Dini ni Utamaduni wa watu fulani

Dini ni Utamaduni wa watu fulani

samahani huku kwetu ni mtume gani alishushwa?
Katib Mkoa kuna Sanaa ya utawanyikaji wa watu ambayo ni somo refu kidogo halitakiwi kuwa kwenye position ya reply Bali uzi kamili. Ila kwa ufupi tu ni kwamba;

Dunia nzima ilianzia mashariki ya kati wakati maeneo mengine yoote yakiwa mapori tu; nitakupa mfano wa hapa karibu ili twende sawa Tanganyika wakati inapata Uhuru mwaka 1961 ilikua na watu takribani milioni 9 hivi.

Hapo unazungumzia miaka 59 ambao bado waliozaliwa wapo na hawajachoka kivile kwani umri wa miaka 59 si umri mkubwa kihivyo. Sasa Rudi nyuma miaka mingine 50 nyuma utapata mantiki ya ninachozungumzia.

Kipindi Mwongozo unashuka watu walikua katika center Kama vile unavyosikia miji maarufu ya kale Kama Misepotomia (Iraq), Stlyria, Nk hivyo kutokana na kipindi kupita ilizaliwa migogoro na watu kutawanyika.

Wengime waliamua kutanua miji nk. Hivyo ule muongozo ukaanza kugifia na hatimaye kusahaulika ndipo mitume na manabii walipoanza kushushwa kwa ajili ya kukumbusha mwongozo.

Ukizama kwa undani zaidi utafundua baada ya miongozo ndipo makundi makubwa yalipoanza kutawanyika ikiwa ni pamoja na sababu za kibiashara nk.

TAFAKURI FUPI

1. Nabii Issa au Yesu ana miaka 2020 tangu aondoke duniani (hebu fumba macho na inyang'anye hii dunia miaka 2020 alafu pata picha ilikuaje)

2. Mohammad SAW ana miaka 1449 tangu kifo chake (hebu fumba macho na inyang'anye hii dunia miaka 2020 alafu pata picha ilikuaje)

Hizo research zinazoendelea kwamba sijui mwanadamu aliishi miaka milioni 2 iliyopita ni myth ambazo muda wowote chochote kinaweza kubadilika
 
Umeyapata wapi hayo majibu?
Mimi siyo kwamba nafikiri bali majibu ninayo ya kwanini mitume hawakuanzia huku kwetu.

Sasa wewe ndiyo ujibu swali nililo uliza huko juu.
 
Wewe umesikia wapi mzungu akiruka ndani ya ungo???, Muafrika anaruka ndani ya ungo kwa kutumia sayansi ya giza yenye masharti ya kishenzi, utasikia ukitaka kuruka ndani ya ungo kwanza umuue mama yako au baba yako au nduguyo wa karibu, pili unapotaka kuruka lazima uwe uchi tatu lazima ufumbe macho hadi mwisho wa safari yenu, nne lazima iwe ni usiku.

Sasa angalia sayansi ya mzungu, ipo wazi na hakuna madharti ya kishenzi kama ya Muafrika, kinachofanya ndege ya mzungu ipae angani ni Bernouli principle, lazima kuwe na hewa, lazima ndege itumie injini nk, vyote hivyo vipo wazi kwa kila mtu anayetaka, huo ni mfano mmoja ninaokupa ili uone utofauti kati ya African culture vis a vis European culture.
Kumbe ww ujui kitu wazungu nao wanaruka na fagio, nao wanatoa kafara kama huku ila.tu wanafanya siri sana ili waonekane wao hawafanyi ushirikina.
Nenda New Zealand ndio utavishuhudia maana wao waneona haina aja ya kuvificha
 
Nitajie mtume mmoja tu wa Allah kutoka makabila ya Africa
Katika kila umati Allah alituma mitume, wapo mitume ambao Allah amewataja/amemuhadithia mtume SAW (ndani ya Qur'an) na wapo Mitume ambao hakuwataja, na duniani wamepita mitume zaidi ya laki moja na ushee, hadi huku Africa mitume walikuwepo kwa ajili ya makabila nk.
 
Hawaishi kwa sababu wanazaliwa wengine na wengi wao wanakua kufukia hatua ya wao kuzaa pia. Sasa waarabu waliwezaje kuendeleza kizazi chao ikiwa watoto wao wa kike walikuwa wanauwa katika utamaduni wao?!
Kwanini hujiulizi kila siku watu wanakufa, na hawaishi... ?

Pili, ongeza umakini nilisema walikuwa wanaona ya kuwa na watoto wa kike ni mkosi, hili mosi, pili wakafika mbali na kuwaua watoto hao, ulipo kuja Uislamu ukakataza mila hizo.
 
Haya tunayajua kitambo sana ulikuwa wapi? Waafrika tumekuja kivyetuvyetu kutumia dini hizohizo, yaani tumefanya ni vyama vya kutiana moyo, kuzikana, majadiliano yakisisa kuhusu ukandamizaji wa kikoloni, burudani, huduma za kijamii km shule Hosp. Vyama vya kudai uhuru.
Tulijua kitambo sana kuwa tuliingizwa chaka, tulilazimishwa kuzipokea, tukazibadili bila wababe kujua. Km black america alivobadili kiingereza na kuwa kivingine mpaka leo. Htn haraka. Mkoloni alichoka nakwambia. Ikabidi tuwe tunasali chini ya ulinzi lkn bado haikusaidia, wakatuchanganya na wazungu wenzao mtu kati. Hatukuiga labda nyinyi mlikwenda kikondoo! Bila kuhoji.
 
Kwa nini hapakuwa na haja hiyo?
Swali zuri. Mitume hutumwa kwa watu ambao wamechupa mipaka katika kufanya maovu, na hao ambao mitume wametumwa kwao wamekidhi hili, waarabu walichupa mipaka, mayahudi kadhalika na mfano wao.
 
Nani amekufundisha hivi?
Swali zuri. Mitume hutumwa kwa watu ambao wamechupa mipaka katika kufanya maovu, na hao ambao mitume wametumwa kwao wamekidhi hili, waarabu walichupa mipaka, mayahudi kadhalika na mfano wao.
 
Hawaishi kwa sababu wanazaliwa wengine na wengi wao wanakua kufukia hatua ya wao kuzaa pia. Sasa waarabu waliwezaje kuendeleza kizazi chao ikiwa watoto wao wa kike walikuwa wanauwa katika utamaduni wao?!
Jibu liko hapo hapo, tatizo hauko makini, mpaka wanawake wanazaliwa na kuzaa watoto wa kike, ujue uzao ulikuwepo na kulikuwa na taratibu za kuwauwa watoto hao.

Bila shaka umeelewa sasa.
 
Mipaka gani ambayo waarabu na wayahudi walichupa lakini Wazungu, Waafrika, Wahindi, Wahindi wekundu na Wachina hawakuchupa?
Swali zuri. Mitume hutumwa kwa watu ambao wamechupa mipaka katika kufanya maovu, na hao ambao mitume wametumwa kwao wamekidhi hili, waarabu walichupa mipaka, mayahudi kadhalika na mfano wao.
 
Unazijua hizo taratibu za kuwaua watoto au unadhania tu?
Jibu liko hapo hapo, tatizo hauko makini, mpaka wanawake wanazaliwa na kuzaa watoto wa kike, ujue uzao ulikuwepo na kulikuwa na taratibu za kuwauwa watoto hao.

Bila shaka umeelewa sasa.
 
Dini yako ya uislamu iliyoanzia Uarabuni ndio imekuambia sababu ya Waafrika kutohitaji mitume Waafrika?
Kwanza nakusahihisha, Uislamu umegawanyika sehemu kuu mbili, moja Uislamu wa Ujumla ambao huu upo hata kabla ya nabii Ibrahiim. Uislamu khasa (maalumu ambao amekuja nao mtume).

Bila shaka kabisa,Waafrika hatukufikia makosa na uovu ambao walikuwa wanafanya watu weupe. Kwahiyo kila jambo lazima liwe lina mwanzo wake kisha lina tangaa.
 
Mipaka gani ambayo waarabu na wayahudi walichupa lakini Wazungu, Waafrika, Wahindi, Wahindi wekundu na Wachina hawakuchupa?
Mingi sana, hakuna watu walio kuwa wana vitimbi kuwazidi hao, wao walikuwa wakiletewa mitume wana waua, wakifanyiwa miujiza wanakanusha, mpaka wakawa wanaletewa vyakula toka mbinguni lakini mwisho wa siku wanakadhibisha na kutenda maovu, bali waliwafanya binadamu wenzao kuwa ndiyo miungu na mfano wake.
 
Nani alikufundisha hivi?
Unafahamu waarabu sio watu weupe?
Kwanza nakusahihisha, Uislamu umegawanyika sehemu kuu mbili, moja Uislamu wa Ujumla ambao huu upo hata kabla ya nabii Ibrahiim. Uislamu khasa (maalumu ambao amekuja nao mtume).

Bila shaka kabisa,Waafrika hatukufikia makosa na uovu ambao walikuwa wanafanya watu weupe. Kwahiyo kila jambo lazima liwe lina mwanzo wake kisha lina tangaa.
 
Back
Top Bottom