lembu
JF-Expert Member
- Dec 31, 2009
- 19,696
- 25,910
Mashabiki wamepanga maandm,ano kumpinga Behdad Eghbali na SDsMtakuja kumwelewa Maresca baadaye.
Tatizo halikuwa Maresca kama mnafuatilia habari kwa makini. Tatizo ni hawa wamiliki wa klabu. Lengo lao kuu ni faida ya kifedha tu. Wanataka kocha ambaye atakuza wachezaji kama mifugo ili baadaye wauzwe kwa bei ya juu sokoni.
Behdad Eghbali hasa, hana nia ya kuona timu ikishinda makombe. Kwake, kushinda hakulipi — maana kunahitaji gharama kubwa. Badala yake, anaona faida kununua mchezaji kwa milioni 5 na kumuuza kwa milioni 80.
Kila mechi, Wakurugenzi wa Michezo (SDs) pamoja na wamiliki walikuwa wakiingia dressing room, wakimnyima Maresca uhuru wa kuchagua kikosi chake na kupanga mbinu za ushindi.
Mkielezwa kinachoendelea nyuma ya pazia, mtabadilisha mtazamo wenu kuhusu Maresca. Chuki mliyonayo kwake si ya haki — ni matokeo ya mfumo wa uendeshaji wa klabu unaotanguliza biashara kuliko ushindani wa kweli.
🚨 HABARI ZA HIVI PUNDE:
Inaeleweka kuwa maandamano rasmi yamepangwa… 👇🏻
🚨 Maandamano ya Mashabiki wa Chelsea dhidi ya Behdad Eghbali na Idara ya Usimamizi wa Michezo (Sporting Directorship).
⚽️ Chelsea vs Brentford, 17 Januari
🏟️ Britannia Gate, Stamford Bridge
⏰ Maandamano yanaanza saa 7 mchana
“Wafuasi wa Chelsea wanahimizwa kuungana kwa pamoja katika maandamano ya amani kupinga mfumo na mkakati wa uongozi, hususan Behdad Eghbali na Wakurugenzi wa Michezo wa #CFC.”
⚠️ UKWELI HALISI ⚠️
- Matumizi ya Rekodi – Mkakati wa kusajili vijana pekee umeshindwa kuinua viwango.
- Kutokuwa na Utulivu wa Kikosi – Kikosi kisicho na mizani, kisicho na uzoefu, kinachobadilika kila mara huku makocha wakibebeshwa lawama.
- Mkakati Ulioshindikana – Wingi kupewa kipaumbele kuliko ubora ili kuongeza thamani ya kuuza baadaye kwa faida. Chelsea si Brighton tajiri wala Red Bull.
- Machafuko ya Kiufundi – Uteuzi wa makocha wasiovutia ili wafanane na “mfumo wa ndani na mradi” — mfumo huohuo uliowashindwa Graham Potter, Mauricio Pochettino na Enzo Maresca.