Tetesi za kufukuzwa uanachama, bwana Kafulila zilijitokeza toka kwa wana Paparazi siku nyingi tu kabla hata ya yeye mwenyewe kukutana na waandishi wa habari.
Habari zilivuma huku wasomaji wakidai vyanzo vya habari hizo bila mafanikio. Leo hii kuna chanzo maalum ikwa ni yeye mwenyewe akithibitisha kufukuzwa uanachama. Kinachonisikitisha mimi ni pale anapoonyesha kuukubali uamuzi huo kwa shingo upande, pale asemapo: "Ninaondoka CHADEMA kwa uchungu mkubwa kwasababu ya lengo thabiti kwamba lazima niitumikie nchi yangu katika harakati za siasa, na. Nitaikumbuka sana CHADEMA kwakuwa nilimwaga damu katika ujenzi wa chama hiki, ninalazimika kukaa pembeni."
Huwezi kuitumikia nchi yako ipasavyo ukiwa ndani ya chama ambacho kinamapungufu mengi kama aliyoyaeleza Kafulila katika pres conf. Aidha anaendelea kusema kuwa " ".......ninawaheshimu sana viongozi wa CHADEMA." Huwezi hata kidogo ukawaheshimu viongozi wasiojua kazi yao au wanaotaka kuendeleza ufisadi ndani ya CHAMA. Kwa maneno mengine wanakiandaa chama kushika nchi ili kuendeleza ufisadi. Ni kosa kabisa kuwaheshimu viongozi kama hao. Kwanza kazi, ndio baadae heshima. Ukichemsha katika kazi hakuna heshima. Kwa upande mwingine nahisi kama vile Kafulila anajilaumu, kuwa kwanini alianzisha kuhoji utawala katika chama, kwani asingefanya hivyo bado angekuwa anakula kuku.
Katika pres conf yake, kulijaa tuhuma zifuatazo zikiwaendea viongozi wajuu wa CHADEMA wakiwemo, M/Kiti, Freema Mbowe, Dr Slaa n.k
1. Matumizi mabaya ya Ruzuku
2.Taratibu za fedha ndani ya Chama
3.Ufinyu wa Demokrasia (Mbowe vs Zitto/uchaguzi M/Kiti. Uchaguzi M/kiti vijana, yeye mwenyewe akiwa mgombea)
Kifupi yote hayo hapo juu ni mambo ya FWEZA, kazi ipo. Sasa chama kisichokuwa wazi katika mambo ya fedha, tutadiriki vipi kukipa nchi. Matatizo haya niliyajadili siku za nyuma, si mara moja bali mara nyingi tu. Lakini kwa bahati mbaya kama alivyoeleza Kafulila, kuwa wana CHADEMA ni wagumu sana kujirekebisha. NA MBISHI HAFAIDI MPAKA SIKU YA IDD.
Kafulilo ameendelea kwa kutoa ujumbe muhimu sana kama ninavyounukuu hapa chini:
"Taifa linapita katika kipindi kigumu sana chenye misukosuko ambayo msingi wake ni siasa duni ambazo msingi wake ni upinzani dhaifu kwa upande mmoja na Chama tawala kilicho choka kwa upande wa pili"
Yote hayo ni tisa, lakini kumi kama anajihisi kuwa kafulia bila kukusudia basi aombe msamaha kwa CHADEMA na arudi madarakani.