Dkt. Mpango: 26.4% ya Watanzania wanaishi chini ya kiwango cha umasikini wa kipato

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,814
11,991


Dkt. Philip Mpango, Makamu wa Rais wa Tanzania amesema “Malengo makuu ya dira ya Mwaka 2025, Maisha bora kwa kila Mtanzania, Kudumisha amani, usalama na umoja katika Nchi, Utawala bora, Jamii iliyoelimika vyema na inayojifunza, tano ni uchumi imara na shindani.”

Pamoja na hatua kubwa ambayo Nchi imepiga bado kuna changamoto mbalimbali zilizosababisha malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2000-2025 kutofikiwa kikamilifu mfano:

“Changamoto ya umasikini wa kipato na lishe duni, kwa mujibu wa utafiti wa Mapato na Kaya, takribani 26.4% ya Watanzania wanaishi chini ya kiwango cha umasikini wa kipato, ambayo ni zaidi ya Robo na Wananchi masikini zaidi wanaishi vijijini 31.3%.

Kuna mikoa, nitataja michache Kagera, Kigoma, Singida, Tabora na Dodoma ambayo kiwango cha umasikini ni kikubwa zaidi kwa sababu mbalimbali kutokana ikiwemo matatizo ya Kihistoria na miundombinu duni.

Aidha, tofauti ya kipato miongoni mwa Watanzania imeendelea kuongezeka licha ya kufanya vizuri katika kigezo cha kufanya vizuri uchumi jumla.

Kiwango cha tofauti ya kipato kwa kutumia kipimo cha uwiano kiliongezeka kutoka 0.34 Mwaka 2011/12 mpaka 0.38 Mwaka 2017/18.

Katika kipindi kama hicho, kipimo hicho cha tofauti ya kipato kwa maeneo ya Mijini nacho kiliongezeka kutoka 0.37 hadi 0.41.

30% ya Watoto chini ya miaka mitano wana udumavu Nchini
Akizungumza katika uzinduzi wa Mchakato wa Maandalizi ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mpango amesema takwimu hizo ni kwa mujibu wa utafiti wa Mapato na Kaya.

Amesema “Utafiti wa Afya ya Uzazi na Mtoto na viashiria vya Malaria kwa Mwaka 2022 unaonesha kuwa 30% ya Watoto wenye Umri chini ya miaka mitano wana udumavu na 9% ya Watoto wana udumavu mkali.”


Dkt. Mpango: Elimu yetu haikidhi mahitaji ya soko la ajira
Kwa upande wa kuwa na jamii iliyoelimika na inayojifunza, tumepata mafanikio ya kuridhisha ikiwemo kuongezeka kwa Wanafunzi katika ngazi zote za elimu.

Viwango vya ufaulu vimeongezeka, uwezo wa kusoma na kuandika Nchini unakadiriwa kuwa 92%.

Pamoja na mafanikio hayo bado vijana wengi wanaomaliza masomo hawapati fursa za ajira, pia elimu yetu haikidhi mahitaji ya soko la ajira wala kuwezesha wahitimu kujiajiri.

Jitihada za kurekebisha hali hiyo zinaendelea ikiwemo kupitia sera ya elimu na mitaala.
 
Kwamba Robo ya Watanzania ni masikini

Wahaya
Wanyaturu
Wagogo
Wanyamwezi
Waha

Tatizo ya hiyo mikoa haitaki kuchangamana na mikoa mingine, wanaweka ukabila sana
 
Kwamba Robo ya Watanzania ni masikini

Wahaya
Wanyaturu
Wagogo
Wanyamwezi
Waha

Tatizo ya hiyo mikoa haitaki kuchangamana na mikoa mingine, wanaweka ukabila sana
Hakuna sababu ya umaskini kama hiyo ...Jaribu kuwa huru kutoa maoni hakuna anayefurahi so jaribu kufanya utafiti utajua
 


Dkt. Philip Mpango, Makamu wa Rais wa Tanzania amesema “Malengo makuu ya dira ya Mwaka 2025, Maisha bora kwa kila Mtanzania, Kudumisha amani, usalama na umoja katika Nchi, Utawala bora, Jamii iliyoelimika vyema na inayojifunza, tano ni uchumi imara na shindani.”

Pamoja na hatua kubwa ambayo Nchi imepiga bado kuna changamoto mbalimbali zilizosababisha malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2000-2025 kutofikiwa kikamilifu mfano:

“Changamoto ya umasikini wa kipato na lishe duni, kwa mujibu wa utafiti wa Mapato na Kaya, takribani 26.4% ya Watanzania wanaishi chini ya kiwango cha umasikini wa kipato, ambayo ni zaidi ya Robo na Wananchi masikini zaidi wanaishi vijijini 31.3%.

Kuna mikoa, nitataja michache Kagera, Kigoma, Singida, Tabora na Dodoma ambayo kiwango cha umasikini ni kikubwa zaidi kwa sababu mbalimbali kutokana ikiwemo matatizo ya Kihistoria na miundombinu duni.

Aidha, tofauti ya kipato miongoni mwa Watanzania imeendelea kuongezeka licha ya kufanya vizuri katika kigezo cha kufanya vizuri uchumi jumla.

Kiwango cha tofauti ya kipato kwa kutumia kipimo cha uwiano kiliongezeka kutoka 0.34 Mwaka 2011/12 mpaka 0.38 Mwaka 2017/18.

Katika kipindi kama hicho, kipimo hicho cha tofauti ya kipato kwa maeneo ya Mijini nacho kiliongezeka kutoka 0.37 hadi 0.41.

30% ya Watoto chini ya miaka mitano wana udumavu Nchini
Akizungumza katika uzinduzi wa Mchakato wa Maandalizi ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mpango amesema takwimu hizo ni kwa mujibu wa utafiti wa Mapato na Kaya.

Amesema “Utafiti wa Afya ya Uzazi na Mtoto na viashiria vya Malaria kwa Mwaka 2022 unaonesha kuwa 30% ya Watoto wenye Umri chini ya miaka mitano wana udumavu na 9% ya Watoto wana udumavu mkali.”


Dkt. Mpango: Elimu yetu haikidhi mahitaji ya soko la ajira
Kwa upande wa kuwa na jamii iliyoelimika na inayojifunza, tumepata mafanikio ya kuridhisha ikiwemo kuongezeka kwa Wanafunzi katika ngazi zote za elimu.

Viwango vya ufaulu vimeongezeka, uwezo wa kusoma na kuandika Nchini unakadiriwa kuwa 92%.

Pamoja na mafanikio hayo bado vijana wengi wanaomaliza masomo hawapati fursa za ajira, pia elimu yetu haikidhi mahitaji ya soko la ajira wala kuwezesha wahitimu kujiajiri.

Jitihada za kurekebisha hali hiyo zinaendelea ikiwemo kupitia sera ya elimu na mitaala.

Hivi kweli viongozi hawana hofu ya Mungu au huwahawanaga aibu kwa nchi yao kuwa na umasikini wakati uwezo wa kuutoa huo umasikini wanao, wanapotembelea nchi zingine huko duniani huwa hawaoni aibu huku kwao ni umasikini mkubwa, Mimi kwa miaka kama tisa nimefanya kazi singida wilaya sote na tabora kwakweli raia wanaishi kwa kudra za Muumba waowanateseka mno viongozi mkipewa fursa za kuwatumikia wananchi muwatumikiye na viongozi wainueni ndugu na jamaa wote ulionauwezo nao
 
Hivi kweli viongozi hawana hofu ya Mungu au huwahawanaga aibu kwa nchi yao kuwa na umasikini wakati uwezo wa kuutoa huo umasikini wanao,
Mungu wako si mungu wao. Wanachofanya ndio haswa wanatekeleza malengo na matakwa ya mungu wao.

Siku yao haiko mbali sana, wacha waendelee kututesa.
 
Kuna umasikini gani mwingine zaidi ya umasikini wa kipato??
Umaskini wa akili huzaa umaskini wa kipato?

La! "umaskini" ni sawa na "ufukara"?

Kukosa uongozi wenye dira, ni "umaskini"?

Kwani "kukosa kipato" husababishwa na nini?

Nikifika kwako na kukunyang'anya kila ulicho nacho na kinachokuingizia "kipato" nitakusababishia "umaskini"?
(Tafadhali, sina maana ya kutumia maguvu ya mwili, ninaweza kutumia njia mbalimbali katika unyang'anyi)

Ni baadhi ya maswali tu, mkuu 'Yoda' yanayozuka kwenye mijadala kama hii.
 
Hivi kweli viongozi hawana hofu ya Mungu au huwahawanaga aibu kwa nchi yao kuwa na umasikini wakati uwezo wa kuutoa huo umasikini wanao, wanapotembelea nchi zingine huko duniani huwa hawaoni aibu huku kwao ni umasikini mkubwa, Mimi kwa miaka kama tisa nimefanya kazi singida wilaya sote na tabora kwakweli raia wanaishi kwa kudra za Muumba waowanateseka mno viongozi mkipewa fursa za kuwatumikia wananchi muwatumikiye na viongozi wainueni ndugu na jamaa wote ulionauwezo nao
Nimekusoma na nimeguswa na ushuhuda wako.
Mkuu, tunao hadi maprofesa kabisa kama akina kapuya/Lipumba wanaoyaelewa vizuri sana haya mambo. Siyo kwamba nchi hii inao tena upungufu wa watu walio na elimu ya kuinua hali za wananchi wake wote.
Raslimali ipo ya kutosha kabisa kubadili hali hizo ulizoziona huko ulikotembelea; lakini viongozi hawana utashi wa kutuongoza tuondokane na hali hiyo duni.
Tunao viongozi sasa wanaoona ni bora zaidi kutembelea gari la Tsh 600 milioni, mtu mmoja mwenye hadhi kubwa, kuliko kufanya mipango ya kuwainua hao maskini uliowaona huko katika safari zako.

Na Bado.

Sasa tunapambania nasi tuwe na mabilionea wengi zaidi ili tuwe na hadhi kama za wenzetu majirani.

Hiki kipimo cha "umaskini" hakitatusitua sana tukishakuwa na mabilionea kadhaa hapa hapa kwetu.

Hiyo ndiyo Tanzania wanayoipambania viongozi wetu.
 
W
Umasikini wa Akili huu upo kwa Watanzania 90%
Watanzania wameathiriwa kisaikolojia. Wamefanywa kuamini kwamba kupambania haki zao ni kuvunja sheria hivyo wamechagua kuwa wapole ili wasivunje sheria.

Otherwise demokrasia ni ya makaratasi tu.
 
Back
Top Bottom