Ulinichukulia kadi ya CHADEMA ama kunipa kambi humo?
Yaani mapungufu yakisemwa basi ishakuwa masuala ya makambi. Acheni kulazimisha siasa za fikra na mawazo mgando.....
Ili kuendelea ni wajibu kuwepo na mitizamo na fikra tofauti na mapungufu na hata mafanikiwa kusemwa wazi bila ya uzandiki, ukada na hata unafiki...
Tanzanianjema itajengwa na Utanzania na sio ukada.....na ushabiki wa kimakundi uliojaa unafiki
omarilyas
Kumbe kuna wakati akili zako huwa zinafanya kazi vizuri?Zitto ni msomi mwenye upeo mkubwa sana. Uwepo wake katika siasa za Tanzania ( Bungeni ) umeleta mwelekeo mpya wa uendeshaji wa bunge letu na siasa kwa kitaifa kwa ujumla wake.
Kama binadamu ana mapungufu yake, lakini by far mapungufu yana out-weigh mazuri.
Sakata la mikataba ya madini, ufisadi na hata kuanguka kwa serikali nzima (Richmond-gate) kote huko kna mkono wa Zitto.
Jamaa kwa umri wake na hata elimu yake amefanya makubwa sana kwenye siasa zetu kuliko akina Mzindakaya ambao tuna wasikia toka tukiwa wadogo, tunasoma na mpaka tu watu wazima. Wengine kwenye mabenchi yao bungeni kuna vishimo kwa kupiga makofi kuunga mkono miswada mbalimbali ya serikali.
Hakuna ubaya kutoa criticism kwani kwa namna bora kunamjenga na kumsadia mlengwa, lakini wengine mnakuwa critical kwa minajili ya kumkatisha mtu tamaa kwa sababu tu ya msimamo wake fulani ambao kwa namna moja au nyingine mtu haukumfurahisha. Nitoe mifano miwili ya haraka; suala la Zitto kugombea uenyekiti Chadema na yaliyojiri kutokana na hatua hiyo yameacha makovu kwa baadhi ya watu, lakini we need to get over it and move on. Whether it was bad move or good one let by gone be by gone. La pili suala la Dowans, hili limewagawa watu ( hususan washabiki/wenye mapenzi na Zitto ) kwenye mapande mawili. Ninachotaka kusema hapa ni kuwa katika hili Zitto kaweka msimamo wake tena very firm na if anything jamaa ndio kiongozi pekee alie wa face watanzania na kuwaeleza nini kifanyike kuliko hata hao wenye dhamana waliojifungia ndani na kushindwa kusema kitu. Haikuwa nia yangu kuleta mjadala wa Dowans hapa, lakini ninachotaka kusema Zitto ni zaidi ya Uenyekiti wa Chadema na Dowans, ana potential kubwa sana kwa taifa apewe ushirikiano sio kukatishwa tamaa na kama kuna criticism then basi ziwe constructive one.
Kama upo Tanzania ama unaweza kwenda katika mitandao mingine zaidi ya jamiiforums basi nenda katika THE CITIZEN la jumapili upate jibu lako. Kama serikali ingekuwa na nia/uthubutu ya kununua mitambo ya DOWANS amabyo ukweli si CHAKAVU kama vijembe vya kisiasa visemavyo nina uhakika ingeweza kununuliwa hata kwa nusu ya thamani yake. Ukiangalia hali ya kisiasa na uwezekano na gharama pamoja na deni la mabilioni DOWANS wanayodaiwa na serikali ni wazi kukipataikana negotiators wenye mapenzi na uzalendo uliotukuka na nchi hii, mitambo hiyo inaweza kununuliwa hata kwa nusu ya thamani yake ambayo THE CITIZEN wanadai ni bilioni 60. Na hapo bado faida ya kuepuka ngarama za kuibadili kutumia gesi kwani tayari inaweza kutumika hivyo(kadiri nijuavyo mimi).
.Huku ndiko kunaitwa kujistukia. Ni lini Zitto amewahi kusema ama hata kuwataja hao kina Mwakyembe? Yaani waboronge kwa faida na nafasi zao kisiasa halafu waanze kutafuta mchawi wa makosa yao?
Yaani ninyi kama kitu hakijaandikwa magazeti basi ni lazima hakikufanyika? Uliwahi kuhudhuria vikao vya kamati yake na Tanesco ama Wizara ya nishati ama hata BOT na ukaona kuwa Zitto hajawahi kuhoji hayo maswali? Hivi pia unadhani matatizo tunayokumbana nayo sasa yataisha kwa kununua mitambo ya kuzalisha umeme halafu basi. Unajua mchakato wa ENERGY BILL ulivyokwenda na nini kinaendelea kuhusu NATIONAL ENERGY MASTER PLAN pamoja na masuala mengie ya KISERA? Je umejaribu kufuatilia nini mchango wa Zitto katika hayo yote?
Again, acha uzandiki na kujistukia....Lini alisema hayo? Yaani mtu kueleza hatari zinazokumba taifa na kutoa mawazo yake jinsi ya kulishughulikia suala hilo kama alivyofanya Zitto wewe ulichoweza kusikia ni maneno yasiyokuwepo.
Hivi kati ya Zitto na hao MASIHA FEKI wenu ni nani ameishia kuwa distraction? Yaani anayekuja na maoni ya jinsi ya kushughulikia tatizo na anayekuja na msemo wa tukae na giza ili mradi adui wao ndani ya chama chao asiweze kufurukuta kama wanavyodai wao, yaani nchi isimame hadi hapo watakapomalizana wao, ni nani anaplay politics of distraction?
Zitto has always been proactive on issues however controversial or risky they entail, kitu ambacho wengi wetu tumejengewa mentality ya kukiogopa ama kutokiamini......
Acha mitizamo ya kuna uwezekano, unashindwa kufanya utafiti wa kujua anayoyafanya, basi hata hili la kujua marafiki ama washauri wake unashindwa kulifanya? Do ur work ndugu, hapo ndipo tutakuwa na mamia ya kina Zitto ....
Sasa kama chama chake kimekosa uthubutu ama kimegubikwa na ugoigoi wa kimikakati ama wameamua kuchukua hoja nyepesinyepesi kama ufisadi tu ambayo tayari wameshanyang'anywa, bado tu unataka kumlazimisha asubiri misimamo yao.
Lakini pia una uhakika kuwa matamshi yake hayana mahusiano na chama chake ama mradi umesikia wenzake wachache wenye kuweka mbele tofauti zao binafsi na kuzifanya za kichama wanapodai kuwa huo sio msimamo wa chama basi ndio hivyo. Wakati alipoitisha mkutano wa waandishi wa habari hakuwa na watu wa chama chake? Hivi Tumbo sio mkurugenzi wao wa habari? ama mpaka akiwa na kina Mrema, Wilbord, Mbowe, Ndesamburo ndio utakuwa mtazamo wa CHAMA?
Omary tatizo lako huna kazi na hivyo umebakia na kazi moja ya kuandika ambayo unafikiri ni ya kumjenga Zitto huku ukiwatukana wengine wote kwa sababu tuu hawako tayari kuunga misimamo ya Zitto mkono ambayo inayumba .
Tangu huyu Omarillyas amalize chuo pale mlimani na Zitto mwaka 2002 ameishia kukaa karibu na wakina Membe hapo wizara ya mambo ya nje na kutumwa kama messanger wa wizara mara leo yuko naye Sullivan huku akijua kabuisa kuwa mkutano wa Sullivan uko ama ulikuwa kwa ajili ya wafanya biashara na wajasiriamali yeye humo alienda kama nani wengine hatujui.
Pili , kila mara anaenda Newyork kwenye ubalozi wa Tanzania kule na amekuwa mzigo kw3a wafanyakazi wa ubalozi na mpaka sasa wizarani kuna malalmiko mengi sana juu ya majungu yake ambayo amekuwa akiyaleta kwa sababu anazozijua yeye binafsi kutokana na yeye kujikuta yupo karibu na Membe pamoja na wakina Jack Gotham enzi zile za Great lake region....
Omary kukusaidia wewe nenda katafute kazi ya kufanya ili uwe bize na hilo litaweza kumpunguzia Zitto presha ambazo zinatokana na wewe kukosa kazi ya kufanya na hivyo kila mara unakuwa unampotosha .
Lingine tafuta chama cha siasa na jiunge nacho kama hao CHADEMA hawakufai wewe nenda kajiunge na kingine utakachoona kuwa kunafaa zaidi.
Ondoa kambi ya Salim kwani mpaka sasa JK ndio anaongoza hivyo hata ukiwa na hasira za kunyimwa kazi Foreign usitake kuwahusisha CHADEMA.
Nimempa ushauri huyu mdogo wangu kwani naamini sasa yeye ndio anatumiwa kuwavuruga viongozi wa CHADEMA na haswa kwa kumtumia Zitto katika kufanikisha kazi hiyo ambayo anaifanya.
Kuhusu Zitto, anapaswa kutulia na kuondoa vinyongo na visasi, anayempinga asimuone kama adui ila awe tayari kukaa naye na kumuuliza sababu za huyo mtu kumpinga na akiona ana sababu za msingi ajifunze ila akiona hazina maana basi ampuuze ila kimoyomoyo na kuondoka zake.
Pili, aachane na wapambe ambao ni nuksi na kila anachowaambia wao hawatofautiani naye , hao hawatamfikisha popote pale zaidi ya kumwangamiza kisiasa.
Zitto Kabwe said:Kwa kuwa mapendekezo ya TANESCO ya kununua mitambo ya kampuni ya Dowans yalipingwa na baadhi ya wanasiasa wenzangu na hatimaye kutonunuliwa na hivyo kusababisha mgawo uliopo hivi sasa, na kwa kuwa mitambo ile inaweza kuingiza 125MW katika gridi ndani ya siku moja na kumaliza kabisa mgawo uliopo hivi sasa na kuliokoa Taifa na kuhami uchumi wetu, na kwa kuwa mitambo ya Dowans inahusishwa na mkataba wa kifisadi wa Richmond, ninaishauri serikali itaifishe mara moja kampuni ya Dowans.
Wana JF tukiendekeza post kama hizi, kesho watasemwa wake zetu humu na watoto wetu.
Kama umeshamweleza hayo 'madhaifu' yake unaandika hapa ili iweje? tujue unamjua sana Omarlyas, na je uluyoyaandka ni ya kweli? yeye anaufahamu wewe kwa jina halisi? maan yeye anajiandika kwa jina halisi!
Hii aina faida si kwako tu, bali hata kwa JF kwa ujumla, tarifa hii ipeleke kwa Shigongo ili auze magazeti, akugawie japo hela kidogo
Mwisho, kujificha ficha ni ishara ya uoga, mface mweleze, SISI TUNATAKA IDEAS TU HAPA, NA SIO FULANI JANA KALA DAGAA , LEO KAENDA MAREKANI! soooo whaaat!!
Omary tatizo lako huna kazi na hivyo umebakia na kazi moja ya kuandika ambayo unafikiri ni ya kumjenga Zitto huku ukiwatukana wengine wote kwa sababu tuu hawako tayari kuunga misimamo ya Zitto mkono ambayo inayumba .
Tangu huyu Omarillyas amalize chuo pale mlimani na Zitto mwaka 2002 ameishia kukaa karibu na wakina Membe hapo wizara ya mambo ya nje na kutumwa kama messanger wa wizara mara leo yuko naye Sullivan huku akijua kabuisa kuwa mkutano wa Sullivan uko ama ulikuwa kwa ajili ya wafanya biashara na wajasiriamali yeye humo alienda kama nani wengine hatujui.
Pili , kila mara anaenda Newyork kwenye ubalozi wa Tanzania kule na amekuwa mzigo kw3a wafanyakazi wa ubalozi na mpaka sasa wizarani kuna malalmiko mengi sana juu ya majungu yake ambayo amekuwa akiyaleta kwa sababu anazozijua yeye binafsi kutokana na yeye kujikuta yupo karibu na Membe pamoja na wakina Jack Gotham enzi zile za Great lake region....
Omary kukusaidia wewe nenda katafute kazi ya kufanya ili uwe bize na hilo litaweza kumpunguzia Zitto presha ambazo zinatokana na wewe kukosa kazi ya kufanya na hivyo kila mara unakuwa unampotosha .
