David Kafulila ajivua uanachama CHADEMA

David Kafulila ajivua uanachama CHADEMA

Status
Not open for further replies.
Ila Kijana ana confo za kutosha nilikuta anamalizia mahojiano yake na Mlimani TV
 
Si vizuri kuropoka ropoka anadhani huku ankoenda ndio kuna amani. Angalia hata CCM wanavyotafunana wenyewe kwa wenyewe. Yeye alitakiwa kutulia kuomba msamaha ili aanze upya. Hata katika dini ukikiuka taratibu zake unatengwa, kinsingi unakuwa umejitenga mwenyewe na Mungu. Kumbuka kila taasisi ina maadili yake. Kusaini hundi Mwenyekiti is not an issue.
 
Kafulila Kaflila Kafulila!!! Ni kweli naipenda CHADEMA? Kwa nini unaiterekeza hasa wakati umegundua ina viongozi wenye CHUKI wanapohojiwa khsu ukweli? Kafulila naondoka CHADEMA ili uende chama gani? Kafulila unaamini hatua uliochukua inajenga CHADEMA?? Kafulila hko uendako unaenda kukua au kufa kisiasa??Kafulila hivi unafahamu vizuri CHADEMA inamaanisha nini kwa watanzania makini hasa vijana??Kafulila ume-retreat au ume-surrender??Why Kafulila??Heri ipi na kwa nani unaitaka Kafulila??Kilichoanzishwa na Mungu, wanadamu hawawezi kukishinda.
 
nimesikiliza mahojiano ya kafulila mlimani tv...kwa kifupi ni kijana ambaye hata kwa mpangilio wa hoja zake ..anaaonyesha bado anahitaji malezi ya kisiasa....nadhani haukuwa wakati muafaka kwake kuhama ....nitamshauri tu asifanye kosa kwenda CCM ..kwani hatapata cheo anachotarajia.....ni vema akaenda chama kidogo kama NCCR ambacho kule kigoma kinajulikana ..ili aendelee kujijenga kisiasa..au la afikirie upya msimamo wake na kubakia CHADEMA.

Nadhani tubadilike kifikra ...kuhama vyama kwa tofauti ya kimtazamo kumepitwa na wakati ...internal power strugle kwenye association yeyote ni jambo la kawaida......na unatakiwa upiganie mabadiliko ndani ....kabla ya kutaka umaarufu nje..ya kundi au chama chako...that is normal political evolution....

ndio maana unaona hata rebels wa CCM wanapigana wakiwa ndani....ninafurahisha hata muheshimiwa zitto ..anakubaliana na dhana ya kupigania mabadiliko ndani ....kwa ndani...hiyo ndiyo siasa...historia haiwapi nafasi nzuri sana rebels wanao ditch boat...kwani angalia looosers kama kina kabourou,hiza tambwe na wengine...zaidi ya kupata pesa ya kununua mkate kurudi nao nyumbani jioni...they lack a really constituets as of now......ndani hawaaminiki ..na nje hawaaminiki....

na si vema mwanasiasa kujijengea legacy ya kutoaminika.....bora uwe na msimamo hadi mwisho....
 
Chama cha Demokrasia na maendeleo kinaelekea kuzimu kwa hatua zote ambazo kimekua kikipitia hadi sasa! walianza kwa kuhitilafiana na Dr warid, Marehemu chacha wangwe, kina Mzirai na hatimaye Kafulila.
Uwezekano wa Chadema kuelekea kuzimu ni mkubwa sana kwa kuwa historia ya mparaganyiko wa vyama vya siasa ni mparaganyiko pale swala la fedha linapoguswa! Wangwe alilalamikia matumizi ya ruzuku, kina Mzirai matumizi ya ruzuku, Kafulila matumizi ya Ruzuku aagh! kwa sisi wa mikoani hasa Tabora mjini ni aibu kweli kweli hasa unapozungumzia ofisi za Chadema, wanatumia kipande cha Gogo la mnazi lililolazwa chini huku Mwenyekiti wa Chadema na katibu wake wa Mkoa wakifanya biashara ya kukodisha baiskeli 2 (mbili) kama mradi wao waotegemea wakati vigogo wao wakiishi kwa neema huku wakiitaka ubunge na Urais Aibu!
 
Haya ni sehemu ya aliyoyasema kijana kafulila kwenye press conf.



TAMKO LA DAVID KAFULILA KUHUSU UAMUZI WA CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA) ULIOZUA UTATA NCHINI.



1.0 UTANGULIZI
Kwanza niwashukuru wanahabari kwa kuchag kuja kunisikiliza mimi niliye mdogo sana kimamlaka katika siasa za nchi hii kiasi cha baadhi ya viongozi wenye heshima kuufananisha ubinadamu wangu na sisimizi. Nawashukuru kwakuwa mmethibitisha kuwa waumini wa dhana ya “binadamu wote ni sawa”, wanastahili heshima kwa thamani yao.Nawapongezeni kwa hilo kwakuwa hiyo ni moja ya tunu imara ambayo watanzania tulirithishwa na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

2.0 SABABU ZILIZOSABABISHWA KUTENGULIWA KWA MUJIBU WA CHADEMA
Mnafahamu na mmekuwa mkiripoti mwenendo wa siasa ndani ya CHADEMA kuhusu kadhia ya kinachoitwa mgogoro ndani ya CHADEMA kufuatia taarifa za kikao cha siri kilichofanyika Dodoma chini ya uenyekiti wa Freeman Mbowe. Mpaka sasa mengi yamesemwa na viongozi mbalimbali akiwemo, Mwenyekiti wa kwanza na Mwasisi wa CHADEMA-Mzee Edwini Mtei, Mwenyekiti wa pili-Mzee Bob Makani, Mwenyekiti wa sasa Freeman Mbowe, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu, na baadhi ya wajumbe wa Kamati Kuu..

Aidha, mengi pia yamesemwa na wanachama, wafuasi na wadau wa siasa nchini kwa misingi ya siasa na hata dini kuanzia mkoani kwangu Kigoma na Taifa kwa ujumla. Kwa kutambua nafasi yangu kama kijana mwenye ndoto ya kuchangia mabadiliko makubwa katika medani siasa za nchiini, naomba nichukue nafasi hii kueleza zinazoitwa sababu zilizopelekea CHADEMA kufikia uamuzi ilioufikia dhidi yangu.

Sababu inayoelezwa ni mimi kutotambua kikao cha siri kilichoendeshwa na Mwenyekiti Freeman Mbowe Dodoma na baadhi ya viongozi wa chama. Binafsi nilikiri na bado ninakiri kwamba sikufahamu kuhusu kikao hicho kwakuwa hakipo kwa mujibu wa katiba, kanuni, maazimio na hata ratiba ya chama. Na nikiri pia kutotambua kikao hicho kwa msingi wa jukumu la kumvua mtu uanachama wa CHADEMA kama nilivyoulizwa na mwandishi wa habari, kwani kwa mujibu wa katiba, kikao cha kujadili uanachama wa mwanaCHADEMA sio kikao cha siri. Huo ndio ulikuwa msingi wa kwanza wa majibu yangu kwenye kikao cha sekretariet ya Novemba10,2009.

Pamoja na kikao hicho kutotambuliwa kwa mujibu wa katiba, kanuni na hata maazimio ya chama, binafsi sikuwa na fursa yoyote kufahamu kikao hicho kwakuwa; kwanza Mkurugenzi wa Habari na Uenezi ambaye ni Mkuu wangu katika idara kwa makusudi au bahati mbaya hakuniaga na wala kunikaimisha Ofisi kitu ambacho kingenisaidia kujua kwamba kuna kikao Dodoma. Hata aliyekuwa Kaimu Katibu Mkuu wakati huo, Mzee Victor Kimesera alikiri kwenye kikao cha sekretariet ya Novemba10,2009 kwamba hakuwa na taarifa kuhusu kikao hicho kilichohusu wakurugenzi walio chini yake,na kwamba alipewa taarifa tu kwamba kuna wakurugenzi wako nje ya mkoa kwa shughuli za chama Dodoma wakiwa wamesha ondoka…Sio hapo tu, hata Novemba4, 2009 usiku nilipowasiliana na wajumbe wa sekretariet kuwakumbusha kuhusu kikao cha kesho yake (Novemba05, 2009), ambao sehemu yake walikuwa kwenye kikao hicho cha siri, bado sikujulishwa kwamba kuna wajumbe walikuwa nje ya Dar es Salaam wakiendelea na kikao kingine na kwamba wasingeweza kufika kwenye kikao rasmi cha sekretariet siku ya Novemba5,2009..

Nimeona nitoe ufafanuzi huo kwa ajili ya kuweka kumbukumbu sahihi ya nini kilichotokea kwakuwa pamekuwapo upotoshaji wa taarifa kuhusu jambo hili, kiasi cha wengine kuandika kwamba nina kosa la kutoa siri za chama. Napenda kuwajulisha kwamba sijachukuliwa hatua kwa kosa la kutoa siri za chama, bali kwa kilichoitwa kosa la kutotambua kikao cha siri chenye mamlaka ya kumvua mtu uanachama.Kwa mujubu wa katiba kikao cha kumfukuza mtu uanachama hakiwezi kuwa siri kwa mujibu wa katiba na kanuni. Na kwamba mwanachama makini wa chama makini hawezi kufukuzwa kwa vikao visivyo rasmi.

TATIZO LA MSINGI NI NINI CHADEMA ;
Kwakuwa pamekuwapo upotoshaji mkubwa kuhusu suala hili unaofanywa kupitia vyombo mbalimbali vya habari, ninaomba kuwaeleza vijana wenzangu wa CHADEMA ukweli uliopelekea hali hii;

1.AUMUZI WANGU WA KUHOJI KUHUSU UKWELI NDANI YA CHAMA.

Nilimwambia Dr Slaa, na sasa naomba niwaambie wanachadema kwamba tatizo nililoitiwa kuhojiwa halikuwa tatizo husika.Chanzo cha matatizo yote haya ni uamuzi wangu wa kuhoji ili kama chama TUJISAHIHISHE.

A.Nilihoji kuhusu matumizi ya ruzuku .
Mchakato wa kunifukuza makao makuu haukuanza leo. Nakumbuka februari 2009, wakati nilipokuwa nikihoji kuhusu matumizi ya milioni35 za mwezi desemba2008,Mkurugenzi wa Fedha alithubutu kumwambia Katibu Mkuu kwamba “Huyu Kafulila sio mjumbe wa kikao, kwaiyo hapaswi kuwa anahoji kwenye sekretariet, yeye ni mwandishi tu”. Hapa nilimhoji Dr Slaa ambaye alikuwa Mwenyekiti wa kikao “Kwanini tangu mwaka 2007 nimeruhusiwa kuingia kwenye kuandika na kuchangia hoja, iweje leo nisiruhusiwe kuchangia hoja?, kwasababu ninahoji masuala ya taarifa za fedha?”.

B.Nilihoji kuhusu taratibu za fedha ndani ya chama.
Chuki zaidi iliongezeka baada ya kushinikiza kwenye vikao vya sekretariet kuhusu kuundwa kwa Kamati ya manunuzi badala ya Mkurugenzi wa Fedha kuwa muamuzi katika hatua zote za manunuzi. Hoja hii haikupendwa na ndio sababu pamoja na kuundwa kwa Kamati hiyo ya manunuzi bado masuala yote ya manunuzi yameendelea kufanywa na Mkurugenzi wa Fedha kama zamani. Ikiwa ni takribani miezi nane tangu kamati ya manunuzi iundwe, bado haijawahi kukaa kikao chochote kuamua manunuzi ya chama.

Sio hayo tu, hata mpango wa sasa wa kuchangisha fedha kwa SMS hauna usalama wa fedha hizo kwasababu watia saini(signatories) ni Mwenyekiti Freeman Mbowe na Anthony Komu ambao hawakuteuliwa na kikao chochote kuwa signatories.

C.Mwendelezo wa chuki kabla na baada ya uchaguzi mkuu wa chama.
Katika kikao cha kwanza cha sekretariet baada ya uchaguzi mkuu wa chama, Katibu Mkuu alinifokea na kuniambia “mlango uko wazi” kwa madai kuwa nilishiriki kumfanyia kampeni Zitto Kabwe. Kwaiyo mimi nilitakiwa kuchukuliwa hatua kwa kumpigia kampeni zitto kabwe, lakini akina John Mnyika, John Mrema, Anthony Komu, Benson Kigaila hawakuchukuliwa hatua kwasababu tu walikuwa wakimfanyia Mbowe kampeni.

D.Mbowe na Slaa hawakutaka Kafulila awe kiongozi.
Baada ya kuanza kuhoji kuhusu uhalili wa masuala mbalimbali ya chama, Mbowe na Slaa walihakikisha kwamba David Kafulila hawi kiongozi wa chama. Mwaka jana wakati wa mchakato wa kumpata Mkurugenzi wa vijana, jina la David Kafulila lilipingwa vikali na wapambe wa Mbowe na Slaa. Lakini kwakuwa walijua kwamba nina sifa za kushika nafasi hiyo, kila walipotaka kupeleka majina ya wanaopendekezwa na sekretariet kwenye kamati kuu ili kumpata Mkurugenzi wa vijana, agenda iliahirishwa kwa hofu ya Kafulila kuibuka mshindi. Ni kwa utaratibu huu ajenda ya pendekezo la jina la Mkurugenzi wa vijana iliahirishwa mara tatu, mapaka tukaingia kwenye uchaguzi mkuu wa kwanza wa Baraza la vijana. Ambao nilishinda, lakini kwasababu zilezile za chuki, matokeo hayakutangazwa.

Naomba kutamka rasmi kwa nia njema kabisa , na kwa lengo lile lile nililosema hapo juu, kuanzia sasa mimi David Kafulila napenda kuutaarifu umma kuwa sio mwanachama wa CHADEMA…Na bado ninatafakari kwa mazingira yangu njia mbadala ya kufikia lengo lile lile la kujenga upinzani imara nchini. Najua ni uamuzi mgumu. Najua utapokewa kwa kila sura hapa nchini, Lakini sina mbadala wa uamuzi huu. Ninawaheshimu sana wanachadema, ninawaheshimu sana viongozi wa CHADEMA.

Mwisho, ninaipenda nchi yangu, ninawapenda watanzania. Ninafahamu kwamba Taifa linapita katika kipindi kigumu sana chenye misukosuko ambayo msingi wake ni siasa duni ambazo msingi wake ni upinzani dhaifu kwa upande mmoja na Chama tawala kilicho choka kwa upande wa pili…

Ninaahidi sintowaangusha katika ujenzi wa upinzani imara na hatimaye serikali madhubuti. Na ninawaonya CCM wakome kutumia migogoro katika vyama vya upinzani kujihalalishia utawala, na badala yake wanapaswa kujihalalishia utawala kwa kujenga ustawi wa watanzani. Ninaondoka CHADEMA kwa uchungu mkubwa kwasababu ya lengo thabiti kwamba lazima niitumikie nchi yangu katika harakati za siasa, na. Nitaikumbuka sana CHADEMA kwakuwa nilimwaga damu katika ujenzi wa chama hiki, ninalazimika kukaa pembeni.

Nawatakia kila la heri

Hapa nina tatizo moja na Kafulila
ktk huo mstari wa mwisho anamaanisha nini? alimwaga damu ya nani? maana nielewavyo mimi unaposema kumwaga damu maana yake ni kuua.Ama ana maana gani?
 
Tusubiri next move kama sio CUF basi ni kulekule kwa "Mwenda tezi na omo, marejeo ngamani'. Its only a matter of time!.
 
Huyu Kafulila kwangu mimi naona kafulia kweli kweli.

Katika maelezo yake hakuna mahali ambapo kuna nguvu ya Hoja ya kumfanya atimue toka CHADEMA. Unaposoma katikati ya mistari inaonekana kuwa Kafulila amekuwa anatumia na nguvu kutoka nje ili kuivuruga CHADEMA.

Kama kweli yeye alikuwa upande wa Zitto Kabwe wakati wa Uchaguzi Mkuu wa CHADEMA na alimfanyia kampeni Zitto ili amwangushe Mwenyekiti Freeman Mbowe basi matokeo ndiyo haya.

Tatizo la vyama vyetu vingi vya Siasa ni kuwa kila mtu anataka kuwa maarufu ndani ya Chama. Zitto Kabwe ameanza kujiona kuwa ni bora na ni maarufu kuliko hata waasisi wa CHADEMA. Hilo ni kosa la wazi. Ni utovu wa nidhamu kama siyo kukosa adabu kupingana na wazazi wako kwa kile wanachokiona ni bora kwa familia.

Zitto Kabwe anataka ku-gain popularity kupitia CHADEMA. Ndiyo maana ana thubutu kujaribu kupingana na Wakuu wake ndani ya Chama.Hilo ni kosa.

Zitto anatakiwa kusoma alama za nyakati na kuangalia nyuma kule chama kilikotoka. Wazee wa CHADEMA kina Edwin Mtei na Bob Makani waliwapisha kina Freeman Mbowe na kina Slaa kwa ustaarabu kabisa bila matatizo.

Kwamba wazee hawa waliamua kung'atuka kuwapisha vijana! Zitto alitakiwa ajifunze kutokea hapo.Yeye ana haraka gani ya kuchukua chama? Kwa nini asisubiri wakti kina Mbowe watakaposema hawataki tena Uenyekiti wa Chama? Mbona hata CCM wana ustaarabu wa kuachiana kiti cha Mwenyekiti kwa ustaarabu?

Kwangu mimi naona kuwa CHADEMA imeshaanza kuhujumiwa na CCM. Siwezi kushangaa kusikia kuwa mtu kama Kafulila ni mamaluki wa CCM aliyepandikizwa ndani ya CHADEMA. Bado nafuatilia nyendo za Mhe. Zitto Kabwe kuona kama na yeye ameshaanza kutumiwa na mafisadi kuivuruga CHADEMA.

TUKUMBUKE KUWA CHADEMA NDIYO WALIOSABABISHA kuyumba kwa serikali ya Kikwete kwa kutaja yael majina 11 ya mafisadi(List of shame). Mwanzo CCM walianza kwa kupinga kabisa kuwa madai ya CHADEMA hayakuwa kweli lakini baada ya ushahidi kuanza kuibuliwa na CHADEMA, CCM wakabadili mwelekeo. Wakakubaliana na CHADEMA kwa shingo upande kitu ambacho kimewagharimu sana CCM.

Jambi hili halijaifurahisha CCM hata kidogo kwa hiyo inafanya kila mbinu kupenya ndani ya ngome ya CHADEMA ili kuisambaratisha kabla ya uchaguzi wa 2010. Huo ndiyo ukweli.
 
. Nitaikumbuka sana chadema kwakuwa nilimwaga damu katika ujenzi wa chama hiki, ninalazimika kukaa pembeni.



unazidi kuniweka mbali na siasa. Haya mambo ya kuropoka ropoka kwenye vyombo vya habari haya?
 
yaani pasipo madaraka watu hawawezi kukaa upinzani?

Na hicho ndo kinachowasababisha watu wanashindwa kuendelea kukaa katika vyama vya upinzani.Mtu akishapata kaumaarufu kidogo basi alishajiona yeye ndo chama huku akijivimbisha kichwa kwamba anaweza kwenda kokote na akawa mtu katika watu.wengi wa walio upinzani hawana uvumilivu hasa wale wenye damu ya ccm.
 
nimesoma vizuri andiko lake David kafulila kwa vyombo vya habari iliyowekwa humu kwenye Jf, nimestushwa na kauli yake ya kusema kuwa amemwaga damu chadema, hivi kivipi jamani.mi ninavyojua nchi yetu haijamwaga damu yoyote eti kwaajili ya ukombozi, atuambie vizuri anahusika katika mauaji na anataka kuuambia nini uma kuwa chadema kimeshamwaga damu kwenye movement zake? au ni huku kutapatapa.......

kama ni kutapatap kweli umeanguka kabisa my broo.
 
Sasa swali hili si-ungeuliza kwenye thread yenye hilo andiko kwa vyombo vya habari, kulikuwa na umuhimu gani kuanzisha thread mpya..?MNI
 
halafu wewe MOD unaefuta post,narudia tena kusema mzimu wa wangwe unaikomesha CHADEMA.
 
Kijana kafulia....Mtu yeyote unapopata mitihani kama hii ndio kwanza unazidisha mapambano ndani ya chama chako. Kuondoka kama mwanachama sio solution hata kidogo.
Na anaposema alimwaga damu hii inatisha! tunahitaji maelezo zaidi...
 
Baada ya habari zake kuandikwa sana nilichukua hatua za kumtafuta huyu Kafulila ni mtu wa namna gani, na nilipata majibu yafuatayo;
1. huyu jamaa ni mtu anapenda sana kujiona anauwezo kumbe hana ,na hili ni kwa mujibu wa watu waliokuwa nae kwenye maeneo mbalimbali na haswa alipokuwa na vijana imara wa CUF kwenye vikao vya TCD.
2.Nimeambiwa kuwa alikuwa anasoma UDSM kozi ya BBA Evening programme ila alidisco.
3.Nimeambiwa aliwahi kuanguka kutoka gorofa ya kumi hotel moja kariakoo ,sikumbuki jina nililotajiwa .

Nilipofika hapo nikaona sina haja ya kumjua zaidi kwani ni mtu ambaye hata shule ilimshinda ,tena evening class kudisco , na ukichanganya na kuanguka kutoka gorofani basi unapata jibu kuwa inawezekana amechanganyikiwa.

Kama taarifa nilizopewa na jamaa wanaomfahamu ni sahihi basi sintaendelea kumjadili wala kumfuatilia kwani nimeshaweka maoni yangu-kifupi nampuuza tuu.

Nilimfuatilia kwani nilitaka kumshawishi ajiunge na chama dume , ila hafai.
 
Unajua kikwetu KAFULILA ni mtu ALIYEFULIA, kwa mtazamo wangu kama kweli Kafulila alikuwa na dhamira ya kweli ya kujenga upinzani ulio na nguvu asingeongea mambo yote hayo baada ya kujitoa. Hii inaonyesha alikwenda chedema kutafuta madaraka au kama mamluki. Siamini kama amekwenda kukuza chama ndo maana aliponyang'anywa uongozi akaona hakuna tena faida zaidi ya kutoa lawama.
Kama kweli alikuwa anaitakia mema chadema angekaa na kupambana humohumo au kukaa kimya ili akina mbowe wadhihilishe kwamba wao ndo tahira lakini kwa picha ilivyo sasa Kafulila si mtu wa kuaminika. kwanza hafai hata kuwa baba kwani atakuwa anatoa siri za mkewe na nyumbani kwake.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom