Mauricio Pochettino adai kuwa kikosi cha vijana cha Chelsea hakijazoea ratiba ya EPL iliyosongamana.
"Ukiwa na umri wa miaka 52, unatambua kwa haraka kama timu iko tayari kushindana au la. Labda kundi hili halijakomaa vya kutosha kushindana katika michezo kila baada ya siku tatu...
"Ni timu mpya na bado tunajifunza kuhusu wasifu wao. Mchakato siku zote huchukua muda, sio jambo la ajabu ni mradi, mchakato wa miaka mitatu au mitano wa kujenga timu...
"Tuko katika nusu fainali ya Kombe la FA. Hatukuwa katika nafasi nzuri mwanzoni, lakini hiyo ni kawaida. Tunatakiwa kukubali sasa na kufanya kazi kujaribu kurekebisha matatizo yetu."
Juzi alisema ni majeruhi, leo timu haiwezi kucheza kila baada ya siku 3, kesho sijui atakuja na sababu ipi
Mlalamikaji sana huyu kocha, hiyo inatosha kujua picha yake halisi ya moyoni. Hayuko tayari kupambana bali kutoa visingizio tu
Hivi makocha wengine wanalalamika hivi kweli?