Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Tunaweza kuwa tunawakat mgumu kumpata kocha ajaye maana vilabu vingi vikubwa nao wanataka kocha.
Liverpool
Bayern
Barcelona

Tunakaz kubwa sana kumshawishi kocha ajae kama tukimtimua yule Tapeli wa Argentina
Na mradi wetu unaogopwa zaidi kuliko hizo zingine, Kocha ajaye kama Pochettino ataachishwa kazi msimu wa kiangazi atakuwa na changamoto sana kwenye hii klabu kwa sababu ya wachezaji wengi wachanga, pili demand ya fanbase ya Chelsea ni kubwa na yenye kumuweka kwenye wakati mgumu kila kocha atakayejaribu kuchukua hii kandarasi ya kuirudisha meli iliyozama mahali pake
Kitu ambacho nadhani itasaidia ni kwamba hadi wakati huu hawa wamiliki wamejifunza, nasikia pia hata walifikia sehemu hawaelewani kwa sababu ya jinsi mradi unavyoendeshwa
Kocha atakayefanikiwa Chelsea ni lazima kwanza awe ni
  1. kocha wa kaliba za juu na mwenye mbinu nyingi za kushinda makombe.
  2. Pia awe na uzoefu wa kuwanoa vijana wadogo kama akina Mudryk, Madueke, na wengine ambao wanaonyesha ishara ya kuja kuwa wachezaji wakubwa kule mbeleni.
  3. Pia kocha ajaye aweze kujua pancha za hii timu ziko wapi na awe na ujasiri wa kuwataka viongozi na wamiliki wasaidie kwenye kuziba hizo pancha
  4. Pia kocha ajaye apewe madaraka zaidi juu ya usajili management na uuzwaji wa wachezaji
 
Mauricio Pochettino anaomba subira kwa mashabiki jamani.

Anasema "anajiamini" wamiliki wanamuunga mkono.

Anaamini kufuzu kwa ligi za Uropa sio muhimu kuweza kulinda kibarua chake.

Na kuwataka mashabiki wa Chelsea kuukubali na kuuzoea "ukweli".

Pochettino 'confident' of long-term Chelsea future as pressure mounts #CFC
1709092195365.png
 
Mkurugenzi Mtendaji wa Shakhtar Donetsk Serhiy Palkin kuhusu Mudryk:

"Naweza kukuambia kwamba, kwangu, Mudryk ndiye mchezaji mwenye vipaji na wa kipekee zaidi duniani. Ninaamini kwamba ili kupata kiwango cha juu kutoka kwa Mudryk, kama wanavyotarajia, unahitaji kuwekeza kwake. Na uwekezaji huu sio pesa.

Uwekezaji ni muda na makocha wa kumfundisha na kuwasiliana naye na kufanya kazi naye kwa karibu. Kwa sababu yeye ni mvulana mdogo, alibadili mazingira kutoka ligi ya Ukraine kwenda Ligi Kuu ya Uingereza. Ni ulimwengu tofauti kabisa, wenye viwango tofauti kabisa kwenye mpira wa miguu ambao ni tofauti kabisa. Ninaamini kwamba ikiwa timu ya makocha itajitolea kwa muda fulani kwake, atarudi mara tatu, nne au tano zaidi.

Watu wanasema Pochettino kamtengeneza Dele Ali na Kane, huu ni uongo mtupu
Kipimio cha kwamba Pochettino anaweza kudevelop vijana wadogo kuja kuwa malegend ni kwa huyu Mudryk
Pochettino akishaona mtu haingii kwenye anga zake anamtelekeza
Tuchukue case ya Maatsen alivyomuacha na kumlazimisha Colwill acheze nafasi yake
Ninawasiwasi na akina Chukwu, Lavia, Daivid, Angelo, na wengine. Kuna kati yao watakaoharibiwa kabisa na approach za Poche kwa hao vijana wadogo
Mungu asaidie tupate kocha anayefit kwenye anga za hao vijana

1709099383701.png
 
TODDY - Chelsea fc ni Project UCHWARA na KITAPELI.

1. Wakurugenzi wa ovyo
2. Kocha kilaza
3. Wachezaji mazagazaga

"BLUE BILLION POUND BOTTLE JOB"
Hii sala yako ya Bwana asubuhi mchana na jioni imekosewa sana
Wachezaji waliopo ni wazuri sana, tunza haya maoni uje baada ya kocha kubadilishwa na akaletwa anayewajulia hao vijana
 
Pochettino hawekezi chochote kuwaendeleza watoto hao. Alimchanganya Maatsen mpaka akaondoka. Sasa anafanya vivyo hivyo kwa Mudryk, Daivid, Casadei, Alfie. Nashangaa atakabiliana vipi na wanaoingia kama Angelo, Paez na wengineo. Hata Nkunku hatendewi ipasavyo
 
Hans Flick yupo free , why tuzimchukue yule tactician ?

Sent from my Nokia 6.2 using JamiiForums mobile app
Hio timu yenu sio kila kocha atafaa, tafuteni kocha yoyote mwenye rasta mtakuja kunishukuru baadae.
Mkimpata kocha wa Cameron Rigobert Song matatizo yenu yote mtakuwa mmemaliza, timu imejaa marastafarians halafu mnaleta kocha anaekula nyama halafu hajawahi kuvuta hata banghe hio ni akili au matope?
1709110667792.jpg
 
Hio timu yenu sio kila kocha atafaa, tafuteni kocha yoyote mwenye rasta mtakuja kunishukuru baadae.
Mkimpata kocha wa Cameron Rigobert Song matatizo yenu yote mtakuwa mmemaliza, timu imejaa marastafarians halafu mnaleta kocha anaekula nyama halafu hajawahi kuvuta hata banghe hio ni akili au matope? View attachment 2919028
Hahahaha umenichekesha sana.

Tunataka tubadilishe timu iwe ya basketball
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom