makaveli10
JF-Expert Member
- Mar 27, 2013
- 28,586
- 82,445
Hivi hamuoni matatizo yaliyopo au mnafanya utani?Huduma zetu zinaendelea vyema tafadhali endelea kutufuatilia , yajayo yanafurahisha.
Overload rebound, damping factor in advanceKwahiyo mlifuta utaratibu wa kadi ili mvune hizo hamsini hamsini zinazobaki mikononi kwenu? Utaratibu wa malipo ya kadi ulikuwa rafiki sana na ulipunguza msongamano kwenye vituo vya tiketi..!
mwanza mtahitaji kampuni yenu, kama ilivyo kila mkoa una mamlaka zake za maji, ndivyo itavyokuwa kwa mabasi ya aina hii kila jiji litakuwa na kampuni yake ya usafirishajiAsante kwa kuja.
Ni lini hayo mabasi mtayapeleka Mwanza pia ili wananchi wapate huduma ya usafiri..??
Sababu jiji la Mwanza limekua na tayari limechangamka na mkituletea hizo Bus zikaanzia route ya Kisesa, Igoma, Neshno, Buzuruga, Mabatini, Nata, Pepsi, Mkuyuni, Nyegezi, Buhongwa, Nyashishi hadi Usagara and Return.
ushauri wa bure, uwapo kituoni kama una haraka, na huna mahitaji maalum, ni mzima wa afya na nguvu zako, panda basi lolote linaloekea uelekeo wako, simama usitake siti, ukifika mbele shuka pamda lengine hadi ufike uendakoBASI LA MWENDOKASI (KIMARA _KIVUKONI) LAPITA NA ABIRIA WA KOROGWE HADI KIBAHA
Leo 30/11/2023 basi la mwendokasi limeenda na abiria waliopanda korogwe ili wageuze na basi kutokana na changamoto ya mabasi asubuhi ya leo!
Mabasi yalikuwa yanatoka kimara mwisho yakiwa yamejaa hivyo abiria kusubiri kituoni kwa muda mrefu!!
Basi lilipo fika kimara mwisho licha ya wingi wa abiria kituoni, supervisor aliwataka abiria kushuka na kukata tiketi upya ili waweze kuendelea na safari!
Wengine walioweza kukata tiketi walishuka pamoja na wanafunzi walio kuwa na mitihani iliwabidi wawahi shule!
Wengine tuliobakia tulihitaji kufaulishwa basi jingine bila tiketi mpya au la basi liendelee na safari!
Supervisor akabadili basi route kwenda KIBAHA
Abiria tuliopandia korogwe tukachanganywa na wa KIBAHA !
Njiani tuliomba msaada kwa traffic akampa maelekezo dereva wa basi kuwa akifika mbezi Luis aingie ili supervisor wa mbezi atufaulishe basi la mjini, lakini tulivyo fika mbezi Luis dereva alikaidi hakuingia, akapitiliza!!
Tumefika KIBAHA tukatakiwa tena kukata tiketi ya kurudi mjini kama ilivyo awali na ustaarabu wetu tukamuita askari ili kutatua mzozo, haikuwa rahisi mpaka alivyo kuja kiongozi wa LATRA mkoa wa Pwani kuja kutatua mzozo!!
Ni kweli tumefika makazini kwa kuchelewa (kucheleweshwa) lakini tulikuwa tunasimama kwenye haki, unaweza vipi kukaa dk45 kituoni kusubiri mwendokasi, na magari yanakuja hayasimami???
Wasimamizi walishindwa nini kutoa taarifa kuwa kituo cha korogwe kimejaa watu zije gari tupu kuondoka kadhia???
Supervisor aliona hasara gani sisi abiria wa KOROGWE kupandia basi kimara mwisho??
Ukweli hakuna asiye jua changamoto iliyopo sasa kwenye mwendokasi, lakini hakuna anaye taka kutatua!
Pamoja na uchache wa mabasi kwa sasa lakini bado asubuhi unakuta mabasi yame_paki na abiria wanapata shida!!
Tunalazimika kupanda mwendokasi kwasababu daradara ziliondolewa kwenye route ya mwendokasi, sasa kama mzigo umekuwa mkubwa waruhusu daradara kama awali!
Wasitufanyie kama TTCL walivyo tuachia vumbi hapa ndani
😂😂😂Wasitufanyie kama TTCL walivyo tuachia vumbi hapa ndani
😂😂😂😂Bila support yangu kama mshauri hamtoboi.
Mkafie mbali huko wezi sana nyie mmepewa mabasi 100 ya kuanzia saiz yamekufa yoteView attachment 2625074
DART Tumeanzisha ukurasa huu rasmi wa Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART) kwa lengo la kupata maoni, ushauri , mrejesho na hata malalamiko yanayohusu huduma zetu. Aidha tunawahakikishia watumiaji wa huduma zetu kuwa maoni, ushauri, malalamiko, Pamoja na hoja zenu juu ya huduma zetu yatafanyiwa kazi kwa uharaka na hatua stahiki zitachukuliwa ili kuboresha huduma.
Kwa kupata msaada wa haraka kuhusu huduma zetu unaweza kutupigia simu 0800110147 ni bure. Kuanzia saa 11 alfajiri hadi saa tano na nusu usiku
Pia unaweza kutufuatilia katika tovuti ya www.dart.go.tz na mitandao yetu ya kijamii ya Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka ya FACEBOOK, INSTAGRAM, (X)TWITTER, LINKEDIN, YOUTUBE.
Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka
Anuani
S.L.P 724, 16103
Ubungo Maji, Morogoro Road
Dar es Salaam, Tanzania
Barua pepe: info@dart.go.tz.
#usafiri wa umma nadhifu
#mwendokasi app
😂😂😂Nyakati za asubuhi na jioni watu hujaa Sana vituoni,inakua Haina tofauti na Banda la mbuzi,magari machache,halafu inakuaje hata kutangaza vituo imeshindikana,si wote wenyeji,mpaka tuchungulie kila kituo utadhani twiga anapelekwa mbuga za chato-burigi
Maoni yanapokelewa na yanafanyiwa kazi ni kwa vile tu watanzania wengi hatupendi kuwa na subra wakati huu ambao serikali inatatua changamoto ya uchache wa Mabasi.Mimi naona ni kama kupotezeana mda tu,..hata tutoe maoni hamtobadilika sababu ya urasimu na upigaji mwingi.
Acha vichekesho. Kuna watu wanaochagua magari na uchache huu wa mabasi!? Gari zimajaan mpaka zote zinageuka express!ushauri wa bure, uwapo kituoni kama una haraka, na huna mahitaji maalum, ni mzima wa afya na nguvu zako, panda basi lolote linaloekea uelekeo wako, simama usitake siti, ukifika mbele shuka pamda lengine hadi ufike uendako
mwendokasi ukidharau kupata siti, na kusimama, na kupansa basi lolote mradi lin uelekeo uutakao na upande basi la kituo chako mbele kwa mbele, hutakaa ulalamike unacheleweshwa, kwasababu mabasi yenyewe yanakufikisha haraka uendako, shida ni wingi wa watu uliozidi mabasi
Sent from my TECNO KI5k using JamiiForums mobile app
Kuna. Basi Kimara Kariakoo limewapeleka abiria Muhimbili badala ya GerezqniBASI LA MWENDOKASI (KIMARA _KIVUKONI) LAPITA NA ABIRIA WA KOROGWE HADI KIBAHA
Leo 30/11/2023 basi la mwendokasi limeenda na abiria waliopanda korogwe ili wageuze na basi kutokana na changamoto ya mabasi asubuhi ya leo!
Mabasi yalikuwa yanatoka kimara mwisho yakiwa yamejaa hivyo abiria kusubiri kituoni kwa muda mrefu!!
Basi lilipo fika kimara mwisho licha ya wingi wa abiria kituoni, supervisor aliwataka abiria kushuka na kukata tiketi upya ili waweze kuendelea na safari!
Wengine walioweza kukata tiketi walishuka pamoja na wanafunzi walio kuwa na mitihani iliwabidi wawahi shule!
Wengine tuliobakia tulihitaji kufaulishwa basi jingine bila tiketi mpya au la basi liendelee na safari!
Supervisor akabadili basi route kwenda KIBAHA
Abiria tuliopandia korogwe tukachanganywa na wa KIBAHA !
Njiani tuliomba msaada kwa traffic akampa maelekezo dereva wa basi kuwa akifika mbezi Luis aingie ili supervisor wa mbezi atufaulishe basi la mjini, lakini tulivyo fika mbezi Luis dereva alikaidi hakuingia, akapitiliza!!
Tumefika KIBAHA tukatakiwa tena kukata tiketi ya kurudi mjini kama ilivyo awali na ustaarabu wetu tukamuita askari ili kutatua mzozo, haikuwa rahisi mpaka alivyo kuja kiongozi wa LATRA mkoa wa Pwani kuja kutatua mzozo!!
Ni kweli tumefika makazini kwa kuchelewa (kucheleweshwa) lakini tulikuwa tunasimama kwenye haki, unaweza vipi kukaa dk45 kituoni kusubiri mwendokasi, na magari yanakuja hayasimami???
Wasimamizi walishindwa nini kutoa taarifa kuwa kituo cha korogwe kimejaa watu zije gari tupu kuondoka kadhia???
Supervisor aliona hasara gani sisi abiria wa KOROGWE kupandia basi kimara mwisho??
Ukweli hakuna asiye jua changamoto iliyopo sasa kwenye mwendokasi, lakini hakuna anaye taka kutatua!
Pamoja na uchache wa mabasi kwa sasa lakini bado asubuhi unakuta mabasi yame_paki na abiria wanapata shida!!
Tunalazimika kupanda mwendokasi kwasababu daradara ziliondolewa kwenye route ya mwendokasi, sasa kama mzigo umekuwa mkubwa waruhusu daradara kama awali!
umeongea kitu cha muhimu sana magari ya mbezi ,kibaha yatolewe yaje yasaidie yanayopita mfumo wa BRT maana kuongeza magari imekua anasa
kumtoa udart sababu hakidhi vigezo imekua mtihani.
Bila DART kuongeza mbia mwingne wakurugenzi watendaji watabadilishwa sana maana UDART( kampuni ya msajili wa hazina) amekua boss hawezekani kutoka wanachokifanya DART ni kazi bure
hata ya mbagala akija kupatikana mtoa huduma ndani ya mwaka 2024-2025 naondoka jamiiforum nawambia mods wafute acc yangu
Kweli hata Mimi nilikua nikifarijika sana na matumizi ya kadi ili kupunguza msongamano usio wa lazimaKwahiyo mlifuta utaratibu wa kadi ili mvune hizo hamsini hamsini zinazobaki mikononi kwenu? Utaratibu wa malipo ya kadi ulikuwa rafiki sana na ulipunguza msongamano kwenye vituo vya tiketi..!
Hao askari unawalaumu Bure TU. Ni kama hapo Kimara, gari zikishachelewa sana na abiria kuwa wengi askari waliopo hawatoshi wala hawawezi kudhibiti vurugu mechi gari zinapokuja .Mimi naona changamoto pale Mbezi Louis. Wake askari hawafanyi kazi sawasawa, hawaangalii mistari ya abiria mpaka inavurugika ndo utawaona na pia hawana kauli nzuri ya huduma kwa wateja. Pili naona ni muda muafaka wa kurudisha kadi na Sisi tuwe tunachanja maana tumezidiwa na TERESA wao wana kadi kwenye vivuko vya kigamboni