi ya Escrow kupitia Stanbic kwenye mifuko ya sandarusi.
We jamaa utahamisha magoli mpaka na familia yakonutaihamisha!!
 
Tatizo kesi za ufisadi huwaga zinacreat attention kubwa mwisho wa siku inatoka hukumu ya kijinga, yaani haina tofauti na watu walioalikwa ktk sherehe alafu wanafanyiwa surprise ya kunawisha mikono na mafuta ya kula, vichwani mwao wanajua labda Kuna vinono kumbe MAFENESI.Ila naipongeza serikali kwa 50%, 50% nyingine na baki nayo manake yasijekuwa yale ya MRAMBA na YONA.
 
Kwa wewe mleta mada unayeshabikia siasa za kujipendekeza kwako hii ni point ya kisiasa dhidi ya wapinzani wako na fursa kujipendekeza upate cheo. Kwa mtanzania anayeipenda nchi yake hii ni historia muhimu sana kwa nchi yetu kuwa kila fisadi litaonja jela bila kujali itikadi. Katika maamuzi magumu kama haya ni bora watanzania kuungana na kuipa support serikali kuliko watu kutugawa kwa lengo la kupata sifa za kisiasa
 
Utaratibu kuwachuchumalisha na kuwapigisha magoti??? Duh!
Kukuchumalisha ni njia ya usalama kwa mahabusu.Mahabusu anapokuwa mahakamani hatakiwi kufungwa pingu,labda kwa sababu maalumu,ili kulinda usalama wa mahabusu wanapokuwa transi(kutoka chumba cha mahabusu mahakamani,kumsubiri hakimu)lazima wachuchumae ili waweze kudhibitiwa vizuri.
Huyu kalasinga akitimua mbio akiingia mitaa ya uhindini huko nani atampata
 
Ndiyo yeye Kenya walimshindwa ila hapa TZ hachomoki!

Mkuu;
Chonde chonde; kwetu kuna kamsemo; Kuona ganda la ndizi zio kuila. Umetangulia kutuhabarisha kuwa; Wenzetu Kenya walimshindwa. Hukumbuki ni nini kilimtoa kwenye lile tundu la sindano?? Huyu jamaa hali peke yake. Kumbuka kuwa, wale waliobeba mihela kwa mifuko ya sandarusi kutoka pale Bank hadi leo, hata tu kuwataja majina yao ni kukufuru. Upo hapo?? Huwezi mwita mama mkwe wako kwa jina lake. Leo, Sigh atawatajaje hao waliojibebea mihela ile?? Sio rahisi kama ufikiriavyo. Aweza chomoka hivi hivi ukimuangalia na ukaambiwa, ni marufuku kufukua kaburi lake
 
Mzee Mwanakijiji naona siku hizi unatembea mulemule kwa Global Publisher, weredi kwishnei ni mwendo wa mipasho tu siku hizi.

Kweli kwenye mapambano ya madawa ya kulevya hakuna kichwa kitaachwa salama

Mtazamo tu mkuu
 
Mkuu;
Chonde chonde; kwetu kuna kamsemo; Kuona ganda la ndizi zio kuila. Umetangulia kutuhabarisha kuwa; Wenzetu Kenya walimshindwa. Hukumbuki ni nini kilimtoa kwenye lile tundu la sindano?? Huyu jamaa hali peke yake. Kumbuka kuwa, wale waliobeba mihela kwa mifuko ya sandarusi kutoka pale Bank hadi leo, hata tu kuwataja majina yao ni kukufuru. Upo hapo?? Huwezi mwita mama mkwe wako kwa jina lake. Leo, Sigh atawatajaje hao waliojibebea mihela ile?? Sio rahisi kama ufikiriavyo. Aweza chomoka hivi hivi ukimuangalia na ukaambiwa, ni marufuku kufukua kaburi lake

Hiki ndicho ninachozungumzia; mbele ya Magufuli Singh itabidi aaumue alale nacho au azungumze. Nilivyomuona tu leo ile hofu aliyokuwa nayo inakuambia ataimba kama kasuku...
 
Nimeota TZ tumezindua noti ya shilingi laki moja ina picha ya Magu anacheka na kwa nyuma imeandikwa hapa kazi tuu
 
Utaratibu kuwachuchumalisha na kuwapigisha magoti??? Duh!
Hahahahaha. Mmeanza kuwatetea. Nyie akina Tobo Lisu nyie mungu anawaona.

Kwa hiyo kwa hadhi yao haikutakiwa kuchuchumalishwa?
Hakuna umaarufu ukishaitwa accused
 
One cannot bet against someone who does not know his own position.

Of course don't bet against Magufuli.

He is like a non collapsing quantum wave, able to exist and not exist at once, to be against and for corruption at once, to be magnificently game changing and despicably ill prepared at once.

How do you even to bet against someone who knows no rules and makes everything as he goes along?
Well, many politicians and lawyers of great repute have predicted gloom and doom for Magufuli from day one. Many fell on their faces.

MMK is just reminding the likes of them not to engage in fools errands anymore.
 
Back
Top Bottom