Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Vipi kuhusu hili au ndio mtasema wachezaji wabovu

Kila week tunafunga magoal yale yale
IMG_1776.jpg
 
POchetino lazima atafukuzwa tu ni swala la muda. Ila tukubali tukatae baadhi ya wachezaji nao ni janga

IMG_1777.jpg



Tuchel kitu cha kwanza kufika alijua madhaif yetu ni yapi akarudi 3 at the back na tukawa solid, sisemi turudi 3 atb but poch anaona mapungufu yetu ni yapi anashindwa nini kuweka mfumo utakayoyaficha

Kila game tunaruhus magoal yale yale
 
Kocha kashindwa tengeneza mfumo wa kuwasuit hawa wachezaji .

Atapokuja kocha wakujielewa ndio mtaelewa hichi kitu.

Kama system ya team haiko vizuri hakuna mchezaji atakaeonekana mzuri
Siku zote huwa haunielewi halafu ni kama unahisi tunashindana katika hili. Wewe kuna siku uliwahi kusema waxhezaji wanafunga magoli kwa juhudi zao wenyewe. Sasa hivi utalalamikiwa mfumo wa uchezaji haueleweki, Poch ni tatizo, na blah blah nyingine nyingi.

Tuanzie kwa Antonio Conte, Maurisio Sarri, Lampard, Tuchel na sasa tuna Poch. Katika wote hao kila mmoja ana kocha wake ambaye anasema hapa tulikua na jembe kweli. Lakini mwisho wa siku nini kilitokea? Nachotaka kumaanisha ni kwamba haijalishi kocha ana deficience gani kwenye kazi yake hata awe mzuri au mbaya vipi atafukuzwa tu kukitokea defficience yoyote.

SImtetei Poch kama wengi mnavyo ni address humu. Nasimama na Chelsea yangu nje ya Poch tuna wachezaji wabovu ambao ni average, tuko hapa tulipo kwa sababu ya fukuza fukuza ya makocha, leo hii ukiulizwa style ya uchezaji wetu ni ipi huwezi elewa. Atleast Conte, Mourunho na Ancelotti walieleweka na ndio waliotupa EPL tittle.
 
6 months now na tunaplay once a week. Ila ukiuliza pattern yetu ya uchezaji ni ipi hakuna yeyote anaeweza jibu hilo swali
Na inconsistency ya matokeo inatia mashaka , why hakuna muendelezo mzuri wa matokeo ?
Patern ya uchezaji hamna pia
 
Wewe ndie umesema

Caicedo sio attacking midfielder kama unajua soka
Enzo ni Cm
Caicedo ni CM
Wote kwa pamoja ni box to box midfielders
Roles ya Enzo anakuwa mzuri akicheza deep na Caicedo akicheza advanced

Kumbuka Kante alipokuja Chelsea alikuwa akicheza box to box lakini kwenye role ya DM zaidi hadi akawa anajulikana kama DM
Alipokuja Sarri ili amuweke mtoto wake Jorgginho kama regista alimpeleka Kante mbele, hapo haikuwa na maana kwa Kante ni attacking midfielder bali alipewa advance role ambayo baadaye alikuja kuimudu sana ndipo hata makocha waliokuja baada ya Sarri waliendelea kumchezesha advanced role

The same to Caicedo
Wewe unahisi sisi hatujui profile ya Caicedo kama ni defensive mid?

Kwahiyo unataka kusema wakati Liverpool wanataka kumsajili Caicedo kama mbadala wa Fabinho kwenye DM, walikua hawana akili?

Wewe unahisi kwanini mpaka sasa Klopp hana defensive mid?
 
POchetino lazima atafukuzwa tu ni swala la muda. Ila tukubali tukatae baadhi ya wachezaji nao ni janga
Hata kama wako wachezaji wabovu ila wengi wao wamefanywa kuwa hivyo na Pochettino
Nilidanganyika kuamini kuwa Rudiger ni CB mbovu wakati wa Lampard ila alipoikuja TT ndipo nikajua kumbe ubovu wa mchezaji unasababishwa na kocha.
Ndio maana sasa huwezi kuniaminisha kuwa hawa wachezaji ni wabovu kushindwa kupata hata nafasi ya 7. Kwa sababu ya kukosa uzoefu wanaweza wasiweze kugombea ubingwa au kuingia top 4 lakini kushiriki Conference no. hawa wachezaji sio wa kushika na. 10--20 no, I disagree. Poche hawezi, ameshindwa
  1. Siamini kama Mudryk ni mbovu
  2. Siamini kama Enzo ni mbovu
  3. Siamini kama Caicedo ni mbovu
  4. Siamini kama Gusto ni mbovu
  5. Siamini kama Disasi ni mbovu
  6. Siamini kama Badiashile i mbovu
  7. Siamini kama Colwill ni mbovu
  8. Siamini kama Noni Madueke ni mbovu
  9. Siamini kama Nicolas Jackson ni mbovu
  10. Siamini kama Carney Chukwuemeka ni mbovu
  11. Siamini kama Andrey Santos ni mbovu
  12. Siamini kama Ian Maatsen alikuwa ni mbovu
  13. Siamini kama Alfie Gilchrist ni mbovu
  14. Siamini kama Catsledine ni mbovu
  15. Siamini kama Cesare Casadei ni mbovu
 
Wewe unahisi sisi hatujui profile ya Caicedo kama ni defensive mid?

Kwahiyo unataka kusema wakati Liverpool wanataka kumsajili Caicedo kama mbadala wa Fabinho kwenye DM, walikua hawana akili?

Wewe unahisi kwanini mpaka sasa Klopp hana defensive mid?
Binadamu yeyote anaweza akawa na akili na anaweza asiwe na akili, hilo ndilo jibu
 
Kocha kashindwa tengeneza mfumo wa kuwasuit hawa wachezaji .

Atapokuja kocha wakujielewa ndio mtaelewa hichi kitu.

Kama system ya team haiko vizuri hakuna mchezaji atakaeonekana mzuri
Iko simple and direct, haitaji hata elimu ya darasa la pili kuelewa hii logic na connection
 
Siku zote huwa haunielewi halafu ni kama unahisi tunashindana katika hili. Wewe kuna siku uliwahi kusema waxhezaji wanafunga magoli kwa juhudi zao wenyewe. Sasa hivi utalalamikiwa mfumo wa uchezaji haueleweki, Poch ni tatizo, na blah blah nyingine nyingi.

Tuanzie kwa Antonio Conte, Maurisio Sarri, Lampard, Tuchel na sasa tuna Poch. Katika wote hao kila mmoja ana kocha wake ambaye anasema hapa tulikua na jembe kweli. Lakini mwisho wa siku nini kilitokea? Nachotaka kumaanisha ni kwamba haijalishi kocha ana deficience gani kwenye kazi yake hata awe mzuri au mbaya vipi atafukuzwa tu kukitokea defficience yoyote.

SImtetei Poch kama wengi mnavyo ni address humu. Nasimama na Chelsea yangu nje ya Poch tuna wachezaji wabovu ambao ni average, tuko hapa tulipo kwa sababu ya fukuza fukuza ya makocha, leo hii ukiulizwa style ya uchezaji wetu ni ipi huwezi elewa. Atleast Conte, Mourunho na Ancelotti walieleweka na ndio waliotupa EPL tittle.
Kama kocha hawezi, wachezaji experience YES wanajituma wenyewe kihivyo
Kocha anainfluence ya uchezaji wa timu kwa asilimia 90+% ebu tuacheni kurudiarudia mambo yale yale ambayo yako wazi
 
Katika hii timu ya Chelsea, wachezaji wengi ni wachanga, hiyo ni kweli na haina ubishi ila Kocha ni mchanga kuliko wachezaji
Kwa nini
Dalili kubwa ya kwanza ya kocha mchanga kwenye soka ni kushindwa kuifanya timu iwe solid
Pili kushindwa kuifanya timu ibalance kwenye idara zote za nyuma. katikati a mbele
Lampard kilichomsumbua ni hicho
Sasa kuna tofauti gani kati ya Lampard na Pochettino?
 
Siku zote huwa haunielewi halafu ni kama unahisi tunashindana katika hili. Wewe kuna siku uliwahi kusema waxhezaji wanafunga magoli kwa juhudi zao wenyewe. Sasa hivi utalalamikiwa mfumo wa uchezaji haueleweki, Poch ni tatizo, na blah blah nyingine nyingi.

Tuanzie kwa Antonio Conte, Maurisio Sarri, Lampard, Tuchel na sasa tuna Poch. Katika wote hao kila mmoja ana kocha wake ambaye anasema hapa tulikua na jembe kweli. Lakini mwisho wa siku nini kilitokea? Nachotaka kumaanisha ni kwamba haijalishi kocha ana deficience gani kwenye kazi yake hata awe mzuri au mbaya vipi atafukuzwa tu kukitokea defficience yoyote.

SImtetei Poch kama wengi mnavyo ni address humu. Nasimama na Chelsea yangu nje ya Poch tuna wachezaji wabovu ambao ni average, tuko hapa tulipo kwa sababu ya fukuza fukuza ya makocha, leo hii ukiulizwa style ya uchezaji wetu ni ipi huwezi elewa. Atleast Conte, Mourunho na Ancelotti walieleweka na ndio waliotupa EPL tittle.

Makocha wote uliowataja hapo Conte,Sarri, hakuna hata wachezaji wa sasa alikuwa hapo

Tuchel ni Sterling,Silva,cucurella,James n Chilwel wengine wote niwapya

Lampard interim

Poch almost Team yote ameanza nayo Tangu pre season sehem ipi ya uwanja tunaonekan ni bora kuliko team zingine, style yetu ya uchezaji ni ipi huwez jibu hili swali,

Wachezaji ambao unasema ni wabovu almost team zote kubwa zilikuwa zinawahitaji.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom