Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Maresca amedhibitisha kuwa ni kocha mzuri na angekuwa mzuri zaidi kama angepewa wachezaji aliowataka. Difensi ni eneo kubwa ambalo Maresca ana ugomvi mkubwa na uongozi. Maeneo yote matatu ya Mabeki, kiungo na ushambuliaji una watoto zaidi na ilihitaji angalau mchezaji mmoja mmoja mzuri mwenye uzoefu angalu kuanzia miaka 25 badala yake analetewa Tosin wa bure soko0ni na mzito kupita maelezo.
Alitaka mawinga wenye kuweza kuwapita mabeki kwenye 1V1 akaletewa Garanacho ambaye hawezi kazi hiyo na Gittens ambaye bvado yuko mbichi kabisa. Alitaka striker aina ya Jackson ila clinical mwnye kuweza kukaa na mpira na kuwaptoka mabeki, Jackosn kaondoka akaletewa Joaoi Pedro, Delap na Marc Guiu. Wote hao hawasogeleo hata kidogo kwenye profile aliyotaka Maresca. Alitaka replacement ya Levi Colwill uongozi ukanyamaza kimya kana kwamba hakuna kinachoendelea. Sasa mabeki hawa wanaachia magoli tu kama malaya. Caicedo nna Enzo wakichoka replacement hakuna. Cole Palmer akiumia tumeletewa Facundo kutoka Brighton. Kama Maresca akiondoka naomba iwe fundisho kwa hawa wamiliki kuwa hakuna kocha mzuri atakayekubaliana na utumbo wao
Hawa wamiliki ni shida lakini pia kocha matatizo mengine kajitakia mwenyewe anafanya rotation za ajabu timu mpaka inakosa kikosi cha kwanza kila mechi anafanya mistake za ajabu
 
Chochote ndo kombe gani mkuu🤠🤠....bwabwaja sana ila tafadhali sana j2 tunaomba sana iwe London is always blue🤠🤠...msituangushe ndugu zetu wazee wa pira singeli
Hahahaha ......... jipambanieni wenyewe jirani, hiyo london always blue tutakutana nayo huko mbele vs Arsenal.
 
wakiendelea hawa hawa Sporting Director tuseme kwamba sisi na mafanikip bye bye.

Sahiv tunaongozwa vibaya mno,Sijawah ona wajinga wanaorudia same mistake kila mda bila na wenyewe kujiangalia.

Wasipobadilika tutaendelea kutia aibu mpka basi
 
Tayari uko 🤣🤣🤣🤣Yani caicedo anaenda kumfukuzisha kazi baba wa watu
skysportsfootball_14041011_014056268.jpg
 
Kibarua cha Enzo Maresca kiko mashakani kufuatia mfululizo wa matokeo mabovu na sintofahamu inayoendelea kati yake, bodi ya uongozi na wamiliki wa klabu. Hali hii imezua maswali makubwa kuhusu mustakabali wake ndani ya timu.

View attachment 3523327
Maresca kosa lake kubwa ni kumuendekeza garasa Caicedo. Hakuna kiungo pale ndio maana tangu asajiliwe hakuna kombe lolote la maana. Ni liability hata aje nani as long as caicedo ndio kiungo timu yenu lazima ipigwe
 
Acha kumtetea kocha ni kizibo, na rotation zake za kipuuzi. Ni kikosi gani anataka tofauti na alichonacho , huwezi ukawa na kikosi chote akina messi.

Hivi unajua City wana wachezaji wa kawaida sana! huyo Doku angekua ndio kanunuliwa chelsea sahizi angekua yupo bench na Estevao wanaprotectiwa, Maresca ana wachezaji wazuri tu ila wale wabovu ndio marafiki zake.

Kocha wa hovyo, pasi nyingii wanapasiana mabeki, kuna moja juzi Estevao alimaindi kashafungua anaita kbs apewe pasi Gusto karudisha kati dah! Niliongea na tv kama ananisikia vile mamaee ila kocha ndio kamfundisha hivyo.
Haya akitoka Maresca unadhani nani mzuri zaidfi yake wa kumridhi
 
Enzo Maresca, ni kocha mzuri hata kama mara nyingine hufanya maamuzi ya kutatanisha kama Alejandro Garnacho. Hakuna kocha asiye na mapungufu; kila mmoja ana dosari zake. Lakini Maresca aliendana na kikosi hiki. Mchanganyiko wa wachezaji waliopo si aina ambayo kila kocha anaweza kuimudu.

Kwa upande mwingine, tatizo kubwa liko kwa wamiliki, kwa sababu hawatamleta kocha bora kuliko Maresca kama wengi wanavyodhani. ataletwa puppete wa kutekelezwa matakwa ya wamiliki tu.

Endapo Maresca ataondoka na wakaanza mchakato mwingine wa kutafuta kocha, wale mnaoshangilia aondoke mtaachwa midomo wazi—kama ilivyotokea Thomas Tuchel alipoondolewa na wakamleta Graham Potter. Sasa wakimfukuza Maresca, au Maresca mwenyewe akiamua kujiuzulu, msishangae wakileta Vítor Pereira au Ange Postecoglou.
 
Enzo Maresca ametofautiana na Behdad Egbhali.
(@alex_crook)

Enzo Maresca hampendi Behdad Eghbali, Mauricio Pochettino hakumpenda Behdad Eghbali, mashabiki hawampendi Behdad Eghbali, na hata Todd Boehly—ambaye ni mmiliki mwenza wa klabu pamoja na Eghbali—hawampendani.

1767229569334.png
 
Leo ndio siku ambayo Enzo Maresca na Chelsea wanaweza kuachana kabisa. Inabashiriwa kuwa Enzo Maresca hatakuwepo kwenye mechi ya Chelsea dhidi ya Mancity siku ya jumanne. Kuna uwezekano Chelsea wakacheza na Man City chini ya uangalizi wa Willy Cabalero Kipa wa zamani wa Man City
 
Ikiwa Maresca ataondoka Chelsea leo, atakuwa na orodha ya kuvutia ya mafanikio katika msimu wake wa kwanza:
1) Kushinda Conference league,
2) Kuinua FIFA CWC na kuifanya Chelsea kuwa timu pekee iliyoshinda mataji yote makubwa
3) Kurudisha timu kwenye Champions league baada ya kuwa nje kwa miaka 3
1767231051954.png
1767231119152.png
 
Je, Chelsea wakiamua kumuajiri Cesc Fàbregas au Roberto De Zerbi, kweli unaona hao ni upgrade ya Enzo Maresca?

1767232013848.png
 
Hiyo record yenu mtakuja kuivunja wenyewe Arse88, sisi city watupige saba tu zinatutosha. Halafu hasira zetu tunajua tutazishushia wapi.
Hivi kuna timu mmeifunga tano kuanzia misimu mitatu nyuma? Na hili swala la kocha wenu kutaka kuondoka unalionaje
 
Yani kocha yoyote atakaye waendekeza caicedo na lavia lazima atimuliwe. Hakuna wachezaji humo.
 
Maresca akiondoka Chelsea kuna timu nkubwa kubwa tu zinamsubiria huko nje.
1767253140453.png
 
Hivi kuna timu mmeifunga tano kuanzia misimu mitatu nyuma? Na hili swala la kocha wenu kutaka kuondoka unalionaje
Unazifunga timu 6 au 5 halafu msimu unatoka mikono mitupu!!, sisi hatunaga uvumilivu na matapeli, kama nyie mnavyomvumilia huyo tapeli wenu Arteta.

Maresca kaja kachukua makombe tunafukuza, atakuja mwingine atachukua,Tapeli wenu yupo tu anawadanganya na phase, hivi mpo phase ya ngapi vile?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom