figganigga
Platinum Member
- Oct 17, 2010
- 26,654
- 59,077
*Amebainisha kuwa matokeo ya mwaka huu yanaonesha wazi dhamira ya wananchi ya kusonga mbele kwa umoja na maendeleo.
Rais Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amekabidhiwa rasmi Hati ya Kuchaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tukio linaloashiria kuanza kwa mhula mpya wa uongozi utakaodumu hadi mwaka 2030.
Kwenye hotuba yake ya kwanza, Dkt. Samia ameishukuru Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Msajili wa Vyama vya Siasa, vyombo vya Ulinzi na usalama, pamoja na wagombea wenzake wa kiti cha urais kwa namna walivyoshiriki katika mchakato wa uchaguzi mkuu kwa amani
Rais Mteule, katika hotuba hiyo, amesema kuwa uchaguzi wa mwaka huu ni wa kihistoria, kwani Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imewezesha wagombea wote kuzunguka pande zote za Tanzania. Aidha, amebainisha kuwa matokeo ya mwaka huu yanaonesha wazi dhamira ya wananchi ya kusonga mbele kwa umoja na maendeleo.
Vilevile, Dkt. Samia ametoa ahadi kwa niaba yake na Makamu wa Rais Mteule, Dkt. Nchimbi, akisema "Mimi pamoja na Makamu wa Rais SAN Mteule, Dkt. Nchimbi, tunakwenda kufanya kile tulichoahidi kukifanya ambacho tumekubaliana ndani ya Ilani yetu ya Chama cha Mapinduzi (CCM)." Alisema Rais Mteule.
Hafla hiyo ya kihistoria imefanyika, Novemba 1, 2025, jijini Dodoma, na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kitaifa na kimataifa, wawakilishi wa taasisi za umma na binafsi.
Rais Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amekabidhiwa rasmi Hati ya Kuchaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tukio linaloashiria kuanza kwa mhula mpya wa uongozi utakaodumu hadi mwaka 2030.
Kwenye hotuba yake ya kwanza, Dkt. Samia ameishukuru Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Msajili wa Vyama vya Siasa, vyombo vya Ulinzi na usalama, pamoja na wagombea wenzake wa kiti cha urais kwa namna walivyoshiriki katika mchakato wa uchaguzi mkuu kwa amani
Rais Mteule, katika hotuba hiyo, amesema kuwa uchaguzi wa mwaka huu ni wa kihistoria, kwani Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imewezesha wagombea wote kuzunguka pande zote za Tanzania. Aidha, amebainisha kuwa matokeo ya mwaka huu yanaonesha wazi dhamira ya wananchi ya kusonga mbele kwa umoja na maendeleo.
Vilevile, Dkt. Samia ametoa ahadi kwa niaba yake na Makamu wa Rais Mteule, Dkt. Nchimbi, akisema "Mimi pamoja na Makamu wa Rais SAN Mteule, Dkt. Nchimbi, tunakwenda kufanya kile tulichoahidi kukifanya ambacho tumekubaliana ndani ya Ilani yetu ya Chama cha Mapinduzi (CCM)." Alisema Rais Mteule.
Hafla hiyo ya kihistoria imefanyika, Novemba 1, 2025, jijini Dodoma, na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kitaifa na kimataifa, wawakilishi wa taasisi za umma na binafsi.