David Kafulila ajivua uanachama CHADEMA

David Kafulila ajivua uanachama CHADEMA

Status
Not open for further replies.
Maslahi ya chama always. Serikali inaogopa kumchukulia hatua Rostam kulinda maslahi ya chama. Waziri wa utawala bora anawafyatukia wenzake ili kulinda maslahi ya chama. Maslahi ya chama hayawezi kuwa juu ya maslahi ya taifa. CHADEMA walikuwa sahihi kumvua uongozi Kafulila, ni vema hilo jimbo la Kigoma kusini wakalikosa kuliko kulipata kwa gharama ya kuvuruga chama.
 
MKANDARA wrote:
zote zinaandikwa na watu wenye chuki ya kimakundi, wapo washabiki wa Zitto kina Omar na wapo washabiki wa upande wa pili. Vita hii inafanana kabisa na vita ya Mwakyembe na Mwakalinga

Kaka nitake radhi kaka,

Mimi sio mshabiki wa Zitto na wala sina kundi huko na CHADEMA. Mimi ni rafiki wa Zitto. Urafiki wetu sio wa nafasi za kisiasa ama kijamii, ila ni wa kiitikadi (wote tunaamini katika ujamaa), kimitizamo (wote tunaamini katika constructive criticism/engagement), ki-ajenda (wote tunaamini katika demokrasia makini na sio bora demokrasia), Vision (wote ni waumini wakuu wa muungano wa Afrika – Panafricanism), Misingi (Siasa ni utumishi na sio uheshimiwa) na mengineyo. Sasa huko kwenye upambe kwa kweli itakuwa ni kunitusi. Una haki ya kuona hivyo lakini mimi binafsi sijioni hivyo kamwe na naamini hata Zitto pia.

Pia ni muhimu ukanikumbusha wapi ambapo mimi niliwahi kumchafulia ama kumtuhumu MBOWE ama Dr Slaa zaidi ya kusema kuwa kuna watu ambao wako karibu yake ni wafitini wakubwa kitu ambacho hata wewe unakubaliana nacho katika moja ya michango yako hapa.

Na zaidi nilichowahi kufanya hapa ni kujaribu kuondoa sumu iliyokuwa /inayoendelea kupandwa dhidi ya Zitto na watu humu na kwengineko ambao baadhi yao wanatoka CHADEMA na na wengine kutoka katika makundi mengine ya kisiasa. Sasa mimi kuja kuelezea jinsi nimjuavyo Zitto ikiwa ni tofauti na majungu na fitina hizo ndiyo nimekuwa mbaya ama muendeleza makundi. Ulitaka ninyamaze kimya ili wanajamiiforums na watanzania wengine wajenge mtazamoa/maoni hasi dhidi ya Zitto kwa mujibu wa majungu na fitina za maadui zake na sio utetezi wa marafiki zake?

Na zaidi ndugu yangu huku kunifananisha na wapambe wa hawa WAJASIRIAMALI WA SIASA uliowataja hapo juu ndio tusi kubwa zaidi…

omarilyas
 
Maslahi ya chama always. Maslahi ya chama hayawezi kuwa juu ya maslahi ya taifa. CHADEMA walikuwa sahihi kumvua uongozi Kafulila, ni vema hilo jimbo la Kigoma kusini wakalikosa kuliko kulipata kwa gharama ya kuvuruga chama.

Mimi sikati kulinda nidhamu nadani ya CHAMA lakini nachopingana nacho ni hatua zilizochukuliwa, CHADEMA wana namna nyingi sana namna ya kutengeneza amani ndani ya CHAMA. Wakati tunaongoza migomo Chuoni wakati ule (Zitto akisoma) Tulikuwa tukiwa na ajenda nzito na tumefukuzwa chuo na hoja ya mgomo inapaswa kujadiliwa na Council (tuliwakilishwa na wanafunzi 5 tu) sio kuwa tulikuwa tunakurupuka kuingia kwenye council bila kujipanga kimkakati. Kwanza tulikuwa tunawajua wajumbe wa council kabla ya kikao, pili tunagawana hao wajumbe ambao tunaona ni waelewa na wanaweza kununua hoja yetu, tatu tunatafuta wanafunzi wenye uwezo wa kujenga hoja (sio lazima rais wa serikali ya wanfunzi), nne tunawafuata hao wajumbe wa council na kujadili nao hoja yetu nje ya kikao (hiyo tunaiita Lobbying). Kesho maningia kwenye kikao unapewa dakika 5 kuwakilisha ajenda yako na mwenyekiti, usitegemee kwa dakika tano unaweza kuwashawishi wajumbe wa council wakuelewe. Ndio maana ilikuwa muhimu kuwaona nje ya kikao.

Nacho taka kusema hapa M/kiti wa CHADEMA na viongozi wengine waandamizi wana nafasi kubwa ya kujenga chama bila kuumizana. Wasitegemee kupeana feedback kupitia magazeti. Kwa mfano kama Mh. Mbowe angemwalika Mh. Zitto nyumbani kwake kama rafiki na mdogo wake, wakakaa dinner, wakala wakacheka pamoja as friends alafu wakazungumza habari zao wapi wanatofautiana bila jaziba kunauwezekanao mzuri sana wa kuelewana kuliko kutupiana hayo maneno kupitia JF.

Kama Zitto angempigia simu Dr. Slaa na kumsalimia na kumfahamisha kuwa ana enjoy autumn ya ujerumani sasa, na badaye akafanya appointement ua kuongea kwa kirefu juu ya nini kinaendelea ndani ya chama na kumulewesha sera yake ya kuogopa siasa za kuvizia na bali kucheza kwa siasa za kujipanga, pia kumuelewesah jinsi anavyoikubali falsafa ya Raila Odinga ya kurudi nyuma ukajipanga unapoona kuna kisiki mbele bila shaka wangelimaliza hili. Kama Slaa angemuita Kafulila ni mtendaji wake anamuelewesha jinsi matamshi yake yanavyoweza kuhatarisha uhai wa chama na kusababisha vurugu na kumwmabia ni kwanini wana invest kwake na matumaini watanzania waliyojenga kwa CHADEMA na watendaji wake akiwemo kafulila, hili lingeisha hata sisi akina Kalumekenge tusingeweza kunusa.

Ndio hapo naposema CHADEMA wanapaswa kujua nani anawaongoza kwenye Ukweli. Nani mwenye sera na itikadi ya kukikuza Chama na hatimaye kushika dola. Ndugu zangu tuspokubali ukweli CHADEMA watakuwa ni kama Boat inayoelea tu haizami lakini haiendi mbele wala kurudi nyuma, wawashe injini wasonge mbele.
 
You know what!!
The best deals go early. The early bird gets the worm, By Chacha Wangwe.
 
Kafulila kafukuzwa au kaachia ngazi mwenyewe? Moja linaloonekana hapa, kama ilivyokuwa kwa marehemu Wangwe, tatizo ni lile lile, Mbowe na Ruzuku. Hivi haya hayatatuliki kukiokoa chama?
Kaulimbiu ya siasa za bongo ya" Ukimwaga mboga sisi tutamwaga ugali" sasa pia yatawala vyama vingine nlidhan ni CCM tu kumbe umekua ni upupu poleni CHADEMA
 
Kafulila amefulia!! Ukiama chama bila kuwa na sababu ya kiitikadi siku zote utaitwa mamluki kama walivyo Tambwe Hiza na Dr. Aman Kaborou. Political Migrant.
 
kwani Zanzibar sio Tanzania? ni sawa na mtu aseme CHADEMA ina wabunge wengi kutoka Kilimanjaro na haina mbunge hata mmoja kutoka Zanzibar. Wanapopiga kura bungeni haijalishi ni mbunge wa kutoka Mtwara Corridor au Kanda ya ziwa, Kutoka nyanda za juu kasikazini au nyanda za juu kusini, ni idadi ya wabunge wa bunge la JMT. Kwa hiyo ninachosema hapa ni kuwa Makakati wa kuongeza wabunge bungeni ungekuwa ni mkakati wenye tija kwa CHADEMA na unaotekelezeka.

Mfano kama CHADEMA mwakani wanapata wabunge asilimia 60 na Mh. JK Nashinda kwa asilimia 60 kwenye nafasi ya urais. Je hoja ya kuwa na waziri Mkuu kutoka Chadema haitakuwa na nguvu? Au uundwaji wa serikali ya mseto hautakuwa bayana? Kama unafuatilia sana matamshi ya viongozi wa CHADEMA utaona kabisa ni nani anaona mwenendo wa CHADEMA kwa kipimo sahihi na anaweka mikakati sahihi, ni huyu Mh. Anayekataa siasa za kuvizia na anapenda siasa za kujipanga. Ndio maana kwa hili naungana naye kuwa Inawezekana CHADEMA hawana mkakati wa kushika dola. Hata Mzee mwanakijiji ameshawaonya several times kwenye masuala mbali mbali kuwa haoneshi kama wapo serious kutaka kushika dola kweli.

Sorry iff of point "Elizabeth Gupta - BBA Revolution, Mwaka huu ni wetu pia " Naona signature yako kama ime-expire vile!!!
 
Sorry iff of point "Elizabeth Gupta - BBA Revolution, Mwaka huu ni wetu pia " Naona signature yako kama ime-expire vile!!!

Asante mkuu lakini kwanini unadhani ime-expire? ha ha ha ili niifanyie maboresho
 
😕
Kafulila alikuwa mtumishi wa chadema aliyeajiriwa kwa mujibu wa sheria za kazi na kua analipwa mshahara kila mwezi. So kusitishwa kwa ajira yake hakuwezi kusababisha chadema kuyumba.
 
Maslahi ya chama always. Serikali inaogopa kumchukulia hatua Rostam kulinda maslahi ya chama. Waziri wa utawala bora anawafyatukia wenzake ili kulinda maslahi ya chama. Maslahi ya chama hayawezi kuwa juu ya maslahi ya taifa. CHADEMA walikuwa sahihi kumvua uongozi Kafulila, ni vema hilo jimbo la Kigoma kusini wakalikosa kuliko kulipata kwa gharama ya kuvuruga chama.
hawawezi kulikosa jimbo kwa sababu ya Kafulila!!! Winners never quit and Quiters never win!!!!!!!! Kafulila kwa kuondoka CHADEMA amefulila na hataweza kushinda as he has quited! watch out this space.
 
Mjadala huu pamoja na kujaa uongo na hisia nyingi umenisaidia kujua jambo moja kubwa nalo ni kuwa CHADEMA ni chama kikubwa na ndio maana mtu yeyote anaweza kuwa maarufu na hata kuandikwa na vyombo vya habari na kuuza magazeti yao simply anajitoa ama anajiunga na CHADEMA.

Kuna haja ya watu kuutafuta ukweli kama wanataka kuujua anyway, kuna wengine kazi yao ni kuandika hisia ambazo kimsingi hazipo kabisa , wengine wanaishi kwa maneno ya kuambiwa na ya kutungwa ambayo nayo hayapo.

Kumbukeni kuwa ukweli ni mmoja na haugawanyiki.

Kafulila leo anajadiliwa na kujaza kurasa za JF simply kwa sababu alikuwa CHADEMA,

ukitaka uwe maarufu Tanzania leo wewe jiunge na CHADEMA , kisha tafuta maneno aliyokuwa anasema mtu yeyote aliyejitoa Chadema nawe yuaseme utaandikwa tuu tena front page.

Kumbukeni kuwa CHADEMA ,pamoja na misukosuko yote kiliyopitia bado ni chama imara na kinakua kwa kasi kubwa sana na umaarufu wake unaongezeka.

Kuna kitu kinaitwa intelligence attack-----ukiweza kuishinda hiyo unakuwa umeimarika kama taasisi , sasa CHADEMA kwa muda mrefu tumekuwa tukipitia hatua hiyo na ushindi ni dhahiri.

watu wasonge mbele na wenye mapenzi mema wachangie kwa njia ya sms , watume neno CHADEMA kwenda 15710 na hapo hapo wanaweza kujiunga na chama na kukichangia kwa ajili ya uchaguzi ujao.
 
.....Jambo moja kubwa nalo ni kuwa CHADEMA ni chama kikubwa .
UMEKIPIMA KWA KIGEZO KIPI?
Asante mheshimiwa, Inawezekana mumelewa sifa sasa, kwa hiyo hamfikirii njia mbadala za kusolve matatizo ya CHAMA kwa amani bila kutoa ufa wa kukikosesha nafasi yakuvuna wanachama wengine na pia kupata wabunge wengi bungeni. Umesoma post zangu tatu za nyuma kwenye hii thread? Mumebeba ajenda za watanzania, Mumebeba matumaini yetu, tunawajadili kwa kuwa tunaawamini kuwa ninyi ndio ukombozi wa kweli kujadili kwetu huku ni kutokana na kuwa upepo unaovuma unaonyesha mwelekeo usio kuwa sio. Tunajaribu kuwakumbusha msilewe sifa za kuwa na washabiki wengi, kuweni na mkakati madhubuti wa kuweza kuabadirisha hali ya nchi, nayo ni kuliteka bunge, ndoto inayoweza kutimia kirahisi kabisa (bila hata bajeti ya helkopita,)maana kwa kufanya hivyo mtaibeba ajenda ya watanzania sawa sawa. Umenipata?
 
Asante mheshimiwa, Inawezekana mumelewa sifa sasa, kwa hiyo hamfikirii njia mbadala za kusolve matatizo ya CHAMA kwa amani bila kutoa ufa wa kukikosesha nafasi yakuvuna wanachama wengine na pia kupata wabunge wengi bungeni. Umesoma post zangu tatu za nyuma kwenye hii thread? Mumebeba ajenda za watanzania, Mumebeba matumaini yetu, tunawajadili kwa kuwa tunaawamini kuwa ninyi ndio ukombozi wa kweli kujadili kwetu huku ni kutokana na kuwa upepo unaovuma unaonyesha mwelekeo usio kuwa sio. Tunajaribu kuwakumbusha msilewe sifa za kuwa na washabiki wengi, kuweni na mkakati madhubuti wa kuweza kuabadirisha hali ya nchi, nayo ni kuliteka bunge, ndoto inayoweza kutimia kirahisi kabisa (bila hata bajeti ya helkopita,)maana kwa kufanya hivyo mtaibeba ajenda ya watanzania sawa sawa. Umenipata?

Na ndio maana chama kinaendelea na program zake kama kawaida, tuchangie ili tuweze kuwafikia watanzania ambao hawawezi kuingia kwenye huu mtandao nawe andika neno CHADEMA tuma kwenda 15710 na hii ni mitandao ya voda na zain tuu.
 
Kigezo kilichotumika na hata kwa kuangalia , anayesemwa sana na watu ndio anajulikana hata kama anasemwa kwa ubaya ama uzuri -lengo letu ni kuwatumikia watanzania , na tuliingia humu tukijua kuwa kuna challenge nyingi na dawa sio kuzikimbia ila kuzikabili.
 
Kigezo kilichotumika na hata kwa kuangalia , anayesemwa sana na watu ndio anajulikana hata kama anasemwa kwa ubaya ama uzuri -lengo letu ni kuwatumikia watanzania , na tuliingia humu tukijua kuwa kuna challenge nyingi na dawa sio kuzikimbia ila kuzikabili.

lakini mumnegkuwa mmefanya jambo la maana kama mngefanya mikakati ya msingi kabisa ya kuyatunza majimbo ambayo mlikuwa na nafasi ya kuyachukua. Mathalani Jimbo la kigoma kusini lilikuwa jimbo lenu (kutokana na matamshi ya humu ndani) sasa hivi kushinda mtahitaji kuwekeza nguvu kubwa sana, resources zitakazo tumika huko zingeweza kutusaidia katika maeneo mengine. Hakuna sababu ya kutoa mwanya wa kushindwa kwasababu za habari za kwenye magazeti.

Kama kambi ya vijana wanaogombania nafasi ya Uenyekiti Vijana inaleta shida, ilishindikana vipi kuwakalisha wawili hawa vinara wa mgogoro kutatua hilo? kama lilivyotatuliwa suala la kugombea nafasi ya Uenyekiti taifa, wagombea wote wawili wamekubali hadaharani kuwa yameisha na wapo pamoja, mumeshindwa nini kwa idara ya vijana?

Kama Kafulia alijibu swali la mwandishi vibaya, je haikuwezekana wazee wa chama kukaa naye chemba kumuelimisha na kumfahamisha umuhimu wake kwenye kipindi hiki hasa tunapoelekea uchaguzi. mnawezekana mnaendelea na program zenu ndio, lakini ni program za kuifanya CHADEMA isizame ibaki inaelea na sio kuifanya isonge mbele na safari yake. nadhani tuanze kusahau ndoto ya CHADEMA kushika dola ndani ya Miaka 10 ijayo.
 
hawawezi kulikosa jimbo kwa sababu ya Kafulila!!! Winners never quit and Quiters never win!!!!!!!! Kafulila kwa kuondoka CHADEMA amefulila na hataweza kushinda as he has quited! watch out this space.

EF,
Naomba hapo juu pasomeke.....''Winners never quit and early quiters never win....!''

Kama kuchomoka kwa Kafulia ilikuwa mapema sana, yes hiyo statement inaweza kuhold.....but inawezekana kaondoka wakati muafaka.....then hiyo was the best decision......!
 
UMEKIPIMA KWA KIGEZO KIPI?
Asante mheshimiwa, Inawezekana mumelewa sifa sasa, kwa hiyo hamfikirii njia mbadala za kusolve matatizo ya CHAMA kwa amani bila kutoa ufa wa kukikosesha nafasi yakuvuna wanachama wengine na pia kupata wabunge wengi bungeni. Umesoma post zangu tatu za nyuma kwenye hii thread? Mumebeba ajenda za watanzania, Mumebeba matumaini yetu, tunawajadili kwa kuwa tunaawamini kuwa ninyi ndio ukombozi wa kweli kujadili kwetu huku ni kutokana na kuwa upepo unaovuma unaonyesha mwelekeo usio kuwa sio. Tunajaribu kuwakumbusha msilewe sifa za kuwa na washabiki wengi, kuweni na mkakati madhubuti wa kuweza kuabadirisha hali ya nchi, nayo ni kuliteka bunge, ndoto inayoweza kutimia kirahisi kabisa (bila hata bajeti ya helkopita,)maana kwa kufanya hivyo mtaibeba ajenda ya watanzania sawa sawa. Umenipata?

sifa wapi?
wakati sifa wanajipa wenyewe, sifa gani za namna hiyo?
Kweli mtu mkomavu unaweza sikia watu wakikuongelea na wewe ukatoka kifua mbele na kusema ... Sasa kweli nimeamini mimi ni mtu mhimu sana sana ktk jamii kwa sababu jamii inaniongelea sasa.

Yani kweli mtu unashindwa kutambua kuwa binadamu anaweza ongelewa kutokana na sababu kuu mbili
1. Hasi
2.Chanya
Mfano Joseph Konny wa uganda anaongelewa sana ktk media.Osama bin Raden anaongelewa sana.

Sasa mtu mwenye hekima hawezi kukurupuka from no where na kusema nasikika sana midomoni mwa watu hivyo nina hekima. Jambazi pia naye huongelewa sana kwenye media na kokote kule,

Hivyo mwenye busara hawezi zipima sifa wanazomuongelea yeye mwenyewe na kuzitangaza ktk kadamnasi, subiri watu waje wakupe sifa hizo sio tathimini zako mwenyewe na kama unazo zako kaa nazo moyoni sio kutokana nazo kifua mbele mbele ya kadamnasi.Vinginevyo utaonekana chizi. .
 
Na ndio maana chama kinaendelea na program zake kama kawaida, tuchangie ili tuweze kuwafikia watanzania ambao hawawezi kuingia kwenye huu mtandao nawe andika neno CHADEMA tuma kwenda 15710 na hii ni mitandao ya voda na zain tuu.

Mpaka Kieleweke,
Pesa yetu mnaitaka lakini;
  1. Ushauri wa matumizi hamsikilizi
  2. Uwazi wa matumizi unaolalamikiwa haupo
  3. Wanaosaini Check lazima iwe ni Mbowe na Komu na mara chache Dr.Slaa, why?
Kwa nini msirekebishe haya kabla ya kuja kutuchomoa?
 
Mpaka Kieleweke,

Pesa yetu mnaitaka lakini;
  1. Ushauri wa matumizi hamsikilizi
  2. Uwazi wa matumizi unaolalamikiwa haupo
  3. Wanaosaini Check lazima iwe ni Mbowe na Komu na mara chache Dr.Slaa, why?
Kwa nini msirekebishe haya kabla ya kuja kutuchomoa?

Ulitaka nani asaini cheque?
Wanaosaini si wanasaini kwa vyeo vyao? kama leo yuko Komu ndio mkurugenzi wa fedha ulitaka asaini afisa habari? ama mkurugenzi wa mambo ya nje?

Mbona hujiulizi kwanini Makamba anasaini cheque? sio kwa sababu yeye ni Makamba ila ni cheo chake.

Na anayesema eti Lipumba hasaini cheque ni muongo wa kutupwa na hajui, ukweli ni kuwa anasaini na ipo account moja inaitwa ya uchaguzi ambayo wanaosaini ni Lipumba na Maalim tuu.
 
Ulitaka nani asaini cheque?
Wanaosaini si wanasaini kwa vyeo vyao? kama leo yuko Komu ndio mkurugenzi wa fedha ulitaka asaini afisa habari? ama mkurugenzi wa mambo ya nje?

Mbona hujiulizi kwanini Makamba anasaini cheque? sio kwa sababu yeye ni Makamba ila ni cheo chake.

Na anayesema eti Lipumba hasaini cheque ni muongo wa kutupwa na hajui, ukweli ni kuwa anasaini na ipo account moja inaitwa ya uchaguzi ambayo wanaosaini ni Lipumba na Maalim tuu.

kama ni hivyo nadhani sio sahihi na haivutii machoni mwa watu wa kawaida. Ndio maana inakuwa ngumu kum-separate mwenyekiti Mh. Mbowe na kashfa za Ufisadi wa pesa za ruzuku ndani ya Chama. Mimi nadhani mwenyekiti asingekuwa signatory, kazi ya kusaini abaki nayo Katibu Mkuu (Slaa) (na awe ndio afisa fedha mkuu, yaani mwangalizi) alafu mkurugenzi wa fedha (Komu) na Mtu mwingine mtakavyoona inafaa, mathalani mjumbe mmoja wa kamati ya Fedha (kama ipo). M/kiti kuwa signatory inatoa picha mbaya, hiii sio kampuni mkuu,
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom