Ladslaus Modest
JF-Expert Member
- Jun 27, 2008
- 635
- 27
Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda ndiye Rais wetu mtarajiwa hapo mwaka 2015 baada ya Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete kumaliza muda wake.
Unajua mkuu mimi swali hili najiuliza kila siku,kwani magufuli amemkosea nini kikwete au ni kwa sababu yuko karibu sana na che Nkapa,au inawezekana hayumo katika mtandao!Maana naona kikwete amezamilia kabisa kumpoteza,lakini mie kila siku nasema kipaji hata siku moja akipotei.Si mnaona kampeleka uvuvi kumechangamka,najua ataipa jina wizara ya uvuvi mwisho wa siku watamnyang'anya,lets wait and see.pamoja na mapungufu yake,jamaa anafaa kuwa kiongozi wa watu.
kwa kigezo cha umahiri na ufisadi ni lowassa, kwa kigezo cha umakini na uaminifu ni pinda.
Chagua moja......
Tanzanianjema
Tatizo la Lowasa ni ufisadi but jamaa ni mchapakazi kuliko Pinda
Huyu Pinda namuona kama ROBOT linaloendeshwa kwa remote
Ukweli nimeuona.
Japokuwa Lowasa alituhumiwa kuwa alishiriki sakata la RIchmond, Lowasa ni chapakazi. I can see the difference in short time.
Nachukia mafisadi, lakini Nahisi Lowasa ameshajifunza. Kama ni mtu mwenye utashi na akili atakuwa makini katika maamuzi ya Tenda.
Naomba au Nashauri apewe Unaibu Uwaziri Mkuu. Hii inawezekana. Hata Kipindi kile Mzee Ruksa alimpa Mhe Lyatonga Mrema Unaibu.
Hapo vipi wadau
Lowasa ana tamaa zinazomfanya awe papara.Hajatulia. Mizengo mwoga kuact.
WOTE HAWAFAI!!!!!. WALA HAWATAFAA! WHAT IF PINDA ANAFANYA KAZI BILA VYOMBO VYA HABARI(HATAKI POPULARITY)?. HUYU MWINGINE(LOWASA) NI MUUAJI NA IMETHIBITIKA HIVYO!
WOTE HAWAFAI-PINDA KASHINDWA KUFANYA LOLOTE KUHUSU UFISADI
waberoya
Nadhani ukitaka kuwalinganisha vizuri mawaziri hawa wakuu unatakiwa pia kufuatilia utendaji wa mawaziri wakuu wastaafu.... mfano... Sumaye, Malecela, Msuya, Salim A. Salim. Warioba.
Kwa kifupi sana utendaji wa kuongea na kusikika kwenye vyombo vya habari... nimeuona kwa Lowassa na Malecela.
Utendaji kupitia kwa mawaziri na Goverment system bila kupiga makelele mengi while wengi wakidhani waziri mkuu muhusika hafanyi kazi nimeshuhudia kwa Msuya na Warioba.
Mpaka sasa sina hakika... maana kwa hakika muda ni mfupi sana.... sijajua kama Pinda anafiti vizuri kwenye kundi la Msuya na Warioba au vipi...
Lakini kwa hakika mtoa hoja anatoa ujumbe mzuri tu kwamba Pinda hayuko kwenye kundi la Lowassa na Malecela.
Nilichosema ni kushabihiana kwa utendaji sisemi... Lowassa na Malecela wako sawa, kwa nidhamu zao, au kwa mitizamo yao etc. etc. etc...
Mwisho Magufuli hana sifa za kuwa waziri mkuu mzuri wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania... nawashangaa watu wanaodhani huyu bwana anafaa...