DAWASA Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na ushauri

Hello DAWASCO ni lini huku Bunju A mtaleta huduma zenu tupate maji kwa uhakika huu utaratibu wa Wakala unatutesa sana...maji yanatoka kwa mgao na mara nyingine hayatoki kabisa.....tafadhalini tufikishieni miundombinu yenu.
 
Hivi baada ya kulipia kuunganishiwa maji unakaa muda gani ndio mpaka ufungiwe maji maana mimi niko Kunduchi huu ni mwezi wa pili sijafungiwa maji na bomba kuu linapita mbele ya nyumba yangu
 
Wakazi wa Salasala Mboma road, tunakosa maji kwa muda wa wiki ya pili sasa. Wakati mnatandaza bomba kubwa kuelekea kilimani kwenye tank mlitupa mgawo kwa siku ya alhamisi na jumapili. lakini sasa hivi huo mgao hakuna na haieleki muelekeo wenu.
tukiwapigia simu wahusika wa huku wanakimbilia kutupa namba za simu za magari ya kuuza maji. Je kukosekana huku kwa maji sio mkakati wa kibiashara baina ya wenye magari ya maji na watendaji wa dawasco.
Karibuni wakazi wa Salasala tueleze kero hiii.
 
DAWASCO naona mnarudi nyuma mlikotoka badala ya kusonga mbele na teknolojia. Huu mfumo wenu wa kulipia maji wa hovyo, yaani mwenye nyumba ananiambia kila mwezi nikapange foleni kulipia maji benki, je hakuna njia nyingine?

Huduma kwa wateja kwenu ni mbovu mno. Namba za simu hazipokelewi, za nini mmeziweka hapa sasa, au ili muonekane kuwa mnafanya kazi?
Nyie ni majipu kabisa na bado mnafanya kazi kwa mazoea na mifumo ya kizamani
 
Dawasco maji yenu yametoweka, Bili tunalipa matatizo yako wapi. Maeneo ya mbezi beach yote maji hakuna. Toeni taarifa tuhifidhi maji mapema
 
Mfumu mlioleta wa kulipia maji unatuibia pesa ,nimelipa kwa mfumo huo Mpya ila mwezi huu deni limekuja kama lilivyokuwa na kutokana na majukumu ya kazi sina muda kwenda kulalamika Kimara namba yenu haipokelewi wakati mwingine haipatikani .....ninafanyeje?
 
DAWASCO ; Kwa muonekano huu wa kuchelewesha kujibu hoja za wateja, inaonyesha hii Special Thread haijakuwa assigned kwa mtu specific wa kushughulikia kujibu kero za wananchi. Kama mmenuia kutumia njia hii kuwa karibu na wateja wenu, ni vyema mkamu-assign mtu 'informed' wa customer service awe na kazi ya kujibu kero za wananchi mmoja mmoja na ku-coordinate na wahusika ili kuleta tija kwa jamii.

Kuwa na special thread kusiwe fashion, kwa sababu taasisi nyingine wanayo. Ni fursa ambayo mkiitumia vema mtapata taarifa nyingi za kusaidia kuboresha huduma zenu, kulinda miondo mbinu yenu, kupunguza foleni ndefu (zisizo na tija) kwenye maofisi yenu na kupunguza rushwa na vishoka.
 
Kuna tatizo kuhusu mfumo MPYA wa kulipia bili kwa kutumia reference number yenye tarakimu 12. Mfumo haukubali kulipia kwa Simu kama tunavyoambiwa. Nilijaribu Mara NNE kulipia kwa tigo pesa! Unafuata hatua zote mpaka kuweka mamba ya siri lakini bado malipo hayafanyiki. Mpaka nikalazimika kwenda kulipia CRDB kwa kupoteza pesa kwa kulipa nauli na kupoteza muda kwenye foleni!! Huu mfumo haufai!!!
Pili reference number ingekuwa ni moja tu kwa kila MTEJA kwa muda wote kuliko hii ya kupewa reference number MPYA kila mwezi.
Tatu, pamoja na kuwa wana namba Yangu nilisubiri reference number kwa miezi miwili bila mafanikio mpaka nikalazimika kwenda ofisini kwao!!!!
Warudishe mfumo wa mwanzo uliokuwa rafiki zaidi wa kutumia akaunti namba ambapo tulikuwa tunalipia kwa Simu bila matatizo.

Sent using Jamii Forums mobile app
Juzi walikuwa wanatangaza mfumo wa mita mpya za malipo ya Prepaid[Mfumo kama wa malipo ya LUKU] Sijui utaanza mwaka gani, lakini walizindua tarehe 23.07.2018. Huuu ndio utakuwa mwarobaini. Wasoma mita za maji wahuni wataondoka ktk system, na itasaidia ukusanyaji wa mapato wale wasoma mita watabaki kukagua kuna utoroshwaji wa maji wapi? Maana kampuni ina wafanyakazi wengi lakini ufanisi mdogo sana na watu wanaiba sana maji na wakifunga izo mita mpya ziwe zina uwezo wa kutoa report ya kuanzia bomba kubwa ulipoungwa na mpaka kwy mita yako, tatizo linaloikumba Dawasco kuna wafanyakazi wenye umri Mkubwa ambao kasi ya technology imewatupa na wapo kitengoni, ndio iyo unakuta MTU ana diploma yeye ndio boss anasimamia sehemu alafu wasoma mita wana degrees, sasa apo kwy kugawanya madaraka inakuwa ngumu sana. Unakuta kunakuwa na ubishani na ukwamishaji ukwamishaji,. MTU ana degrees ya uhandisi wa maji lakini ataki kuchafuka na kuchimba ili kuweka bomba la maji sawa. Mimi hii ilishanikuta mtu, anakuja kurekebisha bomba muda wote yupo kwy simu Mara uku Mara Kule mpaka, nikamtafutia MTU wa kuchimba ndio akaaunganisha bomba
 
DAWASCO ; Kwa muonekano huu wa kuchelewesha kujibu hoja za wateja, inaonyesha hii Special Thread haijakuwa assigned kwa mtu specific wa kushughulikia kujibu kero za wananchi. Kama mmenuia kutumia njia hii kuwa karibu na wateja wenu, ni vyema mkamu-assign mtu 'informed' wa customer service awe na kazi ya kujibu kero za wananchi mmoja mmoja na ku-coordinate na wahusika ili kuleta tija kwa jamii.

Kuwa na special thread kusiwe fashion, kwa sababu taasisi nyingine wanayo. Ni fursa ambayo mkiitumia vema mtapata taarifa nyingi za kusaidia kuboresha huduma zenu, kulinda miondo mbinu yenu, kupunguza foleni ndefu (zisizo na tija) kwenye maofisi yenu na kupunguza rushwa na vishoka.
heri hata mliyounganishiwa huduma mm nipo kiwalani maji dawasco nayasikia tu sijui yanafananaje
 
DAWASCO HILI SI JAMBO SAHIHI

Hii ni zaidi ya kero
Huku Kimara mavurunza ni wiki ya tatu maji hayajawahi kufika na huwa ni kawaida yetu kuoga maji ya kununua kwenye magari.

BILL
wakati wa kuleta bill sasa bill kubwa huduma mbovu achana na hili Tumeshalizoea

Juzi tu mwezi huu huu
Wamekuta watu wa Dawasco wakitutaka tulipe deni la nyuma kwa maana tunadaiwa laki moja ambayo haijalipwa
Cha kushangaza sisi tumeunganishiwa na huduma ya maji mnamo mwaka 2017 mwezi August, tangu tumeunganishiwa hatujawahi kuacha kulipa wala kulimbikiza bill ya maji nasisitiza hatujawahi kuacha kulipa au kulimbikiza

Sasa wanakuja kudai T-SH 100,000 eti ni deni la zamani

Tumewaomba waje wachukue mita yao ili twende sawa, yaani maji yanatoka kwa mwezi mara 2 halafu tunalipa kila wakileta bill
Leo hii mseme kuna deni!
 
Naomba kuuliza hyo kampuni inayofunga mita za, maji za luku inaitwaje? Na je wameanza maeneo gani?

Je plan yao kufikia jiji zima upoje
 
Naomba kuuliza hyo kampuni inayofunga mita za, maji za luku inaitwaje? Na je wameanza maeneo gani?

Je plan yao kufikia jiji zima upoje
Iyo mifumo kama itakuwa na uwezo kujua maji yanayokuwa yanamwagika kuanzia maungio makubwa mpaka kwa mteja. Itakuwa nzuri lakini kama aitaweza kugundua kiwango cha maji yamwagikayo basi, watu wengi wataiba sana maji
 
Mko slow sana kuziba mabomba tangazeni namba zenu kama.ilivyo polisi na iwe bure mtu yeyote akiona bomba limepasuka awapigie
 
Kwangu hakujawai kutoka maji tangu 2005 na bado bill nikawa mnaleta na nilishawaandikia barua na kuwapa taarifa lakini bado bill mmeendelea kuleta mpaka imefika 1 milioni na wakati maji sijawai kutumia mpaka mliponiunganisha tena 2013 na taarifa nimewapa lakini bado mnataka nilipe deni lenu,naomba mrekebishe hili mnakera kubabimbikia watu madeni ambayo sio ya halali mana ni wizi huo hilo sitalipa mje kukata maji yenu na mahakamani tufikishane siwezi kubabimbikiwa deni kizembe hivyo.
 
Mikocheni karibu na Club 327, barabara ya rose garden kuna bomba lina karibu mwezi sasa linamwaga maji. ni bomba kubwa la Dawasco. tumesharipoti mpaka tumechoka. tunawaachia wenyewe siku mkipita mlione maana na nyie mmezidi. kujituma ni janga la kitaifa
 
Mikocheni karibu na Club 327, barabara ya rose garden kuna bomba lina karibu mwezi sasa linamwaga maji. ni bomba kubwa la Dawasco. tumesharipoti mpaka tumechoka. tunawaachia wenyewe siku mkipita mlione maana na nyie mmezidi. kujituma ni janga la kitaifa

Hali iko hivyo karibu kila eneo serekalini ! Sasa Magufuli akiwatumbua analaumiwa....
 
Back
Top Bottom