Dini ni Utamaduni wa watu fulani

Dini ni Utamaduni wa watu fulani

Waislamu waafrika wanaaminishwa amali zipo mbinguni kwaiyo tusiuhangaikie utajiri wafe masikini duniani mbinguni wameandaliwa kila kitu wao wafanye ibada tu uhai wao wote wakati uyo aliyemletea UISLAM anaishi kifahari wasaudia matajiri sio mchezo, Waislamu wauarabuni matajiri kwelkwel.


Wakristo waafrika wameaminishwa ktk manabii mtu akifanya miujiza kidogo bas anatunukiwa unabii anaabudiwa. nonsence kabisa manabii kila siku wanaongezeka mara wawalishe wahumin wao nyasi, petrol, tissue wanadai wamepewa maono.

UKIHOJI UNAAMBIWA UNAKUFURU


Kwani huo utajiri wa waarabu si umekuja hii miaka ya 70s tu, baada ya kupanda bei ya mafuta ??

mbona uislamu upo miaka mingi kabla na hali zao zilikuwa ni za kimasikini ??

Na huko ulaya na Marekani utajiri umekuja karibuni tu, hapo kabla na wao walikuwa ni masikini ??
 
W
Nitangulie kwa kusema Utamaduni ni neno pana linalojumuisha mfumo mzima wa Maisha, lengo la Uzi huu ni kuonesha ni jinsi gani tulivyoubeba utamaduni wa kigeni na kuufanya dini zetu na pengine tumenufaika nao ama kuumizwa nao pasipo kujua.

Nitawapitisha kwenye vipengele vya utamaduni 'Culture'. Hapa Ukristo nitauita 'Jewish Culture', Uislam kama 'Arabic Culture' na dini ya mwafrika ambayo ni 'African Traditional Religion' nitaiita African Culture. Kwahiyo nitazungumzia utamaduni wa kiyahudi, kiarabu na kiafrika. Sitarajii kupata maswali ya NINI MAANA YA DINI. Hapa hiyo dini yako naijadili Kama tamaduni tu wa watu fulani.

1. Uongozi na siasa. Waafrika walikuwa na tamaduni zao za kupata kiongozi, pia sheria na kanuni zao kabla ya kuletewa tamaduni mpya za kiarabu zilizoletwa na wa Asia hasa waarabu na kiyahudi zilizoletwa na wazungu. Kwenye makabila mengi, kiongozi wa kijadi alivaa kofia mbili, ya kisiasa na kidini kwenye matambiko. Ukristo ukaleta taratibu zake, siasa na dini zilitenganishwa. Huu ni utamaduni wa kiyahudi ambao haukuwa na uhusiano kati ya makuhani na magavana wa kirumi.
Uislam Kama ilivyo utamaduni wa kiarabu. Siasa na dini hufungamana. Ndiyo maana kuna nchi zinazofuata 'Sharia' za kiislam/kiarabu katika kuamua na kuongoza. Hizo zote ni tamaduni tu za watu, siyo maagizo ya Mungu.

2. Music. Waafrika wana vyombo vyao vya muziki 'music instruments' na styles zao za uimbaji 'musical notations'. Zeze, filimbi, ngoma, pembe za wanyama nk... Wakristo wakachukua muziki wa kiyahudi na kirumi uliotajwa kwenye Biblia. Baragumu, tarumbeta, zeze, vinanda...kuwa muziki safi wa kumwimbia Mungu. Kwa wakatoliki Papa Gregory akapendekeza Tuni fulani itumike duniani kote 'Gregorian music'. Hali kadhalika Waislam na kaswida, dufu ambazo ni musical notation za kiarabu wakazifanya nyimbo za kumsifu Mungu. Ni utamaduni tu, Mungu hana aina fulani ya kuimbiwa.

3. Language. Lugha zetu za kibantu zilitumika kuomba na maombi yakapokelewa. Viongozi wa kimila walitambika kwa Lugha zao kwa Miungu yao. Wazungu wakatuletea ukristo katika lugha ya kilatini. Ibada na misa zilifanyika kwa Lugha hii kwa karne kadhaa. Warumi ndiyo walikifanya kilatini kiwe lugha ya Mungu ingawa Mambo yalibadilika badae. Uislam kwakuwa ni utamaduni wa kiarabu, wao Hadi leo huamini Mungu anajua kiarabu tu. Hakijabadilika chochote. Ni utamaduni tu, hata kichina na kijapani Mungu anakisikia.

4. Food. Chakula katika utamaduni wa kiafrika una makatazo na kanuni za kula chakula. Kulikuwa na hadithi zenye kukataza au kuruhusu chakula/mnyama fulani. Utamaduni wa kiyahudi hali kadhalika, Kuna chakula haram na kisicho haramu, ingawa warumi wamefanya yao kugeuza masndiko. Kuna wakristo wanaokula kila kitu na wale wanaochagua kulingana na mapokeo ya agano la kale la kiyahudi. Waislam pia, utamaduni wa kiarabu katika chakula umebebwa kama ulivyo. Haram na Halal ni kadiri ya utamaduni wa kiarabu ambao walifungamana sana na wayahudi. Ndiyo maana, haram zilizopo katika Agano la kale utazikuta kwenye Qur'an.

5. Art, craft and Architecture. Sanaa na ubunifu. Waafrika tulikuwa na styles zetu za ujenzi wa nyumba za kuishi na ibada michoro na mapambo. Lakini leo hii nyumba za ibada zetu ni sawa na mahekalu ya kiyahudi na kirumi kwa wakristo, kukiwa na nakshi za misalaba. Kwa waislamu nako ni ramani za nyumba za kiarabu, michoro ya kiarabu na alama za 'Mwezi' ambao ni Mungu wa kiarabu aliyeabudiwa hata kabla ya Uislam. Ni tamaduni za watu tumejitwika.

6. Social interaction. Jamii za kiafrika zilikuwa na namna yake ya kuingiliana na kuhusiana kulingana na umri na jinsia. Ukristo wa kale ulibagua sana wanawake Kama ilivyo tamaduni za kiyahudi. Mwanamke alikuwa ni mtu wa 'kusitiriwa' lakini mambo yakabadilika badae, leo hii anasimama Hadi madhabahuni.
Waislam wao wameichukua tamaduni ya kiarabu Kama ilivyo ya kumsitiri mwanamke na kumfanya kiumbe dhaifu. Hachangamani na mwanaume iwe kwenye ibada hadi matukio ya kifo. Hii ni tamaduni ya kiarabu hadi leo, si maagizo ya Mungu, Ni utamaduni tu.

7. Tradition. Hii dhana ni pana.
~Dressing style, waafrika tulikuwa na namna yetu ya uvaaji, Kama ya masai na wengine, lakini ukristu ukatuletea kanzu na majoho. Hayo ni mavazi ya makuhani wa kiyahudi, si kwamba ukivaa shuka la kimasai Mungu hakusikii. Waislam nao kanzu, juba, hijab ambayo ni mavaz ya kiarabu yakafanywa kuwa mavazi rasmi. Ni utamaduni tu, Mungu hakuagiza uvae hayo ili uwe wake.

~Eating style. Namna ya kula kwa waafrika wa zamani ni tofauti na jamii za leo zilizoathiriwa na tamaduni za kiyahudi na kiarabu. Wapo wanaoamini kuwa na namna fulani ya ukaaji,(mezani au mkeka) Mungu hapendi, kisa tu myahudi au Mwarabu alifanya hivyo. Ni tamaduni zao tumezigeuza kuwa dini.

~Festivals. Sherehe na kumbukizi za kiafrika wa kale ni tofauti na za leo. Mtoto wa kiafrika akizaliwa kulikuwa na taratibu zake hadi anaingia utu uzima. Kuanguka kitovu, siku 40... Kwa wakristo utasikia kuna ubatizo, kipaimara (kipaimara ni hatua ambayo ipo hadi leo kwa wayahudi ambao siyo wakristu).... Pasaka pia ilikuwepo kabla ya ukristo. Na Waislam wana yao kama 'Hakika'..... Ambayo hufanyiwa watoto wa kiarabu kadiri ya tamaduni zao, si maagizo ya Mungu.

~Mazishi. Waafrika tukizika kwa namna tofauti tofauti kulingana na tamaduni ya kabila husika. Kuuacha mwili kwenye mapango na kuhama makazi, kufukia chini.... Ukristu umeleta style yake na Uislam hali kadhalika. Matumizi ya sanda, jeneza, kukafini, kuosha maiti ni tamaduni tu za kiarabu na kiyahudi, siyo maagizo ya Mungu.

~Tohara. Kwa waafrika hili jambo lilikuwepo kwa baadhi ya makabila. Wengine hadi Leo hawatahiriwi. Ni utamaduni wao. Kwa wayahudi ni utamaduni wao tangu kale, hali kadhalika waarabu. Kutahiri kumefanywa Jambo la kidini ingawa Ni utamaduni tu. Si agizo la Mungu kwamba hapokei kiumbe chenye 'govi' kwenye makao yake ya milele. Wapo wazungu na waafrika ambao hadi leo hawatahiriwi.

Karibuni kwa mjadala, kusiwe na malumbano ya kupigania Utamaduni wa kiyahudi Wala kiarabu hapa. Tujadili kwa hoja. Huu ni mtazamo wangu tu, unaweza kuwaza tofauti.
Wayahudi hawajawahi kuwa wakristo bora ukristo ungeuita Roman culture,wayahudi wana wana dini yao ya Yuda yaan Judaism na siyo wakristo.
 
Narudia tena
Kama Adam,Eve, Ibrahim na Musa hawakuwa na dini yoyote basi hakuna dini iliyoshushwa na Mungu.
Na hata hizi zilizopo hakuna iliyo Bora au juu ya zile zilizokwepo kabla hazijaja hizi.
 
Uko 2000% right mkuu
Siku: Jumatano
Tarehe : kumi na tano /7/2020
Kipindi : witness
Tv: al jazirra
Master Wa temple ACC : Hui Liu
Nchi:Malawi

Ni kipindi kilichokuwa kikionesha jinsi M Buddha kutoka nchini Taiwan walivyokuwa wakichukua watoto na kuanza kuwafundisha watoto Wa Kimalawi utamaduni wao Wa ki Buddha na kusema wazi kuwa wamechelewa kuja Africa na kufundisha utamaduni wao huo(dini) na Laiti wangeanza wao kuja Africa Basi na sisi tungekuwa ms Buddha badala ya kuwa waislamu na wskristo, nikajiuliza waafrika tumekosea wapi? Kwanini Kila imani utufanye punching bag na kuleta maimani yao kwetu?
Big up kwa wamalawi waliokinukisha na kupigana na M master wa ki Buddha na kawaleta polisi na ma master wa ki Taiwan hao kurudishwa kwao
Dole la kati nawaonesha familia ya enock ambaye ma Buddha Hawa walimpa jina la alu(hajui lina maana gani kwa kichina) kwa kumshinikiza dogo enock aende Taiwan na kujifunza zaidi tamaduni hizi za kigeni.
Africa tukataeni hizi tamaduni za wageni (uislam ,ukristo,u Buddha n.k)
Nalog off
Waafrika wengi vichwa vyetu nikama ubao kila mwenye chaki anakuja na kuandika cha kwake na tunakipokea tunaona ni bora kuliko chetu
 
We ndo umeharibu kabisa sasa[emoji3][emoji3][emoji3]

Utamaduni sio sehemu ya dini, bali dini ndo sehem ya utamaduni. Rudi shule ukasome elements of culture mkuu[emoji3]
Thanks kwa kumjibu vizuri kabisa, dini ni sehemu ya utamaduni wa jamii husika na tafsiri ya culture ni total way of living of a given society (Walter Rodney) kama yalivyofafanuliwa vizuri kabisa na mleta mada. Yanajumuisha dini/Ibada, kula, kuvaa, kumkaribisha mtoto anayezaliwa, kumuaga anayekwenda kuanza maisha ya ndoa, kumuaga/kumpumzisha aliyefariki nk nk nk nk.
 
Uislam Kama ilivyo utamaduni wa kiarabu. Siasa na dini hufungamana. Ndiyo maana kuna nchi zinazofuata 'Sharia' za kiislam/kiarabu katika kuamua na kuongoza. Hizo zote ni tamaduni tu za watu, siyo maagizo ya Mungu.

~ Waislam wao wameichukua tamaduni ya kiarabu Kama ilivyo ya kumsitiri mwanamke na kumfanya kiumbe dhaifu. Hachangamani na mwanaume iwe kwenye ibada hadi matukio ya kifo. Hii ni tamaduni ya kiarabu hadi leo, si maagizo
ya Mungu,
Ni utamaduni tu.
~
Mungu hakuagiza uvae hayo ili uwe wake.

Nimenakili baadhi ya maneno yako hapo juu, ili kujenga hoja.
Wewe wasema HAYO YOTE SI MAAGIZO YA MUNGU.
Laini ulinimaliza Nguvu pale uliposema kuwa ''Tujadili kwa hoja. Huu ni mtazamo wangu tu, unaweza kuwaza tofauti''.
nikapwaya.
hata hivyo , ujuwe kuwa mawazo kila mtu anayo na ndio ubinadamu.
sasa nikuulize swali
Wewe unaamini uwepo wa Mungu MMOJA Muumba?

Je wewe Umeshawahi quisoma na kuifahamu Qur-an?
Je wewe umesha wahi kuisoma na kuifahamu Bibilia?
Umefahamu Azimio zima la Dini katika vitabu hivyo?
Tunajuwa wazi kuwa tamaduni za watu ziko tofauti ,Lakini Dini pia Inautamaduniwake Makhsusi, Je uliwahi kulijua hilo?
 
W
Wayahudi hawajawahi kuwa wakristo bora ukristo ungeuita Roman culture,wayahudi wana wana dini yao ya Yuda yaan Judaism na siyo wakristo.
Kuna wayahudi wakristo Israel, ingawa ni wachache.
Pia Judaism imejikita kwenye vitabu vitano vya Musa tunaita 'Pentateuch' au Hebrew Bible, au Torah au five books of Mosses.
~Genesis,
~Exodus,
~Numbers,
~Leviticus na
~Deuteronomy.
Hivyo vyote vipo kwenye Biblia wanayoitumia Wakristo kwenye Agano la kale.
 
Nimenakili baadhi ya maneno yako hapo juu, ili kujenga hoja.
Wewe wasema HAYO YOTE SI MAAGIZO YA MUNGU.
Laini ulinimaliza Nguvu pale uliposema kuwa ''Tujadili kwa hoja. Huu ni mtazamo wangu tu, unaweza kuwaza tofauti''.
nikapwaya.
hata hivyo , ujuwe kuwa mawazo kila mtu anayo na ndio ubinadamu.
sasa nikuulize swali
Wewe unaamini uwepo wa Mungu MMOJA Muumba?

Je wewe Umeshawahi quisoma na kuifahamu Qur-an?
Je wewe umesha wahi kuisoma na kuifahamu Bibilia?
Umefahamu Azimio zima la Dini katika vitabu hivyo?
Tunajuwa wazi kuwa tamaduni za watu ziko tofauti ,Lakini Dini pia Inautamaduniwake Makhsusi, Je uliwahi kulijua hilo?
Maswali ni mengi sijui nianze lipi, ila kiufupi bandiko langu linaashiria kabisa kuwa Nina imani ya uwepo wa Mungu Mmoja. Kama umesoma vizuri.

Pia suala la kuisoma Biblia na Qur'an, vyote nimevisoma ABC's zake nazijua ndizo zilizonifanya niweze kuandika Uzi huu. Yawezekana wewe umesoma zaidi Ilimu hiyo Kama profession yako, tuendelee na mjadala. Tupo hapa kujifunza.
 
Shs 500/=, yaani Jero??!!, halafu unatamba humu ndani ya ukumbi wa Jf kwamba eti nawe huwa unatoa pesa!!!??, kweli wewe ni Tajiri kichwa sio Tajiri pesa.

Kumbe umeelewa eeh ..kunywa maji mengi upunguze jaziba
 
Kumbe umeelewa eeh ..kunywa maji mengi upunguze jaziba



Umesema ukitoa mwisho ni mia 5, kwani hiyo ni shs ngapi?, sio shs 500/=, yaani Jero??!!.--- kama ni sawa basi wewe ndiye uliyelewa konyagi na kama sio sawa basi mimi ndiye niliyelewa. 🤓
 
Kwani huo utajiri wa waarabu si umekuja hii miaka ya 70s tu, baada ya kupanda bei ya mafuta ??

mbona uislamu upo miaka mingi kabla na hali zao zilikuwa ni za kimasikini ??

Na huko ulaya na Marekani utajiri umekuja karibuni tu, hapo kabla na wao walikuwa ni masikini ??
Na umasikini hawauendekezi, Binadamu wa leo mfia dini akiona unamiliki vitu vya thaman kama magari wanaanza kuingiza kifo kwamba fanya ibada ayo magari tutayaacha,

ni Mungu yupi anapenda wanadamu wake waishi kwa dhiki. uku mtaani kwetu ukiwa tajiri basi wew sio mwamini mungu. tunakufa masikin kwa kukosa akili
 
Mfia dini , mbna unapenda mabishano yasiyo na hoja ndani yake ? Mtoa mada ameeleza kinaga ubaga kuwa sisi tumeiga / tohoa tamaduni za watu ambazo zimeenda sambamba na Dini zao .
Mkuu samahani sana kama nimekukwaza .

Binafsi hujanikwaza.

Ila nimeuliza bila matusi wala kejeli ila nimeweka alaza za kuuliza ambazo zinaashiria kuwa nauliza.

Sijajua kitu gani nimekosea,ila niseme tena samahani sana kama nimekukera mkuu naomba niendelee na mtoa mada..
 
Kiufupi naamini Mungu yupo, na amejidhihirisha wazi kabisa. Kila jamii dunia mzima nguvu ya Mungu ipo. Kuna dini kubwa sita duniani. Kote Mungu anajionesha. Kuna
~Judaism
~Christianity
~Islam
~Hinduism
~Budhism
~Sikhism
Mtawa(monk) wa kibudha anaweza fanya maajabu makubwa sana ya kutembea juu ya maji au kutembea bila kukanyaga ardhi(kupaa) Kama Yesu. Lakini si mkristu Wala mwislam.
Nimekusoma mkuu.

Ila naomba nijue kwa uwazi kuhusu swala langu..

Tumekubaliana kwamba Mungu anajidhihirisha kwetu kupitia dini mbali mbali kama ambavyo umetoa dini kadhaa.

Ila ninachouliza mimi ni kuwa..
wewe unatumia mizani ama kipimo gani kujua kuwa haya kweli yanatoka kwa Mungu na haya yanatoka kwa watu tu ?
 
Kuna wafia dini wa kufata mkumbo ukijaribu kuwaeleza mambo wanakupinga

Kwenye sWala la uvaaji hapo wanawake wanapovaa nguo na kuacha vitovu wazi wanakwambia sio utamaduni wetu tena nilisikitishwa sana kuskia kauli kama hii ikitoka kwa mkuu wa nchi, nakumbuka kipindI cha nyuma hata wadada wanaovaa nguo fupi barabarani walikuwa wanaadhibiwa kwa kigezo kuwa sio utamaduni wetu,

Leo hii mtu akienda kwa mganga wa asili hata kutibiwa magonjwa ya kawaida anaonekana mchawi
tumeitupa mizimu yetu tumemuinua yesu wa wazungu na Muhammad wa waarabu

Inasikitisha sana
Huo utamaduni ambao unadhani ni wetu mkuu ni ule wa miaka gani ?
 
Kabisa mkuu. Yani tumekubali kutenganishwa kwa mambo ya kijinga sana. Imagine mwafrika mwenzenu mnaishi nae mnasaidiana kwenye shida na raha ni mwenzenu pengine alikuwa na msaada mkubwa kwenu jamii yake anaoishi nao lakini eti anakufa mnamzika kama mbuzi au mbwa kisa hakuwa dini yenu. Au mnakataa kumzika. Utu uko wapi? Tumeletewa ubaguzi baina yetu. Inauma sana
 
tunakipokea tunaona ni bora kuliko chetu


Chenu kilichobora ni kipi wewe muafrika??-- hiyo simu au laptop unayoitumia kuandika malalamiko yako hapa ni muafrika gani katengeneza???, Uchawi na kulogana na kuuana ndicho pekee mnachojua na maneno tu.
 
Chenu kilichobora ni kipi wewe muafrika??-- hiyo simu au laptop unayoitumia kuandika malalamiko yako hapa ni muafrika gani katengeneza???, Uchawi na kulogana na kuuana ndicho pekee mnachojua na maneno tu.
Hatuja zungumzia technology tumezungumzia dini na tamaduni.
 
Mfano kabla ya ujio wa wageni tulikua tuna abudu nini hasa babu zetu na kufa kwao je watachakuliwaje? maana hakukua na ukristo Wala uislamu na pia kwanini dini hizi mbili zilichelewa kufika Afrika
 
Back
Top Bottom