Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,437
- 5,235
Mahakama Kuu ya Tanzania, Masijala Kuu Dodoma, imetoa muda wa siku tano kwa Serikali kujibu kesi iliyofunguliwa na chama cha ACT Wazalendo na mwanachama wake, Luhaga Joelson Mpina, dhidi ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Katika kesi hiyo, ACT Wazalendo na Mpina wanadai kuwa INEC ilikiuka Katiba, Sheria na Kanuni za Uchaguzi wakati wa mchakato wa uteuzi wa wagombea wa Urais uliofanyika Agosti 27, 2025.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, maamuzi ya karibuni yametolewa tarehe 28 Agosti 2025, Jaji wa Mahakama Kuu amesema Mahakama imeipa Serikali muda wa siku tano pekee kujibu madai ya ACT na kwamba ombi la upande wa Serikali la kuongezewa siku 14 kwa ajili ya kuwasilisha majibu limekataliwa.
Soma Pia: ACT wanaituhumu INEC kuwa ni aibu kwa tume kumzuia mpina kurejesha fomu
Aidha, Mahakama imebainisha kuwa endapo itajiridhisha kuwa INEC ilikiuka Katiba, Sheria na Kanuni katika kumzuia Mpina kurejesha fomu, inaweza kutoa amri ya kumpa fursa ya kurejesha fomu na kuteuliwa kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Katika uamuzi huo, Mahakama pia imesisitiza maslahi mapana ya kitaifa yaliyomo kwenye kesi hiyo.
“Kwa kuzingatia kuwa shauri hili lina maslahi mapana ya kitaifa na umma, Mahakama imetoa maagizo kwamba kesi itatajwa na kuanza kusikilizwa kwa njia ya mtandao tarehe 3 Septemba 2025, saa 3:00 asubuhi. Wananchi wote wamekaribishwa kufuatilia mwenendo wa kesi kupitia kiunganishi (link) kitakachotolewa na Mahakama”, imeeleza taarifa ya ACT.
Mapema katika matamko yake, ACT-Wazalendo ilieleza kuwa uamuzi wa INEC unakwenda kinyume na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Sheria za Uchaguzi na haki za kiraia za mgombea. Chama hicho kimeiomba Mahakama kutoa amri ya dharura ya kusitisha utekelezaji wa uamuzi huo ili kumruhusu Mpina kuendelea na mchakato wa kugombea Urais.
Chanzo: Jambotv
Katika kesi hiyo, ACT Wazalendo na Mpina wanadai kuwa INEC ilikiuka Katiba, Sheria na Kanuni za Uchaguzi wakati wa mchakato wa uteuzi wa wagombea wa Urais uliofanyika Agosti 27, 2025.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, maamuzi ya karibuni yametolewa tarehe 28 Agosti 2025, Jaji wa Mahakama Kuu amesema Mahakama imeipa Serikali muda wa siku tano pekee kujibu madai ya ACT na kwamba ombi la upande wa Serikali la kuongezewa siku 14 kwa ajili ya kuwasilisha majibu limekataliwa.
Soma Pia: ACT wanaituhumu INEC kuwa ni aibu kwa tume kumzuia mpina kurejesha fomu
Aidha, Mahakama imebainisha kuwa endapo itajiridhisha kuwa INEC ilikiuka Katiba, Sheria na Kanuni katika kumzuia Mpina kurejesha fomu, inaweza kutoa amri ya kumpa fursa ya kurejesha fomu na kuteuliwa kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Katika uamuzi huo, Mahakama pia imesisitiza maslahi mapana ya kitaifa yaliyomo kwenye kesi hiyo.
“Kwa kuzingatia kuwa shauri hili lina maslahi mapana ya kitaifa na umma, Mahakama imetoa maagizo kwamba kesi itatajwa na kuanza kusikilizwa kwa njia ya mtandao tarehe 3 Septemba 2025, saa 3:00 asubuhi. Wananchi wote wamekaribishwa kufuatilia mwenendo wa kesi kupitia kiunganishi (link) kitakachotolewa na Mahakama”, imeeleza taarifa ya ACT.
Mapema katika matamko yake, ACT-Wazalendo ilieleza kuwa uamuzi wa INEC unakwenda kinyume na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Sheria za Uchaguzi na haki za kiraia za mgombea. Chama hicho kimeiomba Mahakama kutoa amri ya dharura ya kusitisha utekelezaji wa uamuzi huo ili kumruhusu Mpina kuendelea na mchakato wa kugombea Urais.
Chanzo: Jambotv