DECI Tanzania: Ilivyoanza, ilipo na hatma yake

DECI Tanzania: Ilivyoanza, ilipo na hatma yake

Mwizi hana dini! Na hawa wenye kutumia dini ndiyo wakati mwingine ni wezi wakubwa kabisa. Binafsi naamini wachungaji hawa ni wale ambao Ezekieli alisema ni "ole kwa wachungaji" kwani "wanakula vilivyonona" huku kondoo wao wakifa njaa. Ni wachungaji wa matumbo yao. Hawa wanatakiwa kutiwa pingu ili waende kuhubiri katika selo za magereza ambako huko kuna kulia na kusaga meno!

Mwanakijiji naona wachungaji hao hawana tofauti na wafuasi wa Sultani CCM.
 
Tatizo ni kwamba siku hizi dini imegeuka kuwa biashara yaani imejikita sana kibiashara kuliko malengo yake makuu kumfariji muumini kiroho....angalia kuna madhehebu siku hizi yanaibuka kama uyoga Tanzania. Mkoa wa Mbeya na Arusha inaongoza kwa kuwa na madhehebu kibao zaidi ya 750. Hata mimi na wewe tunaweza kuanzisha letu na tukapata waumini watakao tuunga mkono.
 
DECI kamwe haiwezi kuleta MTIKISIKO WA IMANI - kinachowaliza hao wote sio DECI ni PESA - HATA YUDA ALICHUKUA PESA AKAMSALITI YESU - WACHA SERIKALI ILISHUGHULIKIE ILI UWE MWISHO WA UTAPELI HUU TANZANIA - IMANI SIO MANENO MATUPU NI MATENDO - WANASEMA HALELUYA HUKU WANAWEKA 15% MFUKONI KWENYE ACCOUNTS ZAO - POLE KWA WALIOINGIZWA MJINI KWA KUTUMIA NENO HALELUYA - TUKUMBUKE DECI SIO KANISANI - NI KAMPUNI/SHIRIKA (WHATEVER) WALIDANGANYA WANA KIBALI CHA BOT - KIKO WAPI? NINA MARAFIKI WENGI NILIWAONYA KUTOWEKA AKIBA ZAO PALE ILA MH! ILIKUWA NGUMU KUELEWA - MUNGU AWASAIDIE - NDIO MAPITO YA MAISHA HAYO - mtaka yote kwa pupa - hukosa yote
 
Kwangu hii DECI na hii VUNAVUNA NA SETO ya kwenye TV hakuna tofauti.
Ujinga unakuja wakati kimoja kinaonekana sawa na vingine kuonekana si sawa. Hivi vyote viko designed kuibia wananchi na vyote viondolewe kwa sababu hatuitaji pesa ya bure. Unasemaje hapo MMKJJ?
 
Hili jambo wala lisituumize vichwa,sheria iko wazi ambayo inaharamisha upatu na haiwezekani uvunje sheria kwa kujificha nyuma ya pazia la dini,chama cha siasa,klabu ya mpira etc halafu uachwe tu.sheria ichukue mkondo wake na wahusika wakamatwe watupwe lupango,kwisha kazi.kama ni pesa zitakazopatikana zikusanywe watu warudishiwe hata kama ni kwa hasara wenyewe wataalam wanaitwa pari passu.
 
Kwa hakika mauala yote ya DECI yashughulikiwe kwa ungalifu mkubwa sana. Ni vema tahadhari zichukuliwe na si kukurupuka. Wengi walijiingiza DECI hawana ujuzi sana na uchumi, ni wachache sana wanaojua huenda siku moja itayumba. for sure mtu kama mimi nikiamua kujiunga DECI najua for 100% nipo katika risk investment kwa mantiki hiyo sitawekeza kiasi kikubwa sana.

Viongozi wake wafanyiwe mahojiano makali kupata ukweli wa namna fedha zinazunguka na kuweza kulipa kiasi kikubwa hivyo cha interest kwa siku chache. Ni investments gani kubwa na zinazozalisha hivyo DECI wanazo (quick returns investments)?? Lazima watoe kwa mtiririko nmana ambavyo wanapata ile fedha. Watuhakikishie kuwa hakuna swala la LIFO.
 
Kwangu hii DECI na hii VUNAVUNA NA SETO ya kwenye TV hakuna tofauti.
Ujinga unakuja wakati kimoja kinaonekana sawa na vingine kuonekana si sawa. Hivi vyote viko designed kuibia wananchi na vyote viondolewe kwa sababu hatuitaji pesa ya bure. Unasemaje hapo MMKJJ?

Hiyo vuna vuna ifanywaje? Kutumia neno "vuna" tu haina maana ni illegal activity.
 
Serikali ikiendelea kuachilia watu wachache kujitafutia njia rahisi za kupata mali, dhana ya uzalishaji mali itaondika na wengi kufikiria hizi njia rahisi za kupata pesa na mwisho wake kila mmoja wetu atakuwa msanii kwa mwenzake (matapeli) hebu tuangalie wenzetu Nigeria, Cameroun walipita katika misukosuko kama hii kwa watu kujitafutia njia rahisi za kupata pesa na wengi wao wakawa matapeli na hata kutaka kuvamia ukanda wa kwetu.

Mimi nawashauri watanzania wenzangu kufikiria zaidi juu ya miradi midogo midogo itakayopelekea baadae kuwa mamilionea. Jamani mbona Tanzania bado tuna "opurtunities" nyingi tu za kupata pesa. Hebu turudi kwenye dhana ya ujasiliamali, kwani fursa hii ya kuanzishwa saccoss na vyombo vinginevyo ilikuwa na kumwezesha mjasiliamali ambaya tatizo lilikuwa ni mtaji.
 
DECI ni taasisi inayotoa mavuno kwa aliyepanda mbegu,utaratibu huu ni sawa na upatu lakini Kanisa limetumiwa kuficha mantiki hiyo. BOT ilipotanga kuwa haitambui DECI wadau wake walikuja juu kwa kudai kuwa wamekuwa wakifaidika bila kujua kuwa watafaidika wa mwanzo lakini wa mwisho wanaweza kuhujumiwa bila mtetezi kwa kuwa Serikali haiwatambui DECI.

Umasikini wa Watanzania,Uongozi mbovu na ufisadi ndio chanzo cha haya yote.Ukibwetere ulianza hivi hivi,dini fulani kujitokeza kuteka nyoyo za waumini na hatimaye kuwadhuru. Halikadhalika wanamaombi masalia ni hivi hivi,viongozi waangalie mambo haya na kuyapatia ufumbuzi mapema. Wana JF tuelimisha hapa kuhusu haya ya DECI.
 
YOU DESERVE TO BE YOU....!
DECI lazima ipigwe vita na watu kama (wao) kwa sababu haipo kwa ajili ya WENYE NACHO bali wasio nacho!
madokta,maprofesa,wachumi, ma-B.A holders, M.A holders, matajiri, wafanyabiashara wakubwa na wanyonyaji wengine ambao hupenda kuona mtu wa chini anabaki chini.
Sisi watu wa chini ambao employment opportunities kwetu ni ndoto, nafasi za mikopo kwetu ni ndoto na hata tukikaribia kuipata kwa masharti magumu
DECI REMAIN OUR MKOMBOZI...!
 
UDINI, ISLAMIC BANK, PRIDE (IDD SIMBA), WATU 700,000 BEHIND DECI, ant-christianity....etc!
 
..wachukuliwe hatua za Kisheria.

..Dini isiwe kigezo cha kuwabembeleza.
 
mnakuja na kila mada...! UDINI,ONYO TOKA BOT, UPATU, POLISI KUCHUNGUZA, PYRAMID ,PONZ......! KADHA WA KADHA....!
KAMA DECI KUFA ITAKUFA KWA MASHINIKIZO TOKA KWA WASOMI NA MATAJIRI NA SI KUFA KUTOKANA NA KUSHINDWA KUJIENDESHA....!
PILI PILI YA SHAMBA YAWAWASHIA NINI????
 
YOU DESERVE TO BE YOU....!
DECI lazima ipigwe vita na watu kama (wao) kwa sababu haipo kwa ajili ya WENYE NACHO bali wasio nacho!
madokta,maprofesa,wachumi, ma-B.A holders, M.A holders, matajiri, wafanyabiashara wakubwa na wanyonyaji wengine ambao hupenda kuona mtu wa chini anabaki chini.
Sisi watu wa chini ambao employment opportunities kwetu ni ndoto, nafasi za mikopo kwetu ni ndoto na hata tukikaribia kuipata kwa masharti magumu
DECI REMAIN OUR MKOMBOZI...!
Kama ni hivyo muwashauri waisajili ili ifanye kazi zake kihalali,la sivyo ni kosa kanisa kufanya biashara ya fedha badala ya kushughulika na imani.
 
WAKATI HAKUNA MALALAMIKO TOKA DECI MEMBERS MWAENDA KUCHUNGUZA.....!
Wakati sehemu zilizojaa malalamiko, rushwa , foleni kadhia zote zaachwa....!
TOENI KWANZA MABANZI KTK MAJICHO YENU WANDUGU....!
PALE wanachama wa DECI wakija na kulalamika fanyeni uchunguzi wa kina,
KINACHOTAKIWA SASA NI KUIPONGEZA DECI
 
Ndo tatizo la kuwa "man of one book" unakua haujui mambo mengi sana ya muhimu, pia wamewalenga kwa sababu ni watu ambao wanaoperate on faith, faith haihitaji sayansi wala hesabu na utawaeleza finance mpaka uchoke hakuna atakayesikia, lakini askofu akisema lolote linakubalika.
Hii ni disaster kubwa sana kwa nchi yetu, kama kweli wana wanachama wengi kiasi wanachodai.
 
Huu nauita upeo mdogo wa kufikiri, hao DECI ninani alisha walalamikia?
Tatizo wabongo mnapenda kukurupuka wanachama wenyewe hawasemi pesa zao ,Unakuta jimtu linatokwa na povu DECI ,DECI sasa nyinyi imewafanya nini pesa hiyo ni yako?
Unawashwanini muwe mnajitizama, Pesa ya EPA mbona imeliwa na nyinyi mkaa tuli.

Jaribuni kupima akili zenu na ufikilie nini kina kuwasha mpaka usitulie, Ni hajabu kuona kwanini hamjishangai maana Wenye pesa zao hawalalamiki lakini wewe ambaye hata hujui DECI ninini unatokwa na POVU mdomoni naomba mbadilike na kuacha unafiki mtu akija kwenye mabenki yenu mtampa hiyo pesa au mmetumwa?
 
Huu nauita upeo mdogo wa kufikiri, hao DECI ninani alisha walalamikia?
Tatizo wabongo mnapenda kukurupuka wanachama wenyewe hawasemi pesa zao ,Unakuta jimtu linatokwa na povu DECI ,DECI sasa nyinyi imewafanya nini pesa hiyo ni yako?

Unawashwanini muwe mnajitizama, Pesa ya EPA mbona imeliwa na nyinyi mkaa tuli.
Jaribuni kupima akili zenu na ufikilie nini kina kuwasha mpaka usitulie, Ni hajabu kuona kwanini hamjishangai maana Wenye pesa zao hawalalamiki lakini wewe ambaye hata hujui DECI ninini unatokwa na POVU mdomoni naomba mbadilike na kuacha unafiki mtu akija kwenye mabenki yenu mtampa hiyo pesa au mmetumwa?
 
Ndo tatizo la kuwa "man of one book" unakua haujui mambo mengi sana ya muhimu, pia wamewalenga kwa sababu ni watu ambao wanaoperate on faith, faith haihitaji sayansi wala hesabu na utawaeleza finance mpaka uchoke hakuna atakayesikia, lakini askofu akisema lolote linakubalika.
Hii ni disaster kubwa sana kwa nchi yetu, kama kweli wana wanachama wengi kiasi wanachodai.

Wewe inakuuma nini watu kama madhara walisha pata raha gani watu waliyo nayo hili la DECI ndio umeona , Je madawa feki tunayoletewa na watendaji wa serikali wanaruhusu yapite hauoni ila DECI ndio umeona au umetumwa.

Ruhusu Ubongo wako ufikilie kwanini mpaka sasa tren ni mbovu na haifahi hata kidogo? jiulize vitu kama hivyo. Kwanini Hospital mpya na kubwa za kisasa hazijengwi?

Unakaa unatokwa na povu eti DECI blah blah. Yaaaani ilo ndio umeona bonge la inshu wakati mafukara wanaifurahia na hakuna aliye lalamika.
 
"...........ndo niligundua kuwa, kumbe ilikuwa designed haswa kwa walokole, na si watu wote, walipoona watu wengine wanalalamika wakikataliwa, ndo wakaanza kuchukua watu wa dini zingine. asilimia 99% pale ni wakristo, waislam ni wachache sana, ndo maana ukienda pale mazungumzo mengi utakuta haleluya, wapendwa katika bwana, ameni ameni nakadhalika. nilijulishwa kuwa, hii ilianzishwa na mchungaji wa kilokole.

the point is, hii issue inawagusa wakristo wooote Tanzania, hasa wasio na elimu, in a very sensitive way, kiasi kwamba watu wako tayari kwa lolote kama ulishawahi kuhudhuria mkutano wao wowote. huwezi amini. watu wana gadhabu sana, kwasababu wengi walitia miguu yote pale na kuifuta ni kugusa mioyo ya wengi. wengi wamejenga nyumba nimeshuhudia, wengi waliweka viinua mgongo, wengi wameweka mishahara hasa waalimu, wanajeshi, maaskari nk kwasababu hapo ndo palikuwa panalipa.........."

******************************
Kidzogolae:

Hebu kidogo tufikirie hypothesis hii: Kwa mfano ndiyo ingekuwa masheikh wa Kiisilamu ndiyo wameanzisha na kuendesha kitu hicho....unafikiri ingekuwaje?
nadhani serikali bila kusita ingeingilia kati na kuwakamata wahusika na pia tungesikia kauli kutoka watu mbali mbali za kusema wanafanya kwa niaba ya Al-Qaeda etc etc.

Nadhani pia Marekani (yaani wapelelezi wao wa FBI/CIA wangetoa msukumo kwa serikali kufanya hivyo na hata kutoa kauli kwamba wana wasiwasi hela hizo wanazochangisha ni kwa ajili ya ugauidi etc etc!!
 
Back
Top Bottom