Mlete thread kidogo ukutenda haki kwa wote si kwa Diamond ama Mbunge wake Halima Mdee.Niliiishuhudia kuwa hakuna kitu chochote Diamond alichosema kibaya hayo maneno ya mwenye thread kamlisha Diamond maneno.Diamond aliomba Serikali iangalie hiyo barabara ya kwenda kwake kuwa kuna kipande fulani si kizuri kina mashimbo hivyo akaomba Serikali iangalie.
Ila kuna dada muongeaji sana hana break ndani ya show, ndio aliyekuwa anajaribu kutafuta Mbunge wa eneo analotoka Diamond,katika utafutaji huo ndio akaonekana Mbunge wa Makazi ya Diamond ni Halima Mdee.
Diamond ana kaufahamu fulani kwa kuwa katika maombi yake yeye yalilenga Serikali yake iangalie eneo lake hiilo,kijimdada kile kwa kutokujua pa kuelekeza fikra zake kikaangalia mwenye wajibu wa kudeal na barabara ni Mbunge...Kazi ya Mbunge ni kuwakilisha wanajimbo katika kusimamia na kuyasemea maendeleo ya jimbo lake, si kazi ya Mbunge kutengeneza barabara kwa kuwa hana mfuko wa kutengeneza na kugharimia barabara na shughuri za maendeleo ya jimbo lake.
Inaonekana mwadika thread alikutana na mdada huyo mwongeaji kupitiliza wa 360 akiwa anamwagika kama chiriku kiasi kuwa alimnyima mtangazaji mwenzie nafasi ya kuuliza maswali akadominate, mjadala japo alionyesha kuwa initiative za kufikishwa Diamond kwenye mahojiano hayo alifanya yeye mwenyewe as if Clouds hawana vitengo ama desk lasmi wa kuinvite watu kwa mahojiano...
Please Halima, Diamond hakusema chochote kibaya wala kumind Mbunge wake....haya maneno ni kutengeneza Diamond aonekane Mkolofi kwako...tena kwa vile uwa anatumika na CCM basi wakujengee mazingira kumuona alikukamia jambo.ASILIMIA kubwa inaonyesha uenda pia inawezekana hakuwa anajua Mbunge wa uko ni nani...na kama anajua uenda alipotezea kiujana kawaida ndio maana kwa ufahamu ule hakultea jina la Halima kwenye mjadala.
Na Clouds mfungeni huyo binti break uwa mwepesi sana kuongea vitu kwa kukatisha wenzie ....mpigeni shule on how to be a LADY anapokaa na wanaume...uwa naona anawaboa wanaume anaokuwa nao pale.Manake anatakiwa kuwa na Subira kusubilia mtu amalize kuongea kisha akiona kuna pozi la few sekonds ndio achukue mada kuongea...akiwa yeye utaona anaingilia maongezi maradufu kwenye topic mpaka ina kera.
Ni vizuri kuwa na binti pale lakini kama hakuna mwingine basi afundishwe manners ...jinsi gani anaongea na wanaume ukizingatia ile ni television sio saloon pale...