David Kafulila ajivua uanachama CHADEMA

David Kafulila ajivua uanachama CHADEMA

Status
Not open for further replies.
Ulitaka nani asaini cheque?
Wanaosaini si wanasaini kwa vyeo vyao? kama leo yuko Komu ndio mkurugenzi wa fedha ulitaka asaini afisa habari? ama mkurugenzi wa mambo ya nje?

Mbona hujiulizi kwanini Makamba anasaini cheque? sio kwa sababu yeye ni Makamba ila ni cheo chake.

Na anayesema eti Lipumba hasaini cheque ni muongo wa kutupwa na hajui, ukweli ni kuwa anasaini na ipo account moja inaitwa ya uchaguzi ambayo wanaosaini ni Lipumba na Maalim tuu.

Na ndio maana mnaambiwa hamuambiliki. Anaposaini check Mbowe (Chairman), nani atakayepinga matumizi yake?

Komu ni ndugu/mpambe wa Mbowe wa karibu sana, kwa hiyo hata kama kimadaraka alitakiwa asaini, kiutendaji kunakuwa na conflict of interest. Why not change to avoid kelele and mistrust?

Haya mengine nayo vipi?
  1. Ushauri wa matumizi hamsikilizi
  2. Uwazi wa matumizi unaolalamikiwa haupo
 
kama ni hivyo nadhani sio sahihi na haivutii machoni mwa watu wa kawaida. Ndio maana inakuwa ngumu kum-separate mwenyekiti Mh. Mbowe na kashfa za Ufisadi wa pesa za ruzuku ndani ya Chama. Mimi nadhani mwenyekiti asingekuwa signatory, kazi ya kusaini abaki nayo Katibu Mkuu (Slaa) (na awe ndio afisa fedha mkuu, yaani mwangalizi) alafu mkurugenzi wa fedha (Komu) na Mtu mwingine mtakavyoona inafaa, mathalani mjumbe mmoja wa kamati ya Fedha (kama ipo). M/kiti kuwa signatory inatoa picha mbaya, hiii sio kampuni mkuu,[/QUOTE]

Umejibu vyema kuwa hii sio kampuni bali ni chama cha siasa, hivyo ukumbuke pia kuwa viongozi wa vyama wanachaguliwa na mamlaka hiyo wanapewa na wanachama waliowachagua, sasa unataka wachaguliwe halafu wasipewe mamlaka ya kusimamia fedha?
Hapa naona tatizo ni kujenga hoja kwa hisia , kwa kuwa Mbowe ameandikwa sana eti anakula ruzuku ndio maana watu mnahoji.

Cheque za chama zinasainiwa na watu 3 ambao ni mjumbe mmoja wa baraza la wadhamini, Mwenyekiti/Katibu Mkuu na mkurugenzi wa fedha.
Na hilo ni suala ambalo lipo kikanuni na kikatiba, sasa jiulize hivi siku ikatokea kuwa Mwenyekiti na Katibu Mkuu hawaelewani kumbuka kisa cha NCCR =na Mwenyekiti sio mtia sahihi atawezaje kujua mmoja wapo kuwa mwenzake ameshakiibia chama?

Cha msingi ni kuwa pawepo na njia nzuri ya kufuatilia ,na kusimamia na ndio maana CHADEMA kamati kuu inakaa kila ndani ya miezi minne na ni lazima taarifa ya fedha ipelekwe na kujadiliwa , sasa huyo anayehoji eti Komu , sijui Mbowe ,sijui Slaa alitaka apewe yeye kusaini?

Tusiwe wepesi wa kulishwa hoja dhaifu nasi tukaanza kuzidakia na kuzijadili .
Inawezekana kabisa kuwa Kafulila ana ugomvi binafsi ama na Komu, Mbowe ama Slaa ndio maana anahoji sasa alipaswa aulizwe alitaka wasaini kina nani ndio aridhike?

Issue hapa ni position na sio individuals/personalities.
 
Kwa ushauri huu nakubali kabisaa kuwa CHADEMA ya Mbowe ni NGO.

Mbowe and Mtei have to go for CHADEMA to survive.

Hivi kwa dunia ya leo visenti vya ruzuku vinaweza kukiendesha chama kama CHADEMA?
 
Na ndio maana mnaambiwa hamuambiliki. Anaposaini check Mbowe (Chairman), nani atakayepinga matumizi yake?

Komu ni ndugu/mpambe wa Mbowe wa karibu sana, kwa hiyo hata kama kimadaraka alitakiwa asaini, kiutendaji kunakuwa na conflict of interest. Why not change to avoid kelele and mistrust?


Haya mengine nayo vipi?
  1. Ushauri wa matumizi hamsikilizi
  2. Uwazi wa matumizi unaolalamikiwa haupo
Kaful;ila alisema mwenyewe kuwa wanaojadili matumizi ya fedha na ni kila mwezi ni vikao vya secretariati na hupanga bajeti, sasa kama alivyosema mwenyewe kuwa yeye alikuwa akihudhuria hivyo kama alishiriki kupanga matumizi na sasa anaona kuwa kuna matumizi mabaya ya ruzuku ambayo alishiriki kupanga matumizi hayo basi naye allishiriki kupanga matumizi mabaya ya fedha za chama.

all in all vikao vinakaa na kupanga matumizi na sio watu binafsi wanajiamulia tuu.

Ushauri huo ulitolewa na nani? na lini na wapi ulikataliwa? na kama ulikataliwa je?alipewa sababu za kukataliwa kwa ushauri wake? muulize hayo maswali then lete hoja tujadili.
 
Ulitaka nani asaini cheque?
Wanaosaini si wanasaini kwa vyeo vyao? kama leo yuko Komu ndio mkurugenzi wa fedha ulitaka asaini afisa habari? ama mkurugenzi wa mambo ya nje?

Mbona hujiulizi kwanini Makamba anasaini cheque? sio kwa sababu yeye ni Makamba ila ni cheo chake.

Na anayesema eti Lipumba hasaini cheque ni muongo wa kutupwa na hajui, ukweli ni kuwa anasaini na ipo account moja inaitwa ya uchaguzi ambayo wanaosaini ni Lipumba na Maalim tuu.

Mwenyekiti sio mtendaji hataki kusaini hundi.hiyo uliyosema ya CUF ni temporary account. pesa za ruzuku haziingizwi huko kwenye account ya uchaguzi.

bwana mdogo mmeshammaliza Kafulila unaona haitoshi leo umekuja kukesha hapa JF.
Msijidanganye kumgusa Zitto hamumuwezi.amejijenga toka chini na ana kundi kubwa la wanachama ndio maana bosi wako alifanya kila njia kumzuia asigombee.
 
Kaka nitake radhi kaka,

Mimi sio mshabiki wa Zitto na wala sina kundi huko na CHADEMA. Mimi ni rafiki wa Zitto. Urafiki wetu sio wa nafasi za kisiasa ama kijamii, ila ni wa kiitikadi (wote tunaamini katika ujamaa), kimitizamo (wote tunaamini katika constructive criticism/engagement), ki-ajenda (wote tunaamini katika demokrasia makini na sio bora demokrasia), Vision (wote ni waumini wakuu wa muungano wa Afrika – Panafricanism), Misingi (Siasa ni utumishi na sio uheshimiwa) na mengineyo. Sasa huko kwenye upambe kwa kweli itakuwa ni kunitusi. Una haki ya kuona hivyo lakini mimi binafsi sijioni hivyo kamwe na naamini hata Zitto pia.

Pia ni muhimu ukanikumbusha wapi ambapo mimi niliwahi kumchafulia ama kumtuhumu MBOWE ama Dr Slaa zaidi ya kusema kuwa kuna watu ambao wako karibu yake ni wafitini wakubwa kitu ambacho hata wewe unakubaliana nacho katika moja ya michango yako hapa.

Na zaidi nilichowahi kufanya hapa ni kujaribu kuondoa sumu iliyokuwa /inayoendelea kupandwa dhidi ya Zitto na watu humu na kwengineko ambao baadhi yao wanatoka CHADEMA na na wengine kutoka katika makundi mengine ya kisiasa. Sasa mimi kuja kuelezea jinsi nimjuavyo Zitto ikiwa ni tofauti na majungu na fitina hizo ndiyo nimekuwa mbaya ama muendeleza makundi. Ulitaka ninyamaze kimya ili wanajamiiforums na watanzania wengine wajenge mtazamoa/maoni hasi dhidi ya Zitto kwa mujibu wa majungu na fitina za maadui zake na sio utetezi wa marafiki zake?

Na zaidi ndugu yangu huku kunifananisha na wapambe wa hawa WAJASIRIAMALI WA SIASA uliowataja hapo juu ndio tusi kubwa zaidi…

omarilyas
Mkuu wangu kwanza nakuomba samahani kama ulivyotaka nitangulize...lakini pia naomba maelezo yangu kuyaweka wazi na uyapokee..
Kwanza ni kutokana na majibizano yenu ndio yaliyonisukuma mimi kusema nilichoandika.. Na nitarudia kusema hakuna kundi la Zitto na Mbowe isipokuwa kuna kundi la Zitto na wale wanaompinga wakitumia jina la Mbowe kuweka uzito wa utetezi wao kwani binafsi naamini kabisa kwamba hakuna uhasama wowote baina ya Mbowe, Dr.Slaa na Zitto isipokuwa ni watu wanaotafuta kukibomoa chama aidha makusudi au kwa kutofahamu wanfanya hivyo kutokana na chuki zao binafsi kwa baadhi ya viongozi hawa.
Na nimeongezea tu kusema inafanana na malumbano ya Mwakyembe na Mwakalinga kwa sababu hoja kubwa ya wananchi ni KYELA na sii Mwakyembe wala Mwakalinga. Na kile kinachosukuma great mind kuzungumzia zaidi Idea ni pale unapoweka issue at hand kuwa aidha ni CHAMA, KYELA au WANANCHI wake badala ya issue nzima kuwa Mwakyembe au Mwakalinga.. Unapoanza na Mtu kuwa the main issue ni vigumu sana kujenga mawazo mbadala nje ya mtu isipokuwa mawazo ya kumjenga au kumbomoa mtu huyo.

Sasa basi maadam mimi ni mtu mzima na mwenye kuelewa hadithi za kutunga nafahamu fika kwamba Zitto na Mbowe sii issue hata kidogo, matatizo ya Chadema kama YAPO are deeper than Zitto au Mbowe na Dr.Slaa kwani navyoelewa mimi hawa watu sii maadui wala hawana uhasama isipokuwa washabiki wake ndio wanaozusha mambo haya kuwa makubwa kiasi ambacho wanataka wananchi waanze kupima umuhimu wa Zitto vs Mbowe au Dr. Slaa ndani ya chama.

Kama sikosei kuna mwana JF Invincible, mara kibao aliwahi sema Chadema ni kubwa kuliko Mbowe, Dr. Slaa na Zitto..sijui kama nyote mlielewa uzito wa maneno yake..
Kwa hiyo kaka, maneno yangu ya kusema ushabiki umetokana na ukweli kwamba umechukua muda mrefu kumlinda Zitto na sii ideology unayo amini. Ningefurahi sana kama ktk utetezi wako ungetumia zaidi imani yako ili kuunganisha na matukio yanahusiana na Zitto. Lakini utetezi wako ulivutwa na mvuto wa kutetea soul partner wako kiasi kwamba ukaingia ktk mkumbo wa kusema Zitto is not a problem (an Issue) but someone else is!.

Ndipo napokataa na kusema sasa huu ni ushabiki kwani matatizo ya Chadema yanasukwa tu.. hakuna mtu anayesababisha matatizo ya Chadema isipokuwa kuna watu wanaotafuta kuzua matatizo hayo kwani nimemsoma vizuri Bi. Asha na yaonyesha wazi kuna uelewano mkubwa baina yao ktk sekta ambazo wengi wetu tunaziwekea mashaka. Zitto, Dr. Slaa, Mbowe wote wanaendelea kusema hakuna matatizo Chadema iweje hapa JF ndipo tunaoina matatizo baina ya viongozi hawa watatu!..Je kuna ambalo hatulifahamu na kama lipo who is telling the truth!

Mkuu wangu kweli unaweza kuwa rafiki wa Zitto kutokana na imani yako ktk itikadi na nadhani hili hata mimi nipo upande wake.. Mimi pia nimekuwa interested sana na chama Chadema kwa sababu hiyo pekee na sii mtu yeyote na nitayatetea yale tu yaliyomo ktk msahafu wa imani yangu..kwa hiyo itikadi hii inatuweka sote pamoja lakini kama Zitto atakosea nitakuwa rafiki wa kwanza kumkosoa, kumkanya, kumuasa na kumbumbusha malengo ya imani hii inavyopingana na matendo yake.
Na viongozi hawa wa Chadema kwa kuacha watu wanakivuruga chama, watu wanaongea na waandishi wa habari wakati wa kikao cha chama Dodoma kuelezea kufukuzwa kwa mtu kiasi kwamba gazeti linamtafuta mhusika na kumuuliza kama anayo habari kuhusiana na mkutano huo ndio UNAFIKI mkubwa utakao kibomoa chama.
Rev. Kishoka ameshuka na kitu na hakika TTTP ambayo ni pigo kubwa sana kwa Chadema strategically, haya ndio mambo ya kutazama kwa nini mtu kama Rev kafikia kufungua chama with new edition inachofundisha Gospel yetu..Tunafanya makosa wapi na tunaweza vipi kuweka ushawishi kwa vijana ambao wamefikia kuona kwamba hata Chadema hawana mpango wa kuchukua madaraka..Kwa mtazamo wangu kufikia mwaka 2015, Chadema haitakuwa Chadema ikiwa mambo kama haya ya Zitto vs Mbowe yataendelea kukuzwa wakasahau malengo ya Upinzani ni kuchukua madaraka na sii kuwa ranked underdog.
 
Kaful;ila alisema mwenyewe kuwa wanaojadili matumizi ya fedha na ni kila mwezi ni vikao vya secretariati na hupanga bajeti, sasa kama alivyosema mwenyewe kuwa yeye alikuwa akihudhuria hivyo kama alishiriki kupanga matumizi na sasa anaona kuwa kuna matumizi mabaya ya ruzuku ambayo alishiriki kupanga matumizi hayo basi naye allishiriki kupanga matumizi mabaya ya fedha za chama.

all in all vikao vinakaa na kupanga matumizi na sio watu binafsi wanajiamulia tuu.

Ushauri huo ulitolewa na nani? na lini na wapi ulikataliwa? na kama ulikataliwa je?alipewa sababu za kukataliwa kwa ushauri wake? muulize hayo maswali then lete hoja tujadili.

Kama Mwenyekiti na rafiki yake Komu ndio wanaosaini checks, uwajibikaji wa matumizi utatoka wapi? Nani atampigia kelele mwenyekiti bila kuambiwa hana heshima na kufukuzwa? CHADEMA sio kampuni binafsi ambapo bosi ndiye mwenye uamuzi wa mwisho.

Malalamiko ya matumizi ya pesa yalikuwapo siku nyingi tokea enzi za marehemu Wangwe na riport ya uchunguzi ya Mziray ilithibitisha hayo. Sasa kama Wangwe alikuwa kichaa, Kafulila naye ni kichaa pia?

Mapato na matumizi mbona hatuyaoni tena wakati tuliambiwa yatakuwa kwenye mtandao?
 
Kama Mwenyekiti na rafiki yake Komu ndio wanaosaini checks, uwajibikaji wa matumizi utatoka wapi? Nani atampigia kelele mwenyekiti bila kuambiwa hana heshima na kufukuzwa? CHADEMA sio kampuni binafsi ambapo bosi ndiye mwenye uamuzi wa mwisho.

Malalamiko ya matumizi ya pesa yalikuwapo siku nyingi tokea enzi za marehemu Wangwe na riport ya uchunguzi ya Mziray ilithibitisha hayo. Sasa kama Wangwe alikuwa kichaa, Kafulila naye ni kichaa pia?

Mapato na matumizi mbona hatuyaoni tena wakati tuliambiwa yatakuwa kwenye mtandao?
Ya CCM yako wapi?
Lengo lenu limeshutukiwa na magazeti yenu ya mafisadi , subiri mkono uanguke ,looo fisi mpaka leo anaufuatilia mkono.
 
Mwenyekiti sio mtendaji hataki kusaini hundi.hiyo uliyosema ya CUF ni temporary account. pesa za ruzuku haziingizwi huko kwenye account ya uchaguzi.

bwana mdogo mmeshammaliza Kafulila unaona haitoshi leo umekuja kukesha hapa JF.
Msijidanganye kumgusa Zitto hamumuwezi.amejijenga toka chini na ana kundi kubwa la wanachama ndio maana bosi wako alifanya kila njia kumzuia asigombee.

Kafulila , kama amejijenga amejijenga mwenyewe na kama amejimaliza kajimaliza mwenyewe.
 
Kama Mwenyekiti na rafiki yake Komu ndio wanaosaini checks, uwajibikaji wa matumizi utatoka wapi? Nani atampigia kelele mwenyekiti bila kuambiwa hana heshima na kufukuzwa? CHADEMA sio kampuni binafsi ambapo bosi ndiye mwenye uamuzi wa mwisho.

Malalamiko ya matumizi ya pesa yalikuwapo siku nyingi tokea enzi za marehemu Wangwe na riport ya uchunguzi ya Mziray ilithibitisha hayo. Sasa kama Wangwe alikuwa kichaa, Kafulila naye ni kichaa pia?

Mapato na matumizi mbona hatuyaoni tena wakati tuliambiwa yatakuwa kwenye mtandao?

Heshima Kwako Kubwajinga

Chukua tano ndugu yangu kubwajinga yaani umemaliza kabisa sema jamaa wa CHADEMA wanapenda ligi za kitoto watakuja hapa na utetezi wa kipuuzi lakini wenye akili tayari tumeshawagundua.
 
wakubwa habari za siku, Mimi sioni cha ajabu heti mwanachama kujivua uanachama. Labda kwa mtu asiyejua maana ya uanachama sasa kama mtu kaona ama kuonyeshwa kuwa haendani na chama hicho atabaki wa kazi gani ? Wangapi waliama na wengine kufukuzwa ktk vyama na bado vikabaki imara? SIDHANI KAMA CHADEMA NAKO KUNA YALE YA NYUMBA YA PILI AMBAKO KTK VIKAO VYA CHAMA MTU MMOJA ANAWEZA KUDAI KUWA YEYE NDO CHAMA NA PSIPO YEYE CHAMA HAKIENDI. kila la kheri kafulila ndo uhuru wa democrasia.
 
Kubwajinga

Kama Mwenyekiti na rafiki yake Komu ndio wanaosaini checks, uwajibikaji wa matumizi utatoka wapi? Nani atampigia kelele mwenyekiti bila kuambiwa hana heshima na kufukuzwa? CHADEMA sio kampuni binafsi ambapo bosi ndiye mwenye uamuzi wa mwisho.

Tatizo lako KJ unazungumzia watu zaidi ndiyo maana hoja zako zinakosa mashiko! Tatizo ni Mbowe kusign au Mwenyekiti?

Kubwajinga

Malalamiko ya matumizi ya pesa yalikuwapo siku nyingi tokea enzi za marehemu Wangwe na riport ya uchunguzi ya Mziray ilithibitisha hayo. Sasa kama Wangwe alikuwa kichaa, Kafulila naye ni kichaa pia?
Mapato na matumizi mbona hatuyaoni tena wakati tuliambiwa yatakuwa kwenye mtandao?

Sasa unakwenda Mbali mpaka unamwita Kafulila Kichaa

Kafulila

Kwa mfano, Mh Chacha anazungumza hadharani kuwa ruzuku ya chama haiendi mikoani. Lakini anasahau kuwa Kamati Kuu ilisha agiza kuwa kila mkoa ufungue akaunti utumiwe sh 100,000/=(laki moja kwa mwezi). Je Chacha anaweza kutoa mfano wa mkoa uliokwisha fungua akaunti na haujatumiwa pesa hiyo?..Sio hayo, kila wilaya yenye diwani na zile za makao makuu ya mkoa ziilikwishaagizwa kufungua akaunti ili zitumiwe sh 200,000/= kwa mwezi tangu mwaka 2007.

Na ikumbukwe kuwa CHADEMA kinapata ruzuku ya kiasi cha takribani milioni60 kwa mwezi,dhidi ya CCM inayopata ruzuku ya bilioni1.2 kwa mwezi(takribani mara20 ya ile ya CHADEMA). Ruzuku ya CCM kwa mwezi ni takribani sawa na jumla ya ruzuku ya CHADEMA kwa zaidi ya mwaka mmoja na nusu.

Zaidi ya fedha hizo kutumwa, Chama kinatengeneza vifaa vya uenezi kama vitabu, bendera,nk na kusambaza wilayani bure ili kuhakikisha chama kinafanya kazi. Viongozi wa taifa wanafanya ziara mikoani mara kwa mara.Kwa mfano, kwa miezi miwili tangu mei2008, Viongozi wamefanya ziara mikoa mbalimbali. Zitto Kabwe amefanya ziara ya Chama Tanga kwa siku nne, na Kigoma kwa wiki mbili. Ilhali Dk Slaa emefanya ziara Singida na Manyara., Ni bahati mbaya kwamba wakati wengine wanaendelea kujenga chama wengine wanahaha huku na kule kutafuta jinsi ya kubomoa badala ya kwenda bungeni au mikoni kufanya kazi.

Wakati Mh Chacha Wangwe anasema CHADEMA imeshindwa kufanya kazi Dar es Salaam , anasahau kuwa mpaka sasa kuna timu ya kuhamasisha chama mkoa wa Dar es Salaam , na wanatumia fedha za chama. Wamefungua matawi Temeke na sasa wanaendelea Kigamboni. Mh Chacha anafahamu hilo kwasababu imeripotiwa kwenye Kamati Kuu ambayo yeye ni mjumbe. tayari zaidi ya matawi ishirini yamefunguliwa Temeke, Kinondoni na yanaendelea kufunguliwa Kigamboni kwa fedha hiyo ya ruzuku na msaada wa makao makuu. Si katai Mh Chacha kutaka uenyekiti, lakini muhimu ni awe mkweli. Aseme mambo ya hakika kwasababu CHADEMA imejijengea heshima ya kuwa na viongozi wanaozungumza hoja kwa vielelezo. Hali sasa ambapo anajikuta anazungumza mambo yasiyo na hakika alimradi kuusaka uenyekiti sio ustaarabu na ni hatari kwa demokrasia nchini. Ni vema akabainisha sifa zinazomfanya afae kuwa Mwenyekiti badala ya kutafuta kuungwa mkono kwa kubomoa chama kwani inamvunjia heshima.
 
Heshima Kwako Kubwajinga

Chukua tano ndugu yangu kubwajinga yaani umemaliza kabisa sema jamaa wa CHADEMA wanapenda ligi za kitoto watakuja hapa na utetezi wa kipuuzi lakini wenye akili tayari tumeshawagundua.

Na wewe hii ligi unayoiendeleza ni ya kikubwa au kizee?
 
Hivi kweli kisha rudisha kadi au ndio maneno ya watu kumuondoa kabisa ktk Picha..
 
Mkandara,

Leo Mnyika alikuwa TBC, na kati ya aliyoongelea ni pamoja na kuondoka kwa Kafulila, hivyo kuhama kwake ni confirmed. Hata hivyo maelezo ya bwana Mnyika yamethibitisha kitu ambacho nimekuwa na wasiwasi nacho kwa muda mrefu. Kwa mujibu wa Mnyika, Kafulila alipelekwa CHADEMA na Mnyika 2005 baada ya Kafulila kuvutiwa na kampeni za chama pale Ubungo.

Nimekuwa na wasiwasi kwa muda pale mtu anapojiunga na chama leo na kutunukiwa uongozi kesho. Tumeyaona kwa Akwilombe, Guninita, Mtemelwa, Kafulila na wengine, sasa mtu unajiuliza chama hakina wanachama wenye uwezo wa kushika hizo nafasi hadi tusubiri hawa wanaojiunga na chama kufata ulaji?

Ushauri wangu kwa Mnyika na viongozi wote wa CHADEMA ni kuwa makini na wanachama ambao mradi wao ni siasa. Watu ambao nje ya siasa hakuna maisha ndio sumu kwa vyama vyetu.
 
Haya ni sehemu ya aliyoyasema kijana kafulila kwenye press conf.


TAMKO LA DAVID KAFULILA KUHUSU UAMUZI WA CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA) ULIOZUA UTATA NCHINI.

1.0 UTANGULIZI

Kwanza niwashukuru wanahabari kwa kuchag kuja kunisikiliza mimi niliye mdogo sana kimamlaka katika siasa za nchi hii kiasi cha baadhi ya viongozi wenye heshima kuufananisha ubinadamu wangu na sisimizi. Nawashukuru kwakuwa mmethibitisha kuwa waumini wa dhana ya "binadamu wote ni sawa", wanastahili heshima kwa thamani yao.Nawapongezeni kwa hilo kwakuwa hiyo ni moja ya tunu imara ambayo watanzania tulirithishwa na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

2.0 SABABU ZILIZOSABABISHWA KUTENGULIWA KWA MUJIBU WA CHADEMA
Mnafahamu na mmekuwa mkiripoti mwenendo wa siasa ndani ya CHADEMA kuhusu kadhia ya kinachoitwa mgogoro ndani ya CHADEMA kufuatia taarifa za kikao cha siri kilichofanyika Dodoma chini ya uenyekiti wa Freeman Mbowe. Mpaka sasa mengi yamesemwa na viongozi mbalimbali akiwemo, Mwenyekiti wa kwanza na Mwasisi wa CHADEMA-Mzee Edwini Mtei, Mwenyekiti wa pili-Mzee Bob Makani, Mwenyekiti wa sasa Freeman Mbowe, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu, na baadhi ya wajumbe wa Kamati Kuu..

Aidha, mengi pia yamesemwa na wanachama, wafuasi na wadau wa siasa nchini kwa misingi ya siasa na hata dini kuanzia mkoani kwangu Kigoma na Taifa kwa ujumla. Kwa kutambua nafasi yangu kama kijana mwenye ndoto ya kuchangia mabadiliko makubwa katika medani siasa za nchiini, naomba nichukue nafasi hii kueleza zinazoitwa sababu zilizopelekea CHADEMA kufikia uamuzi ilioufikia dhidi yangu.

