Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Mnakumbuka niliwambia hii kitu? Kiufupi hatuna Kocha, Poch ni kilaza sana. Huyo jamaa ni wakufukuza hafai kuwa Chelsea.
Tumeshinda ki bahati tu, hamna timu pale. Caisedo na Enzo hawa ni viungo gani wanatoa pasi mkaa, pasi hazifiki kwa mlengwa, inasikitisha sana viungo wa bei kubwa kiasi kile ata kupiga pasi ifike mahala husika hawawezi. Mabeki wetu ni hamna kitu kabisa, kocha ndio kilaza kabisa hamna mtu mle. Kiufupi ukimtoa Palmer na Petrovic wengine wote ni matakataka, huo ndio ukweli mchungu.
 
Mnakumbuka niliwambia hii kitu? Kiufupi hatuna Kocha, Poch ni kilaza sana. Huyo jamaa ni wakufukuza hafai kuwa Chelsea.
Wataalamu wa mpira wakija hapa watakuambia ni wachezaji
Enzo chini ya kilaza Potter alikuwa hot
Caicedo chini ya Dizerbi alikuwa hot
Hawa wachezaji ni kama watoto, usipowasukuma wacheze vizuri hawatacheza
PEP sio tu amekaa pale na popcorn halafu akina Foden wakacheza vizuri, wanasukumwa ile mbaya na saa nyingine wanatukanwa
Arteta wale watoto akina Bukaya Saka wanatukanwa dressing room ile mbaya wakati ule wanacheza hovyo, ona sasa walivyobadilika
Huyu wa kwetu anawadekeza sana hawa watoto halafu na wachezaji na eti wanasema wanampenda. wameshamfanya mjomba au babu
Tuna kazi sana na hii timu kwa sababu hata wamiliki wameshabadilishwa na mahubiri ya Poche kuwa mradi unahitaji mchakato wa muda mrefu
 
Huyu Dean naye hadi juzi alikuwa ni mpambe wa kumfia Pochettino, lakini baada ya mechi amesalimu amri
Kwa Pochettino kila anayejiita ni mpenzi wa Chelsea na kumsupport Pochettino atatoka humo, bado kidogo wote tutaongea lugha moja.
1712558956577.png
 
Kwa hali ya kawaida tulipaswa kuchekwa sare ya 2-2 na team ya mwisho epl lakini wapinzani wanasikitika tulipofikia ,hii chelsea ya kinyonge kuiona hata kabla ya Roman the Don him self
 
Chelsea ni ya pili kwa kutengeneza nafasi baada ya city hadi sasa kwenye ligi. lakini haipo hata kwenye top 10 kwenye kupiga mashuti. Tuna walemavu kule mbele, hili ni moja ya mambo Pochettino ameshidwa kulifanyia kazi

1712565724884.png


1712565823962.png
 
Jamie Redknapp: "Chelsea ingekuwa kwenye vita vya kushuka daraja kama si Cole Palmer."
 
Wanadhani kuwa mrefu sijui ndio kigezo.

Tulikuwa na Ivanovic/Carvalho walikuwa wafupi ila lilipokuja swala la mipira ya juu ulioma kabisa jinsi walivyokuwa wanajilinda

Waangalie Arsenal Gabriel anaurefu sawa na Disasi
Badiashile kawazidi urefu Gabriel na Saliba wote kwa pamoja
Kiwior almost anataka kulingana na Silva na Colwill

Waangalie wakina Marquinho ni wafupi ila mipira ya juu angalia wanavyodefend

Mkubal Poch ameshindwa isuka defenc yetu
Issue ya urefu na ufupi kwenye mpira ni siasa tu,urefu hauchezi mpira tunaangalia skills. Mfano upewe konate na silva halafu umchague konate? Utakuwa hujitambui Chelsea imeishiwa mbinu tukubali tu
 
pochettino msimu ujao.. anapaswa kupewa mechi 10 tu za mwanzo kuweza kujua kama kuna progress yoyote hasa kwenye patterns of play.
 
Jana Disasi alikuwa busy kurudisha mipira kwa kipa au silva, very bussy, RB mbovu kuwahi kutokea kwenye jezi ya Chelsea. Akicheza CB anakuwa afadhali kidogo. Pochettino yeye anaona hayo ni sawa kabisa, tukimtukana kuna wapenzi wake hapa wanakuja kumtetea

Jana Cole Palmer alikasirishwa mara kwa mara na Axel Disasi kwa kutopeleka mipira mbele vya kutosha na alimzomea mara nyingi kuwa katika nafasi nzuri ya kutoa nafasi kwa washambuliaji.
 
Mauricio Pochettino alisema kuwa falsafa, miundo, mtindo wa uchezaji, iwe unakaba au kutawala mchezo sio muhimu.

Lakini wachezaji wanahitaji kuhisi unawatakia mema, ameelezea kwa nini hakuna mfumo wa kucheza Chelsea, hakuna kufundisha.

Kukimbia tu na msaada wa kihisia

English:
Mauricio Pochettino said that philosophy, formations, style of play, whether you defend or dominate a game isn't important.

But players need to feel you want the best for them, explains why there's no system at Chelsea, there's no coaching. Just running and emotional support.

Maoni yangu

Inawezekana hii clip ujumbe wake haukutimia kwa sababu imekatwa ila kama kasema falsafa, play pattern, formation sio muhimu basi ana wazimu.
Ndio maana wachezaji wanacheza watakavyo kama watoto wa mtaani
Hakuna chochote kuhusu mbinu, maelekezo, muundo. Ni wachezaji wanaokimbia tu. Poch lazima aondoke.

 
Chelsea wameamua kuwaibia wapinzani wao na kumsajili nyota wa Athletic Bilbao Nico Williams.

{Football Insider}

1712601046265.png
 
Makocha hutengeneza au kuharibu timu.

Frank Lampard alisema wachezaji wa Chelsea (kabla ya Tuchel) hawakuwa tayari kushindania makombe. Ilikuwa ni "Managerial failure".

Miezi mitano baadaye, Thomas Tuchel alisema ataijenga timu ambayo kila mpinzani hatataka kukutana nayo. Aliwajen ga kisaikolojia wachezaji wale wale aliokuwa nao Frank Lampard na kuwafanya kuwa washindi wakuu wa Ligi ya Mabingwa. Ulaya. Ilikuwa ni "managerial success".

Anachofanya Pochettino sasa ni "Managerial Failure" kwa kuwaita kila siku vijana hawako tayari kushinndana, bado ni wachanga, hawana uzoefu kwenye ligi, hawawezi kucheza mara mbili kwa wiki katika ligi iliyosongamana, mradi huyu ni mchakato unaoweza kuchukua miaka mitatu hadi mitano. Too much negativity kwenye media na press conference zake. Hizi negativity zikiwa nyingi na za mara kwa mara kama propaganda ya siasa au vita inawafanya wachezaji wafanane na hizo propaganda zilizojaa negativity na hivyo kushindwa kucheza vizuri kama ambavyo wangeweza kucheza wakiwa chini ya kocha kama Tuchel
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom