DECI Tanzania: Ilivyoanza, ilipo na hatma yake

DECI Tanzania: Ilivyoanza, ilipo na hatma yake

Utaratibu wa kupanda na kuvuna utakuwa pale pale benk itakuwa subsidiary company ya DECI

Maendeleo hayo ndugu!!
Anything must grow

Enjoy while it lasts kwani mwisho mtalia na kusaga meno. Msije mkasema kuwa hamkuonywa
 
Hivi in mid 90's sii tulishakuwa na DECI like scheme ikawaliza watu wengi sana.. na serikali ikaifungia?

Wakati ule kuna watoto walikuwa wanapewa ada wanalipa nusu na nusu DECI! basi mwishoni ilikuwa ni kilio na kusaga meno!
 
Fact: Si rahisi hata siku moja kwa mtawala mdanganyifu (mwanasiasa fisadi) kumhadaa mtu mwenye pesa, amchague kwa kumpigia kura za ubunge au urais. Hilo haliwezekani.

Fact: Daima watawala wetu hawataki watu maskini wawe na uwezo, wa kujikwamua kutokana na lindi la umaskini.

Fact: DECI wamegundua njia ya kufanya kazi nje ya mfumo wa kibenki wa Tanzania, jambo ambalo limewatisha watawala na wamiliki wa mabenki haya. Watu wakizidi kuhamisha pesa zao kutoka kwenye benki hizo, na kuzipeleka DECI, uhai wa benki hizo utakuwa mashakani. Hakuna benki yenye uwezo wa kuwapa watu faida ya 125% kwa muda wa miezi 4. HAKUNA!

Kama DECI wamekiuka sheria, na kama kweli wamewatapeli au wana nia ya kuwatapeli Watanzania, wafungiwe, lakini kama sivyo, ndugu zanguni mnapiga vita nafasi ya kuachana na umaskini, tena kwa pupa bila kuchuja pumba na chuya! Kalaghabaho! Wenzenu wanavuna wanachopanda, nyie mnakalia, matapeli... nani ametapeliwa?

Kilichotokea Kenya si lazima kitokee hapa nchini... kumbukeni, Kenya wao ni rahisi sana kushika silaha na kupigana... si mnakumbuka yaliyotokea hivi majuzi, baada ya uchaguzi mkuu wao kufanyika? Sisi hapa tunaweza kweli kukatana mapanga kwa sababu ya tofauti za kisiasa? Sisi ni wapenda amani, na kamwe hatuwezi kuwa na mfumo wa kitapeli nchi nzima.

DECI inawasaidia Watanzania wasiokopesheka, maskini wanaolala kwenye nyumba za udongo, tena wasio na uhakika wa hata mlo mmoja. Leo mnasema IFUNGWE? Ina maana wao hawana haki ya kuachana na umaskini? Acheni ROHO MBAYA!

Kama wewe una uwezo, ni wewe, waacheni wasio na uwezo wawezeshwe. Hii ni Maisha Bora kwa Kila Mtanzania KWA VITENDO! Msiungane na MAFISADI!

Kama kuna atakayechukia, basi, namwomba radhi, lakini binafsi siungi mkono Serikali kuifungia DECI, kwa sababu, hii ni REVOLVING FUND, sio PYRAMID SCHEME! Kwenye PYRAMID SCHEME unaambiwa nenda ulete wanachama wengine, kwenye DECI ni wewe mwenyewe na mtaji wako. Wapi na wapi ndugu zanguni?

Kama kuna ambaye amelizwa na DECI hapa Tanzania, vyombo vya sheria viko wazi, aende akashtaki. Hajazuiwa. Lakini kama mnasema tu, bila kuchuja, bila kufikiria, mnawasaidia mafisadi kuwakandamiza Watanzania wanyonge, walio wengi, maskini, fukara wa kufukarika!

Maisha Bora kwa Kila Mtanzania yanawezekana! Tusiyapige vita!

./Mwana wa Haki
 
Fact: Si rahisi hata siku moja kwa mtawala mdanganyifu (mwanasiasa fisadi) kumhadaa mtu mwenye pesa, amchague kwa kumpigia kura za ubunge au urais. Hilo haliwezekani.

Fact: Daima watawala wetu hawataki watu maskini wawe na uwezo, wa kujikwamua kutokana na lindi la umaskini.

Fact: DECI wamegundua njia ya kufanya kazi nje ya mfumo wa kibenki wa Tanzania, jambo ambalo limewatisha watawala na wamiliki wa mabenki haya. Watu wakizidi kuhamisha pesa zao kutoka kwenye benki hizo, na kuzipeleka DECI, uhai wa benki hizo utakuwa mashakani. Hakuna benki yenye uwezo wa kuwapa watu faida ya 125% kwa muda wa miezi 4. HAKUNA!

Kama DECI wamekiuka sheria, na kama kweli wamewatapeli au wana nia ya kuwatapeli Watanzania, wafungiwe, lakini kama sivyo, ndugu zanguni mnapiga vita nafasi ya kuachana na umaskini, tena kwa pupa bila kuchuja pumba na chuya! Kalaghabaho! Wenzenu wanavuna wanachopanda, nyie mnakalia, matapeli... nani ametapeliwa?

Kilichotokea Kenya si lazima kitokee hapa nchini... kumbukeni, Kenya wao ni rahisi sana kushika silaha na kupigana... si mnakumbuka yaliyotokea hivi majuzi, baada ya uchaguzi mkuu wao kufanyika? Sisi hapa tunaweza kweli kukatana mapanga kwa sababu ya tofauti za kisiasa? Sisi ni wapenda amani, na kamwe hatuwezi kuwa na mfumo wa kitapeli nchi nzima.

DECI inawasaidia Watanzania wasiokopesheka, maskini wanaolala kwenye nyumba za udongo, tena wasio na uhakika wa hata mlo mmoja. Leo mnasema IFUNGWE? Ina maana wao hawana haki ya kuachana na umaskini? Acheni ROHO MBAYA!

Kama wewe una uwezo, ni wewe, waacheni wasio na uwezo wawezeshwe. Hii ni Maisha Bora kwa Kila Mtanzania KWA VITENDO! Msiungane na MAFISADI!

Kama kuna atakayechukia, basi, namwomba radhi, lakini binafsi siungi mkono Serikali kuifungia DECI, kwa sababu, hii ni REVOLVING FUND, sio PYRAMID SCHEME! Kwenye PYRAMID SCHEME unaambiwa nenda ulete wanachama wengine, kwenye DECI ni wewe mwenyewe na mtaji wako. Wapi na wapi ndugu zanguni?

Kama kuna ambaye amelizwa na DECI hapa Tanzania, vyombo vya sheria viko wazi, aende akashtaki. Hajazuiwa. Lakini kama mnasema tu, bila kuchuja, bila kufikiria, mnawasaidia mafisadi kuwakandamiza Watanzania wanyonge, walio wengi, maskini, fukara wa kufukarika!

Maisha Bora kwa Kila Mtanzania yanawezekana! Tusiyapige vita!

./Mwana wa Haki
 
Maaskofu wajitosa sakata la DECI, Kutoa tamko zito leo , DCI bado achunguza, Wadau presha yapanda

Tuesday, 07 April 2009 16:18
Na Mwandishi Wetu
Majira

KATIKA kile kinachoonekana kutokubaliana na msimamo wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kupinga shughuli za kampuni ya upatu ya DECI (T), Baraza la Maaskofu wa Makanisa ya Pentekoste Tanzania (PCT) linakutana leo Dar es Salaam kutoa mustakabali wa suala hilo.

Akizungumza na Majira kwa simu jana, Mwenyekiti wa maandalizi ya mkutano huo Askofu Bartholomew Sheggah alisema wamesikitishwa na hatua hiyo kwani DECI imesaidia wanyonge wengi nchini.

Mwenyekiti huyo anayetoka Kanisa la Faith Community Pentecostal Church (FCPC), alisema mkutano huo utafanyia ukumbi wa PTA, uliopo Viwanja vya Maonesho vya Mwalimu Nyerere maarufu kama Sabasaba, Barabara ya Kilwa kuanzia saa tatu asubuhi.

Alisema utashirikisha maaskofu wote wa makanisa ya pentekoste Dar es Salaam na mikoa jirani na kuhudhuriwa pia na Katibu Mkuu wa PCT, Askofu David Mwasota na wadau mbalimbali.

Askofu Sheggah alisema hawaoni sababu za kufungiwa DECI kwani imesaidia wananchi wengi masikini kupata maisha bora.

Katika mkutano huo, wataieleza Serikali kuhusu mambo mbalimbali ya DECI na namna jamii ilivyonufaika kupitia biashara hiyo ambayo sasa imekumbwa na utata.

"Tutaishauri Serikali juu ya DECI. Chombo hiki kimesaidia watu wengi kupata maisha bora, kimeboresha uchumi wao, kimeinua biashara zao, wengine wamepata elimu na ajira," alisema Askofu Sheggah.

Aliongeza wao wakiwa viongozi wa dini wana wajibu wa kuishauri Serikali kwani wanakutana na kuishi na jamii mbalimbali mitaani, hivyo wanaelewa matatizo yao.

"Tumeona wanawake, wakiwemo wajane wakilia kupitia vyombo mbalimbali vya habari baada ya kusikia kufungwa shughuli za DECI," alisema.


Hata hivyo Askofu huyo alikataa kubainisha kwa undani kuhusu tamko lao kwa madai ni mapema mno na uamuzi wote mzito utajulikana kesho.

Alipotakiwa kueleza watachukua hatua gani endapo DECI itapigwa marufuku, alisema hana jibu la moja kwa moja kwani uamuzi huo umejikita ndani ya nafsi za wadau hivyo hawezi kujua nafsi ya kila mmoja itamtuma kufanya nini.

"Tumejitahidi sana kuwatuliza watu. Sisi tutazungumza na Serikali, tunaamini tukiishauri itatusikiliza kwani imekuwa ikienda vizuri bali mtiririko huo unaharibiwa na wachache," alisema bila kuwataja watu hao.

Juzi BoT katika mkutano wake na waandishi wa habari Dar es Salaam ilisema biashara inayoendeshwa na DECI ni batili kwa kuwa haina leseni.

Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa BoT, Bw. Joseph Massawe alikaririwa kuwa biashara hiyo ni batili kwa kuwa DECI ilipewa leseni ya kukopesha fedha si kuchangisha na kuchezesha upatu maarufu kwa jina la 'Vuna kutokana na Mbegu Unayopanda.'

Alisema BoT ilipokea barua ya DECI mwaka 2007 ikiomba idhini ya benki hiyo ili Ofisi ya Biashara na Viwanda itoe leseni ya biashara ya kukopesha fedha.

Bw. Massawe alisema BoT ilishangaa kuona kampuni hiyo ikiwachangisha wananchi fedha kwa njia ya upatu na kukielezea kitendo hicho kuwa ni kosa la jinai.

DECI inasimamiwa na kuendeshwa chini ya madhehebu ya kipentekoste.

Naye Peter Masangwa anaripoti kuwa Mkurugenzi wa Upelelezi na Makosa ya Jinai (DCI), Bw. Robert Manumba amesema kamati iliyoundwa kuichunguza DECI bado inaendelea na uchunguzi na taarifa itatolewa baada ya kukamilika uchunguzi huo.

Akizungumza kwa simu jana baada ya waandishi kufika ofisini kwake kwa lengo la kupata taarifa ya DECI kama ilivyoripotiwa na baadhi ya magazeti (siyo Majira) kuwa angetoa taarifa hiyo, Bw. Manumba alisema bado kamati inaendelea na uchunguzi.

"Mimi sikuitisha press conference (mkutano na waandishi wa habari) nashangaa kila mmoja anasema leo (jana) nitatoa taarifa ya DECI. Suala hili linashughulikiwa na kamati maalumu iliyoundwa," alisema Bw. Manumba.

Mbali na DECI kujihusisha na shughuli hiyo tangu Novemba mwaka jana na Jeshi la Polisi kupewa jukumu la kuchunguza kampuni hiyo tangu Januari mwaka huu taarifa hiyo bado haijakamilika, hivyo kuwapa wakati mgumu wateja kuchukua uamuzi wa kuendelea kuwa wanachama au kujitoa.

Naye Said Mwishehe anaripoti kuwa wakazi wa Dar es Salaam ambao walikuwa wamepanda fedha zao DECI baadhi yao wameanza kupunguza kiwango cha kupanda kwa kuhofia huenda wakatapeliwa kama inavyodaiwa na baadhi ya watu.

Hatua hiyo inatokana taarifa iliyotolewa na BoT kuwa DECI haijasajiliwa na haitambuliki kisheria ambapo maeneo mbalimbali kumekuwa na mijadala isiyoisha juu ya kuwepo kwa taasisi hiyo ambayo tangu ilipoanza kutoa huduma hiyo ya kifedha baadhi ya watu wanadai wamefanikiwa.

Uchunguzi uliofanywa na Majira tangu ilipotolewa taarifa ya BoT umebaini kuwa wakati baadhi ya wanachama wakipunguza kiwango cha kupanda wapo wengine wameamua kusimama kabisa hadi watakapopata uhakika kuwa hawatatapeliwa kama inavyodaiwa.

Pia lipo kundi lingine la wanachama ambao wao wameamua kupanda fedha kama kawaida na wapo tayari kwa lolote linaloweza kutokea.

Bi. Mariam Juma, mmoja wa wana-DECI alisema binafsi amefaidika na kuwepo kwa taasisi hiyo lakini kutokana hali ilivyo sasa ameamua kupanda kiasi kidogo tofauti na mwanzoni.

"Nimeamua kupanda kidogo tu, naogopa kwani hata nilipoona tangazo la BoT nilipata presha nikajua sasa fedha yangu imekwenda. Lakini wahusika wanatupa matumaini, hivyo naendelea lakini nipo makini hata wakikimbia nisipate hasara," alisema.

Bw. Ramadhan Mwinsina wa Kimara alisema ataendelea kupanda lakini si kama alivyokuwa akifanya zamani kwa kuweka fedha nyingi zaidi ili kuepusha matatizo kama yatatokea.

Mkazi wa Mbagala, Bw. Jafar Salum alisema ingawa BoT imetoa hadhari ataendelea kupanda kwani amenufaika kwa kiasi kikubwa na DECI na anaona ni mkombozi wa maisha yake.
 
BOT inacheza na bonge la disaster hapa!
Jinsi Pyramid Scheme inavyozidi kuendelea ndo watu wengi watakuja kuumia, naanza kuamini kuna mkubwa anachukua share hapa!
 
Maaskofu wa Kipentekoste kwa kawaida ni watu wenye elimu ndogo sana. Hata hivyo nadhani wanaelewa hii ni pyramid scheme, na kwamba ikiachwa kuendelea basi itafika mahali watu wengi sana watapoteza fedha zao. Ni uchu tu wa fedha ndio unafanya wapiganie kuendelea kuweko hii scheme.

God made man,
Man made money,
Money made man mad.
 
Tatizo watu hawana kumbukumbu ya historia.. .. Natumaini serikali na wananchi watapa kijarida cha "Cheche"kesho!!
 
Tatizo watu hawana kumbukumbu ya historia.. .. Natumaini serikali na wananchi watapa kijarida cha "Cheche"kesho!!

Ni kawaida kwa watu waliokata tamaa, wanapopata neema, hupoteza kumbukumbu zote za taabu, shida na mateso yao yote, haswa kama mpango wenyewe umepenyezewa kwenye imani kupitia kanisa, wanaamini ni Mwenye Enzi Mungu ndiye anayeneemesha hizo pesa wanazopanda hivyo hayo mavuno ya pesa ni kama mana kwa wana wa Israeli jangwani wakitoka utumwani Misri.

Tunaisubiri Cheche leo. 'upatu wa kidunia kama dollar jet ilikuwa ni kazi ya binadamu. Vuna pesa ni kazi ya Bwana'.
 
Kuna askofu alikua TBC sasa hivi, anatetea DECI kwa nguvu mno, akibanwa na swali anasema sio msemaji! kazi ipo.
 
Hivi mnaoilalamikia DECI ambao hamjatoa hata senti tano kujiunga MNAKERWA na nini? Mbona hamsimami kidete kuona fedha zinazotolewa na Serikali kwa ajili ya kuwasaidia wananchi na haziwafikii hampigi kelele k.m. Serikali inatoa Fedha za Pembejeo kuwasaidia wakulima lakini fedha hazifiki zinaishia kwenye mifuko ya watu, Mbona hamkerwi na maisha duni ya Mtanzania ambaye kila kona anapofanya biashara zake ndogondogo ananyag'anywa na city tena kwa kuwaibia kwani vitu wanavyochukua maaskari wa city wanagawana, mbona hawa hamwahurumii hata kidogo. Lakini mnakerwa sana maskini huyo anapopata fedha angalau ya kununua dagaa Roho zinawauma.

