Dar inawapotezea watu muda

Dar inawapotezea watu muda

Dar Maisha sio magumu ni ww umejipanga namna gani, mm baada ya kumaliza chuo nilipata Ajira Arusha kwa ujumla sikupenda kufanya kazi tofauti na mikoa hii, Morogoro, Pwani na Dar
Kwa kifupi nimekaa mwaka mmoja akili haifanyi kazi Arusha pesa ipo sana shida matumizi pia nayo ni makubwa mwisho wa siku nimeshindwa hata kununua Kiwanja.....
Sasa nipo na mwaka mmoja Dar nimeshanunua Kiwanja na nimeanzisha
Biashara mkoa.....
Na ujenzi upo mbioni hivyo Dar ni sehemu ya kuja kupata fulsa hata ukitoka dar kurudi mkoa jua hiyo ni Faida ya Dar na utaonekana una kipato kikubwa na watu watakuogopa kumbe ni wa Hali ya kawaida.
 
Yaaani we uliesema raslimali watu nakuonea huruma sana watu wenyewe kina nani wa kuwageuza raslimali siku hizi kila mtu mjanja utampata nani awe fursa kwako
Labda anazungumzia walinzi wa kimasai na ma beki tatu ambao hata wao kuwapata sahii ni changamoto. Dar hamna mtu anaekubali kuwa daraja sahizi.
 
Dar kwa fursa sawa kwa kuishi No. Naamini kungekua kuna usafiri affordable na realible lets say bullet train kutokea Dar to Arusha au usafiri wa ndege usingekua anasa kwamba hata mtu wa kipato cha kati angeweza kuafford watu wengi wasingeishi Dar.
Ila pia ukumbuke kungekuwa na effect ya watu kutoishi Dar. Kama kila mtu angekuwa halali Dar means makazi yangekua mikoani Hio biashara ingefanyikaje?
 
Dar inataka hisabati wenye uwezo wa kukokotoa milinganyo ndio hawa mnaowasifu...wenye uwezo kinyume chake wanakimbia au kupaponda...binadamu yeyote anaetumia akili yake vizuri,alimradi ana siha njema anao uwezo wa kuishi mahali popote ambapo binadamu wengine wanaishi.

Aisee maisha yakubanana kwny "viskwata" vya 15 by 15 nani ataweza mjomba?
 
Pole mkuu, joto kali ni kuanzia December, ila miezi hii na kurudi hadi wa sita hali sio mbaya. Foleni ni sifa ya jiji lolote kubwa si London,si New York....labda ukae huko huko mikoani na vijijini. Ku-relax ni mipangilio yako tu.
Kiongozi unaonekana unaishi upanga, oysterbay au masaki. Hongera sana maana navyoona hizo ndio sehemu ambazo utaamka saa 2 uwahi kazini. Na zina ku favor kuishi lavish lifestyle! Sie wakolomije tunasaga meno tu.
 
Kila Mkoa ni mbaya kama haina dili la Maana la kufanya.kwa hiyo dar kama huna mchongo utaiona mbaya kweli kweli, Maana dar Kila Kitu ni pesa.ila dar ina fursa nyingi na ukiweza kutumia fursa na kuzishinda starehe za dar na vishawishi vyake,unaweza kutoboa.maisha ni popote mradi utapata maslahi Weka kambi
 
Uko jumla jumla sana MKUU.Maisha ni popote akili yako tu.

Mnadanganywa maisha ni popote na unaamini,Mo dewji alikimbia kuishi Manhattan sababu ya maisha ghali sembuse sisi dhoofu bin hali tunaodanganyana maisha ni popote.
 
Kiongozi unaonekana unaishi upanga, oysterbay au masaki. Hongera sana maana navyoona hizo ndio sehemu ambazo utaamka saa 2 uwahi kazini. Na zina ku favor kuishi lavish lifestyle! Sie wakolomije tunasaga meno tu.
Nakaa Kigamboni ofisi Makumbusho, natoka home 0800 nafika Makumbusho 0845/0900.
Sasa hivi napita Central police
 
Doh naona hata hatuelewani umeng'ang'ania dar tu kuna maisha mazuri, mada haikuwa dar na mkoani wapi kuna maisha mazuri, mada inasema dar na mkoani wapi ni rahisi kufanikiwa kimaisha ,
Typical mindset ya watu wa dar , hatukubali kuonekana tumefshindwa hata kidogo especially unapofanya argument na mtu unayedhani ni wakuja !!!
Naona mada ya chini hapo unampinga kwa nguvu zote mdau aliyesema kuwa dar kuna joto ,
Kama wewe unavyong-ang-ania mkoani ndio kuna maisha mazuri. Namjibu yoyote kwa hoja. Na facts sio hisia.
 
Kiongozi unaonekana unaishi upanga, oysterbay au masaki. Hongera sana maana navyoona hizo ndio sehemu ambazo utaamka saa 2 uwahi kazini. Na zina ku favor kuishi lavish lifestyle! Sie wakolomije tunasaga meno tu.

Niliwahi kuishi tabata afu ofisi iko tegeta aisee chamoto nilikipata sana tu,saa 2 asubuhi uwe mzigoni.
 
100% huu ndio ukweli,wengi wanaoishi dar wanakufa na tai shingoni ni vile tu watafanya nini.
Yeah na wanawake wadangaji wanapapenda kwa sababu ya watu wenye vipato vikubwa excess wapo hapo.
Mi sikufichi, Dar kwa hali ya sasa kama huna kipato cha elfu 80 mpaka laki kwa siku utapaona pachungu hasa kama unapenda kuishi comfortably, uendeshe gari na home familia ile vizuri, ule bata bila kusahau ku save kwa ajili ya maendeleo! Gharama za maisha ni kubwa sana.
Comfortability ya maisha ya mtu anaeingiza laki kwa siku Dar ni sawa na ya mtu anaeingiza elfu hamsini kwa siku kwa mikoa mingi tofauti na Dar.
 
Kama wewe unavyong-ang-ania mkoani ndio kuna maisha mazuri. Namjibu yoyote kwa hoja. Na facts sio hisia.
Wapi nimesema mkoani kuna maisha mazuri mkuu?
Nilichosema ni kuwa mkoani ni rahisi kutoka kuliko dar , baas !!! Hakuna sehemu yoyote ambayo nimesema maisha ya dar ni mabaya , Nilichosema ni kuwa najutia muda niliopoteza kuishi dar
Umeamua kunitafrisi unavyotaka wewe na kujenga hoja kutokana na tafsiri yako, Again typical mindset ya sie watu wa dar !
 
lile tu joto kwangu huwa naona kama nipo ahela,yaani joto kulidhibiti unatumia gharama?
 
Yeah na wanawake wadangaji wanapapenda kwa sababu ya watu wenye vipato vikubwa excess wapo hapo.
Mi sikufichi, Dar kwa hali ya sasa kama huna kipato cha elfu 80 mpaka laki kwa siku utapaona pachungu hasa kama unapenda kuishi comfortably, uendeshe gari na home familia ile vizuri, ule bata bila kusahau ku save kwa ajili ya maendeleo! Gharama za maisha ni kubwa sana.
Comfortability ya maisha ya mtu anaeingiza laki kwa siku Dar ni sawa na ya mtu anaeingiza elfu hamsini kwa siku kwa mikoa mingi tofauti na Dar.
Sahihi kabisa ,
 
Mtoa mada alitakiwa aseme baadhi ya mikoa kutoboa ni rahisi kuliko Dsm mana ipo mikoa maisha ghali sana kuliko Dsm hasa ukiwa unafanya kazi rasmi pia ubaguzi na changamoto nyingi ukiingia kwenye uwekezaji kuliko Dsm
 
Back
Top Bottom