Dodoma: Rais Samia anazindua Mkakati wa Uhamasishaji wa Sensa ya Watu na Makazi 2022

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,947
141,922
Tukio liko mubashara ITV, TBC na Channel ten

Rais Samia anazindua zoezi la uelimishaji na uhamasishaji wa sensa ya watu na makazi 2022 katika uwanja wa Jamhuri Dodoma.

=====

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amesema bila kuwa na hesabu au takwimu sahihi, haiwezekani kugawa rasilimali na kutoa huduma kwa Haki na uwiano

Amesema hayo leo Jijini Dodoma katika uzinduzi wa Mkakati wa Uelishaji na Uhamasishaji wa Sensa ya Watu na Makazi mwaka 2022

Amesema, "Huwezi kushughulikia changamoto ya Ajira endapo hujui watu wasio na Ajira. Huwezi kupelekea huduma na kushughulikia matatizo ya watu wenye mahitaji maalum kama Wazee na wenye Ulemavu"

Rais ametoa wito kwa Watanzania wote kujiandaa kuhesabiwa zoezi la Sensa litakapoanza akisema, ili mchakato huo uweze kukidhi mahitaji ya kufanikisha malengo ni lazima watu wote washirikishwe

Kuhusu hoja za kwanini Tanzania iingie kwenye zoezi hilo na kutumia fedha zilizopangwa amesema "Nimekuwa nikiona hoja hizo zikipita na kuulizwa. Sababu ni kwamba kama tunaweza kufanya wenyewe na kupata idadi yetu kwanini tutumie idadi inayotolewa na Vyombo vingine vya Kimataifa?"

Pia amesema zoezi hilo likifanyika taarifa za majengo, nyumba na hesabu ya watu katika kila Kitongoji

F16BC686-48AB-4825-9212-DDFD39C9127F.jpeg


D7492804-604E-4222-A120-BAC03A2B84D6.jpeg


254F78C5-0EF5-491B-B9D0-2E6AAECE88F8.jpeg
 
Tunaendelea kufuatilia atakaloongea mtukufu rais katika uzinduzi wa uhamasishaji wa sensa ya watu na makazi
 
Haka kamama hakana swaga kabisa.
Kamepoa mnoo kisiasa.
Kadri muda unavyozidi kwenda kanazidi kupotezewa na watu.
Ipo siku katazira kufanya ziara na kuzindua.
 
Yaani antony mtaka anawahamasisha watu kwa shangwe lakini watu na uwanja umepoa ....Dah mpaka huruma yaani.
 
Ni zoezi muhimu sana kwa Taifa letu kwa ajili ya maendeleo yetu. Naamini Rais wetu Hangaya Samia Suluhu Hassan atalifanikisha tofauti na aliyokumbana nayo JK. Muhimu wasirikishe zaidi zaidi viongozi wa dini na muepuke ubaguzi wa kivyama hasa wakati wa kugawa vibarua kwa wasimamizi mbalimbali. Hii sio nchi ya Wana CCM pekee na tujue na tuamini hivyo kila wakati. Maendeleo hayana vyama wala dini. Kazi iendelee HE Hangaya.
 
... kutakuwa na swali la dini sensa ijayo? Sheikh Ponda anawacheki tu!
 
Ni zoezi muhimu sana kwa Taifa letu kwa ajili ya maendeleo yetu. Naamini Rais wetu Hangaya Samia Suluhu Hassan atalifanikisha tofauti na aliyokumbana nayo JK. Muhimu wasirikishe zaidi zaidi viongozi wa dini na muepuke ubaguzi wa kivyama hasa wakati wa kugawa vibarua kwa wasimamizi mbalimbali. Hii sio nchi ya Wana CCM pekee na tujue na tuamini hivyo kila wakati. Maendeleo hayana vyama wala dini. Kazi iendelee HE Hangaya.
Ni kweli nchi hii ni yetu sote!
 
Hivi Maja yuko wapi?
Na yule mpango kazi zao hizi, afadhali Maja anaonekana kuzindua visima.
Makamu ni unfit wangemwacha apumzike tu kwanza maana kila nikimskiliza akipewa mike no ni kama wanamwonea tu.
Apumzishwe ahudumiwe
 
Tunataka katiba mpya yeye anatuletea sensa NI bora hizo pesa angemalizia mchakato wa katiba
 
There goes our hard earned Cash.....

Katika uelimishaji huu tusingatie ubanaji matumizi (in this day and age tunaweza kuelemisha kwa gharama ndogo tu)
 
Back
Top Bottom