GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,551
- 108,882
Kuna watu wangu (wana medani) jirani na Kawe niliwatembelea siku ya Jumapili na wakati huo nilikuwa sijui nini kinaendelea hadi pale wenyeji wangu hao waliponiambia kuwa, ilikuwa ni siku ya kura za maoni kwa wagombea wa nafasi za wenyeviti wa Serikali za Mitaa.
Nakumbuka nilikuwa eneo hilo la Kawe hadi usiku wa saa tatu ambapo kwa kujiridhisha zaidi ilinibidi nizungukie maeneo mawili muhimu ya kiuchaguzi kwa Kawe ya Mzimuni alipo mkongwe Mzee Ngonyani (ambaye inasemekana alishakatwa na hatakiwi kugombea tena ila ndiyo kinara wa fitina zote akisaidiwa na Mwenezi wake aitwae Poti Poti ) na Ukwamani alipokuwa kijana makini Sultani Jeta (ambaye kwa bahati mbaya alisema kuwa hatogombea tena kwa sababu zake binafsi).
Mheshimiwa Katibu Mkuu wa CCM sitaki kujua ‘ vimbwanga ‘ vya maeneo mengine ya Mkoa wa Dar es Salaam vilivyotokea hiyo juzi (Jumapili ) ila kwa kilichotokea katika haya maeneo ya Mzimuni na Ukwamani ‘ nimekitathmini ‘ kwa kina na kugundua kuwa kama wana CCM hasa nyie mlio ngazi za juu msipokuwa makini, basi kuna hatari mwakani vyama vya upinzani vikashinda na hamtoamini macho na masikio yenu.
Haya ni baadhi ya mambo niliyopata kutoka hayo maeneo ya Kawe Mzimuni na Ukwamani:
Rushwa za wazi wazi wana CCM kwa wana CCM
Usaliti wa wana CCM uliopitiliza
Fujo ambako kuna muda wana CCM walikuwa wakionyesha kuwa hata wao fani ya ubondia wanayo pia.
Ushirikina wa wazi wazi na kuna mtu mmoja wa Kawe Mzimuni ‘Mkongwe' ambaye nimemtaja hapo juu anajulikana na kuogopeka sana ‘Kiuchawi' kwani na ‘Uchawi ‘ wenyewe nao anaujua mno, kasema kwa kuwa jina lake mlilikata huko juu kwa juu basi na yeye hakubali na ataondoka na mtu ‘ kindumba' kiasi kwamba kuna baadhi ya watu (Wagombea) makini sasa wanatafakari kujitoa kwa ‘kumuogopa' huyo Mzee ambaye amedumu hapo Mzimuni kwa miaka takribani 20 ila ameshindwa tu hata kuitafutia gari ya wagonjwa Hospitali ya Shamba Kawe ambayo ipo mita chache na ofisi yake.
Upandikizaji wa watu ambako inasemekana kuna Mbunge mmoja (jina kapuni) aliandaa watu wake ambao wengine walikuwa ni wa Kiume ila walivalia ‘ Hijab' na waliletwa na Usafiri wa Bajaji (ambao aliwahonga pesa nzuri tu) ili waje wawapigie Kura za Maoni hao Wagombea wa CCM ambao huyo Mbunge ‘ Fulani ‘ anawamudu ili kama kawaida mwakani awatumie tena katika Kukisaliti Chama na aweze Kupita kama ambavyo baadhi yao walimsaidia huko nyuma ( bado nasisitiza kuwa hii ni Tetesi kwani hata Mimi GENTAMYCINE basi sijaithibitisha wala kuiamini kwa 100% )
Vitisho kwa baadhi ya wana CCM wa hayo maeneo kwamba kama hawatowapigia Kura basi Wao wakitumia Ujanja wao na kupita watakuja ‘ Kuwakoma ‘ na lazima tu watawafanyia tu Kitu mbaya. Na wengi wanaotishiwa hivi ni wale wana CCM ambao wanaendesha Bishara zao katika Soko la Kawe lile la Ukwamani na hili jipya lilipo Mzimuni pamoja na wale wengine waliopo mazuri kwa ‘ Fursa ‘ za Kibiashara.
Nikupongeze pia Katibu Mkuu wa CCM Dkt. Bashiru Ally kwa ‘ Kuamuru ‘ Uchaguzi huu wa ndani wa CCM urejewe / urudiwe baada ya hizo ‘ Sarakasi ‘ ila kupitia tu huu Uzi wangu GENTAMYCINE nakuomba kama itawezekana basi nakuomba katika Siku ya Uchaguzi ( ambayo bado hamjaipanga ) tafadhali omba Msaada wa Kiusalama kutoka Kituo cha Polisi Kawe au hata ikibidi hawa Jamaa zangu wana ‘ Medani / Wanajeshi ‘ wasimamie tu hivi Vituo viwili vya MZIMUNI na UKWAMANI kwani kama hili halitotendeka basi tegema taarifa za Watu ‘ Kujeruhiana ‘ vibaya na hata ‘ Kuuana ‘ pia kwani hali si nzuri kabisa.
Nakumbuka nilikuwa eneo hilo la Kawe hadi usiku wa saa tatu ambapo kwa kujiridhisha zaidi ilinibidi nizungukie maeneo mawili muhimu ya kiuchaguzi kwa Kawe ya Mzimuni alipo mkongwe Mzee Ngonyani (ambaye inasemekana alishakatwa na hatakiwi kugombea tena ila ndiyo kinara wa fitina zote akisaidiwa na Mwenezi wake aitwae Poti Poti ) na Ukwamani alipokuwa kijana makini Sultani Jeta (ambaye kwa bahati mbaya alisema kuwa hatogombea tena kwa sababu zake binafsi).
Mheshimiwa Katibu Mkuu wa CCM sitaki kujua ‘ vimbwanga ‘ vya maeneo mengine ya Mkoa wa Dar es Salaam vilivyotokea hiyo juzi (Jumapili ) ila kwa kilichotokea katika haya maeneo ya Mzimuni na Ukwamani ‘ nimekitathmini ‘ kwa kina na kugundua kuwa kama wana CCM hasa nyie mlio ngazi za juu msipokuwa makini, basi kuna hatari mwakani vyama vya upinzani vikashinda na hamtoamini macho na masikio yenu.
Haya ni baadhi ya mambo niliyopata kutoka hayo maeneo ya Kawe Mzimuni na Ukwamani:
Rushwa za wazi wazi wana CCM kwa wana CCM
Usaliti wa wana CCM uliopitiliza
Fujo ambako kuna muda wana CCM walikuwa wakionyesha kuwa hata wao fani ya ubondia wanayo pia.
Ushirikina wa wazi wazi na kuna mtu mmoja wa Kawe Mzimuni ‘Mkongwe' ambaye nimemtaja hapo juu anajulikana na kuogopeka sana ‘Kiuchawi' kwani na ‘Uchawi ‘ wenyewe nao anaujua mno, kasema kwa kuwa jina lake mlilikata huko juu kwa juu basi na yeye hakubali na ataondoka na mtu ‘ kindumba' kiasi kwamba kuna baadhi ya watu (Wagombea) makini sasa wanatafakari kujitoa kwa ‘kumuogopa' huyo Mzee ambaye amedumu hapo Mzimuni kwa miaka takribani 20 ila ameshindwa tu hata kuitafutia gari ya wagonjwa Hospitali ya Shamba Kawe ambayo ipo mita chache na ofisi yake.
Upandikizaji wa watu ambako inasemekana kuna Mbunge mmoja (jina kapuni) aliandaa watu wake ambao wengine walikuwa ni wa Kiume ila walivalia ‘ Hijab' na waliletwa na Usafiri wa Bajaji (ambao aliwahonga pesa nzuri tu) ili waje wawapigie Kura za Maoni hao Wagombea wa CCM ambao huyo Mbunge ‘ Fulani ‘ anawamudu ili kama kawaida mwakani awatumie tena katika Kukisaliti Chama na aweze Kupita kama ambavyo baadhi yao walimsaidia huko nyuma ( bado nasisitiza kuwa hii ni Tetesi kwani hata Mimi GENTAMYCINE basi sijaithibitisha wala kuiamini kwa 100% )
Vitisho kwa baadhi ya wana CCM wa hayo maeneo kwamba kama hawatowapigia Kura basi Wao wakitumia Ujanja wao na kupita watakuja ‘ Kuwakoma ‘ na lazima tu watawafanyia tu Kitu mbaya. Na wengi wanaotishiwa hivi ni wale wana CCM ambao wanaendesha Bishara zao katika Soko la Kawe lile la Ukwamani na hili jipya lilipo Mzimuni pamoja na wale wengine waliopo mazuri kwa ‘ Fursa ‘ za Kibiashara.
Nikupongeze pia Katibu Mkuu wa CCM Dkt. Bashiru Ally kwa ‘ Kuamuru ‘ Uchaguzi huu wa ndani wa CCM urejewe / urudiwe baada ya hizo ‘ Sarakasi ‘ ila kupitia tu huu Uzi wangu GENTAMYCINE nakuomba kama itawezekana basi nakuomba katika Siku ya Uchaguzi ( ambayo bado hamjaipanga ) tafadhali omba Msaada wa Kiusalama kutoka Kituo cha Polisi Kawe au hata ikibidi hawa Jamaa zangu wana ‘ Medani / Wanajeshi ‘ wasimamie tu hivi Vituo viwili vya MZIMUNI na UKWAMANI kwani kama hili halitotendeka basi tegema taarifa za Watu ‘ Kujeruhiana ‘ vibaya na hata ‘ Kuuana ‘ pia kwani hali si nzuri kabisa.