Dhana duni ya 'Mfumo Kristo'

Dhana duni ya 'Mfumo Kristo'

Status
Not open for further replies.
Zomba, wakubaliana kuwa mfumo uliopo na hizo verse ulizotoa haviendani. Ni mfumo wa upande mwingine kabisa wala sio wa Kristo.

Leo nimebandika nyuzi ambayo inauliza chadema watawakinaisha vipi Waislaam wawape kura zao. Imefutwa haraka haraka, kama si mfumo kristo ni nini huo?
 
CCM ni akina nani mpaka wawe maadui wa CDM. Zomba fikiria kabla hujaandika, ni kama vile hutaki watanzania wawe huru kushiriki siasa. Toka lini kutofautiana kimawazo, kiideology ikawa ni uadui. Ni lini mtajifunza kuwa wastaarabu, CCM tendeni yanayowapasa kwa wananchi hakuna atakayewasumbua na chama chenu. Kwa kuwa mmekengeuka na kuwa wanyama mmesahau wajibu wenu. Kwa sentensi yako UPINZANI ni uadui, basi tangazeni kuwa mwataka chama kimoja tu cha siasa watu wajue kuwa hamtaki demokrasi.
 
Kila kukicha,
unajitokeza ushahidi kwamba kiwango cha kufikiri miongoni mwa wa-Tanzania wengi ni duni. Siku hizi, kwa mfano, imeibuka hii dhana ya mfumo Kristo.

Unaruhusiwa kupinga hoja za wengine na siyo kuwatukana watoa hoja husika, kaa humo.

Walioibuni dhana hii na ambao wanaieneza wana ajenda ya kujenga hoja kuwa mfumo wa utawala na uchumi Tanzania unaendeshwa kwa misingi ya kiKristu, na kwa lengo la kuwanufaisha wa-Kristu na kuwakandamiza na kuwanyima wa-Islam fursa na haki wanazostahili, katika nyanja mbali mbali, kama vile elimu na uongozi.

Hii ndio dhana ya msingi ya hiki kinachoitwa mfumo Kristo. Wanaojenga hoja hii wanadai kuwa serikali ya Tanzania yenyewe inaendeshwa na maaskofu kama sehemu ya uendelezaji wa huu wanaouita mfumo Kristo.

Kwanza napenda kusema, kama ninavyosema daima, kuwa kila mtu ana uhuru wa kutoa mawazo yake. Uhuru huu ni pamoja na uhuru wa kuyahoji au kuyapinga mawazo ya wengine, kufuatana na mchakato wa kujielimisha na kutafakari masuala. Ni pamoja na uhuru wa kuyapinga mawazo yako mwenyewe.

Nashangaa kwa nini mfumo mbovu uhusishwe na jina la Yesu Kristu. Dini zote mbili, u-Islam na u-Kristu, zinamtambua na kumheshimu Yesu. Yesu anatambuliwa kama Mungu katika u-Kristu. Na katika u-Islam, anatambuliwa kama mtume maarufu. Dini zote zinamheshimu sana Yesu.

Kama mfumo wa Tanzania umeoza kama inavyosemwa, hauwezi kuwa mfumo Kristo. Kuuita mfumo Kristo ni dhihaka isiyo kifani. Huwezi kuuhusisha uchafu wowote na Mungu au mtume. Kama kweli maaskofu wanaendekeza na kuulinda mfumo wa dhuluma, wanakiuka mafundisho na maadili ya Kristo. Huu si mfumo Kristo. Mfumo Kristo ni mfumo wa haki na maadili aliyotufundisha Kristo.

Sidhani kama inahitaji akili ya pekee sana kuitambua hoja hii. Lakini ni wazi kuwa watu wengi Tanzania wana kiwango duni cha kufikiri au kuelewa mambo. Kwa dhana yao ya mfumo Kristo, wanaudhihaki u-Kristo, na pia wanaudhihaki u-Islam. Ila, kutokana na akili zao duni, hawatambui hilo. Kilichopo ni kuwaombea dua njema, waweze kujitambua na kujirekebisha.

Mkuu, unachanganya Mfumo na AWAMU za utawala, ulichokizungumzia kuwa kimeoza ni serikali ya awamu hii ambayo inajulikana kama AWAMU YA 4, lakini mfumo ulioutaja ni tangu tumepata uhuru ndiyo uliopo na unaotumika isipokuwa awamu hii tu inuangusha(yaani haifanyi kama mfumo unavyotaka), tangu awamu hiyo ya kwanza mnayoipamba na kuiita kuwa ilikuwa bora mfumo ulikuwa huu huu so, msiukane sasa kwa kuwa serikali ya wakati huu inauchafua, mtu hakuthubtu kuusema mfumo huu wakati ule kwa kuwa angeweza kuozea kusikojulikana na ndiyo maana hata wewe hufahamu chochote kuhusu hilo unakurupuka na kupinga badala ya kijifunza, kuna mikataba iliyofungwa wakati huo kati ya kanisa na nyerere/serikali yaani kwa namna gani nchi hii indeshwe na unatekelezwa.Mfano; Kwa akili yako wewe ni sawa serikali inaingia mkataba na kanisa kuipatia fedha kila mwaka kwa jina la MoU ili hali nchi hii si ya kanisa pekee? Hilo moja, lingine ni kuwa kuna ushahidi wa waislamu wengi yamewakuta ya kuwakuta kwenye masomo na makazini kwa sababu ya imani yao tu tangu enzi za awamu ya 1, to mention few. Hizi docs watu wanazo, hii hoja siyo nyepesi kama unavyofiria na sasa kuna fursa ya kusema, ndiyo maana watu wanaileta hoja hii ili kupatikane mabadiliko. Nakushauri jifunze kwanza upate data ndipo u argue jambo fulani itakusaidia hata kwenye mambo mengine ya kawaida ya maisha.
Nafahamu kuwa hoja yako ina wafuasi wengi kwa kuwa watu wa aina yako wako wengi sana na hii inatokana na mfumo ulioko huko mliko hauwaruhusu kuhoji jambo, yaani unatakiwa kulibeba kama lilivyo utake usitake yaani "hivi vitu viko vitatu full stop" huna fursa ya kuuliza how?
 
Ritz hebu nisaidie kuwajibu hawa jamaa mimi bado nipo job nikitoka nakuja kukupa kampani,hatutakaa kimya kwa yyte ataeleta kejeli dharau kwenye dini yetu,tutapambana nao mpaka mwisho,maana inayosemwa serikali ambayo wao wanaona wao tu ndio wana haki yakuisema,akisema Mtei nchi haitawaliki huyo sio mchochezi,wakisema waislam kudai haki zao wachochezi,yaani udini umewakaa mpaka kwenye vidole vyao,wao hapa kutwa wanaikosoa hyo serikali ila kwao sawa waislam wachochezi

Wewe brain washed Mteai ni kiongozi wa dini?
 
Radio Iman ni wachochezi,na bila shaka kuna mkono wa serikali nyuma yake,la sivyo ingekuwa imefungiwa tayari.

Jiulize kwanza ujasiri wa kuongea hayo wanaupata wapi?inamaana wao hawaini seriakali au hawajui sheria?auserikali wao hawajasikia hayo yanayoongelewa?nakama wamesikia jiulize wanayapuuzia?jibu litakua wamesikia na wala hawapuuzii.lilichopo nikwamba yanayosemwa niyakweli naserikali wanalazimika kufyata mkia ili ukweli huo usibainike.laiti yangekua hayana ukweli pasingetosha
 
Kwa Waisla leo kudai haki yao mnauona ni uchochezi hivi ni nani asiyejua kwamba Nchi hii hiko chini ya mtandao wa Kanisa Katoliki? Acheni mambo yenu ya kipuuzi mtu mwenye akili zake timamu anatakiwa kutafakari jambo kabla hajaliwakilisha.

wewe kiazi acha kuropoka ..toa mifano hapa ..katoliki kivipi?? Usiropoke kisa shehe gologosi sheke ubwaubwa kakuambia ndio uje kubwabwaja hapa
 
Na hawa vipi wanaitwaje?

Chadema+na+Idd+3..JPG



Kuchukua+chakula.JPG

Kama chadema ya kidini huyo mwenye mavazi ya kiarabu hapo ya middle east ni nani? Ni padri huyo?
 
Mkuu, Kwani wewe ambacho hapo hukifahamu ni nini ? Vatican sio nchi lakini wana Balozi wao hapa nchini weee unadhani anasimamia yapi hasa ?

Alafu usiwe mtu tu wa kulalamika mitandaoni fanya ka utafiti kidogo. Nikuulize kitu pale Kurasini baada ya kupita mivinjeni kama unakwenda kariakoo kabla ya kuikuta ile round about inapoanzia mandela road hapa nyuma kuna geti limeandikwa maandishi flani hivi alafu kuna nembo ya Taifa ( Bibi na Bwana ) kama ile iliyopo getini pale Ikulu. Umeshawahi kujiuliza kuwa ni nini kile ?

Basi acha kutoka mapovu huku mtandaoni na utafanye tafiti ! Mimi nakushauri kuwa hawa jamaa wako sahihi kabisaa !

Kama Vatican sio nchi ni nini kumbe?
 
hivi nyie ndio mulio soma?
bora sie kama tumepata kusoma ni kwa akili zetu, lakini kusoma kwa kusukumwa na NECTA, Kukopia mitihani kusaidiwa tena mpaka huko vyuo vikuu , tumepita huko tunajua mnavonunua degree, tunajua mnavopewa mitihani
leo 90% ya serikali inaongozwa na hawa na ndio wanatufikisha hapa..hasara ilioje...utaliona jitu ati linaongea kiingereza ndo limesoma..dah....
kwa ufupi hii mipango ya kujipendelea imesababisha nchii hii kufa ama kurudi nyuma ..badala ya kuendela ..wenzetu wanasonga mbele sisi tunarejeshwa nyumba ....sometimes huwa naona kinyaa kuwaona hawo wasomi kwenye midahalo wanavo ongea utumbo...
hamna cha kujidai....labda kuvaa suti ndio kuelimika lol

Hadi zanzibari nao nani anawafelisha hao ndugu zenu waislamu?
 
JK atakuwepo kwenye historia ya Dunia, wana JF. Kumbukeni hii kauli atakuwepo kwenye historia ya dunia, for Real we need to pray. Kwa nini nchi inaelekea huko na yeye yupo kimya, je anaamini yu salama kweli. Watu wa ofisini kwake najua mwaingia humu mkamwambie mwambieni atafute namna ya kuweka hili jambo sawa. Hakuna nchi yoyote duniani itaweza kutuaccomodate with such evil and scrap mind, tusije tukawaambukiza ujinga uliokithiri.
 
Pole ndugu, umelishwa sumu ya kutosha, jaribu kufanya utafiti ktk shule ulizodai zina pendelewa
uone mazingira ya shule ikiwemo miundombinu na upatikanaji wa nyenzo za kujifunzia, idadi ya wanafunzi, namna walimu wanavyo fundisha, mchujo unaofanyika
mpaka mwanafunzi kufika siku ya kufanya mtihani wa mwisho (kuna kiwango cha ufaulu hapo).
Kisha linganisha na hizo una zolalamika wamefelishwa utapata jibu.

nimekupa mfano kwa sababu kuna ushahidi wa mwanafunzi aliesoma hapo..hakupendezwa na tabia ile alimsimulia sister wangu na mie nilimuuliza ikiwa ni kweli akatibitisha...hakuna miundo mbinu..kama miundo mbinu nenda pale Al muntanzir hakuna school inayoifikia...kuna kila kitu, walimu watoto wana soma, ushindani mkubwa, lakini NECTA kila siku wana felishwa mpaka sasa wameamua kufanya mitihani ya IGCSE na GCSE ya Cambridge na tangia hapo pale wanafanya vizuri sana ? huu nu ukweli eleimu Tanzania imehijumiwa
 
Hadi zanzibari nao nani anawafelisha hao ndugu zenu waislamu?
zanzibar tatizo shule zote ni za serikali na ukweli kutokana na zengwe lao la muungano nchi imeshindwa kuziendesha shule zao, hakuna walimi hawana vifaa,mwanafunzi wa form 6 ana someshwa na form 6 mwenzake..
wao tatizo lao jengine ..
wao ya kwao ni ya kwao wao wapo wengi waislam itavokuwa watapata nafasu za kusoma mbele ...
tatizo lipo hapa tanganyika kule halihusu
 
Tujenge mtupore tena, zirudisheni kwanza mlizopora then tuendeleze zingine. Duh mjanja kweli wewe ndio umetumwa ushauri hivyo mtupore??
Sote tuliporwa lkn hatukukaa chini na kulalamika tu, tulijipanga upya na kujenga hospital nyingine ambazo selikari
ktk maeneo mengine inazitumia kama hospital za wilaya. Si vibaya kuiga mambo mazuri kwetu hata kama hamkubaliani
nasi kiimani
 
Kama chadema ya kidini huyo mwenye mavazi ya kiarabu hapo ya middle east ni nani? Ni padri huyo?

Mavazi ya kiarabu ni yapi? Hiyo kanzu? Mbona Papa naye anavaa hayo mavazi ya kiarabu ata Pengo naye ndio mavazi yake umeishawahi kumuona Papa au Pengo wamevaa suruali?
 
Nchini Tanzania kumezuka mtafaruku mkubwa juu kile WAISLAM wanachokiita ni MFUMO KRISTO, katika baadhi ya madai yao ni kuwa WAKRISTO kwa kushirikiana na serekali wanaendesha dhuluma na hujuma dhidi ya Uislam.

nimewiwa kuandika haya kutokana na kile ninachokiona kuwa ni UTAPELI MKUBWA unaofanywa na wajanja wachache kujinufaisha KISIASA na KIUCHUMI kwa kupitia mgongo wa DINI huku wakipanda mbegu za chuki na uadui kwenye jamii yetu.

BIBLIA na QURANI vinamtambua SHETANI kama BABA wa uwongo na yeyote anayesema uwongo anaunganishwa na Shetani katika uwongo wake na kuwa kitu kimoja yaani 'shetani' ambaye kwa wakristo wanapaswa kumkemea 'KATIKA JINA LA YESU' na waislam 'KUMLAANI KWA MUJIBU WA QURANI' "ADHUBILAH MINA SHAITWAN RAJIM"

1- katika madai ya baadhi ya wale wanaoupinga MFUMO KRISTO wanamtaja DR SLAA kuwa mwaka wa 1992 alipokuwa katibu mkuu wa baraza la maaskofu la kanisa katoliki TEC akishirikiana na CCT{jumuiya ya makanisaTanzania} walisaini MoU[Memorundum of Understand] kati ya kanisa na serekali,

huu ni uzushi mkubwa, kwani DR SLAA aliondoka TEC mwaka 1991 na siyo 1992, huu ni uongo mkubwa wa shetani anayepaswa kukemewa kwa JINA LA YESU na KULAANIWA KWA MUJIBU WA QURAN "ADHUBILAHI MINA SHAITWANI RAJIM", inavyoonekana hii ni hoja ya KISIASA iliyotengenezwa kipropaganda ili kumdhoofisha mwanasiasa huyu. Hapa napata wasiwasi na kujihoji, ikiwa wamethubutu kudanganya katika hili dogo, JE HAWATAACHA KUTUDANGANYA KATIKA MAMBO MAKUBWA PIA?

2- Watoa madai wanahoji "KWA NINI MKATABA WENYEWE USAINIWE KWA SIRI" hii kwa kweli ni hoja ya KITOTO, ninajua vema ya kuwa wanajua na kutambua kuwa sheria ya jamhuri ya muungano wa Tanzania zinabainisha wazi kuwa "MIKATABA NI SIRI YA SEREKALI" hili halipingiki kwani imekuwa hivyo tangu mwanzo hadi sasa, na wakati huu ndipo watu wanapiga kelele kutaka kipengele hicho cha sheria kifutwe na mikataba yote iwekwe hadharani, hivyo huu ni UWONGO wa pili wa watu hawa wanaopinga mfumo kristo. Vile vile wanasahau kuwa Edward Lowassa alisaini mkataba kama serekali yeye akiwa ni waziri anayetekeleza armi na maagizo halali ya mwenyekiti wa baraza la mawaziri Ndg Al hadji Ali Hassan Mwinyi.

