Pochettino ni mfahidhina sana kubadilisha mbinu au muundo kumzuia mpinzani asidhuru, imekuwa kila wakati, "twende tukajaribu kuwashinda".
Arteta kwa upande mwingine hatajali kucheza kizuizi cha kati au cha chini kushinda mechi. Kushinda mechi hujenga imani na imani. Ikiwa unataka wachezaji wakue haraka na kuamini, unahitaji kuanza kushinda michezo.
Mfano Saka alizuiuliwa vizuri na Cucurella kipindi cha pili akaja na mbinu ya kumtumia White kumuoverload Cucurella na akafanikiwa kuweka kimiani mabao mawili.
Unawezaje kwenda Arsenal na wachezaji wetu mbaya zaidi wa CB wawiuli ndio wanaoongoza kuruhusu magoli mengi. Mfano Badiashile tangu arudi majeruhi amekuwa akiongoza kupoteza mipira maeneo ya hatari? Unaenda Emirate kuwachezesha mawinga wabaya zaidi wa ulinzi kama Madueke na Mudryk? Ikiwa mawinga hawatoshelezi, ongeza viungo na utumie diamond au 3 au mfumo unaofanana na huo? kuna 343, 352, nk. Angalau fanya kitu kumzuia mpinzani wako asikudhuru kama huwezi kumshambulia.
Moja ya masuala yetu makubwa msimu huu, ni wachezaji wa kushambulia kutorudi haraka kuweka mfumo wa ulinzi, hasa mawinga, huwa ni wazembe na wavivu na kocha anaona tu hayo sawa.
Ili kuepusha hilo, kwa nini usitumie muundo ambao utaruhusu wachezaji kudumisha nafasi zao kanda au kupata yadi chache ili kurudi katika umbo la ulinzi?
Kwa jinsi tulivyopata majeraha na timu ni changa, Pochettino amekuwa mkaidi sana kutafuta muundo bora ambao utaficha mapungufu ya wachezaji wake.
Na tukutoa amelezo yote haya kuna watu wanaelekeza shutuma kwa wachezaji ambao ni kama kondoo wanahitaji kupangwa tu
Au kama askari vitani wanahitaji kupangwa na kupewa maagizo tu
Gamu ya Arsenal an Chelsea kuanzia dk ya 30 Chelsea waliwadhibiti Arsenal na almanusura bao lile kurudishwa. Arsenal walbaki wanajilinda tu lakini cha ajabu baada ya mapumziko kocha alienda akawapa maagizo mapya, kila kitu ikavurugika, balance ya timu ikapotea, mabao yakaanza kumiminika na hali hii ya Pochettino kutoa maelekezo mabovu baada ya mapumziko imekuwa ni desturi inayojirudia kila wiki na hata ajirekebishi