Idimi
Platinum Member
- Mar 18, 2007
- 15,625
- 11,635
Kama suala ni demokrasia, nadhani kuanzia CCM hadi upinzani hakuna wa kumcheka mwenzake. Masahibu yaliyompata Mzee Malecela, Horace Kolimba, Salim Ahmed Salim na wengine ndani ya CCM ni ushahidi tosha. Ndo demokrasia hiyo hiyo inayowashinda CUF, kwa kuwa Lipumba ni mgombea pekee wa Uraisi kupitia chama hicho, tangu niifahamu CUF mwaka 1994. Ni yale yae kwa John Cheyo wa UDP na Mrema wa TLP. Kama kuna demokrasia huko mtoa mada anakodhani ipo, kwa nini nafasi ya mwenyekiti wa CCM haishindaniwi, ila ni ya kuachiana?