3- watu hao wanadai kuwa "MoU ni njama dhidi ya Uislam", dai hili ni dai la UZUSHI wa kishetani dhidi ya serekali na kanisa, ikiwa MoU ni njama dhidi ya uislam, mbona IMAMU MKUU WA MADHEHEBU YA WAISLAM WA SHIA DUNIANI 'AGA KHANI' amesaini MoU na serekali?. JE MoU ya IMAMU huyu na serekali ni NJAMA DHIDI YA NANI?

4- wazushi hawa wanahoji, uhalali wa uwepo wa "UBALOZI WA VATCAN " nchini. malalamiko ya uwepo wa ubalozi huu yamezuliwa sana kutokana Tanzania kutokuwa mwanachama wa OIC, wakati wakitambua kuwa Vatcan ni nchi huru ndani ya nchi kama ilivyo kwa TAIWANI ambayo nayo ina balozi sehemu mbalimbali duniani japokuwa TAIWAN sii mwanachama wa UMOJA WA MATAIFA UNO, na ingawa TAIWAN inatambulika kama sehemu ya CHINA,
Hii ina maana kwamba OIC sii nchi bali ni taasisi tofauti na hii la VATCAN, wakitambua hilo vema wakahoji "KWA NINI BALOZI WA VATCANI AWAJIBIKE KWA PAPA" ambaye ni MKUU wa KANISA KATOLIKI linaloendesha mfumo kristo? kwa hoja hii wakawaaminisha watu kuwa huu ni uwakala wa aina yake na ni UDINI MKUBWA. lakini wakati huo huo wanashindwa kujihoji juu balozi wa IRANI ambaye moja kwa moja humwakilisha A SUPREME LEADER 'AYATOLLAH KHOMENEY' kiongozi wa kidini. Hapa napo najihoji JE UWAKILISHI HUU WA KIONGOZI MKUU WA KISHIA NDANI YA TANZANIA NAO SII UDINI?

nchini Msumbiji yupo Sheikh mmoja ameandika kitabu kiitwacho "GOVERNANCE AND VULNERABILITTY IN NORTHEN MOZAMBIQUE" eneo hili la kaskazini ndilo linalokaliwa na waislam wengi nchini humo ambao ni 20% ya wakazi wote wa Msumbiji. madai yao ni kuwa serekali ya nchi hiyo kwa kushirikiana na kanisa linaendesha njama na hujuma dhidi ya waislam na ndiyo maana eneo hilo limekuwa masikini na watoto wao hawaendi shule kwa sababu ya dhuluma za MFUMO KRISTO. wakati huo huo MSUMBIJI ni moja kati ya mataifa masikini zaidi duniani yenye idadi ya watu wanaofikia takribani milioni 19. watu milioni 16 wanaishi chini ya kipato cha dola moja kwa siku na watu milioni 11 hawana maji safi ya kunywa.
jambo la kushangaza ni kuwa nchi hii ni mwanachama wa OIC. swali linakuja ' KWA NINI NCHI HII ISITAJIRIKE WAKATI IPO OIC" vile vile najihoji "IKIWA OIC IMESHINDWA KUWASAIDIA WATU 16MILION WA MSUMBIJI, ITAWEZAKE KUWASADIA WATU WA TANZANIA WAPATAO TAKRIBANI 45MILIONI?" mbali na hivyo najiuliza swali jingine "JE NI KWANINI WAISLAM WA MSUMBIJI WANALALAMIKA WAKATI NCHI YAO NI MWANACHAMA WA JUMUIYA YA NCHI ZA KIISLAM' HAPO NDIPO NAPATA WASIWASI juu ya uhalali wa madai ya mfumo kristo kwani AINA ya UANDISHI wa kitabu hicho unafanana sana na ule wa MOHAMMED SAID,

Hii inaonyesha kwamba hili ni dili la wajanja walilolitengeneza na kuwalaghai watu ili kujipatia utajiri kwa kuuza KASETI, VITABU, CD na DVD kwa namna moja ama nyingine kwa kutumia uwongo huu mwingi na udanganyifu mkubwa ili kufikia malengo yao ya kisera tu,
my take
"IF YOU DON'T KNOW WHERE YOUR COMING FROM, YOU WILL DON'T KNOW WHERE YOUR GOING"
MWANAWAVITTO
 
