Dar inawapotezea watu muda

Najua, na ndio maana nimetoa huo mfano kwa hao wanaojipa moyo mikoani ni kuzuuuri sana. Narudia tena, kwa mujibu wa NBS Dar ndio kuna unafuu wa maisha kuliko sehemu yoyote Tz hasa Mwanza ambako utafiti umeonesha wako chini sana.
Achana na tafiti uchwara hizo nimekwambia iweke hapa hiyo tafiti umeshindwa
 
Point
 
Nliwahi kuskia eti dar wanauza hadi miguu ya kuku na utumbo wake wakati huku mkoan utumbo na miguu tunamwekea mbwa ale. Iv ni kweli au story tu....km ni kweli basi jibu limeshapatikana dar maisha magum.
Ndio tena wenyewe hadi wanatengenezea supu eti halafu na maindi ya kuchoma na chumvi eti ndo msosi huo , dah !
 
Kwani huyaoni maghorofa yaliyojazana Dar? Unadhani yote yanamilikiwa na serikali?
 
Kuna jamaa mmoja mtaani nilipokuwa nakaa Dar ni mfanya biashara wa nafaka ananunua mikoani na kuleta Dar alikuwa na maisha ya kawaida tu sasa sijui alisanuka vipi akaingia mkoa akatafuta mashamba tukawa hatumuoni km miaka kadhaa hivi kuja kuibuka huko jamaa ana Fuso yake mwenyewe na mazao anatoa shambani kwake na kupeleka Dar
 
Wewe endelea kuishi kwenye vinyesi halafu ujipe moyo eti iko karibu na mjini so what ? Yani unachoongea wewe ni sawa na kula kinyesi kwenye restraunt , totally illogical

Mi ninachongea ndio uhalisia na nimeishi hapo for ages , so ninajua life styles za watu wa huo mji zaidi ya unavyofikiri , arrogance inawamaliza nyie watu
 
Umenena ila urudi shamba sio mji mwingine . Wanaoshindwa miji yote ya TZ huwa wanaponea Dar . Hapa kuna mipango mingi hata kuuza maji kwa toroli . Ukishindwa Dar nenda tu shamba ! Lima vitunguu saumu kwa wingi na utatoka ili uje Dar na mtaji wako mnene uonyeshwe njia . Unaweza ukamchungulia Barkiressa kwa umbali na atakuvuta mkono
 
Umenena point muhimu sana, ndo maana mi huwa nasema 'Dar is a good place for senior employees and giant entrepreneurs'
 
Kama unaamini sehemu yenye huduma za kijamii za kutosha (maisha bora),

Kama unaamini sehemu yenye chanzo cha nishati cha kutosha (mtandao wa umeme),

Kama unaamini sehemu yenye mtandao mkubwa wa miundombinu na

Kama unaamini sehemu yenye watu wengi (soko) inakupotezea muda,

WEWE NDIO UTAKUWA UNANIPOTEZEA MUDA.
 
Mkuuu we ni mshabiki mtazamaji wa mafaniko ya wenzako. Sasa hayo magari na majumba mazur we binafsi unanufaika vip nayo. We binafsi unamirik nn. Au ndo wafurahia kuona hayo magari na majumba ya bakharesa. Think out the box
Bila shaka hesabu zinakupiga chenga. Mdau kaelezea "chance ya occurance" kwa kutumia hesabu za probability.
 
Mzunguko wa pesa mkoani mdogo sana. Kutoka sio leo wala kesho.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…