Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Ndio maana nikakwambia tunatofautiana namna tunavyoangalia na kuutafsiri. Ila Enzo huwa hachezi namba 10. Mtu wa mwisho kucheza namba 10 vizuri alikua ni Mount. Sasa hivi tuna ingia toka za mara Galagher, Nkunku, Palmer hata Sterling. Sisi hatuna namba 10 mzuri anayeweza kupiga pass za kueleweka hatuna huyo
Aliwahi kuchezeshwa namba 10 mkuu, tena mechi mbili au tatu au hata zaidi. Mashabiki walilalamika sana baada ya kiwango cha Enzo kushuka na ndipo kocha akamrudisha kwenye CM pivot na Caicedo lakini bado aliendelea kucheza vibaya na ndipo akaenda majeruhi yale madogo. Shida kubwa sasa ya Poche ni kulazimisha Colwill acheze LB, hiyo nafasi anakaba kweli vizuri ila colwill kwa sababu sio LB hawezi kupanda na kupeleka mashabulizi kama anavyofanya Chilwell au angefanya Maatsena hadi anaondoka sijui kama aliwahi kuichezea hiyo nafasi yake. Pochettino mtukutu anaona kabisa hakuna matokeo mazuri ya kumchezesha mchezaji out of position yeye anang'ang'ania tu
 
1705270168845.png
 
Je hii ya PEP ina ukweli ndani yake alipokuwa anamuongelea Kelvin, mimi naona kama ni sawa

Pep
"Sehemu ya goli la mpinzani sio mbinu tu, ni kipaji ndicho kinachotakiwa"
"Kevin de Bruyne ni kipaji halisi. Sio juu ya mbinu, ni juu ya kipaji".

Pep
“The final third is not tactics, it’s talent”
“Kevin de Bruyne is pure talent. It’s not about tactics, it’s about talent”.

Hapa sasa naanza kujirudi, Pochettino tunamuonea bure japo ana sehemu yake ya kuandamwa kwa kuchezesha wachezaji nje ya nafasi zao

Ila hili la kutumbukiza magoli wavuni inatakiwa talent kama alivyosema kipara
1705301293741.png
 
“The final third is not tactics, it’s talent”
“Kevin de Bruyne is pure talent. It’s not about tactics, it’s about talent”.

Hapa Pep amenena vema.

The Blues kuna nafasi za wazi tunazichezeaga kwenye lango la mpinzani

Huwa na imagine tungekuwa na mchezaji aina ya yule Hazard wetu hayo ni magoli tuu.

Arse8 wanachezaga vitatictics vyao uchwara mbele ya goli la mpinzani wanaishia kulaumiana.
Nimekuja na hoja ya kumpinga PEP kwa asilimia 50
Huwezi tegemea talent to ukaleta matokeo
50 tactics na 50 tallents
ebu tuone hii video ya Chelsea goli lilifungwa baada ya pasi 26
Je hiyo ni tallent au tactics?
 
Chelsea have won possession in the attacking (final) third more times (137) than any other team in Europe's top five leagues this season.

Swahili

Chelsea wameweza kunyang'anya umiliki wa mpira katika eneo la ushambuliaji mara nyingi zaidi (137) kuliko timu yoyote kwenye ligi tano bora za Ulaya msimu huu.


Hapa tunahitaji sana wafungaji na mawinga na au viungo wabunifu
 
Je hii ya PEP ina ukweli ndani yake alipokuwa anamuongelea Kelvin, mimi naona kama ni sawa

Pep
"Sehemu ya goli la mpinzani sio mbinu tu, ni kipaji ndicho kinachotakiwa"
"Kevin de Bruyne ni kipaji halisi. Sio juu ya mbinu, ni juu ya kipaji".

Pep
“The final third is not tactics, it’s talent”
“Kevin de Bruyne is pure talent. It’s not about tactics, it’s about talent”.

Hapa sasa naanza kujirudi, Pochettino tunamuonea bure japo ana sehemu yake ya kuandamwa kwa kuchezesha wachezaji nje ya nafasi zao

Ila hili la kutumbukiza magoli wavuni inatakiwa talent kama alivyosema kipara
View attachment 2872353

Huwezi tegemea kila match talent ndio iamue matokeo tho swala zima la kufunga ni juu ya mchezaj ila mpaka hiyo chance inapatikana hapo ndio tactics zinaingia
 
Huwezi tegemea kila match talent ndio iamue matokeo tho swala zima la kufunga ni juu ya mchezaj ila mpaka hiyo chance inapatikana hapo ndio tactics zinaingia
Daima ni tactics+tallent=win
Nimekuja na hoja ya kumpinga PEP kwa asilimia 50
Huwezi tegemea talent to ukaleta matokeo
50 tactics na 50 tallents
ebu tuone hii video ya Chelsea goli lilifungwa baada ya pasi 26
Je hiyo ni tallent au tactics?
View attachment 2872815
 
Oya dingi Mourinho hana kazi ,hii timu apewe Mourinho ,mzee yupo serious na kazi ,atakuwa anavizaba makofi hivi vitoto mpaka akili ziwakae
Mourinho ana damu ya blue ,apewe timu ,fukuza yule pimbi mwenye mashavu makubwa kama panyabuku mwenye mimba
 
THE BLUES ingemfaa sana Morinyo since day 1 Toddy anaichukua timu.

Yale mahela £1B Toddy aliyomwaga kizembe yangemkuta Morinyo angenunua wazee wa kazi kweli kweli.

Binafsi sio muumini wa kujenga timu kupitia kindergarten (TODDY VISION), napenda sana ile vision ya Roman Abramovich (Lete kocha world class + sajili wachezaji experienced = Makombe)
Yeah ! Hii ya kujenga timu kwa kutumia makinda ,tena ambao ndio wanaanza career yao ni mtihani sana , hii timu itakuwa midtable
Timu kubwa successful zote huwa wanafanya mixing , Mfano Madrid pale , sasa Toddy anachofanya ,labda anataka kuifanya Chelsea iwe kama hizo midteams za kukuza vipaji mfano Borusia Dortmund , Leipzig ,salburg , Ajax nk ,na si kutengeneza timu za kutwaa mataji kama Chelsea ilivyozoeleka
 
THE BLUES ingemfaa sana Morinyo since day 1 Toddy anaichukua timu.

Yale mahela £1B Toddy aliyomwaga kizembe yangemkuta Morinyo angenunua wazee wa kazi kweli kweli.

Binafsi sio muumini wa kujenga timu kupitia kindergarten (TODDY VISION), napenda sana ile vision ya Roman Abramovich (Lete kocha world class + sajili wachezaji experienced = Makombe)
Hii squad MOU haitaiweza kabisa, MOU ana wachezaji wake wa kumfaa., MOU hatawezana na asquad isiyokuwa na wazee wa hekima kama akina Silva
 
Oya dingi Mourinho hana kazi ,hii timu apewe Mourinho ,mzee yupo serious na kazi ,atakuwa anavizaba makofi hivi vitoto mpaka akili ziwakae
Mourinho ana damu ya blue ,apewe timu ,fukuza yule pimbi mwenye mashavu makubwa kama panyabuku mwenye mimba
Hii squad MOU atawatukana sana na hadi watoto watafute dirisha ya kutokea
 
Daima ni tactics+tallent=win
Game plan inakuwa na vitu hivi
  1. Strategies
  2. Tactics
  3. Playing Pattern
Hizo zote zinakamilishwa na Tallent binafsi ya mchezaji mmoja mmoja kwenye nafasi yake ndipo ushindi unapatikana kwa urahisi vinginevyo tutasubiri makosa ya adui ndipo tushinde
 
Oya dingi Mourinho hana kazi ,hii timu apewe Mourinho ,mzee yupo serious na kazi ,atakuwa anavizaba makofi hivi vitoto mpaka akili ziwakae
Mourinho ana damu ya blue ,apewe timu ,fukuza yule pimbi mwenye mashavu makubwa kama panyabuku mwenye mimba
MOU aachane tu na mpira, mpira wake ushapitwa na wakati. MOU shughuli yake ilishaishaga kitambo ndio mana kila anapoenda anatimuliwa.
 
Chelsea wanajiandaa kumrudisha kiungo wake Cesare Casadei kutoka kwenye mkopo na Leicester City ili kuchukua nafasi katika kikosi cha kwanza cha Mauricio Pochettino.

@Matt_Law_DT

Maoni yangu

Kuziba nafasi ya majeruhi ya akina Lesley na Lavia
Mpango wa kuuza Gallagher umeiva
Pia wanatengeneza mkopo wa mchezaji mwingine asiyetakiwa
Kumbuka tuna wachezaji hawa wanarudi kundini pia
  1. Angelo Gabriel
  2. Andrey Santos
  3. Ted Curd
  4. Zak Sturge
Tukumbuke kwenye nafasi ya kiungo bado tunao akina
  1. Andrey Santos
  2. Lesley Ugochukwu
  3. Carney Chukwuemeka
  4. Romeo Lavia
  5. Conor Gallagher
  6. Moises Caicedo na
  7. Enzo Fernandez
1705682500883.png
 
Chelsea ni moja ya timu BORA kwenye ligi ya Uingereza ikipata pointi pale inapoanza kuongoza.

Tujenge kutokea hapo

1705687780849.png
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom