MAN CITY..ngoja niwajadili kidogo.
MAN CITY - UDHAIFU.
1. Man City kama ilivyokuwa Everton ina udhaifu kwenye ulinzi. Mabeki wa kati Vincent Kompany ni beki mzuri lakin mara nyingi huwa anafanya maamuzi ya kukurupuka na kupaniki. Mfano kwenye mechi ya LFC v MCFC alibutua mpira bila kuangalia na ukamkuta Courtinho ambaye aliwamaliza na matokeo yakawa 3-2.{najua mnakumbuka}
Beki mwingine ambaye kocha Manuel Pellegrin anampenda ni Dimichelis..huyu 'babu' amecheza muda mrefu na sasa naona anachoka, hana mbio ni rahisi kumpiga machenga ya hatari{hazard atamchosha sana siku hiyo}
Mabeki wa pembeni: Zabaletta na Clich au Kolarov ni wazuri wakati timu inashambulia..lakini watapata shida sana kutushambulia na kujilinda kwa haraka.
Viungo wa kati: Juzi kwneye mechi yao vs Stoke city..Yaya alichoka sana. .alisumbulia na vijana wa Stoke 'warefu' kama yeye akina Nzonzi..na alipongia Adams ndo kabisa Yaya akatulizwa..
Udhaifu mwingine wa city hawana plan B, ukiwazuia kuingia ndani ya boksi basi wanabaki wanazunguka-zunguka tu hapo nje.
Washambuliaji wao Jovetic na Dzeko ni wazuri wa mipira ya juu..lakini kama watazuiwa hawana namna. .