Nadhani Palmer amefanya kitu kizuri mpaka kuaminiwa kuwa mpiga penalty. Hivyo sitatoa penalties zake. Kuna positions Palmer anajikuta yupo ambazo Saka kwa Arsenal haziingii hizo nafasi kwa sana.
Kuna lile goli la juzi juzi hapo ambalo Palmer alifunga baada ya kupenyezewa pasi ya kisigino na Sterling akiwa ana turn. Palmer aliingia ndani ya box maeneo ya katikati hivi akafunga bottom right corner.
Kumkuta Saka katika position ya hivyo huwa si rahisi maana opponents wanalazimisha tucheze kwa kutanua uwanja so kama siyo kwa kubadilishana na Martinelli, Saka huwa yuko pembeni zaidi upande wa kulia na wakimuacha aingie ndani ndipo anawaadhibu wapinzani.
Labda nakosea, ila naona Palmer ana uhuru zaidi kufanya roaming pale mbele akiwa Chelsea kuliko Saka akiwa Arsenal.