Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Viwete, wakati una miaka zaidi 10 hujamfunga, na msimu huu ushakutana nae tayari mara 3 na mara 2 umepasuka
Miaka 10?? Unauhakika?? Hao viwete na vigoli vyao hivyo hivyo vya kona unafikiri watabahatisha hivyo hivyo kila siku.
 
Viwete, wakati una miaka zaidi 10 hujamfunga, na msimu huu ushakutana nae tayari mara 3 na mara 2 umepasuka
Agosti, 22 - 2021 nyumbani kwenu tuliwafumua 2-0
Romelu Lukaku and Reece James wakifunga magoli
 
Confidence, wanapokuwa kwenye timu ndogo wanakuwa na confidence kubwa kwa sababu ni timu ndogo, matarajio madogo, presure ndogo
Wanapokuja kwenye litimu lenye matarajio makubwa kama Chelsea panic inawatawala ahat wanapolala usiku, hawalali vizuri. Sisi mashabiki tu ndio tunaidharau Chelsea ila Chelsea ni lijitu likuwa ambalo hawa vijana wadogo wakifika pale kwanza hawaamini kama wamesajiliwa Chelsea
Wengi wa wanaoichukulia poa Chelsea ni walioanza kushabikia miaka ya 2015. Hawajaiona Chelsea ya asali na maziwa
 
THE BLUES ya sasa hivi imexpire
Wewe ni mfano wa mashabiki waliojichokea, hakuna matumaini tena
Hata hivyo vitani sio lazima wote wawe na imani
Tunasonga mbele, bado viraka vichahce sana ili timu ile ya MOU irudi
Wewe unadhani hawa wamiliki kila siku wapo uwanjani wanapenda Chelsea kufungwa fungwa?
Kuna mambo yanayoendelea nyuma ya pazia kwa ukimya sisi hatujui
 
Hiki ndicho tunachokiita sasa akili ya mpira. Huwezi kuipata kutoka kwa kocha, wala kwenye mazoezi uwanjani. Inatoka moja kwa moja kwenye ubongo — hasa kwenye Prefrontal Cortex. Ndiyo sababu Lionel Messi anacheza kwenye kiwango ambacho wengine hawawezi kufikia. Messi ni genius halisi wa soka.

Hawa wachezaji sasa hivi hawapo
Ingekuwani Pedro Neto hapo angesema asante Mungu na kuutumbukiza wavuni kwenye offside position.

 
James hayupo bado

Chelsea vs Leeds United

4-2-3-1

--Joao Pedro--

Estevao --- Enzo (C) --- Palmer

Santos --- Caicedo

Cucurella — Chalobah — Acheampong — Gusto

--Sánchez--

Bench
  1. Sharman‑Lowe
  2. Fofana
  3. Badiashile
  4. Sarr
  5. Hato
  6. Garnacho
  7. Neto
  8. Delap
  9. Guiu
 
Sub anayejitambua kisoka ni Pedro neto tuu, Hao wengine n wachovu wengine n wala mishahara ya bure.
 
Sub anayejitambua kisoka ni Pedro neto tuu, Hao wengine n wachovu wengine n wala mishahara ya bure.
Hapo ndio utajua kuwa Chelsea bado inatakiwa kuingia sokon baada ya kutumia zaidi ya 2bn
Ila Sarr na Fofana bado ni sub nzuri
 
Kwamba sababu ya cucurela kutoka n ipi?
Ila huyu kocha kuna namna afundishwe namna ya kupanga kikosi
 
Kwa ufupi n kwamba Leeds amenufaika Na Sisi Kwa 100%

Amepata points 4, Huku Sisi tukipata point 1 😂
 
Ile tap in aliyokosa Palmer angekuwa ni Jackson kamati ya lugha chafu ingekaa kikao cha dharula
 
Chelsea inaongoza kwenye ligi kwa kufungwa magoli ya kijinga sana
 
Angalia kabisa jinsi Chelsea wanavyokaba — ni vurugu tupu. Ukiwaona makocha wakimuweka Acheampong benchi, hii aina ya ukabaji wa kitoto ndiyo sababu. Gusto ni beki wa hovyo sana; wamgeuze tu awe winga. Halafu Caicedo, Chalobah, Santos… hakuna anayesaidia kukaba.
Ningekuwa hapo uwanjani ningewachapa wote viboko
 
Palmer na Caicedo leo wametuangusha sana kwenye kuondoka na point tatu
Caocedo katoa penalti ya kijinga sana
Palmer kakosa goli ambalo hakupaswa kukosa
 
1768028259534.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom