DECI Tanzania: Ilivyoanza, ilipo na hatma yake

DECI Tanzania: Ilivyoanza, ilipo na hatma yake

Sure GT
Kama chama la DECI lingekuwa chini ya masheikh kibali mida kingekuwa kishatolewa biashara kama kawa

Aa wapi! Sheria ya nchi imeweka Pyramid Schemes katika Penal Code. Hakuna cha mwislamu au mkristo! Acha kujaribu kupindisha wizi huu wa DECI. Ni wizi full stop!
 
Heshima wanaBodi, kwa kweli bahati nzuri au mbaya mimi naamini kwamba hili ni dili la kuibia watu..... Kama ilivyoandikwa kwenye Cheche, tatizo letu ni kwamba tumezoea "quick and easy bucks". Hivi wewe hujiulizi unaweka pesa leo kesho unachukua zaidi, jamani hebu nasi tuwe na kaupeo kidogo kakuangalia na kukubali kwamba huu ni usanii na utapeli wa hali ya juu....

Kuna kijihabari kakuelezea whatsup nimekasoma kule kwa Michuzi and I must say, jamaa aliyekiandika ameweza onyesha real facts na sio siasa zetu za Kibongobongo, kisaniisanii na mambo kama hayo.....

Hebu angalia hapa:

libeneke la DECI: Wajinga ndio waliwao???
deci.jpeg


Warning Guys!
That's known as pyramid scheme. Very few people get rich, the ones who run this idiotic scheme. It has made a lot of people more poor. It operated in South Africa, Zimbabwe, Germany and UK. In actual fact its a criminal offence in UK and if caught you end up in Jail.

Unaweza google au nenda wikipedia na search Pyramid scheme. Mchongo wenyewe wa kuingizana mjini inakuwa kama ilivyoelezwa hapo chini
--------------------------------------------------


1: Kijiji kina watu 10000

2. Watu wa 10 wa kwanza wasio na fedha wanaanzisha mradi wa DECI. Wanasema kujiunga nao ni Shs. 200,000Watu 1000 wanajiunga kwa kutoa Tsh200,000 kila mmoja. (Kijiji kinabakia na watu 8990. Kwa kiyo Mtaji wa kwanza ni: Tsh. 200,000,000 (za wale watu 10)Hawa wanaambiwa wasubiri miezi minne ili “wavune” faida.


3. Wanatangaza na watu wengine 1500 wanajiunga kijiji kinabakiwa na watu 7490Watu wale 1500 wanaleta mtaji mpya wa milioni 300,000,000 Miezi minne inapopita wale 1000 wa kwanza wanalipwa fedha yao milioni 200, na kila mmoja anapata “faida” ya laki moja moja hivyo kila aliyeingia na laki mbili miezi minne anatoka na laki tatu!


4. Wanaingia watu wengi zaidi sasa nao wanafikia 2000 nao wanataka haya mavuno! Kijiji kinabakiwa na watu 5490 ambao sio wanachama.


5. Wale watu 2000 wanaingia na mtaji wa 400,000,000. Sasa hapa ndipo kuna kitu cha kuangalia vizuria. kuna watu 1500 ambao wanatakiwa kulipwa laki mbili zao (kwa jumla ya milioni 300 za mbegu). Lakini pia wanatajia kupata kila mmoja laki moja zaidi kama faida.b. Hivyo pamoja na kiasi hicho unatakiwa mradi wa milioni 150 zaidi kama faida ya kundi lile la pili.c. Kiasi hicho kinatolewa kwa wale waliokuwa na milioni 400 na hivyo kufanya wale wanaoingia na milioni mia nne kimsingi kuwa wamekingia na milioni 250! (hilo si tatizo kwa sasa). d. So wale wa kundi la pili wanaondoka na wao na laki tatu tatu kwa furaha ya “mvunaji”


6. Hivyo kampuni yetu inaanzisha recruitment drive nyingine na watu wengine 3000 wanajiunga na kampuni yetu hii ya mavuno. Kijiji kinabakiwa na 2490 ambao wengi wao wanaonekana kuwa ni wanachama wa JF!! Hao nao wanaingia na mtaji wa 600,000,000!


7. Hivyo muda umefika wa kuwalipa walioingia na milioni 400! So wale milioni mia nne kwanza wanalipwa “seed money yao) ambayo ni kiasi hicho hicho. Lakini wanataka faida yao ya laki moja moja kila mmoja. - Hivyo zinahitajika milioni 200 nyingine na hivyo kuchukua kabisa mtaji wa wale wa milioni 600, kuwalipa wao na hivyo wale wa milioni 600. So wale wa milioni mia nne wanaondoka kwa furaha kwani wamepata fedha yao.


8 Wale wa milioni mia sita (ambao ni wengi zaidi – 3000) na wenyewe wanaambiwa wasubiri fedha zao hadi mwisho wa miezi minna. 9. Sasa recruitment inaenda na kuwashawishi wale 2490 waliosalia kijijini kujiunga ili “wavune. Nao wanaingia na mtaji wa 498000! (mara moja tunaona kuwa wanaingia na kiasi pungufu. Kampuni yetu ifanye nini basi; 10. Kampuni inawashawishi wale waliokwisha pewa mavuno yao kuzizungusha fedha hizo hizo tena kwenye mfumo huo. Kwa hiyo wale wa 1000, na wale 1500 na wanatakiwa kuzungusha fedha zao humo kwa humo.


NOW THIS HOW THE SYSTEM COLLAPSES
SCENARIO ONE:

a. Baada ya wale 2490 kuingia na kulipa milioni 498 wale wa milioni 600 watajikuta wanapungukiwa Sh 102! Bila ya fedha kuzungushwa tena kundi la milioni 600 wataanza kulalamika.

b. Wakati hao wanaanza kulalamika kundi lile la 2490 linasubiri kiasi walichoingia nacho (kwa maana angalau waliokwishalipwa awali idadi kama yao wawe wamzungusha tena fedha). Na pia wanasubiri milioni 249 kama faida! (kwa maana ya kwamba wanahitajika watu wengine kama 50 hivi kujiunga kuweza kuzalisha hiyo faida.


SCENARIO TWO:

a. Hii inategemea idadi ya watu ambao wako tayari kuzungusha fedha zao ndani kwa ndani. Kinachofanyika hapa ni saikolojia ya fedha. Wakikupa laki moja faida na wakakuambia uziingize tena kwenye system itabadi urudishe laki mbili kwao tena, na wewe unabakiwa na laki moja! Katika mfano halisi wa DECI ni kwamba wanakulipa laki tatu, na unaweza kuzirudisha kwa mafungu laki mbili mbili, hivyo utarudisha kwao zile za kwako (laki mbili) za kwao (laki mbili) na wewe unabakia na laki moja! Ulichofurahia kimsingi ni wewe kuwa na “laki tatu” kwa muda fulani, siyo kuzitumia.




b. Hili hata hivyo linatabia ya kuchosha huwezi kuwa na fedha usiyoitumia! Hivyo collapse ya pili itatokea pale watu ambao wamekuwa wakizungusha fedha zao huko kwenye kampuni watakapoamua kuziondoa kwenye mzunguko! Kwa maneno mengine wale 1000, na wale 2000 na wale wa 3000 watakapoamua kuondoka na fedha zao wale wa mwisho 2490 watajikuta wameliwa karibu milioni 500!
Hahahahaaa, Hapo wadau mkilizwa kwa kuingia mkenge huu kicha kichwa msianze oooohh hamkutustua mapema, mara ooooohh JK mbaya kuruhusu haya, mara oooooohhh kwa nini serikali isipige marufuku kama ilivyokuwa Kenya. Eh Kalagheni baho, ila mnaambiwa hii ni kanyaboya mwenye macho asikie na mwenye masikio na aone!
 
Heshima wanaBodi, kwa kweli bahati nzuri au mbaya mimi naamini kwamba hili ni dili la kuibia watu..... Kama ilivyoandikwa kwenye Cheche, tatizo letu ni kwamba tumezoea "quick and easy bucks". Hivi wewe hujiulizi unaweka pesa leo kesho unachukua zaidi, jamani hebu nasi tuwe na kaupeo kidogo kakuangalia na kukubali kwamba huu ni usanii na utapeli wa hali ya juu....

Kuna kijihabari kakuelezea whatsup nimekasoma kule kwa Michuzi and I must say, jamaa aliyekiandika ameweza onyesha real facts na sio siasa zetu za Kibongobongo, kisaniisanii na mambo kama hayo.....

Hebu angalia hapa:

Morani mtu wa kawaida hafikiri hivyo.. yeye anaangalia faida iliyopo na akilingannisha na hasara inayowezekana basi faida ile inazidi potential problems kwa wakati huu.
 
Heshima wanaBodi, kwa kweli bahati nzuri au mbaya mimi naamini kwamba hili ni dili la kuibia watu..... Kama ilivyoandikwa kwenye Cheche, tatizo letu ni kwamba tumezoea "quick and easy bucks". Hivi wewe hujiulizi unaweka pesa leo kesho unachukua zaidi, jamani hebu nasi tuwe na kaupeo kidogo kakuangalia na kukubali kwamba huu ni usanii na utapeli wa hali ya juu....

Kuna kijihabari kakuelezea whatsup nimekasoma kule kwa Michuzi and I must say, jamaa aliyekiandika ameweza onyesha real facts na sio siasa zetu za Kibongobongo, kisaniisanii na mambo kama hayo.....

Hebu angalia hapa:


Morani.. hiyo ni makala yangu ya Januari 14 ipo hapa kwenye ile makala ya DECI: Ni nini? Kwenye Cheche ya leo nimeipanua kidogo kwenye kuelezea kubomoka kwa Piramidi scheme kwa namna rahisi zaidi bila kutumia namba nyingi.
 
Deci deci decidecideciiii....naona mjadala huu unatuchosha sasa...cha msingi na maazimio ya msingi ni haya
1- DECI NI WIZI MTUPU...MAJIBU YAKE YATATOKE PALE WATANZANIA WOTE 40M WATAKAPOKUWA WAMEWEKA PESA YAO YOTE @ LAKI2 NA JAMAA WAKAPOTEA NA PESA HIYO
2- ZE WAYFORWARD...ACTIONS TO TAKE....maendeleo ya mwanadamu yanaletwa kwa mipangilio mizuri ya sera na utekelezaji wake (SERIKALI NDIO ACTOR MKUU HAPA)...Maendseleo yanaletwa na wananchi wenye KIU na NIA ya kuyapata hayo maendeleo kupitia kufanya kazi kwa bidii na kuserve kiasi wakipatacho katika kazi zao ili kiweze kuwa -invested zaidi kwenye filds zingine...hapa kwa wanachi naomba nigusie tena...wawezeshwe kupata mikopo isiyo au yenye riba kiasi kidogo..not more than 5% na masharti yawe rahisi ili mikopo iweze kumfikia kila mtanzania mwenye nia ya ku-access hizo funds.....mabilioni ya jk sio solution ya matatizo ya watanzania hasa walio duni kimaisha.......
NAOMBA MJADALA UENDELEE KUANZIA NILIPOISHIA MIMI....hitimisho la DECI iwe ni nini kifanyike baada ya kukgundua another AXIS OF EVIL kupitia kwa watumishi wa mungu.
 
Tatizo ni frustrations za maisha za wananchi wetu. Waliahidiwa maisha bora, wakashuhudia wachache wakijichotea mabilioni na wao wakiendelea kubakia hohehahe. Mbaya zaidi, wakaanza kuchkwa kuwa ni wajinga na wanawaonea wivu wajanja wenye peda. Wengine wakafikia hatua ya kukufuru kuwa hizo pesa walizokuwa nazo ni vijisenti tu.

Katika jamii ya watu waliokuwa frustrated namna hiyo , ni rahisi sana kwa matapeli kama hawa wa Deci kujiingizza na kujipatia na wao hata kile kidogo ambacho masikini hawa walidhani kuwa wanacho. Ama kweli, wenye nacho watazidi kuzidishiwa na sisi tunaendelea kugawama umasikini kila siku
 
Morani mtu wa kawaida hafikiri hivyo.. yeye anaangalia faida iliyopo na akilingannisha na hasara inayowezekana basi faida ile inazidi potential problems kwa wakati huu.

Mkuu M.M.M, kwa kweli hapo umesema ukweli usiopingika kuhusu sisi waTanzania, hatuna "vision", sisi twaangalia leo na leo pekee. Kesho, next week, next year, 10 years ahead haya hayapo kwenye vocabulary zetu. Nakumbuka usemi wa "Ponda mali kufa kwaja", nina uhakika hili lilisemwa kwa vile wahenga waliona wapi tulipokuwa tuna pwaya.... Hili la kutokuangalia mbeleni kwa kweli naweza kusema ni sababu kubwa ya matatizo yetu (kama sio yote basi ni asilimia 99%) ya sasa na hata yale ya baadae (angalia umeme, msongamano wa magari, mipango miji, maji safi, maji taka, mafuriko, .... and the list goes on and on and on).

Morani.. hiyo ni makala yangu ya Januari 14 ipo hapa kwenye ile makala ya DECI: Ni nini? Kwenye Cheche ya leo nimeipanua kidogo kwenye kuelezea kubomoka kwa Piramidi scheme kwa namna rahisi zaidi bila kutumia namba nyingi.

Kwalo hilo Mkuu M.M.M naomba niseme "I salute you, your vision and your intel"....... Keep up the good job!!!
 
Ntasubiri ripoti ya tume kama imeundwa na ikionyesha kuwa kulikuwa na oversight upande wa BOT na jamaa wa capital markets Authority na kama watu watapoteza pesa then sawa

wakishamaliza hiyo itakuwa vizuri wakaingilia na ile ponzi sheme ya staff wa Usalama wa taifa kule masaki

maana isije kuwa DECI inabebewa bango lakini zingine zinaachiwa
 
Ntasubiri ripoti ya tume kama imeundwa na ikionyesha kuwa kulikuwa na oversight upande wa BOT na jamaa wa capital markets Authority na kama watu watapoteza pesa then sawa

wakishamaliza hiyo itakuwa vizuri wakaingilia na ile ponzi sheme ya staff wa Usalama wa taifa kule masaki

maana isije kuwa DECI inabebewa bango lakini zingine zinaachiwa

ah nakupata ile ulitaja kuhusu Gavana kujiuzulu na hiyo ikaashiria umeshaorient responsibility kwa Ndullu na si mtu mwingine.

Hiyo ya jamaa wa usalama nayo inaendaje maana kama unavyosema yawezekana DECI ni kubwa iliyogundulika lakini kuna nyingine zinaendelea pembeni. Ifichue tu mkuu watu waichunguze. Si unajua hata DECI iliibuliwa kwanza hapa Januari 13?
 
ah nakupata ile ulitaja kuhusu Gavana kujiuzulu na hiyo ikaashiria umeshaorient responsibility kwa Ndullu na si mtu mwingine.

Hiyo ya jamaa wa usalama nayo inaendaje maana kama unavyosema yawezekana DECI ni kubwa iliyogundulika lakini kuna nyingine zinaendelea pembeni. Ifichue tu mkuu watu waichunguze. Si unajua hata DECI iliibuliwa kwanza hapa Januari 13?

ya jamaa wa uslama iko poa na namjua mtu last week alipata 3million baada ya kuingiza 6 million

na yenyewe huingii hivi hivi lakini mpaka hohe hahe kama mimi nishaletewa basi sidhani kama itakuwa na tatizo...unajua hizi Ponzi schemes huwa ziningia nyani pale wateja walionazo wanapoanza kupungua

DECI walichemsha kuambia watu waandike basua za sababu ya kutaka kutoa pesa zao
 
ya jamaa wa uslama iko poa na namjua mtu last week alipata 3million baada ya kuingiza 6 million

na yenyewe huingii hivi hivi lakini mpaka hohe hahe kama mimi nishaletewa basi sidhani kama itakuwa na tatizo...unajua hizi Ponzi schemes huwa ziningia nyani pale wateja walionazo wanapoanza kupungua

DECI walichemsha kuambia watu waandike basua za sababu ya kutaka kutoa pesa zao

True kwa sababu ukisoma maelezo ya barua zao, wanaonesha bila ya shaka kuwa endapo watu watataka kuchukua fedha zao at will, hawawezi kuwalipa watu wengine.

Hiyo ya usalama unasema iko poa, isije kuwa kama ule mchezo wa Kibati?
 
True kwa sababu ukisoma maelezo ya barua zao, wanaonesha bila ya shaka kuwa endapo watu watataka kuchukua fedha zao at will, hawawezi kuwalipa watu wengine.

Hiyo ya usalama unasema iko poa, isije kuwa kama ule mchezo wa Kibati?


Sikiliza mjomba mji huu kila mmoja ana EPA yake,sema wengine zao ni kubwa kubwa ndio tofauti...the same applies to these Ponzi schemes aka UPATU.

Mimi huo mchongo wa DECI nililetewa sometimes mwaka jana lakini kila nilipodadisi naona nilikuwa napewa majibu vague vague tuuu mfano wanadai wao walijiandikisha kama micro-credit/finance lakini cha ajabu hakuna mtu hata mmoja ninaye mkua including yule jamaa liyelenitea hilo dili

Pili element ya kutoa pesa zangu mwenyewe naambiwa niandike barua ya kujieleza na kama nikishazitoa basi siwezi kurudi tena nikaona ahyaaaaa hivi nililala wapi wakati hawa jamaa all the way from Kenya wameingia?

On a flipside ya jamaa wa usalama imetulia lakini nayo ni hatari kwa sababu kama TISS wana recruit watu wa ajabu ajabu dizaini ile ni kazi kweli kweli kwa sababu inamaana leo wanaanza na ponzi schemes ndogo kama zilde kesho wakija waNyaRwanda kutaka info za kiusalama basi sidhani kama kutakuwa na tatizo maana shida ni pesa ...
 
Sikiliza mjomba mji huu kila mmoja ana EPA yake,sema wengine zao ni kubwa kubwa ndio tofauti...the same applies to these Ponzi schemes aka UPATU.

Mimi huo mchongo wa DECI nililetewa sometimes mwaka jana lakini kila nilipodadisi naona nilikuwa napewa majibu vague vague tuuu mfano wanadai wao walijiandikisha kama micro-credit/finance lakini cha ajabu hakuna mtu hata mmoja ninaye mkua including yule jamaa liyelenitea hilo dili

Pili element ya kutoa pesa zangu mwenyewe naambiwa niandike barua ya kujieleza na kama nikishazitoa basi siwezi kurudi tena nikaona ahyaaaaa hivi nililala wapi wakati hawa jamaa all the way from Kenya wameingia?

On a flipside ya jamaa wa usalama imetulia lakini nayo ni hatari kwa sababu kama TISS wana recruit watu wa ajabu ajabu dizaini ile ni kazi kweli kweli kwa sababu inamaana leo wanaanza na ponzi schemes ndogo kama zilde kesho wakija waNyaRwanda kutaka info za kiusalama basi sidhani kama kutakuwa na tatizo maana shida ni pesa ...


Mzee mtu wa TISS kushiriki kwenye mambo kama haya sidhani inaweza kukushangaza. Si unakumbuka mada yako ya Usalama wa Taifa na baadaye tulipowazungumza kina Mwang'onda. Wale jamaa wamechota fedha bila kutumia Ponzi sasa kama hadi kigogo wao yuko mitaa hiyo huko chini utakutana ni "a few good men"..
 
Sure GT
Kama chama la DECI lingekuwa chini ya masheikh kibali mida kingekuwa kishatolewa biashara kama kawa

Hoja yako ina prejudice ya udini. (Historia inatuambia makanisa ya pentekoste ni champions wa PONZI)

Hoja yako haiendi kwenye misingi ya uhalali wa DECI kisheria.

Pia hukujipa muda kutazama sheria zinazoongoza usajili na uendeshaji wa biashara ya pesa, kwa mashirika yasiyo mabenki.

Lakini inaonesha kuwa huko tayari kujifunza, vinginevyo kwenye thread hii na kwenye ile ya DECI: Nini hasa. Ungepata yote unayohitaji kuelewa kwa nini DECI is not sustainable, na it is inevitable that at some point in time huge losses will be incurred.

Sikio la kufa ...........
 
Anayefahamu walichozungumza hao maaskofu huko kwenye mkutano wao atumwagie hapa tafadhali...!
 
Hoja yako ina prejudice ya udini. (Historia inatuambia makanisa ya pentekoste ni champions wa PONZI)

Hoja yako haiendi kwenye misingi ya uhalali wa DECI kisheria.

Pia hukujipa muda kutazama sheria zinazoongoza usajili na uendeshaji wa biashara ya pesa, kwa mashirika yasiyo mabenki.

Lakini inaonesha kuwa huko tayari kujifunza, vinginevyo kwenye thread hii na kwenye ile ya DECI: Nini hasa. Ungepata yote unayohitaji kuelewa kwa nini DECI is not sustainable, na it is inevitable that at some point in time huge losses will be incurred.

Sikio la kufa ...........

MOD, Please unganisha hii thread na ile iliyopo kwenye Business & Economic forum(Deci ni nini?)
 
Ukweli kwamba hii itafika sehemu kuna wengi watalizwa nadhani unafahamika, tatizo ni kwamba kila mmoja anadhani atakayetapeliwa si yeye. Huenda kila mmoja ana projection yake ya kujua kitu itacollapse lini. Haiingii akilini mtu kusema unapanda, na kuchukua zaidi wakati hao DECI hawafanyi biashara yoyote na hizo hela, watuambie kama wanafanya miujiza ya kuongeza hizo fedha.

Otherwise, inabidi watu tujaribu kutumia ubongo kufikiri, tatizo lipo katika kuwashawishi watu waliowahi kupata, hata mchezo wa karata tatu kuna watu wako busy kuucheza, unashindwa kushangaa.

Hawa maaskofu nao zimo au?
 
Jamani tusitaniane hapa. Hivi DECI ina tofauti gani na mfumo wetu wa utawala - utawala chini ya serikali ya CCM. Kila siku wananchi tunalizwa na hawa mafisadi lakini bado tumeing'ang'ania serikali ya CCM.

Kila uchaguzi wachache tunagawiwa fulana na chumvi lakini mwisho wa siku EPA, Richmond, Meremeta, Kagoda, Dowans na Kiwira wanabaki pale pale. DECI ina tofauti gani na sera za CCM - wote ni matapeli wanaotuahidi maisha bora na kweli wajanja wachache wanatajirika lakini wengi baada ya Kuwasindikiza hawa mafisadi kwenye meza yao ya karamu hurudi kwenye njaa na umasikini wetu.

Hivi sasa pamoja na kujua tunakoelekea si kuzuri na wengi tutalia lakini, kama walivyo wanachama wa DECI, hatusikii wala hatugutuki. Hao viongozi wa dini wamekuwa msitari wa mbele kuwasifu na kuwabariki hawa viongozi wetu wezi, sembuse DECI inayowanufaisha wao - hili ni tendo la kufukuru kwa maana yake halisi !!😡

DECI na CCM ni mapacha kwa matendo na dhamira.
 
Back
Top Bottom