Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,815
- 11,992
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akiwaapisha viongozi wateule Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma leo tarehe 27 Februari, 2023
Dr. Tulia Ackson
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Tulia Ackson amewaasa viongozi wote walioapa leo akiwemo Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi kusoma na kuielewa vyema Ilani ya Chama cha Mapinduzi ili waweze kutekeleza majukumu yao vizuri kama sehemu ya kumuunga mkono Rais Samia na Serikali yake. Amesema kwa kuwa Rais amewaaamini, wanapaswa pia kurudisha imani hiyo kwa wananchi.
Pia, amewataka kutunza ahadi ya kiapo pamoja na Kumshauri Rais kwa hekima. Kiapo hakijasema kitaisha lini hivyo wanapaswa kuendelea kutunza siri Maisha yao yote.
Samia Suluhu Hassan
Rais Samia amesema alidhani atamaliza Mhula wake na Baraza lilelile la Mawaziri lakini haijakuwa hivyo, ndio maana amemteua Mhe. Ulega kuchukua nafasi.
Amewapongeza wote walioapa, amesema kuwa siyo kwamba waliochanguliwa/kubaki hawana makosa, bali yeye kama mama anawalea.
Mabadiliko haya pia yameingiza watu waliokuwa nje ya Serikali ili kuwafanya walete ujuzi wao. Amesema kila anayeonekana ana akili zaidi atanyofolewa aliko ili aingie Serikalini kuongeza uzoefu.
Ameeleza mpango wake wa kuanzisha wizara mpya ambazo zitatangazwa pindi mambo ya kisheria yatakapokaa sawa.
Akitaja sababu za kufanya mabadiliko haya, amesema kuwa Kutokuelewana kati ya watendaji ni miongoni mwa sababu zilizomfanya abadili Watendaji wa Wizara. Amesema hapendi tabia hii na ikiwa itatokea tena, wahusika wote wa mgogoro huo atawaondoa.
Dr. Tulia Ackson
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Tulia Ackson amewaasa viongozi wote walioapa leo akiwemo Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi kusoma na kuielewa vyema Ilani ya Chama cha Mapinduzi ili waweze kutekeleza majukumu yao vizuri kama sehemu ya kumuunga mkono Rais Samia na Serikali yake. Amesema kwa kuwa Rais amewaaamini, wanapaswa pia kurudisha imani hiyo kwa wananchi.
Pia, amewataka kutunza ahadi ya kiapo pamoja na Kumshauri Rais kwa hekima. Kiapo hakijasema kitaisha lini hivyo wanapaswa kuendelea kutunza siri Maisha yao yote.
Samia Suluhu Hassan
Rais Samia amesema alidhani atamaliza Mhula wake na Baraza lilelile la Mawaziri lakini haijakuwa hivyo, ndio maana amemteua Mhe. Ulega kuchukua nafasi.
Amewapongeza wote walioapa, amesema kuwa siyo kwamba waliochanguliwa/kubaki hawana makosa, bali yeye kama mama anawalea.
Mabadiliko haya pia yameingiza watu waliokuwa nje ya Serikali ili kuwafanya walete ujuzi wao. Amesema kila anayeonekana ana akili zaidi atanyofolewa aliko ili aingie Serikalini kuongeza uzoefu.
Ameeleza mpango wake wa kuanzisha wizara mpya ambazo zitatangazwa pindi mambo ya kisheria yatakapokaa sawa.
Akitaja sababu za kufanya mabadiliko haya, amesema kuwa Kutokuelewana kati ya watendaji ni miongoni mwa sababu zilizomfanya abadili Watendaji wa Wizara. Amesema hapendi tabia hii na ikiwa itatokea tena, wahusika wote wa mgogoro huo atawaondoa.