Ni mtazamo tu
Mechi ya leo haikuwa mbaya, approach ya kocha kwenye mechi ilikuwa ina tija na namuelewa kwa ile lineup aliyoanza nayo kwa sababu margin ilikuwa ndogo sana tofauti ya goli moja ukicheza kidogo tu inabadilika na mlima unakuwa mkubwa zaidi kuupanda ndo maana naona kocha alilenga kuhakikisha matokeo yanabaki at least vile vile kwa hata kipindi cha kwanza chote then ndo aingize zile silaha zake yaani palmer na toto tundu
Sehemu ambayo nakubaliana na mzee wa takataka na moja kwa moja hii itamaanisha napingana kidogo na kocha ni kwa john cena delap, jamaa kiukweli kiwango bado na ule upande ulifaa sana mtu hatari toka mwanzo, japo kwa namna nyengine pengine kumuanzisha estevao ambaye hakuwepo na timu kwa siku kadhaa kutokana na changamoto za kifamilia labda kisaikolojia hakuwa fresh ndo maana hakuweza kuanza naye kule kwa delap ila bado binafsi naamini kule angeanza mtu mwengine huenda angeoffer kitu kizuri zaidi
All in all hatuko mbali sana na nchi ya ahadi, na kocha naamini sio mbaya japo binafsi naendelea kumuasses na so far so good, zile nafasi za enzo alizopaisha zile kama tatu hivi angekutana nazo caicedo zileee anyways blue is the color wanangu upchelsea👊