Hawaoni hao waliovimbiwa na fedha za Umma hamuoni jamani. Badala yake mnaona kujiunga na DECI ni umbumbumbu lakini mafedha yanayoibwa na Maafisadi ni Usomi acheni hiyo. Huo siyo utetezi.

Ni vyema kuwatetea wanafunzi wanaosomea chini ya miti hata enzi hizi wakati huo huo serikali inakuwa imeshatoa fedha za ujenzi wa madarasa kwa nini waandishi wazuri wasiende huko. Mbona waandishi wasishabikie wale wanaojitia wana vituo vya kulelea Yatima lakini kumbe Yatima ni matumbo yao - chungezeni hao.
 
Watu wamekata tamaa thats why wanaona DECI kama ni mkombozi. Unadhani hawajui kuwa miaka ya 90 kuna watu walilizwa hela? Wanajua lakini matatizo yaliyombele yao ndiyo kikwazo. Wala si tamaa ya hela kwani mtu mwenye tamaa ni yule aliyenazo na anaendelea kujilimbikizia lakini mtu ambaye akipatacho kidogo kinamwezesha kupeleka watoto shule, kujenga na kufanya vitu vya maendeleo sidhani.

PIA PASCO SI WOTE WAMEINGIA DECI KWA AJILI YA IMANI! WENGI WAMEINGIA KWAKUWA INASAIDIA NA UNAWEZA KUFANYA VITU VYA MAENDELEO.

Mimi nafikiri the best ni kujua system yao ikoje kwani haijasemwa? Pia kuangalia jinsi ya kuboresha ili watu iliowasaidia iendelee kuwasaidia.

Jamaa wameng'ang'ania DECI kuna TUMAINI je huko wameshapeleka wafuatiliaji? Au baadaye ndiyo waje waanze kutoa maneno kuwa haipo kisheria? Maana hii nayo inafanya kazi kama DECI tofauti ni kuwa yenyewe mnakuwa kwenye vikundi vya watu watano wenye lengo fulani.
 
Jamani, Jamani naona huruma kwa wa Tanzania wenzangu, mimi nilikwenda mpaka kwenye ofisi zao za hapa kinondoni.kulikuwa na foleni ndefu sana ya tunaotaka kupanda.nikaambiwa kuwa siku za kuvuna ni mbili kwa wiki yaani alhamis na ijumaa. nikawaza isije kuwa wanakusanya kwanza hera zetu ndipo wawalipe wengine.

lakini kilichonistua zaidi na kunifanya niondoke nikaona kwenye ukuta wao naoni cheti cha TIN peke yake. nikamuuliza mwenyeji wangu hawa jamaa hawalipi vat. akasema ndio. Yaani wanalipa kodi ya 95,000 kwa mwaka wakati wanatunza mamilioni ya watu? akasema ndio, nikaondoka hapo hapo.

Nalikuwa najiuliza hivi nchi hii tuna serikari?
 
Hivi mnaoilalamikia DECI ambao hamjatoa hata senti tano kujiunga MNAKERWA na nini? Mbona hamsimami kidete kuona fedha zinazotolewa na Serikali kwa ajili ya kuwasaidia wananchi na haziwafikii hampigi kelele k.m. Serikali inatoa Fedha za Pembejeo kuwasaidia wakulima lakini fedha hazifiki zinaishia kwenye mifuko ya watu, Mbona hamkerwi na maisha duni ya Mtanzania ambaye kila kona anapofanya biashara zake ndogondogo ananyag'anywa na city tena kwa kuwaibia kwani vitu wanavyochukua maaskari wa city wanagawana, mbona hawa hamwahurumii hata kidogo. Lakini mnakerwa sana maskini huyo anapopata fedha angalau ya kununua dagaa Roho zinawauma.

Hawaoni hao waliovimbiwa na fedha za Umma hamuoni jamani. Badala yake mnaona kujiunga na DECI ni umbumbumbu lakini mafedha yanayoibwa na Maafisadi ni Usomi acheni hiyo. Huo siyo utetezi.

Ni vyema kuwatetea wanafunzi wanaosomea chini ya miti hata enzi hizi wakati huo huo serikali inakuwa imeshatoa fedha za ujenzi wa madarasa kwa nini waandishi wazuri wasiende huko. Mbona waandishi wasishabikie wale wanaojitia wana vituo vya kulelea Yatima lakini kumbe Yatima ni matumbo yao - chungezeni hao.

Hayo yooote unayoyasema tumeisha yakemea na kuyapigia kelele tutaendelea kufanya hivyo LIKIWEMO HILI la DECI. hatujaingiza pesa zetu kwa vile ni UTAPELI, masiki ni hao hao na wanafunzi hao hao unaosema wanateseka ndio hao hao watakaoibiwa pesa zao. NDIO MAANA TUNAWATETEA.

NOTE: Huwezi kutenda maovu kwa kisingizio kuwa kuna wengine wanatenda na hawakamatwa. TUTAWAKAMATA WOTE KWA MPIGO 40 ZIKIFIKA.
 
Watu wamekata tamaa thats why wanaona DECI kama ni mkombozi. Unadhani hawajui kuwa miaka ya 90 kuna watu walilizwa hela? Wanajua lakini matatizo yaliyombele yao ndiyo kikwazo. Wala si tamaa ya hela kwani mtu mwenye tamaa ni yule aliyenazo na anaendelea kujilimbikizia lakini mtu ambaye akipatacho kidogo kinamwezesha kupeleka watoto shule, kujenga na kufanya vitu vya maendeleo sidhani.

PIA PASCO SI WOTE WAMEINGIA DECI KWA AJILI YA IMANI! WENGI WAMEINGIA KWAKUWA INASAIDIA NA UNAWEZA KUFANYA VITU VYA MAENDELEO.

Mimi nafikiri the best ni kujua system yao ikoje kwani haijasemwa? Pia kuangalia jinsi ya kuboresha ili watu iliowasaidia iendelee kuwasaidia.

Jamaa wameng'ang'ania DECI kuna TUMAINI je huko wameshapeleka wafuatiliaji? Au baadaye ndiyo waje waanze kutoa maneno kuwa haipo kisheria? Maana hii nayo inafanya kazi kama DECI tofauti ni kuwa yenyewe mnakuwa kwenye vikundi vya watu watano wenye lengo fulani.

Kweli Ndg. Mugerezi kuna Schemes kama hizi zinaitwa TUMAINI na POWERCLUB lakini serikali na hao BOT na soko la mafisadi la mitaji hawasemi kitu wamekaa kimya wameng'ang'ania DECI tena mwambie na Mwkjj hawa POWERCLUB wako Italy inabidi uconvert madafu yetu kuwa dola ni upande huko kwao fedha zetu zinakwenda nje waziwazi sasa ipi nafuu DECI ya watanzania au POWERCLUB ya Mafioso wa ITALY kule SICILY Manumba sema sema usikike wanyonge na ndugu zako wa kipato cha chini ndio tutakaoumia.
 
Sidhani kama watu wamekata tamaa isipokuwa kuna makundi mawili hapa;

Kundi la kwanza ni la wajanja (DECI) wanakusanya hizo fedha wakijua kabisa hilo zoezi litakufa kwa njia yeyote ile, hata ikibidi DECI wenyewe ndiyo watakaoleta mtafaruku.

Kundi la pili ni la wajinga ambao wanafikiria kutumia njia za mkato kwa ajili ya kupata fedha na kusahau kuwa fedha ya halali haipatikani bila ya jasho. Hawa mimi ninawaonea huruma kwani hawana uchungu na pesa zao, wameamua kuzitupa...wamelizwa!!!

Sielewi kwanini watu ni wasahaulifu kiasi hiki, wengi walilizwa kwenye upatu wa SPA wa yule tapeli Kakete. Halafu wakalizwa katika upatu mwingine pale motomoto. Kana kwamba haitoshi, wakalizwa kwenye Women Empowering Women, kana kwamba haitoshi wakalizwa na yule mganda aliyejifanya ana ofisi NIC kitega Uchumi.
Baadae mtailaumu serikali kwa maamuzi yenu binafsi bila ya kutaka kujua athari zinazoweza kuwakuta.
 
Umaskini ndio unaowafanya watu watetee DECI,hao maaskofu sijui ni wa wapi kwani hawajui walitendalo.
 
Back
Top Bottom