Dar inawapotezea watu muda

Dar inawapotezea watu muda

Nimeishi Dar kwa takribani miaka 13,hakuna cha maana nilichokifanya,ila niliporudi mkoani ndani ya mwaka mmoja maisha yalikuwa tofauti kabisa. Niliacha kufikiria mawazo ya muda mfupi mfano nitakula nini kesho,kodi itakuaje na mengineyo ya kipuuzi..

Sasa hivi nawaza itakuaje baada ya mwaka au miaka kumi nitakuwa wapi. Hilo Dar linaishia kwenye maneno tu,maisha ya Dar yanamfanya mtu awe mtumwa,wana wengi wanaogopa kurudi mahome kwao kwa kuhisi watadharaulika.

Acha fikra potovu rudi ubadili namna ya kufikiri,huku mambo yanaenda ukitia nia.
Dar ndiyo iliyokufungua mawazo,bila kukaa Dar usingeona hizo fursa.Ulipata changamoto Dar ukazifanyia kazi huko kwingine
 
Ni kweli mkuu hata mi niling'atuka mapema sana nikarudi mkoa kwa sasa naujutia muda wangu niliopoteza huko dar. kwa sasa namiliki biashara zangu ,mjengo na nawaza kutafuta usafiri tu
Magufuli alishasema mjini watabaki wanaume
 
Ukiegemea kwenye hesabu za probability, uwezekano wa kutoboa ukiwa Dar ni mkubwa kuliko mkoani. Magari na majumba mazuri yako Dar. Mkoani mtu anayetembelea shangingi ni mkuu wa mkoa pekee, whats ur chance of getting one?

Mkuuu we ni mshabiki mtazamaji wa mafaniko ya wenzako. Sasa hayo magari na majumba mazur we binafsi unanufaika vip nayo. We binafsi unamirik nn. Au ndo wafurahia kuona hayo magari na majumba ya bakharesa. Think out the box
 
kuna mda maisha yakiwabana huwa wanauza vitu vyao na kurudi mkoani hii naiona mara nying kwa wenye umri 50+
 
Mkoani kama huna pesa ni vigumu mno kupata pesa, tofauti na dar.

Kuipta 10000 tu mkoa ni kazi mno tofauti ukiwa hapa mjini aiseeh.

Yote kwa yote kila mtu ana jinsi yake aaminiavyo atatoboa. Mjini si kila mtu katoboa kuna wanaokwama na wanaofanikiwa ni bongo yako tu jinsi gni unaichemsha.
 
Mie Dsm naitembeleaga mwisho wa mwaka kutoa shombo la mikoani. Ofcoarse ni mji mzuri kama unakipato cha kueleweka. Lakini kero ya joto, msongamano wa magari na watu, binafsi sipendelei. Nitaendelea kuishi huku huku sitimbi, labda itokee miujiza ya kuishi Mbezi beach upepo unakovuma hahaha
 
Mkoani kama huna pesa ni vigumu mno kupata pesa, tofauti na dar.

Kuipta 10000 tu mkoa ni kazi mno tofauti ukiwa hapa mjini aiseeh.

Yote kwa yote kila mtu ana jinsi yake aaminiavyo atatoboa. Mjini si kila mtu katoboa kuna wanaokwama na wanaofanikiwa ni bongo yako tu jinsi gni unaichemsha.
Kujishughulisha mkuu.Na mtaji si hela mkuu ni wazo ulilo nalo. Wengi ukiwaambia hivi wanasema mbona mawazo wanayo mazuri tu tatizo ni hela. Lkn ukweli ni kwamba mtaji wa kwanza ni wazo lako ila shida inakuja kwa vijana wengi hawataki kuanzia mahali fulani chini kidogo kidogo anataka aamke asubuhi awe km Bakhresa au Mengi. Kwanza hawataki vitu vya kufikirisha anataka kazi km vile anavyofungua Instagram na kufungua page/akaunti ya diamond
 
Kujishughulisha mkuu.Na mtaji si hela mkuu ni wazo ulilo nalo. Wengi ukiwaambia hivi wanasema mbona mawazo wanayo mazuri tu tatizo ni hela. Lkn ukweli ni kwamba mtaji wa kwanza ni wazo lako ila shida inakuja kwa vijana wengi hawataki kuanzia mahali fulani chini kidogo kidogo anataka aamke asubuhi awe km Bakhresa au Mengi. Kwanza hawataki vitu vya kufikirisha anataka kazi km vile anavyofungua Instagram na kufungua page/akaunti ya diamond
tusiandikie mate na wino ungalipo. Hapa tunabadilishana mawazo kwa faida ya wote. Mkuu upo eneo gani hapa TZ na unajishughulisha na nini? Ikiwezekana embu tubadilishane contact tunaweza discuss mengi zaidi
 
mie sielew mtu anaposema maisha bora dar kuliko mkoani!! MKOANI unamaanisha Wapi? taja specific ni mkoa gani?MIKOA inatofautiana, pia upataji wa kipato unategemea na uchacharikaji wako! ila kiufupi kufanikiwa kimaisha daslam ni ngumu sana! maisha ya dar ni kula kusafiri na kulipa kodi, coz muda mwingi watu wanaupoteza kwenye mafoleni kuliko kwenye kufanya kazi! huwez fananisha dar na majiji km London ambayo system zake za usafir ni zaidi ya kawaida! watu wanafanya kazi mbili kwa siku.
 
Aisee! Kila nikienda mkoa huwa nakuta jamaa zangu tuliokuwa lika moja wapo vile vile wamepauka na vumbi tu, Hana kitu chochote cha maana wengine bado wanakula kwao kabisa.
Wakati me tangu nilipokuja dar nime advance Sana hadi kulekebisha mazingira ya home na kuwahudumia wadogo zangu skonga.
Japo nipo gheto lakini Nina asset nzuri za gheto na mipango ya kuanza Ujenzi mdogo mdogo so dar ni sehemu rahisi kwa utafutaji kuliko eneo lolote hapa TZ.
 
Kweli hata Mimi nililigundua hili nikachomoka fasta sasa nipo mkoa na nimeona utofauti mkubwa uliopo
 
Wengi watakuja kukubeza mtoa mada,ila ukweli wengi walio Dar ni wachumia tumbo,kipato chao chote kinaishia kwenye usafiri,na muda wao mwingi wanaupotezea mabarabarani,hawalali vizuri,wala hakuna sehemu ya kutulia na kuwaza au kupumzika bila bugudha,wengi wanalijua hilo,lkn wakiwaza time waliyoipoteza,wanaona noma kurudisha mpira kwa kipa,bora umewasanua,mimi naamini bado hawajachelewa...hasa kwa wale wenye nia ya kubadilisha maisha yao,maana wengi wao washakata tamaa.
Hapo kwenye kutokulala vzr nakuunga mkono, nilikuwa naamka saa 10 alfajir kwenda kazini ili niwahi foleni na nilikuwa narudi home saa 4 usiku na hata ninachokipata sikioni hela yote inaishia kwenye matumizi ya kawaida nijasanuka
 
Issue ni wewe umepoteza muda Dar ukiwa unashangaa shangaa, siyo Dar imekupotezea muda. Sasa ukiwa miji mikubwa kama NY, Tokyo, London au Jo-burg si ndiyo utafutwa kabisa kwenye ramani ya ulimwengu. Jipange kijana.
 
Mkoani kama huna pesa ni vigumu mno kupata pesa, tofauti na dar.

Kuipta 10000 tu mkoa ni kazi mno tofauti ukiwa hapa mjini aiseeh.

Yote kwa yote kila mtu ana jinsi yake aaminiavyo atatoboa. Mjini si kila mtu katoboa kuna wanaokwama na wanaofanikiwa ni bongo yako tu jinsi gni unaichemsha.
Hata huko mkoa kuna watu kibao wanaishi kwenye ufukara mkubwa.
 
Ni kweli mkuu,ila vijana wengi wanapoteza tu muda wao ktk hilo jiji. kwa kweli mm ninaishi nikipambana na umri wangu unaongezeka kila nukta ili angalao nifanye mambo ya maana kabla ya uzee.
Mkoani hamna watu wanaopoteza muda? Kuna miji watu wenye kipato unawahesabia
 
Issue ni wewe umepoteza muda Dar ukiwa unashangaa shangaa, siyo Dar imekupotezea muda. Sasa ukiwa miji mikubwa kama NY, Tokyo, London au Jo-burg si ndiyo utafutwa kabisa kwenye ramani ya ulimwengu. Jipange kijana.
Nimewaambia hivyo hivyo hapo nyuma naona wakawa kimya
 
Back
Top Bottom