johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 83,947
- 141,922
Tukio liko mubashara ITV, TBC na Channel ten
Rais Samia anazindua zoezi la uelimishaji na uhamasishaji wa sensa ya watu na makazi 2022 katika uwanja wa Jamhuri Dodoma.
=====
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amesema bila kuwa na hesabu au takwimu sahihi, haiwezekani kugawa rasilimali na kutoa huduma kwa Haki na uwiano
Amesema hayo leo Jijini Dodoma katika uzinduzi wa Mkakati wa Uelishaji na Uhamasishaji wa Sensa ya Watu na Makazi mwaka 2022
Amesema, "Huwezi kushughulikia changamoto ya Ajira endapo hujui watu wasio na Ajira. Huwezi kupelekea huduma na kushughulikia matatizo ya watu wenye mahitaji maalum kama Wazee na wenye Ulemavu"
Rais ametoa wito kwa Watanzania wote kujiandaa kuhesabiwa zoezi la Sensa litakapoanza akisema, ili mchakato huo uweze kukidhi mahitaji ya kufanikisha malengo ni lazima watu wote washirikishwe
Kuhusu hoja za kwanini Tanzania iingie kwenye zoezi hilo na kutumia fedha zilizopangwa amesema "Nimekuwa nikiona hoja hizo zikipita na kuulizwa. Sababu ni kwamba kama tunaweza kufanya wenyewe na kupata idadi yetu kwanini tutumie idadi inayotolewa na Vyombo vingine vya Kimataifa?"
Pia amesema zoezi hilo likifanyika taarifa za majengo, nyumba na hesabu ya watu katika kila Kitongoji
Rais Samia anazindua zoezi la uelimishaji na uhamasishaji wa sensa ya watu na makazi 2022 katika uwanja wa Jamhuri Dodoma.
=====
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amesema bila kuwa na hesabu au takwimu sahihi, haiwezekani kugawa rasilimali na kutoa huduma kwa Haki na uwiano
Amesema hayo leo Jijini Dodoma katika uzinduzi wa Mkakati wa Uelishaji na Uhamasishaji wa Sensa ya Watu na Makazi mwaka 2022
Amesema, "Huwezi kushughulikia changamoto ya Ajira endapo hujui watu wasio na Ajira. Huwezi kupelekea huduma na kushughulikia matatizo ya watu wenye mahitaji maalum kama Wazee na wenye Ulemavu"
Rais ametoa wito kwa Watanzania wote kujiandaa kuhesabiwa zoezi la Sensa litakapoanza akisema, ili mchakato huo uweze kukidhi mahitaji ya kufanikisha malengo ni lazima watu wote washirikishwe
Kuhusu hoja za kwanini Tanzania iingie kwenye zoezi hilo na kutumia fedha zilizopangwa amesema "Nimekuwa nikiona hoja hizo zikipita na kuulizwa. Sababu ni kwamba kama tunaweza kufanya wenyewe na kupata idadi yetu kwanini tutumie idadi inayotolewa na Vyombo vingine vya Kimataifa?"
Pia amesema zoezi hilo likifanyika taarifa za majengo, nyumba na hesabu ya watu katika kila Kitongoji