Mkuu naomba nitangulize pole zangu za dhati kwani naona we umewekeza katika DECI. Kama uko tayari naomba nikujibu kwa kutumia facts pia:
Fact: DECI wamegundua njia ya kufanya kazi nje ya mfumo wa kibenki wa Tanzania, jambo ambalo limewatisha watawala na wamiliki wa mabenki haya. Watu wakizidi kuhamisha pesa zao kutoka kwenye benki hizo, na kuzipeleka DECI, uhai wa benki hizo utakuwa mashakani. Hakuna benki yenye uwezo wa kuwapa watu faida ya 125% kwa muda wa miezi 4. HAKUNA!
Mfumo nje ya benki: Sheria ya Tanzania iko wazi kama unaendesha benki unasimamiwa na BoT, kama unaendesha mpango wa fedha nje ya mfumo rasmi wa benki, unasimamiwa na CMSA. Mfano mzuri ni mpango wa Umoja Fund, ambao mpaka leo unaendelea na haijafungiwa.
Faida ya 125% katika miezi 4: Ni kweli hiyo ni fact na nimefurahi umeliona. Hakuna benki, hakuna mpango wa fedha unaoweza kukuahidi hilo. Je DECI wanafanya shughuli gani ya uzalishaji utakaoweza kuzaa faida hiyo? Hakuna, kwa hiyo ni kitu gani kinachofanyika? Unapoweka 40,000 na kulipwa 100,000 baada ya miezi 4 ina maana umepata faida ya 60,000. Je hiyo 60,000 imetoka wapi? Ni pesa za wenzako waliokufuata - watu 3 waliowekeza 20,000. Na baada ya miezi 4 watachukua faida inayotokana na uwekezaji ya wengine 6 au hata 8. That is what a pyramid scheme is. Kwa hiyo kama umewekeza mapema utapata 'faida' lakini wanaofuata ni lazima wapate wenzao wa kuwekeza pesa ili wapate 'faida' This is useless, na si uzalishaji.
Kama DECI wamekiuka sheria, na kama kweli wamewatapeli au wana nia ya kuwatapeli Watanzania, wafungiwe, lakini kama sivyo, ndugu zanguni mnapiga vita nafasi ya kuachana na umaskini, tena kwa pupa bila kuchuja pumba na chuya! Kalaghabaho! Wenzenu wanavuna wanachopanda, nyie mnakalia, matapeli... nani ametapeliwa?
DECI wamekiuka sheria, tena ni kesi ya jinai walichokifanya. Sasa ukiendelea kushikilia bango ujue kuwa hata KUSHIRIKI katika Pyramid scheme ni kosa na unaweza kuchukuliwa hatua za kisheria. Kwa nini? Kwa sababu ulipochukua 'faida' ulichukua pesa za watu.
Kilichotokea Kenya si lazima kitokee hapa nchini... kumbukeni, Kenya wao ni rahisi sana kushika silaha na kupigana... si mnakumbuka yaliyotokea hivi majuzi, baada ya uchaguzi mkuu wao kufanyika? Sisi hapa tunaweza kweli kukatana mapanga kwa sababu ya tofauti za kisiasa? Sisi ni wapenda amani, na kamwe hatuwezi kuwa na mfumo wa kitapeli nchi nzima.
Hivi leo hii ukiambiwa urudishe ile 'faida' uliyochukua na kuitumia, utakuwa tayari kufanya hivyo? Hapana! Mfano wako huu wa Kenya si sahihi na kumbuka kuwa hata huko Philippines na Columbia na kwingne, wananchi ni wapenda amani lakini mbele ya pesa, hakuna uvumilivu amani na upendo.
DECI inawasaidia Watanzania wasiokopesheka, maskini wanaolala kwenye nyumba za udongo, tena wasio na uhakika wa hata mlo mmoja. Leo mnasema IFUNGWE? Ina maana wao hawana haki ya kuachana na umaskini? Acheni ROHO MBAYA!
Kama wewe una uwezo, ni wewe, waacheni wasio na uwezo wawezeshwe. Hii ni Maisha Bora kwa Kila Mtanzania KWA VITENDO! Msiungane na MAFISADI!
Kama kuna atakayechukia, basi, namwomba radhi, lakini binafsi siungi mkono Serikali kuifungia DECI, kwa sababu, hii ni REVOLVING FUND, sio PYRAMID SCHEME! Kwenye PYRAMID SCHEME unaambiwa nenda ulete wanachama wengine, kwenye DECI ni wewe mwenyewe na mtaji wako. Wapi na wapi ndugu zanguni?
Kama kuna ambaye amelizwa na DECI hapa Tanzania, vyombo vya sheria viko wazi, aende akashtaki. Hajazuiwa. Lakini kama mnasema tu, bila kuchuja, bila kufikiria, mnawasaidia mafisadi kuwakandamiza Watanzania wanyonge, walio wengi, maskini, fukara wa kufukarika!
./Mwana wa Haki
Umeongea vitu vingi lakini naomba nigusie vitu 2 muhimu:
Revolving Fund: hii ina maana gani? NI kuwa hamna kinachofanyika kama uzalishaji bali ni kuzungusha pesa za watu. Katika mzunguko huu lazima itafikia tamati maana watu wa kuwekeza wakiisha ni lazima mpango uta-collapse. Hawa DECI wamejisuta wenyewe kwa kutumia neno hili na kuonyesha dhahiri kuwa ni pyramid scheme. Unasema katika pyramid scheme unaambiwa ulete wanachama wenzako na hii haipo katika DECI, lakini si ndivyo unavyofanya? Kwani ulipopata 'faida' si ulienda kutangaza kwa majirani wawekeze kwa kuwa kuna faida kubwa? Unakataa si ndicho ulichofanya? Recruitment siyo lazima iwe kwa fomu, inaweza kuwa word of mouth. Pia makanisa yametumika kutangaza kusifia na kuhimiza watu kuwekeza katika DECI, kitu ambacho ni dhambi kubwa sana, ukiachilia kuwa ni kosa la jinai.
Mafisadi: ujue ya kuwa hata washiriki wote wa DECI ni mafisadi tena wale wabaya maana wameibia maskini watanzania alafu wanaifanya kama vile ni mpango wa kuwasaidia. Wewe binafsi umeonyesha ni jinsi gani umekuwa 'brain washed' Naomba uamke na uachane na ufisadi huu mara moja. Tena rudisha 'faida' uliyopewa ili wenzako warudishiwe pesa zao.
Kama una maswali au unahitaji ushauri niandikie katika inbox
Pole tena na uwe makini!