Sababu inayoelezwa ni mimi kutotambua kikao cha siri kilichoendeshwa na Mwenyekiti Freeman Mbowe Dodoma na baadhi ya viongozi wa chama. Binafsi nilikiri na bado ninakiri kwamba sikufahamu kuhusu kikao hicho kwakuwa hakipo kwa mujibu wa katiba, kanuni, maazimio na hata ratiba ya chama. Na nikiri pia kutotambua kikao hicho kwa msingi wa jukumu la kumvua mtu uanachama wa CHADEMA kama nilivyoulizwa na mwandishi wa habari, kwani kwa mujibu wa katiba, kikao cha kujadili uanachama wa mwanaCHADEMA sio kikao cha siri. Huo ndio ulikuwa msingi wa kwanza wa majibu yangu kwenye kikao cha sekretariet ya Novemba10,2009.

Pamoja na kikao hicho kutotambuliwa kwa mujibu wa katiba, kanuni na hata maazimio ya chama, binafsi sikuwa na fursa yoyote kufahamu kikao hicho kwakuwa; kwanza Mkurugenzi wa Habari na Uenezi ambaye ni Mkuu wangu katika idara kwa makusudi au bahati mbaya hakuniaga na wala kunikaimisha Ofisi kitu ambacho kingenisaidia kujua kwamba kuna kikao Dodoma. Hata aliyekuwa Kaimu Katibu Mkuu wakati huo, Mzee Victor Kimesera alikiri kwenye kikao cha sekretariet ya Novemba10,2009 kwamba hakuwa na taarifa kuhusu kikao hicho kilichohusu wakurugenzi walio chini yake,na kwamba alipewa taarifa tu kwamba kuna wakurugenzi wako nje ya mkoa kwa shughuli za chama Dodoma wakiwa wamesha ondoka…Sio hapo tu, hata Novemba4, 2009 usiku nilipowasiliana na wajumbe wa sekretariet kuwakumbusha kuhusu kikao cha kesho yake (Novemba05, 2009), ambao sehemu yake walikuwa kwenye kikao hicho cha siri, bado sikujulishwa kwamba kuna wajumbe walikuwa nje ya Dar es Salaam wakiendelea na kikao kingine na kwamba wasingeweza kufika kwenye kikao rasmi cha sekretariet siku ya Novemba5,2009..

Nimeona nitoe ufafanuzi huo kwa ajili ya kuweka kumbukumbu sahihi ya nini kilichotokea kwakuwa pamekuwapo upotoshaji wa taarifa kuhusu jambo hili, kiasi cha wengine kuandika kwamba nina kosa la kutoa siri za chama. Napenda kuwajulisha kwamba sijachukuliwa hatua kwa kosa la kutoa siri za chama, bali kwa kilichoitwa kosa la kutotambua kikao cha siri chenye mamlaka ya kumvua mtu uanachama.Kwa mujubu wa katiba kikao cha kumfukuza mtu uanachama hakiwezi kuwa siri kwa mujibu wa katiba na kanuni. Na kwamba mwanachama makini wa chama makini hawezi kufukuzwa kwa vikao visivyo rasmi.

TATIZO LA MSINGI NI NINI CHADEMA ;
Kwakuwa pamekuwapo upotoshaji mkubwa kuhusu suala hili unaofanywa kupitia vyombo mbalimbali vya habari, ninaomba kuwaeleza vijana wenzangu wa CHADEMA ukweli uliopelekea hali hii;

1.AUMUZI WANGU WA KUHOJI KUHUSU UKWELI NDANI YA CHAMA.

Nilimwambia Dr Slaa, na sasa naomba niwaambie wanachadema kwamba tatizo nililoitiwa kuhojiwa halikuwa tatizo husika.Chanzo cha matatizo yote haya ni uamuzi wangu wa kuhoji ili kama chama TUJISAHIHISHE.

A.Nilihoji kuhusu matumizi ya ruzuku .
Mchakato wa kunifukuza makao makuu haukuanza leo. Nakumbuka februari 2009, wakati nilipokuwa nikihoji kuhusu matumizi ya milioni35 za mwezi desemba2008,Mkurugenzi wa Fedha alithubutu kumwambia Katibu Mkuu kwamba "Huyu Kafulila sio mjumbe wa kikao, kwaiyo hapaswi kuwa anahoji kwenye sekretariet, yeye ni mwandishi tu". Hapa nilimhoji Dr Slaa ambaye alikuwa Mwenyekiti wa kikao "Kwanini tangu mwaka 2007 nimeruhusiwa kuingia kwenye kuandika na kuchangia hoja, iweje leo nisiruhusiwe kuchangia hoja?, kwasababu ninahoji masuala ya taarifa za fedha?".

B.Nilihoji kuhusu taratibu za fedha ndani ya chama.
Chuki zaidi iliongezeka baada ya kushinikiza kwenye vikao vya sekretariet kuhusu kuundwa kwa Kamati ya manunuzi badala ya Mkurugenzi wa Fedha kuwa muamuzi katika hatua zote za manunuzi. Hoja hii haikupendwa na ndio sababu pamoja na kuundwa kwa Kamati hiyo ya manunuzi bado masuala yote ya manunuzi yameendelea kufanywa na Mkurugenzi wa Fedha kama zamani. Ikiwa ni takribani miezi nane tangu kamati ya manunuzi iundwe, bado haijawahi kukaa kikao chochote kuamua manunuzi ya chama.

Sio hayo tu, hata mpango wa sasa wa kuchangisha fedha kwa SMS hauna usalama wa fedha hizo kwasababu watia saini(signatories) ni Mwenyekiti Freeman Mbowe na Anthony Komu ambao hawakuteuliwa na kikao chochote kuwa signatories.

C.Mwendelezo wa chuki kabla na baada ya uchaguzi mkuu wa chama.
Katika kikao cha kwanza cha sekretariet baada ya uchaguzi mkuu wa chama, Katibu Mkuu alinifokea na kuniambia "mlango uko wazi" kwa madai kuwa nilishiriki kumfanyia kampeni Zitto Kabwe. Kwaiyo mimi nilitakiwa kuchukuliwa hatua kwa kumpigia kampeni zitto kabwe, lakini akina John Mnyika, John Mrema, Anthony Komu, Benson Kigaila hawakuchukuliwa hatua kwasababu tu walikuwa wakimfanyia Mbowe kampeni.

D.Mbowe na Slaa hawakutaka Kafulila awe kiongozi.
Baada ya kuanza kuhoji kuhusu uhalili wa masuala mbalimbali ya chama, Mbowe na Slaa walihakikisha kwamba David Kafulila hawi kiongozi wa chama. Mwaka jana wakati wa mchakato wa kumpata Mkurugenzi wa vijana, jina la David Kafulila lilipingwa vikali na wapambe wa Mbowe na Slaa. Lakini kwakuwa walijua kwamba nina sifa za kushika nafasi hiyo, kila walipotaka kupeleka majina ya wanaopendekezwa na sekretariet kwenye kamati kuu ili kumpata Mkurugenzi wa vijana, agenda iliahirishwa kwa hofu ya Kafulila kuibuka mshindi. Ni kwa utaratibu huu ajenda ya pendekezo la jina la Mkurugenzi wa vijana iliahirishwa mara tatu, mapaka tukaingia kwenye uchaguzi mkuu wa kwanza wa Baraza la vijana. Ambao nilishinda, lakini kwasababu zilezile za chuki, matokeo hayakutangazwa.

Naomba kutamka rasmi kwa nia njema kabisa , na kwa lengo lile lile nililosema hapo juu, kuanzia sasa mimi David Kafulila napenda kuutaarifu umma kuwa sio mwanachama wa CHADEMA…Na bado ninatafakari kwa mazingira yangu njia mbadala ya kufikia lengo lile lile la kujenga upinzani imara nchini. Najua ni uamuzi mgumu. Najua utapokewa kwa kila sura hapa nchini, Lakini sina mbadala wa uamuzi huu. Ninawaheshimu sana wanachadema, ninawaheshimu sana viongozi wa CHADEMA.

Mwisho, ninaipenda nchi yangu, ninawapenda watanzania. Ninafahamu kwamba Taifa linapita katika kipindi kigumu sana chenye misukosuko ambayo msingi wake ni siasa duni ambazo msingi wake ni upinzani dhaifu kwa upande mmoja na Chama tawala kilicho choka kwa upande wa pili…

Ninaahidi sintowaangusha katika ujenzi wa upinzani imara na hatimaye serikali madhubuti. Na ninawaonya CCM wakome kutumia migogoro katika vyama vya upinzani kujihalalishia utawala, na badala yake wanapaswa kujihalalishia utawala kwa kujenga ustawi wa watanzani. Ninaondoka CHADEMA kwa uchungu mkubwa kwasababu ya lengo thabiti kwamba lazima niitumikie nchi yangu katika harakati za siasa, na. Nitaikumbuka sana CHADEMA kwakuwa nilimwaga damu katika ujenzi wa chama hiki, ninalazimika kukaa pembeni.

Nawatakia kila la heri
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom