Leo, 04 Novemba 2025, Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, John Heche alichukuliwa mahabusu ya Polisi kuwa anahitajika kwa RPC Dodoma.
Heche amechukuliwa huku mke wake akishuhudia akiwa na Katibu wa Kanda ya Kati (CHADEMA) Bi ashura Masoud.
Walijaribu kuongozana na gari la Polisi lakini magari hayo yakaongeza mwendo na kuwaacha nyuma. Walipofika kwa RPC wakaambiwa hana taarifa za Heche kuhitajika hapo na hana kazi naye.
Mpaka muda huu, Mke wake amebaki hapo bila msaada wowote kuwa aelekee wapi.
Vitendo hivi vinaonyesha nia ovu kwa watanzania akiwemo ndugu Heche.
Waliopewa mamlaka ya kutulinda ndo wamekuwa tishio la usalama wetu; tufanye nini sasa?