Dkt. Ndugulile: Uchaguzi wa 2020 ulikuwa na dosari ambayo hatuwezi kuificha, siungi Mkono kupita bila kupingwa

Heparin

Senior Member
Sep 24, 2021
127
420
"Uchaguzi wa 2020 ulikuwa na dosari ambayo hatuwezi kuificha, haiwezekani wagombea wa upinzani tu ndio hawakujua kujaza fomu ipasavyo halafu wagombea wa CCM wakaweza kujaza fomu ipasavyo kila mahali” Dkt. Faustine Ndugulile.

Ndugulile amesema haungi mkono suala la wagombea kupita bila kupingwa “Mtu kama unajiamini kwa nini upite pasipo ushindani..?”

Hata hivyo Ndugulile amesema alikuwa na uhakika wa kuwashinda wapinzani wake kwenye uchaguzi wa ndani ya CCM akiwemo aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Bw Paul Makonda, ambaye kwa sasa ni katibu muenezi wa CCM Taifa.

“Mimi sijawai kuwa na uchaguzi rahisi kigamboni na uwa sipendi uchaguzi mwepesi, hata 2015 niligombea na vigogo wengi akiwemo mtoto wa Rais Mkapa lakini nilishinda” Ndugulile.

 
Back
Top Bottom