Lingine tafuta chama cha siasa na jiunge nacho kama hao CHADEMA hawakufai wewe nenda kajiunge na kingine utakachoona kuwa kunafaa zaidi.
Ondoa kambi ya Salim kwani mpaka sasa JK ndio anaongoza hivyo hata ukiwa na hasira za kunyimwa kazi Foreign usitake kuwahusisha CHADEMA.
Nimempa ushauri huyu mdogo wangu kwani naamini sasa yeye ndio anatumiwa kuwavuruga viongozi wa CHADEMA na haswa kwa kumtumia Zitto katika kufanikisha kazi hiyo ambayo anaifanya.
Kuhusu Zitto, anapaswa kutulia na kuondoa vinyongo na visasi, anayempinga asimuone kama adui ila awe tayari kukaa naye na kumuuliza sababu za huyo mtu kumpinga na akiona ana sababu za msingi ajifunze ila akiona hazina maana basi ampuuze ila kimoyomoyo na kuondoka zake.
Pili, aachane na wapambe ambao ni nuksi na kila anachowaambia wao hawatofautiani naye , hao hawatamfikisha popote pale zaidi ya kumwangamiza kisiasa.
Dkt. Salim Ahmed Salim-The only African south of SAHARA who nearly became the secretary General of UN and lost it because of his ideological stand and that of his Boss Julius Nyerere
Sijui tatizo ni lugha au? Kwa sababu mara ya mwisho kuangalia Kofi Annan kutoka Ghana alikuwa katibu mkuu wa umoja wa mataifa kwa vipindi viwili.
teh teh teh,
Julius, si unajua tena Ghana iko eastern south america or whatever that was and should be. Ghana haiko chini ya sahara kwa mujibu wa wengi tu akiwemo Zitto Kabwe (mb).
Sijui tatizo ni lugha au? Kwa sababu mara ya mwisho kuangalia Kofi Annan kutoka Ghana alikuwa katibu mkuu wa umoja wa mataifa kwa vipindi viwili.
Correct it. Nimepitiwa tu. Nashukuru kwa kunisahihisha. Isomeke the first from Africa south of Sahara...........
Mheshimiwa Zitto,
Ghana ni south of Sahara.
Correct it. Nimepitiwa tu. Nashukuru kwa kunisahihisha. Isomeke the first from Africa south of Sahara...........
Zitto,
kumbe nawe unamkubali Salim A Salim?
Haya mambo ya kijinga kijinga ndio huturudisha nyuma nchini. Umbeya umbeya na majungu majungu. Hoja hapa ni Mbunge anayeitwa Zitto na siyo Omar.
Pili, bila hata ruhusa ya Omar mwenyewe ninataka niseme wazi wazi kuwa Omar ana kazi. Kama mnadhani kazi ni kuajiriwa katika ofisi na kuamka asubuhi kwenda basi lazima kichwani hakuko sawa. Omar amejiajiri na anafanya kazi zake kama consultant. Ubalozini New York huenda kwa sababu ya utafiti wake kuhusu UN.
Tatu, Omar Ilyas ni Msaidizi Maalumu wa Dkt. Salim Ahmed Salim - The President of Tanzania who never became. The longest serving ex Secretary General of the OAU, The only African south of SAHARA who nearly became the secretary General of UN and lost it because of his ideological stand and that of his Boss Julius Nyerere, The only Tanzanian who Nyerere asked to contest (mtasema Mkapa, sio kweli Mkapa alipelekewa na Jenerali Ulimwengu na Patrick Qorro kama alternative ya Salim), The Ex- Premier and Minister of Defence and a Board member of Mo Ibrahim Foundation.
Salim ni chuo Kikuu of his own. Omar ni sawa na mfanyakazi wa library ya chuo kikuu kilichosheheni vitabu vinavyosema.
Unathubutu kusema hana kazi?
Haya mambo ya kutenganisha bara letu ni kasumba ya Kikoloni. Binadamu wote ndugu zangu - kuanzia Ahmed Ben Bella, Boutrous Boutrous Ghali mpaka Trevor Manuel na Jacob Zuma - ndugu zangu na Afrika - kuanzia Cape Town had Cairo - ni Moja! Mungu Ibariki Afrika. Wabariki na Watu wake wote. Amina.