Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Mpira tunaocheza Siku hizi ni wa kiseng€ , hivi ni nini kilimfanya Maresca kubadilisha style ya kucheza ile tuliyokuwa tunatumia miezi mitatu ya kwanza alipoingia Chelsea ? ,ile style ndio inatufaa .Kucheza kwa kasi pasi fupi na ndefu na kumkimbiza adui mwanzo mwisho huku tukimiliki mpira bila kupoza mashambulizi ...........ile style nakumbuka tulizitandika Timu zote tulizokutana nazo na walipata shida hata kujua wamkabe nani ,hasa viungo na mabeki wa timu pinzani tulizocheza nazo .......Wadau naomba mnipe majibu .........Huyu kichwa andazi maresca ananitia kinyaa Sana sasa hivi
Hata Mimi napenda ile style, ile style ndio inafanya mawinga wetu wawe Bora Zaidi kwasababu mipira inawakuta sana but overall namuona Maresca ni kocha mzuri Kwenye suala la makombe tutachukua hasa UEFA, Carabao na FA kwa sababu anajua kucheza dhidi ya team kubwa ila kwa EPL inabidi uongozi umsapoti kwenye usajili haswa wa experience players wakifanya hivyo tutakuwa tupo vizuri
 
Kwenye hili siwezi kumlaumu kocha wachezaji ndio wamezingua walikuwa wanacheza kivivu, Kasi ndogo, hawakabi na second balls zilikuwa zinawashinda kipindi cha Kwanza tulizidiwa sio kwasababu ya kimbinu wachezaji wenyewe walisinzia
Na hii kitu ndo huwa inatugharimu sana mara nyingi, unakuta mechi ya kuchukua point tatu kabisa tunaanza kwa mwendo wa konokono wanatuotea magoli ya faster faster halafu wanarudi kukaa nyuma wote na mechi ndo inakuwa imeisha
 
Na hii kitu ndo huwa inatugharimu sana mara nyingi, unakuta mechi ya kuchukua point tatu kabisa tunaanza kwa mwendo wa konokono wanatuotea magoli ya faster faster halafu wanarudi kukaa nyuma wote na mechi ndo inakuwa imeisha
Na ndio maana kocha anataka wachezqji wazoefu
 
Mkuu City Hana uwezo wa kumfunga Chelsea subiri uone
Mara ya mwisho mnamfunga City ni 2021 kwenye fainali ya CL.

Screenshot_20251221-092453.png
 
Majeruhi ya Levi Colwill na Cole Palmer yameathiri kwa kiwango kikubwa mwenendo wa uchezaji wa Chelsea.

Kwa sasa tunalazimika kutegemea kwa muda mrefu pairing ya Chalobah na Tosin ili kupata pointi 3, jambo ambalo si rahisi wala la uhakika.

Vilevile, kukosekana kwa Nicolas Jackson kumeacha pengo kubwa kwenye safu ya ushambuliaji. Licha ya kukosa nafasi mara kadhaa, Jackson alikuwa analeta uhai mkubwa mbele kupitia link play, kasi ya kuserereka na mpira (sprinting), pressing, na positioning nzuri. Sifa hizi zote washambuliaji waliopo sasa hawawezi kuzitekeleza kwa kiwango hicho.

João Pedro ni mchezaji makini zaidi mbele ya goli ukilinganisha na Jackson, lakini hawezi kupress, ku-link play, wala kusukuma mashambulizi kwa kasi akiwa na mpira. Hali ni hiyo hiyo pia kwa Liam Delap na Marc Guiu.
 
Kiukweli mi naona City gari limewaka. Niamini mimi
City hii inamtegemea sana Halland City ile ninayoijua huwa ilikuwa hategemei kabisa striker walikuwa na wingers wafungaji sio hii ya Sasa ni mafuta yenu tu kuanza kushika ndio imefanya mtofautiane kwa point ndogo
 
Leo na Aston Villa tuomba kipara asijekua ameamka na bipolar akachanganya mambo. Unai hatoona haya kutuadhibu darajani
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom