Renegade
Platinum Member
- Mar 18, 2009
- 7,817
- 8,266
Unalima, Unapanda, Unapalia kisha Unavuna. Hii ndiyo kanuni. Ni kweli unaweza usipalie na ukavuna lakini KUPANDA NA KUVUNA BILA KULIMA !!!.
DECI wangekuwa na miradi (kulima) sawa lakini kupanda na kuvuna tu! Wataalam wa uchumi hebu mtusaidie maana sioni ila wingu zito.
NN
NUNGU NUNGU:
Hii haitaji mtaalamu wa uchumi kupambanua ukweli,michezo ya kupeana pesa bila riba(UPATU) ipo sehemu nyingi kama makazini,kwenye biashara na sehemu nyinginezo, na hii ufanyika kwa kutambua uwezo wa kila mshiriki,mnapangiana zamu , pesa zinakusanywa na mtu mwenye zamu anachukua, Basi.
Lakini inapofika suala la pyramid scheme ni kitu tofauti sana ,Fikiria kwamba pesa haizalishwi, Hakuna Investment ya ku-generate profits, unaweka Tshs. 200,000/- unapata 200,000/- kwa misingi ipi?Maana yake ni kwamba ili mmoja apate 200000/- kuna wengi wanapoteza!
Cha kufanya ,serikali iingilie kati ,isimamishe wanachama wapya wahakikiwe wale wanachama wote walioko kwenye laini ya kuvuna,zihakikiwe amana zote zilizoko kwenye sources zote za DECI kuona kama zinaweza kuwalipa watu wanaotakiwa kuvuna katika vipindi vyote bila kuongeza mwanachama mpya ,mpaka mtu wa mwisho avune na iwapo itaonekana kwamba huo uwezo upo .DECI Waendele kupokea pesa za Watu wapya kwa maana waruhusiwe kuoperate.