Nchini Tanzania kumezuka mtafaruku mkubwa juu kile WAISLAM wanachokiita ni MFUMO KRISTO, katika baadhi ya madai yao ni kuwa WAKRISTO kwa kushirikiana na serekali wanaendesha dhuluma na hujuma dhidi ya Uislam.

nimewiwa kuandika haya kutokana na kile ninachokiona kuwa ni UTAPELI MKUBWA unaofanywa na wajanja wachache kujinufaisha KISIASA na KIUCHUMI kwa kupitia mgongo wa DINI huku wakipanda mbegu za chuki na uadui kwenye jamii yetu.

BIBLIA na QURANI vinamtambua SHETANI kama BABA wa uwongo na yeyote anayesema uwongo anaunganishwa na Shetani katika uwongo wake na kuwa kitu kimoja yaani 'shetani' ambaye kwa wakristo wanapaswa kumkemea 'KATIKA JINA LA YESU' na waislam 'KUMLAANI KWA MUJIBU WA QURANI' "ADHUBILAH MINA SHAITWAN RAJIM"

1- katika madai ya baadhi ya wale wanaoupinga MFUMO KRISTO wanamtaja DR SLAA kuwa mwaka wa 1992 alipokuwa katibu mkuu wa baraza la maaskofu la kanisa katoliki TEC akishirikiana na CCT{jumuiya ya makanisaTanzania} walisaini MoU[Memorundum of Understand] kati ya kanisa na serekali,

huu ni uzushi mkubwa, kwani DR SLAA aliondoka TEC mwaka 1991 na siyo 1992, huu ni uongo mkubwa wa shetani anayepaswa kukemewa kwa JINA LA YESU na KULAANIWA KWA MUJIBU WA QURAN "ADHUBILAHI MINA SHAITWANI RAJIM", inavyoonekana hii ni hoja ya KISIASA iliyotengenezwa kipropaganda ili kumdhoofisha mwanasiasa huyu. Hapa napata wasiwasi na kujihoji, ikiwa wamethubutu kudanganya katika hili dogo, JE HAWATAACHA KUTUDANGANYA KATIKA MAMBO MAKUBWA PIA?

2- Watoa madai wanahoji "KWA NINI MKATABA WENYEWE USAINIWE KWA SIRI" hii kwa kweli ni hoja ya KITOTO, ninajua vema ya kuwa wanajua na kutambua kuwa sheria ya jamhuri ya muungano wa Tanzania zinabainisha wazi kuwa "MIKATABA NI SIRI YA SEREKALI" hili halipingiki kwani imekuwa hivyo tangu mwanzo hadi sasa, na wakati huu ndipo watu wanapiga kelele kutaka kipengele hicho cha sheria kifutwe na mikataba yote iwekwe hadharani, hivyo huu ni UWONGO wa pili wa watu hawa wanaopinga mfumo kristo. Vile vile wanasahau kuwa Edward Lowassa alisaini mkataba kama serekali yeye akiwa ni waziri anayetekeleza armi na maagizo halali ya mwenyekiti wa baraza la mawaziri Ndg Al hadji Ali Hassan Mwinyi.

3- watu hao wanadai kuwa "MoU ni njama dhidi ya Uislam", dai hili ni dai la UZUSHI wa kishetani dhidi ya serekali na kanisa, ikiwa MoU ni njama dhidi ya uislam, mbona IMAMU MKUU WA MADHEHEBU YA WAISLAM WA SHIA DUNIANI 'AGA KHANI' amesaini MoU na serekali?. JE MoU ya IMAMU huyu na serekali ni NJAMA DHIDI YA NANI?

4- wazushi hawa wanahoji, uhalali wa uwepo wa "UBALOZI WA VATCAN " nchini. malalamiko ya uwepo wa ubalozi huu yamezuliwa sana kutokana Tanzania kutokuwa mwanachama wa OIC, wakati wakitambua kuwa Vatcan ni nchi huru ndani ya nchi kama ilivyo kwa TAIWANI ambayo nayo ina balozi sehemu mbalimbali duniani japokuwa TAIWAN sii mwanachama wa UMOJA WA MATAIFA UNO, na ingawa TAIWAN inatambulika kama sehemu ya CHINA,
Hii ina maana kwamba OIC sii nchi bali ni taasisi tofauti na hii la VATCAN, wakitambua hilo vema wakahoji "KWA NINI BALOZI WA VATCANI AWAJIBIKE KWA PAPA" ambaye ni MKUU wa KANISA KATOLIKI linaloendesha mfumo kristo? kwa hoja hii wakawaaminisha watu kuwa huu ni uwakala wa aina yake na ni UDINI MKUBWA. lakini wakati huo huo wanashindwa kujihoji juu balozi wa IRANI ambaye moja kwa moja humwakilisha A SUPREME LEADER 'AYATOLLAH KHOMENEY' kiongozi wa kidini. Hapa napo najihoji JE UWAKILISHI HUU WA KIONGOZI MKUU WA KISHIA NDANI YA TANZANIA NAO SII UDINI?

nchini Msumbiji yupo Sheikh mmoja ameandika kitabu kiitwacho "GOVERNANCE AND VULNERABILITTY IN NORTHEN MOZAMBIQUE" eneo hili la kaskazini ndilo linalokaliwa na waislam wengi nchini humo ambao ni 20% ya wakazi wote wa Msumbiji. madai yao ni kuwa serekali ya nchi hiyo kwa kushirikiana na kanisa linaendesha njama na hujuma dhidi ya waislam na ndiyo maana eneo hilo limekuwa masikini na watoto wao hawaendi shule kwa sababu ya dhuluma za MFUMO KRISTO. wakati huo huo MSUMBIJI ni moja kati ya mataifa masikini zaidi duniani yenye idadi ya watu wanaofikia takribani milioni 19. watu milioni 16 wanaishi chini ya kipato cha dola moja kwa siku na watu milioni 11 hawana maji safi ya kunywa.
jambo la kushangaza ni kuwa nchi hii ni mwanachama wa OIC. swali linakuja ' KWA NINI NCHI HII ISITAJIRIKE WAKATI IPO OIC" vile vile najihoji "IKIWA OIC IMESHINDWA KUWASAIDIA WATU 16MILION WA MSUMBIJI, ITAWEZAKE KUWASADIA WATU WA TANZANIA WAPATAO TAKRIBANI 45MILIONI?" mbali na hivyo najiuliza swali jingine "JE NI KWANINI WAISLAM WA MSUMBIJI WANALALAMIKA WAKATI NCHI YAO NI MWANACHAMA WA JUMUIYA YA NCHI ZA KIISLAM' HAPO NDIPO NAPATA WASIWASI juu ya uhalali wa madai ya mfumo kristo kwani AINA ya UANDISHI wa kitabu hicho unafanana sana na ule wa MOHAMMED SAID,

Hii inaonyesha kwamba hili ni dili la wajanja walilolitengeneza na kuwalaghai watu ili kujipatia utajiri kwa kuuza KASETI, VITABU, CD na DVD kwa namna moja ama nyingine kwa kutumia uwongo huu mwingi na udanganyifu mkubwa ili kufikia malengo yao ya kisera tu,
my take
"IF YOU DON'T KNOW WHERE YOUR COMING FROM, YOU WILL DON'T KNOW WHERE YOUR GOING"
MWANAWAVITTO

Hapo kwenye Red ndipo penye hoja nzito. Ni vizuri ponda na genge lake la wahuni wakajibu hizi hoja.

 
Cha kusikitisha hawa wanaoeneza uzushi na uongo huu wanapata wafuasi miongoni mwa wale walioambiwa waitafute elimu hata kama itawabidi kwenda China....sasa sijui wote hawajenda China wamebakia mambumbumbu tu wasiojua hata alif beeh...sad!
 
Zaidi ya Msumbiji Baadhi ya nchi zingine zilizo OIC ni
1. Guinea Bisau
2. Gambia
3.Sierra leone
4.Togo
5. Somalia (Toba!!!)
6. Chad
n.k
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom